Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sababu Gani ‘Tunaendelea Kuzaa Matunda Mengi’?

Sababu Gani ‘Tunaendelea Kuzaa Matunda Mengi’?

‘Baba yangu anatukuzwa katika hili, kwamba muendelee kuzaa matunda mengi na kujionyesha kuwa wanafunzi wangu.’​—YOH. 15:8.

NYIMBO: 53, 60

1, 2. (a) Yesu alizungumuzia nini pamoja na wanafunzi wake usiku wa mwisho mbele ya kifo chake? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Juu ya nini ni jambo la lazima tukumbuke sababu gani tunahubiri? (c) Tutazungumuzia nini?

USIKU wa mwisho mbele ya kifo chake, Yesu alizungumuza sana na mitume wake. Aliwahakikishia kama aliwapenda sana. Pia aliwaelezea mufano wa muzabibu, wenye tulizungumuzia katika habari yenye ilitangulia. Yesu alipenda kutia moyo wanafunzi wake ‘waendelee kuzaa matunda mengi,’ ni kusema, waendelee kufanya kazi ya kuhubiri ujumbe juu ya Ufalme.​—Yoh. 15:8.

2 Yesu hakuambia tu wanafunzi wake mambo yenye walipaswa kufanya, lakini aliwaambia pia sababu gani walipaswa kufanya mambo hayo. Aliwaambia sababu gani wanapaswa kuendelea kuhubiri. Ni jambo la lazima sisi pia tukumbuke sababu gani tunapaswa kuendelea kuhubiri. Kufikiria jambo hilo kutatuchochea tuendelee kutoa “ushahidi kwa mataifa yote.” (Mt. 24:13, 14) Katika habari hii, tutazungumuzia sababu ine zenye Maandiko yanatoa zenye kutuchochea kuhubiri. Pia, tutazungumuzia zawadi ine kutoka kwa Yehova zenye kutusaidia tuendelee kuzaa matunda.

TUNAMUTUKUZA YEHOVA

3. (a) Kulingana na Yohana 15:8, ni sababu gani ya maana zaidi yenye kutuchochea kuhubiri? (b) Zabibu zenye kuzungumuziwa katika mufano wa Yesu zinafananisha nini, na sababu gani ulinganifu huo unafaa?

3 Sababu ya maana zaidi yenye kutuchochea kuhubiri ni hii: tunapenda kumutukuza Yehova na kutakasa jina lake. (Soma Yohana 15:1, 8.) Wakati alieleza mufano wa muzabibu, Yesu alilinganisha Yehova na mulimaji, mwenye kukomalisha zabibu. Yesu alisema kama yeye mwenyewe alikuwa muzabibu na wanafunzi wake walikuwa matawi. (Yoh. 15:5) Kwa hiyo, katika mufano huo, zabibu zinafananisha matunda yenye wanafunzi wa Yesu wanazaa, ao kazi ya kuhubiri yenye wanafanya. Yesu aliambia mitume wake hivi: ‘Baba yangu anatukuzwa katika hili, kwamba muendelee kuzaa matunda mengi.’ Wakati mizabibu inazaa zabibu za muzuri, hilo linatukuza mulimaji. Vilevile, wakati tunajikaza sana ili kuhubiri habari njema juu ya Ufalme, tunamuletea Yehova heshima ao utukufu.​—Mt. 25:20-23.

4. (a) Namna gani tunatakasa jina la Mungu? (b) Unajisikia namna gani juu ya pendeleo lenye uko nalo la kutakasa jina la Mungu?

