Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 16

Ushikamane na Kweli Juu ya Kifo

Ushikamane na Kweli Juu ya Kifo

“Tunafanya tofauti kati ya neno la kweli lenye liliongozwa na roho na neno lenye kosa lenye liliongozwa na roho.”​—1 YO. 4:6.

WIMBO 73 Tupe Ujasiri

KIFUPI CHA HABARI *

Kuliko kujiunga na wengine ili kufanya desturi zenye hazimufurahishe Mungu, ufariji watu wa jamaa yako wenye wamefiwa na mupendwa wao (Picha hii inapatana na fungu la 1-2) *

1-2. (a) Ni njia gani zenye Shetani ametumia ili kudanganya watu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

SHETANI, “baba ya uongo,” amedanganya watu tangu wakati wa Adamu na Eva. (Yoh. 8:44) Kati ya uongo wa Shetani, kuko mafundisho ya uongo juu ya kifo na juu ya uzima kisha kifo. Desturi na mazoea mingi yenye kuenea sana inategemea ile mafundisho. Kwa hiyo, ndugu na dada zetu fulani wamelazimika ‘kupigania kabisa imani’ yao wakati mutu fulani mu familia yao ao mu eneo lao anakufa.​—Yud. 3.

2 Kama unapambana na majaribu kama hayo, ni nini inaweza kukusaidia ushikamane na mambo yenye Biblia inafundisha juu ya kifo? (Efe. 6:11) Unaweza kufanya nini ili kutia moyo na kutia nguvu Mukristo mwenzako mwenye anakazwa kufanya desturi fulani zenye hazimupendeze Mungu? Habari hii itazungumuzia muongozo wenye Yehova ametutolea. Tuzungumuzie kwanza mambo yenye Biblia inasema juu ya kifo.

KWELI JUU YA HALI YA WATU WENYE WAMEKUFA

3. Uongo wa kwanza ulileta matokeo gani?

3 Mungu hakukusudia watu wakufe. Ili Adamu na Eva waishi milele, walipaswa kumutii Yehova. Aliwapatia amri hii ya mwepesi: “Kuhusu matunda ya muti wa ujuzi wa mema na mabaya, usikule, kwa maana siku yenye utakula matunda yake, hakika utakufa.” (Mwa. 2:16, 17) Kisha Shetani alileta matatizo. Alitumia nyoka ili kumuambia Eva hivi: “Hakika hamutakufa.” Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, Eva aliamini uongo huo na akakula tunda hilo. Kisha, bwana yake naye alikula tunda hilo. (Mwa. 3:4, 6) Ni vile zambi na kifo vilianza.​—Ro. 5:12.

4-5. Namna gani Shetani ameendelea kudanganya watu?

4 Adamu na Eva walikufa kama vile tu Mungu alikuwa amesema. Lakini Shetani hakuacha kusema uongo juu ya kifo. Kisha wakati fulani, alianza kusema mambo ingine ya uongo. Fundisho moja la uongo kati ya ile mambo ya uongo ni hili: kisha mwili kufa, sehemu fulani ya mutu inaendelea kuishi, pengine katika makao ya roho. Uongo mbalimbali wenye kutokana na fundisho hilo la uongo, umedanganya watu wengi mupaka leo.​—1 Ti. 4:1.

5 Juu ya nini watu wengi sana wanadanganywa? Shetani anajua namna watu wanajisikia juu ya kifo na anatumia jambo hilo ili kuwadanganya. Kwa sababu tuliumbwa ili tuishi milele, hatupendake kufa. (Muh. 3:11) Tunaona kifo kuwa adui yetu.​—1 Ko. 15:26.

6-7. (a) Je, Shetani ameweza kufanya kweli juu ya kifo iendelee kufichwa? Fasiria. (b) Namna gani kweli ya Biblia inatusaidia tusiogope watu wenye wamekufa?

