Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 14

Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?

Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?

“Endelea kuhubiri habari njema, timiza kwa ukamili utumishi wako.”​—2 TI. 4:5, maelezo ya chini.

WIMBO 57 Kuwahubiria Watu wa Namna Zote

KIFUPI CHA HABARI *

Kisha Yesu kufufuliwa, alikutana na wanafunzi wake na akawaamuru ‘waende, na wafanye wanafunzi’ (Picha hizi zinapatana na fungu la 1)

1. Watumishi wote wa Mungu wanapenda kufanya nini, na juu ya nini? (Ona picha ku jalada ya gazeti hili.)

KRISTO YESU aliamuru wanafunzi wake ‘waende, na kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mt. 28:19) Watumishi wote waaminifu wa Mungu wanapenda kujifunza namna wanaweza ‘kutimiza kwa ukamili’ utumishi huo wenye wamepewa. (2 Ti. 4:5) Kwa kweli, ile kazi ni ya maana sana, ni yenye kufaa sana, na inapaswa kufanywa haraka sana kuliko kazi zingine zote mu maisha. Lakini, hata kama tunapenda kupitisha wakati mingi mu utumishi wetu, inaweza kuwa nguvu kufanya vile.

2. Tunapambana na magumu gani wakati tunatimiza utumishi wetu?

2 Kuko kazi zingine za maana zenye zinaomba tutumie wakati wetu na nguvu zetu. Pengine tunapaswa kufanya kazi ya kimwili kwa saa mingi kila siku ili kutimiza mahitaji yetu na ya watu wa familia yetu. Pengine ni nguvu kushugulikia madaraka mengine ya familia, ao pengine tuko wagonjwa, tunashuka moyo, ao tunateseka kwa sababu ya maumivu yenye kuletwa na uzee. Tunaweza kufanya nini ili tutimize kwa ukamili utumishi wetu hata kama tunapambana na ile magumu?

3. Maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 13:23, inaonyesha nini?

3 Kama hali zetu hazituruhusu kutumia wakati mingi mu utumishi wa Yehova, hatupaswe kuvunjika moyo. Yesu alijua kama sisi wote hatungekuwa na uwezo wa kuzaa hesabu ileile ya matunda ya Ufalme. (Soma Matayo 13:23.) Yehova anapendezwa sana na kila jambo lenye tunafanya mu utumishi wake, kama tu tunafanya vile kwa uwezo wetu wote. (Ebr. 6:10-12) Lakini, tunaweza kuona kama hali zetu zinaweza kuturuhusu kufanya mengi zaidi. Katika habari hii, tutaona mambo yenye tunaweza kufanya ili kutia utumishi wetu pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu, kuendelea kuwa na maisha rahisi ao mepesi, na kukomalisha ufundi wetu wa kuhubiri na kufundisha. Lakini, tuone kwanza maana ya kutimiza kwa ukamili utumishi wetu.

4. Kutimiza kwa ukamili utumishi wetu, maana yake nini?

4 Kwa kifupi, ili kutimiza kwa ukamili utumishi wetu, tunapaswa kuhubiri na kufundisha kwa bidii sana kulingana na uwezo wetu. Lakini kutimiza kwa ukamili utumishi wetu, hakumaanishe tu wakati wenye tunapitisha mu kazi ya kuhubiri. Yehova anapendezwa na nia yenye kutuchochea kuhubiri. Kwa sababu tunamupenda Yehova na jirani yetu, tunatumika kwa nafsi yetu yote katika utumishi wetu wa Kikristo. * (Mk. 12:30, 31; Kol. 3:23) Kumutumikia Mungu kwa nafsi yote, maana yake kujitoa kabisa, na kutumia nguvu zetu zote katika utumishi wake kadiri tunaweza. Wakati tunaona kuwa ni pendeleo kubwa kufanya kazi ya kuhubiri, tunajikaza kuhubiria watu wengi habari njema kadiri tunaweza.