4 Tayari jina la Mungu ni takatifu. Hakuna jambo lenye tunaweza kufanya ili kufanya jina hilo likuwe takatifu zaidi. Sasa, namna gani tunatakasa jina la Mungu wakati tunahubiri? Ona mambo yenye nabii Isaya alisema: ‘Yehova wa majeshi​—yeye Ndiye munayepaswa kuona kuwa mutakatifu.’ (Isa. 8:13) Tunatakasa jina la Mungu, Yehova, wakati tunaliona kuwa jina kubwa zaidi kuliko majina mengine yote na wakati tunasaidia wengine waelewe kama jina hilo ni takatifu. (Mt. 6:9) Kwa mufano, wakati tunafundisha watu kweli juu ya sifa za ajabu za Yehova na kusudi lake kwa wanadamu la kutaka waishi milele katika Paradiso, tunawasaidia waelewe kama mambo yote yenye Shetani amesema juu ya Yehova ni ya uongo. (Mwa. 3:1-5) Pia tunatakasa jina la Mungu wakati tunasaidia watu wajue kama Yehova anastahili “kupokea utukufu na heshima na nguvu.” (Ufu. 4:11) Ndugu Rune, mwenye amekuwa painia kwa miaka 16, anasema hivi: “Kujua kama nimepewa nafasi ya kutoa ushahidi juu ya Muumbaji wa ulimwengu wote muzima, kunanifanya nikuwe mwenye shukrani. Hilo linanipatia tamaa ya kuendelea kufanya kazi ya kuhubiri.”

TUNAMUPENDA YEHOVA NA MWANA WAKE

5. (a) Ni sababu gani yenye kutuchochea kuhubiri yenye kupatikana katika Yohana 15:9, 10? (b) Namna gani Yesu alisaidia wanafunzi wake waelewe kama walipaswa kuonyesha uvumilivu?

5 Soma Yohana 15:9, 10. Sababu ya pili yenye kutuchochea kuhubiri juu ya Ufalme ni hii: tunamupenda Yehova na Yesu. (Mk. 12:30; Yoh. 14:15) Yesu aliambia wanafunzi wake kama wanapaswa kukaa katika upendo wake.’ Sababu gani Yesu alisema vile? Kwa sababu alijua kama wanafunzi wake walipaswa kuvumilia ili waendelee kuishi kama Wakristo wa kweli. Kwa kweli, katika andiko la Yohana 15:4-10, tunaona kama Yesu alitumia mara nyingi neno ‘kukaa’ ili kusaidia wanafunzi wake waelewe kama walipaswa kuonyesha uvumilivu.

6. Namna gani tunaonyesha kama tunapenda kukaa katika upendo wa Kristo?

6 Namna gani tunaonyesha kama tunapenda kukaa katika upendo wa Kristo na kukubaliwa naye? Ni kwa kumutii. Yesu anatuomba tu tufanye jambo lenye yeye mwenyewe alifanya. Alisema hivi: ‘Mimi nilishika amri za Baba na kukaa katika upendo wake.’ Yesu alituachia mufano wa kuiga.​—Yoh. 13:15.

7. Namna gani kutii kunapatana na upendo?

7 Yesu alionyesha waziwazi kama kutii kunapatana na upendo wakati alisema hivi: ‘Yule aliye na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye ambaye ananipenda.’ (Yoh. 14:21) Amri za Yesu zinatoka kwa Baba yake, kwa hiyo wakati tunatii amri ya Yesu ya kuhubiri, tunaonyesha pia kama tunamupenda Yehova. (Mt. 17:5; Yoh. 8:28) Na wakati tunaonyesha Yehova na Yesu kama tunawapenda, wanatusaidia tubakie katika upendo wao.

TUNAONYA WATU

8, 9. (a) Ni sababu gani ingine yenye kutuchochea kuhubiri? (b) Namna gani maneno ya Yehova yenye kupatikana kwenye Ezekieli 3:18, 19 na 18:23 yanatuchochea kuendelea kuhubiri?