6 Hata kama Shetani amejikaza sana, kweli juu ya kifo haijaendelea kufichwa hata kidogo. Kwa kweli, kuliko wakati mwingine wowote, leo watu wengi zaidi wanajua mafundisho ya Biblia juu ya hali ya watu wenye wamekufa na tumaini lenye Mungu anatoa kwa ajili ya yao, na wanatangazia wengine ile mafundisho. (Muh. 9:5, 10; Mdo. 24:15) Kweli hizo zinatufariji, na zinatusaidia tusikuwe na woga na tusikuwe na mashaka juu ya jambo lenye linapata wanadamu wakati wanakufa. Kwa mufano, hatuogope watu wenye wamekufa; na hatuogope kuwa jambo fulani la mubaya litawapata. Tunajua kama hawaishi na hawawezi kutendea mutu yeyote mambo ya mubaya. Ni kama vile wako katika usingizi muzito. (Yoh. 11:11-14) Tunajua pia kama watu wenye wamekufa, hawajue namna wakati unapita. Kwa hiyo, wakati wa ufufuo, hata wale wenye wamekufa kumepita mamia ya miaka wataona kama wakati wenye umepita ni mufupi sana, ni kama vile kufunga na kufungua jicho.

7 Kwa kweli, unakubali kama kweli juu ya hali ya watu wenye wamekufa iko wazi, iko mwepesi, na inapatana na akili. Iko tofauti sana na uongo wa Shetani wenye kuvuruga watu! Zaidi ya kudanganya watu, uongo huo unamusingizia pia Muumbaji wetu. Ili kuelewa muzuri zaidi matokeo ya mubaya yenye uongo wa Shetani umeleta, tutazungumuzia maulizo hii: Namna gani uongo wa Shetani umemusingizia Yehova? Namna gani umefanya watu waamini kwamba haiko lazima kuwa na imani katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Kristo? Namna gani umeongezea watu huzuni na mateso?

UONGO WA SHETANI UMELETA MAMBO MINGI YENYE KUUMIZA

8. Kulingana na Yeremia 19:5, namna gani uongo wa Shetani juu ya watu wenye wamekufa unamusingizia Yehova?

8 Uongo wa Shetani juu ya watu wenye wamekufa unamusingizia Yehova. Kati ya uongo huo kuko fundisho la uongo lenye kusema kama watu wenye wamekufa wanateseka mu moto wa mateso. Mafundisho kama hayo inamusingizia Mungu! Namna gani? Kwa kweli, inafanya watu waamini kama Mungu mwenye upendo iko na utu kama wa Shetani. (1 Yo. 4:8) Hilo linakufanya ujisikie namna gani? Na jambo la maana zaidi, linamufanya Yehova ajisikie namna gani? Kwa kweli, anachukia matendo yote ya kukosa huruma.​—Soma Yeremia 19:5.

9. Uongo wa Shetani unafanya watu wakuwe na mawazo gani juu ya zabihu ya bei ya ukombozi ya Kristo yenye kuzungumuziwa katika Yohana 3:16 na 15:13?

9 Uongo wa Shetani juu ya watu wenye wamekufa umefanya watu waamini kwamba haiko lazima kuwa na imani katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Kristo. (Mt. 20:28) Uongo mwingine wa Shetani ni kwamba wanadamu wako na nafsi yenye haiwezi kufa. Kama hilo lilikuwa kweli, kila mutu angeishi milele. Yesu hangelazimika kutoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi kwa ajili yetu ili tupate uzima wa milele. Kumbuka kama zabihu ya Kristo njo jambo kubwa zaidi lenye Yehova ametoa ili kuonyesha kama anapenda wanadamu. (Soma Yohana 3:16; 15:13.) Wazia namna Yehova na Mwana wake wanajisikia juu ya mafundisho yenye inafanya zawadi hiyo ya maana sana ionekane kuwa haiko ya lazima!