5-6. Ni mufano gani wenye kuonyesha namna mutu mwenye kuwa na wakati kidogo anaweza kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza?

5 Wazia kijana mwenye anafurahia kupiga gitari. Anafurahia kupiga muziki kila wakati anaweza kufanya vile. Kisha anapata kazi ya kupiga gitari kila mwisho wa juma mu restora fulani ya eneo lao. Lakini, feza zenye anapokea hazimutimizie mahitaji yake yote. Kwa hiyo, anatumika mu duka kuanzia Siku ya Kwanza mupaka Siku ya Tano. Hata kama anatumia wakati wake mingi katika duka, jambo lenye anapenda sana ni kupiga muziki. Anapenda sana kukomalisha ufundi wake wa kupiga muziki ili afanye kazi ya kupiga muziki wakati wote. Kwa hiyo, anatafuta nafasi za kupiga muziki hata kama ni kwa wakati mufupi.

6 Vilevile, pengine haiwezekane upitishe wakati mingi katika kazi ya kuhubiri. Lakini ile njo kazi yenye unapenda kufanya. Wakati unahubiria watu habari njema, unajikaza kukomalisha ufundi wako wa kugusa mioyo yao. Kwa sababu uko na mambo mingi ya kufanya, unaweza kujiuliza namna gani unaweza kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza mu maisha yako.

MAMBO YA KUFANYA ILI KUTIA UTUMISHI WAKO PA NAFASI YA KWANZA

7-8. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Yesu juu ya namna aliona utumishi wake?

7 Yesu alionyesha mufano muzuri zaidi juu ya namna aliona utumishi wake. Jambo la maana zaidi mu maisha yake lilikuwa kuzungumuza na watu juu ya Ufalme wa Mungu. (Yohana 4:34, 35) Alitembea kilometre mingi ili kuhubiria watu wengi zaidi kadiri iliwezekana. Alitumia kila nafasi ili kuzungumuza na watu mu nyumba zao na mahali pa watu wengi. Yesu alitia utumishi wake pa nafasi ya kwanza mu maisha yake.

8 Tunaweza kumuiga Kristo kwa kutafuta nafasi za kuzungumuza na watu juu ya habari njema kila mahali na kila wakati inawezekana kufanya vile. Tuko tayari kujiima mambo fulani ili kuhubiri habari njema. (Mk. 6:31-34; 1 Pe. 2:21) Ndugu na dada fulani mu kutaniko wako mapainia wa pekee, mapainia wa kawaida, ao mapainia wasaidizi. Wengine wamejifunza kusema luga ingine ao wamehamia mahali kwenye kuwa lazima kubwa ya wahubiri. Lakini, kazi kubwa ya kuhubiri inafanywa na wahubiri wa kawaida wa Ufalme, wenye wanahubiri kwa uwezo wao wote. Ikuwe tunaweza kufanya mambo mingi ao kidogo mu utumishi wetu, Yehova hatuombe tufanye mambo yenye kupita uwezo wetu. Anapenda sisi wote tufurahie utumishi wetu mutakatifu wakati tunaendelea kutangaza “habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha.”​—1 Ti. 1:11; Kum. 30:11.

9. (a) Namna gani Paulo alitia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza hata wakati alipaswa kufanya kazi ya kimwili? (b) Matendo 28:16, 30, 31 inaonyesha nini juu ya namna Paulo aliona kazi ya kuhubiri?