8 Sababu ya tatu yenye kutuchochea kuhubiri ni hii: tunapenda kuonya watu juu ya siku ya Yehova yenye kuja. Biblia inaonyesha kama Noa alikuwa ‘muhubiri.’ (Soma 2 Petro 2:5.) Mbele Garika ifike, pengine ujumbe wenye Noa alikuwa anahubiri ulikuwa na onyo juu ya uharibifu wenye ulikuwa unakuja. Sababu gani tunasema hivyo? Kwa sababu Yesu alisema hivi: ‘Kwa maana kama vile walivyokuwa katika siku hizo kabla [ao, mbele] ya garika, wakila na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiolewa, mupaka siku ambayo Noa aliingia ndani ya safina; nao hawakujali [ao, hawakuhangaika] mupaka garika ikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.’ (Mt. 24:38, 39) Hata kama watu wengi hawakumusikiliza, Noa alihubiri kwa uaminifu ujumbe wa kuonya wenye Yehova alikuwa amemupatia.

9 Leo, tunahubiri ujumbe juu ya Ufalme ili kutolea watu nafasi ya kujifunza juu ya mambo yenye Mungu atafanyia wanadamu wakati wenye kuja. Kama Yehova, tunapenda kabisa watu wasikilize ujumbe huo ili ‘waendelee kuishi.’ (Eze. 18:23) Wakati tunahubiri nyumba kwa nyumba na mahali pa watu wengi, tunaonya watu wengi kwamba Ufalme wa Mungu utakuja na kuharibu ulimwengu huu muovu.​—Eze. 3:18, 19; Dan. 2:44; Ufu. 14:6, 7.

TUNAPENDA WATU

10. (a) Ni sababu gani yenye kutuchochea kuhubiri yenye kupatikana katika Mathayo 22:39? (b) Namna gani Paulo na Sila walisaidia mulinzi wa gereza katika Filipi?

10 Sababu ya ine yenye kutuchochea tuendelee kuhubiri ni hii: tunapenda watu. (Mt. 22:39) Upendo huo unatusaidia tuendelee kuhubiri kwa sababu tunajua kama watu wanaweza kubadilisha mawazo yao wakati hali zao zinabadilika. Kwa mufano, wapinzani walitupa Paulo na Sila katika gereza katika muji wa Filipi. Lakini katikati ya usiku, kulitokea tetemeko la inchi lenye lilitikisa gereza na kufungua milango yake. Mulinzi wa gereza aliogopa sana kwamba wafungwa wamekimbia na kwa hiyo alitaka kujiua. Lakini Paulo alimukataza kwa kumuambia hivi kwa sauti kubwa: “Usijiumize!” Mulinzi huyo wa gereza aliuliza hivi: “Nifanye nini ili niokolewe?” Paulo na Sila wakamuambia hivi: “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokolewa.”​—Mdo. 16:25-34.

Tunahubiri kwa sababu tunamupenda Yehova, Yesu, na watu (Picha hii inapatana na fungu la 5, 10)

11, 12. (a) Habari juu ya mulinzi wa gereza inatufundisha nini juu ya kazi yetu ya kuhubiri? (b) Sababu gani tunapenda kuendelea kuhubiri?

11 Habari hiyo juu ya mulinzi wa gereza inatufundisha nini juu ya kazi yetu ya kuhubiri? Tunaona kama ni kisha tu tetemeko la inchi kutokea ndiyo wakati mulinzi wa gereza alibadilisha mawazo yake na kuomba musaada. Vilevile, watu fulani wenye hawapendi kusikiliza ujumbe wa Biblia wanaweza kubadilisha mawazo yao na kutafuta musaada wakati jambo fulani la kuhuzunisha linatokea katika maisha yao. Kwa mufano, wamoja wanaweza kuwa na huzuni kwa sababu wamepoteza kazi ao kwa sababu ndoa yao imevunjika. Wengine wanaweza kuhuzunika sana kwa sababu wamejulishwa kama wako na ugonjwa hatari ao kwa sababu mupendwa wao amekufa. Wakati mambo kama hayo yanatokea, watu wanaweza kuanza kuuliza maulizo juu ya maisha, maulizo yenye hawakukuwa wanafikiria hapo zamani. Wanaweza hata kujiuliza hivi, ‘Ninapaswa kufanya nini ili niokolewe?’ Kwa mara ya kwanza katika maisha yao, wanaweza kupenda kusikiliza ujumbe wetu wenye kutoa tumaini.