10. Namna gani uongo wa Shetani juu ya kifo umeongezea wanadamu huzuni na mateso?

10 Uongo wa Shetani unaongezea wanadamu huzuni na mateso. Wazazi wenye kuwa na huzuni kwa sababu mutoto wao amekufa, wanaweza kuambiwa kama Mungu amechukua mutoto wao, pengine ili akuwe malaika kule mbinguni. Uongo huo wa Shetani unapunguza ao unaongeza huzuni yao? Fundisho la uongo la moto wa mateso limetumiwa ili kutetea tendo la kutesa wengine, kutia ndani kuunguza kwenye muti watu wenye walipinga mafundisho ya kanisa. Kitabu kimoja chenye kuzungumuzia Baraza la Kihispania la Kuhukumu Waasi wa Dini kinasema kama, watu fulani kati ya wale wenye walianzisha ile mateso, pengine waliamini kama walikuwa wanaonjesha wale wenye waliasi dini ya Katoliki namna moto wa mateso ungekuwa ili watubu mbele ya kufa na wasiingie mu moto huo wa mateso. Mu inchi za mingi watu wanaona kama wanapaswa kuabudu wazazi wao wa zamani wenye wamekufa ili kuwaonyesha heshima, ao ili kutafuta baraka kutoka kwao. Wengine wanapenda kutuliza wazazi wao wa zamani wenye wamekufa ili kuepuka malipizi fulani. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, kuamini mambo yenye kutegemea uongo wa Shetani hakulete faraja ya kweli. Lakini, kunaleta mahangaiko na hata woga.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUSHIKAMANA NA KWELI YA BIBLIA?

11. Namna gani watu wa jamaa ao marafiki wenye hawana nia ya mubaya wanaweza kujaribu kutukaza tufanye mambo yenye haipatane na Neno la Mungu?

11 Kumupenda Mungu na Neno lake kunatuchochea tumutii hata wakati watu wa jamaa na marafiki wenye hawana nia ya mubaya, wanajaribu kutukaza tujiunge nao ili kufanya desturi zenye hazipatane na maandiko, zenye kuhusu watu wenye wamekufa. Wanaweza kujaribu kutupatisha haya, pengine kwa kusema kama hatukukuwa tunapenda mutu mwenye amekufa, ao kumuheshimia. Ao wanaweza kusema kama namna tunajiendesha inaweza kufanya mutu mwenye amekufa aumize kwa njia fulani wale wenye kuwa wazima. Tunaweza kufanya nini ili kushikamana na kweli ya Biblia? Fikiria namna unaweza kutumia kanuni za Biblia zenye kufuata.

12. Ni desturi gani juu ya watu wenye wamekufa zenye hazipatane kabisa na maandiko?

12 Uazimie ‘kujitenga’ na imani na desturi zenye hazipatane na maandiko. (2 Ko. 6:17) Katika taifa moja la Karibea, watu wengi wanaamini kama kisha mutu kufa, “roho” yake inaweza kubakia mu eneo ili kupatia malipizi wale wenye walimufanyia mambo ya mubaya. Kitabu kimoja kinasema kama, ile “roho” inaweza hata “kuleta muvurugo mu eneo.” Katika Afrika, watu wako na desturi ya kuwasha moto usiku wote kwenye nyumba yenye kuwa na kilio. Juu ya nini? Watu fulani wanasema kama desturi hiyo inasaidia kukimbiza roho wabaya! Sisi watumishi wa Yehova, hatuamini hata kidogo habari zozote za kuwazia ao kufanya desturi zozote zenye kuchochea uongo wa Shetani!​—1 Ko. 10:21, 22.

Kutafuta kwa uangalifu habari zenye kutegemea Biblia, na kuzungumuza muzuri na watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi kunaweza kukusaidia kuepuka matatizo (Picha hizi zinapatana na fungu la 13-14) *

13. Kulingana na Yakobo 1:5, unapaswa kufanya nini kama uko na mashaka juu ya desturi fulani?

13 Kama uko na mashaka juu ya desturi ao mazoea fulani, usali kwa Yehova, na kumuomba akupatie hekima yake. (Soma Yakobo 1:5.) Kisha utafute habari mu vichapo vyetu. Kama ni lazima, uzungumuze na wazee wa kutaniko lenu. Hawatakuambia mambo yenye unapaswa kufanya, lakini wanaweza kukusaidia kupata kanuni za Biblia, kama zile zenye kuzungumuziwa mu habari hii. Wakati unafanya vile, unazoeza ‘nguvu zako za utambuzi,’ na nguvu hizo zitakusaidia “kufanya tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.”​—Ebr. 5:14.