9 Mutume Paulo alionyesha mufano muzuri wa kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza mu maisha yake. Wakati alikuwa katika muji wa Korinto wakati wa safari yake ya pili ya umisionere, alikuwa na feza kidogo na alipaswa kutumia wakati fulani ili kufanya kazi ya kutengeneza mahema. Lakini, Paulo hakuona kazi ya kutengeneza mahema kuwa kazi ya maana zaidi mu maisha yake. Alifanya kazi hiyo ili kutimiza mahitaji yake ya kimwili katika utumishi wake, kusudi aweze kuhubiria Wakorinto habari njema “bila kuwaomba kitu.” (2 Ko. 11:7) Hata kama Paulo alipaswa kufanya kazi fulani ya kimwili, aliendelea kutia utumishi wake pa nafasi ya kwanza, na alihubiri kila siku ya Sabato. Kisha hali yake kuwa muzuri zaidi, Paulo aliweza kukaza zaidi akili yake juu ya kazi ya kuhubiri. “Akaanza kuhangaikia sana lile neno, akitolea Wayahudi ushahidi ili kuhakikisha kwamba Yesu ndiye Kristo.” (Mdo. 18:3-5; 2 Ko. 11:9) Kisha, wakati alifungwa kwa miaka mbili mu nyumba, katika muji wa Roma, Paulo alikuwa anahubiria wageni wenye walikuwa wanamutembelea na alikuwa anaandika barua mbalimbali. (Soma Matendo 28:16, 30, 31.) Paulo hakuruhusu hata kidogo jambo lolote likuwe la maana kupita utumishi wake. Aliandika hivi: “Kwa kuwa tuko na utumishi huu . . . , hatuache.” (2 Ko. 4:1) Kama mutume Paulo, hata kama tunapaswa kutumia wakati fulani mu kazi ya kimwili, tunaweza kutia kazi ya Ufalme pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu.

Kuko njia za mingi zenye tunaweza kutumia ili kutimiza kwa ukamili utumishi wetu (Picha hizi zinapatana na fungu la 10-11)

10-11. Tunaweza kufanya nini ili kutimiza kwa ukamili utumishi wetu ikiwa tuko na matatizo ya afya?

10 Ikiwa kwa sababu ya uzee ao tatizo fulani la afya hatuwezi kufanya kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kama vile tungependa kufanya, tunaweza kufanya aina zingine za mahubiri. Wahubiri wa wakati wa mitume walihubiria watu kila mahali kwenye walipatikana. Walitumia kila nafasi ili kuzungumuza na watu juu ya ile kweli; walihubiri nyumba kwa nyumba, mahali pa watu wengi, na wakati wowote; kila mahali kwenye ‘walikuwa wanakuta [watu].’ (Mdo. 17:17; 20:20) Kama hatuna uwezo wa kutembea sana, tunaweza kukaa mahali pa watu wengi ili kuhubiria watu wenye kupita pale. Ao tunaweza kuhubiri wakati wowote, kuhubiri kupitia barua, ao kupitia telefone. Wahubiri wengi wenye hawana uwezo wa kufanya mahubiri ya nyumba kwa nyumba kwa sababu ya hali zao, wanapata furaha sana kwa kufanya aina hizo zingine za mahubiri.

11 Hata kama uko na matatizo ya afya, unaweza kutimiza kwa ukamili utumishi wako. Fikiria tena mufano wa mutume Paulo. Alisema hivi: “Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.” (Flp. 4:13) Paulo alikuwa na lazima ya nguvu hiyo wakati aligonjwa katika safari yake moja kati ya safari zake za umisionere. Aliambia Wagalatia hivi: “Ni kwa sababu ya ugonjwa wa kimwili ndiyo nilipata nafasi yangu ya kwanza ya kuwatangazia ninyi habari njema.” (Gal. 4:13) Vilevile, matatizo yako ya afya inaweza kukupatia nafasi ya kutangazia wengine habari njema kama vile wanganga na watu wengine wenye kuhangaikia wagonjwa. Wengi kati ya watu hao wanaweza kuwa kwenye kazi wakati wahubiri wanatembelea nyumba zao.