12 Kwa hiyo, ikiwa tunaendelea kuhubiri kwa uaminifu, tutapatikana wakati watu wako tayari kukubali faraja yenye tunawatolea. (Isa. 61:1) Charlotte, mwenye amekuwa painia kwa miaka 38, anasema hivi: “Leo watu wamepotea. Wako na lazima ya kupata nafasi ya kusikiliza habari njema.” Ejvor, mwenye amekuwa painia kwa miaka 34, anasema hivi: “Kuliko wakati mwingine wowote, leo watu wengi zaidi wameshuka moyo. Ninapenda kabisa kuwasaidia. Hilo linanichochea kuhubiri.” Ni wazi kama, kupenda watu ni sababu ya muzuri sana ya kutuchochea kuendelea kuhubiri!

ZAWADI ZENYE KUTUSAIDIA TUENDELEE KUHUBIRI

13, 14. (a) Ni zawadi gani yenye kuzungumuziwa katika Yohana 15:11? (b) Namna gani tunaweza kupata shangwe yenye Yesu iko nayo? (c) Namna gani furaha inatusaidia katika kazi ya kuhubiri?

13 Usiku wa mwisho mbele ya kifo chake, Yesu alizungumuzia pia zawadi zenye zingesaidia mitume wake waendelee kuzaa matunda. Ni zawadi gani hizo, na namna gani zinaweza kutusaidia leo?

14 Zawadi ya shangwe. Kazi ya kuhubiri ni muzigo kwetu? Hapana kabisa. Kisha kueleza mufano wake juu ya muzabibu, Yesu alisema kama wakati tunahubiri tutapata shangwe ao furaha yake. (Soma Yohana 15:11.) Hilo linawezekana namna gani? Kumbuka, katika mufano wake, Yesu alijilinganisha na muzabibu na alilinganisha wanafunzi wake na matawi. Ili matawi yapate maji na mambo mengine yenye kujenga yenye yanahitaji, yanapaswa kuendelea kubana kwenye muzabibu. Vilevile, tunaweza kuwa na furaha kama Yesu ikiwa tu tunabakia katika muungano pamoja naye na kufuata mufano wake kwa uaminifu. Kisha tutakuwa na furaha yenye alikuwa nayo, furaha yenye mutu anapata wakati anafanya mapenzi ya Mungu. (Yoh. 4:34; 17:13; 1 Pet. 2:21) Hanne, mwenye amekuwa painia kwa zaidi ya miaka 40, anasema hivi: “Furaha yenye ninakuwa nayo siku zote kisha kutoka katika kazi ya kuhubiri inanichochea kuendelea kumutumikia Yehova.” Furaha itatupatia nguvu ya kuendelea kuhubiri hata kama watu wengi hawatusikilize.​—Mt. 5:10-12.

15. (a) Ni zawadi gani yenye kuzungumuziwa katika Yohana 14:27? (b) Namna gani amani inatusaidia kuendelea kuzaa matunda?

15 Zawadi ya amani. (Soma Yohana 14:27.) Wakati fulani mangaribi mbele ya kifo chake, Yesu aliambia mitume hivi: “Ninawapa amani yangu.” Namna gani amani ya Yesu inaweza kutusaidia tuendelee kuhubiri? Wakati tunaendelea kuhubiri, tunakuwa na amani kwa sababu tunajua kama tunafurahisha Yehova na Yesu. (Zab. 149:4; Rom. 5:3, 4; Kol. 3:15) Ulf, mwenye amekuwa painia kwa miaka 45, anasema hivi: “Kazi ya kuhubiri inanichokesha, lakini inaniletea furaha ya kweli na kusudi la kweli katika maisha yangu.” Tuko wenye shukrani kwa sababu tumepata amani yenye kuendelea!