14. Namna gani tunaweza kuepuka kukwaza wengine?

14 “Mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu. Muepuke kuwa vikwazo.” (1 Ko. 10:31, 32) Wakati tunaamua ikiwa tutajiunga na wengine ili kufanya desturi fulani, tunapaswa pia kufikiri ikiwa uamuzi wetu utakuwa na matokeo gani juu ya zamiri za wengine, zaidi sana Wakristo wenzetu. Kwa kweli, hatupendi hata kidogo kukwaza mutu yeyote! (Mk. 9:42) Pia, tunapenda kuepuka kukwaza bila sababu watu wenye hawako Mashahidi. Upendo utatuchochea tuzungumuze nao kwa heshima, na hilo litamutukuza Yehova. Kwa kweli, hatutabishana na watu ao kuchekelea desturi zao. Ukumbuke kama, upendo uko na nguvu sana! Wakati tunaonyesha wengine upendo kwa kuwahangaikia na kuwaonyesha heshima, hilo linaweza kufanya waache kutupinga.

15-16. (a) Juu ya nini ni jambo la hekima kuelezea wengine mambo yenye unaamini? Leta mufano. (b) Namna gani tunaweza kutumia maneno ya Paulo yenye kuwa katika Waroma 1:16?

15 Ujulishe watu wa eneo lako kama uko Shahidi wa Yehova. (Isa. 43:10) Kama mutu fulani wa familia yako anakufa, watu wa jamaa yako na majirani wanaweza kukasirika sana ikiwa haujiunge nao ili kufanya desturi fulani. Kwa hiyo, inaweza kuwa mwepesi zaidi kushugulikia hali hiyo ikiwa unawafasiria mbele ya wakati mambo yenye unaamini. Francisco, mwenye kuishi mu inchi ya Musumbiji (Mozambique), anaandika hivi: “Wakati mimi na bibi yangu Carolina, tulijifunza kweli, tuliambia watu wa familia yetu kama hatutaabudu tena watu wenye wamekufa. Uamuzi wetu ulijaribiwa wakati dada ya Carolina alikufa. Mu eneo letu, inaomba kunawisha maiti kulingana na desturi fulani. Kisha, mutu wa jamaa wa karibu zaidi anapaswa kulala kwa siku tatu mahali kwenye maji yenye ilitumiwa ili kunawisha maiti ilimwangwa. Watu wanaamini kama desturi hizo zinatuliza roho ya mutu mwenye alikufa. Watu wa familia ya Carolina walitazamia kuwa yeye njo atalala mahali kwenye ile maji ilikuwa imemwangwa.”

16 Francisco na bibi yake walifanya nini? Francisco anafasiria hivi: “Kwa sababu tunamupenda Yehova na tunataka kumufurahisha, tulikataa kufanya desturi hiyo. Watu wa familia ya Carolina walikasirika sana. Walisema kama hatuheshimie mutu mwenye alikufa na wakasema kama watu wa familia hawatatutembeleaka tena ao kutusaidia. Kwa sababu tulikuwa tumewafasiria mbele ya wakati mambo yenye tunaamini, hatukuzungumuza nao juu ya jambo hilo wakati walikuwa wenye kukasirika. Hata watu fulani wa jamaa walitutetea, kwa kusema kama tulikuwa tumekwisha kufasiria musimamo wetu. Kisha wakati fulani, watu wa familia ya Carolina walitulia na tuliweza kufanya amani pamoja nao. Kwa kweli, wamoja wamekuja hata kwenye nyumba yetu ili kutuomba vichapo vyenye kutegemea Biblia.” Tusikuwe na haya hata kidogo juu ya musimamo wenye tunakamata ili kutetea kweli juu ya kifo.​—Soma Waroma 1:16.

UFARIJI NA KUTEGEMEZA WATU WENYE WAMEFIWA

Marafiki wa kweli wanafariji na kutegemeza wale wenye wamefiwa na wapendwa wao (Picha hii inapatana na fungu la 17-19) *

17. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe rafiki wa kweli kwa Mukristo mwenzetu mwenye amefiwa?

17 Wakati Mukristo mwenzetu anafiwa na mupendwa wake, tunapaswa kufanya nguvu yetu yote ili tukuwe “rafiki wa kweli . . . , ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.” (Mez. 17:17) Namna gani tunaweza kuwa “rafiki wa kweli,” zaidi sana ikiwa ndugu ao dada mwenye amefiwa anakazwa ili ajiingize katika desturi fulani zenye hazipatane na maandiko? Fikiria kanuni mbili za Biblia zenye zinaweza kutusaidia kufariji mutu mwenye amefiwa.