NAMNA YA KUFANYA MAISHA YAKO KUWA RAHISI

12. Kufanya jicho lako ‘likazie jambo moja,’ maana yake nini?

12 Yesu alisema hivi: “Taa ya mwili ni jicho. Basi, kama jicho lako linakazia jambo moja [ao “liko rahisi,” maelezo ya chini], mwili wako wote utakuwa wenye mwangaza.” (Mt. 6:22) Alimaanisha nini? Alimaanisha kama tunapaswa kufanya maisha yetu ikuwe rahisi ao yenye kukazia muradi moja, ao kusudi moja, na bila kukengeushwa. Yesu mwenyewe alituwekea mufano kwa kukazia akili utumishi wake mu maisha yake, na alifundisha wanafunzi wake waendelee kukazia akili utumishi wao kwa Yehova na Ufalme wake. Tunamuiga Yesu kwa kufanya kazi yetu ya kuhubiri ikuwe jambo la maana zaidi mu maisha yetu, ni kusema, “kutafuta kwanza Ufalme na haki [ya Mungu].”​—Mt. 6:33.

13. Ni nini inaweza kutusaidia tukaze akili yetu juu ya kazi ya kuhubiri?

13 Njia moja ya kukazia akili kazi yetu ya kuhubiri ni kufanya maisha yetu ikuwe rahisi ili tuweze kutumia wakati mingi zaidi juu ya kusaidia watu wamujue Yehova na kumupenda. * Kwa mufano, tunaweza kufanya mabadiliko juu ya saa zenye tunatumia katika kazi ya kimwili ili tuweze kutumia wakati mingi zaidi mu kazi ya kuhubiri katika juma. Ao tunaweza kupunguza wakati wenye tunatumia katika mambo fulani ya kujifurahisha yenye kukamata wakati mingi.

14. Bibi na bwana fulani walifanya mabadiliko gani ili watumie wakati mingi zaidi mu kazi ya kuhubiri na kukaza akili juu ya kazi hiyo?

14 Muzee mumoja wa kutaniko mwenye kuitwa Elias, yeye pamoja na bibi yake walifanya vile. Anaeleza hivi: “Hatungeweza kuwa mapainia wakati huo, lakini tulipaswa kufanya jambo fulani. Kwa hiyo, tulifanya mambo kidogo-kidogo yenye ilitusaidia tupitishe wakati mingi zaidi mu kazi yetu ya kuhubiri. Kwa mufano, tulianza kutumia feza kidogo, tuliacha kutumia wakati mingi mu mambo ya kujifurahisha, na tukaomba wakubwa wetu wa kazi wabadilishe programu yetu ya kazi. Kwa hiyo, tuliweza kupata wakati wa kuhubiri mangaribi, kuongoza mafunzo ya Biblia ya mingi zaidi, na hata kuhubiri katikati ya juma mara mbili katika mwezi. Tulipata furaha kabisa!”

MAMBO YA KUFANYA ILI KUKOMALISHA UFUNDI WAKO WA KUHUBIRI NA KUFUNDISHA

Kutumia mambo yenye tunajifunza ku mukutano wetu wa katikati ya juma kutatusaidia tuendelee kufanya maendeleo katika utumishi wetu (Picha hizi zinapatana na fungu la 15-16) *

15-16. Kulingana na 1 Timoteo 4:13, 15, tunaweza kufanya nini ili kukomalisha ufundi wetu wa kuhubiri? (Ona pia kisanduku “ Miradi ya Kunisaidia Nitimize kwa Ukamili Utumishi Wangu.”)

15 Njia ingine ya kutimiza kwa ukamili utumishi wetu ni kukomalisha ufundi wetu wa kuhubiri na kufundisha. Watu wenye kufanya kazi za aina fulani wanapaswa kupewa mazoezi kwa ukawaida ili kuongeza ujuzi wao na ufundi wao. Ni vile pia juu ya wahubiri wa Ufalme. Tunapaswa kuendelea kujifunza namna ya kukomalisha ufundi wetu mu kazi yetu ya kuhubiri.​—Mez. 1:5; soma 1 Timoteo 4:13, 15.

16 Lakini, tunaweza kufanya nini ili tuendelee kufanya maendeleo mu kazi yetu ya kuhubiri? Tunapaswa kukaza akili yetu juu ya maagizo yenye tunapata kila juma ku Mukutano Utumishi na Maisha. Mukutano huo unatupatia mazoezi ya maana ya kutusaidia tuendelee kufanya ufundi wetu wa kuhubiri ukuwe muzuri zaidi. Kwa mufano, wakati musimamizi anatolea mashauri wale wenye wamefanya migao ya wanafunzi, tunaweza kujifunza mambo fulani yenye inaweza kutusaidia kukomalisha ufundi wetu wa kuhubiri na kufundisha. Tunaweza kutumia ile mashauri wakati wenye kuja, wakati tunazungumuza na mutu fulani juu ya habari njema. Tunaweza kuomba mwangalizi wa kikundi chetu cha mahubiri musaada ao kuhubiri pamoja naye ao pamoja na muhubiri mwingine mwenye kuwa na uzoefu, painia, ao mwangalizi wa muzunguko. Wakati tunaendelea kuwa na ufundi zaidi wa kutumia vyombo vyote vyenye kuwa kati ya Vyombo Vyetu vya Kufundishia, tutafurahia zaidi kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha.

17. Utajisikia namna gani wakati unatimiza kwa ukamili utumishi wako?

17 Tuko na pendeleo kubwa sana kwa sababu Yehova anaturuhusu tukuwe “wafanyakazi pamoja [naye]”! (1 Ko. 3:9) Wakati ‘unahakikisha mambo ya maana zaidi,’ na kukaza akili juu ya utumishi wa Kikristo, ‘utamutumikia Yehova kwa furaha.’ (Flp. 1:10; Zb. 100:2) Kwa sababu uko mutumishi wa Mungu, unaweza kuwa hakika kama atakupatia nguvu yenye uko nayo lazima ili utimize utumishi wako hata kama uko na magumu ao uzaifu gani. (2 Ko. 4:1, 7; 6:4) Ikuwe hali yako inakuruhusu kuhubiri sana ao kuhubiri kidogo, unaweza ‘kuwa na sababu ya kufurahi’ ikiwa unafanya utumishi wako kwa nafsi yote. (Gal. 6:4) Wakati unatimiza kwa ukamili utumishi wako, unaonyesha kama unamupenda Yehova na unapenda watu wengine. “Kwa kufanya vile utajiokoa wewe mwenyewe na utaokoa pia wale wenye wanakusikiliza.”​—1 Ti. 4:16.

WIMBO 58 Kutafuta Marafiki wa Amani

^ fu. 5 Tumepewa kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme na kufanya wanafunzi. Habari hii itazungumuzia namna tunaweza kutimiza kwa ukamili utumishi wetu, hata kama tuko na magumu mingi. Tutajifunza pia mambo yenye tunaweza kufanya ili tukuwe wahubiri wazuri zaidi na kupata furaha mu kazi yetu ya kuhubiri.

^ fu. 4 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Utumishi wa Kikristo unatia ndani sehemu mbalimbali za kazi ya kuhubiri na kufundisha, kazi ya kujenga na ya kutunza majengo yenye kutumiwa kwa ajili ya faida za Ufalme, na kazi ya kutoa misaada wakati wa misiba.​—2 Ko. 5:18, 19; 8:4.

^ fu. 13 Ili kujua mambo saba yenye unaweza kufanya, ona kisanduku chenye kichwa “Namna ya Kufanya Maisha Yako Kuwa Mepesi” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 7, 2016, uku. 8.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa mukutano wa katikati ya juma, dada mumoja anafanya onyesho juu ya namna ya kumurudilia mutu. Kisha, wakati musimamizi anamutolea mashauri, dada huyo anaandika mambo fulani mu broshua yake Kufundisha. Na mwisho wa juma, anatumia katika mahubiri mambo yenye alijifunza ku mukutano.