18. Juu ya nini Yesu alitokwa na machozi, na mufano wake unaweza kutufundisha nini?

18 “Mulie pamoja na wale wenye kulia.” (Ro. 12:15) Tunaweza kuona kama haiko mwepesi kupata maneno ya kuambia mutu fulani mwenye iko na huzuni mingi sana. Wakati fulani machozi yetu inaweza kusema mingi kupita maneno yetu. Wakati Lazaro, rafiki ya Yesu, alikufa, Maria, Marta, na wengine walimulilia ndugu na rafiki yao mupendwa. Kisha siku ine wakati Yesu alifika, naye “akatokwa na machozi,” hata kama alijua kwamba alikuwa karibu kumufufua Lazaro. (Yoh. 11:17, 33-35) Kwa sababu Yesu alilia, hilo lilionyesha namna Yehova alijisikia wakati Lazaro alikufa. Pia, ile machozi ilionyesha kabisa kama Yesu alikuwa anapenda familia hiyo, na bila shaka hilo lilifariji Maria na Marta. Vilevile, wakati ndugu na dada zetu wanaona namna tunawapenda na kuwahangaikia, wanajua kama hawako peke yao lakini wanazungukwa na marafiki wenye wanawahangaikia na kuwategemeza.

19. Wakati tunafariji Mukristo mwenye kuwa na huzuni, namna gani tunaweza kutumia Muhubiri 3:7?

19 “Wakati wa kunyamaza na wakati wa kusema.” (Muh. 3:7) Njia ingine ya kufariji Mukristo mwenzetu mwenye huzuni, ni kuwa tu musikilizaji muzuri. Uache ndugu ao dada yako aeleze namna anajisikia kabisa, na usikwazike kwa sababu ya “mazungumuzo ya ovyoovyo.” (Yob. 6:2, 3) Pengine iko na huzuni zaidi kwa sababu watu wa jamaa wenye hawako Mashahidi wanamukaza afanye jambo fulani. Kwa hiyo, usali pamoja naye. Umuombe “Musikiaji wa sala” amupatie nguvu na uwezo wa kufikiri muzuri. (Zb. 65:2) Kama hali inaruhusu, usome Biblia pamoja naye. Ao usome pamoja naye katika vichapo vyetu habari fulani yenye kupatana na hali yake, kama vile habari juu ya maisha ya watu yenye kutia moyo.

20. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

20 Tuko na pendeleo kubwa kwa sababu tunajua kweli juu ya watu wenye wamekufa na tunajua tumaini la muzuri sana lenye Mungu anatoa kwa ajili ya wale wenye kuwa mu makaburi ya ukumbusho! (Yoh. 5:28, 29) Kwa hiyo, kupitia maneno na matendo yetu, tushikamane kwa uhodari na kweli ya Biblia na tuelezee wengine juu ya kweli hiyo kila wakati wenye kufaa. Mu habari yenye kufuata, tutaona njia ingine yenye Shetani anatumia ili kujaribu kufanya watu wabakie katika giza la kiroho; njia hiyo ni kupashana habari na pepo wachafu. Tutaona juu ya nini tunapaswa kuepuka mazoea na mambo ya kujifurahisha yenye kuwa na upatano na mutego huo wa Shetani.

WIMBO 24 Njooni Kwenye Mlima wa Yehova

^ fu. 5 Shetani na pepo wake wachafu wanadanganya watu juu ya hali ya watu wenye wamekufa. Uongo huo umetokeza desturi za mingi zenye hazipatane na maandiko. Habari hii itakusaidia uendelee kuwa muaminifu kwa Yehova wakati wengine wanajaribu kukukaza ujiunge nao ili kufanya desturi kama hizo.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati mutu wa familia iko na huzuni kwa sababu amefiwa na mupendwa wake, watu wa jamaa yake wenye kuwa Mashahidi wanamufariji.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Kisha kutafuta habari juu ya desturi za maziko, mutu wa familia fulani mwenye kuwa Shahidi anafasiria watu wa jamaa yake mambo yenye anaamini.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Wazee wa kutaniko wanafariji na kutegemeza Shahidi mumoja mwenye amefiwa na mupendwa wake.