16. (a) Ni zawadi gani yenye kuzungumuziwa katika Yohana 15:15? (b) Namna gani mitume wa Yesu wangeendelea kuwa marafiki wake?

16 Zawadi ya urafiki. Kisha Yesu kuambia mitume wake kama anapenda wakuwe na shangwe, aliwaelezea sababu gani ni jambo la maana waonyeshe upendo wenye hauna uchoyo. (Yoh. 15:11-13) Kisha akasema hivi: “Nimewaita ninyi rafiki.” Ni zawadi ya ajabu kabisa kuwa rafiki ya Yesu! Lakini, namna gani mitume wangeendelea kuwa marafiki wake? Yesu alieleza hivi: Musonge mbele na kuendelea kuzaa matunda.’ (Soma Yohana 15:14-16.) Ni kusema, muendelee kuhubiri. Miaka mbili hivi mbele ya hapo, Yesu aliambia mitume wake hivi: Munapoenda, muhubiri, mukisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’” (Mt. 10:7) Ndiyo sababu usiku mbele ya kifo chake, Yesu alitia moyo wanafunzi wake waendelee kufanya kazi ya kuhubiri. (Mt. 24:13; Mk. 3:14) Kwa kweli, Yesu alijua kama haingekuwa mwepesi kutimiza amri yake. Lakini wangeweza kufanya kazi hiyo na kuendelea kuwa marafiki wake. Namna gani? Kwa musaada wa zawadi ingine.

17, 18. (a) Ni zawadi gani yenye kuzungumuziwa katika Yohana 15:7? (b) Namna gani zawadi hiyo ilisaidia wanafunzi wa Yesu? (c) Ni zawadi gani zenye kutusaidia leo?

17 Zawadi ya majibu kwa sala zetu. Yesu alisema hivi: ‘Muombe lolote munalotaka nalo litatukia kwenu.’ (Yoh. 15:7, 16) Ahadi hiyo ya Yesu ilipaswa kutia mitume nguvu kabisa! * (Ona maelezo ya chini.) Mitume hawakuelewa muzuri kama Yesu alikuwa karibu kufa. Lakini hilo halikumaanisha kama wangebakia bila musaada kisha kifo cha Yesu. Yehova alikuwa tayari kujibia sala zao na kuwasaidia katika kazi yao ya kuhubiri. Na alifanya hivyo. Muda mufupi kisha kifo cha Yesu, mitume walimuomba Yehova awapatie ujasiri, na Yehova alijibia sala zao.​—Mdo. 4:29, 31.

Tunaweza kuwa hakika kama Yehova atajibia sala zetu za kumuomba musaada (Picha hii inapatana na fungu la 18)

18 Mambo yako hivyo pia leo. Wakati tunaendelea kufanya kazi ya kuhubiri, tunaendelea kuwa marafiki wa Yesu. Na tunaweza kuwa hakika kama Yehova iko tayari kujibia sala zetu za kuomba musaada wakati tunaona kama ni vigumu kufanya kazi ya kuhubiri. (Flp. 4:13) Tuko wenye shukrani sana kwa sababu Yehova anajibia sala zetu na kwa sababu Yesu ni rafiki yetu. Zawadi hizo kutoka kwa Yehova zinatutia nguvu ili tuendelee kuzaa matunda.​—Yak. 1:17.

19. (a) Sababu gani tunaendelea kuhubiri? (b) Ni nini inatusaidia tumalize kazi yenye Mungu ametupatia?

19 Katika habari hii, tumejifunza sababu ine zenye kutuchochea kuendelea kuhubiri: (1) ili kumutukuza Yehova na kutakasa jina lake, (2) ili kuonyesha kama tunamupenda Yehova na Yesu, (3) ili kuonya watu, na (4) ili kuonyesha kama tunapenda watu. Tumejifunza pia juu ya zawadi ine: shangwe, amani, urafiki, na majibu kwa sala zetu. Zawadi hizo zinatutia nguvu ili tumalize kazi yenye Mungu ametupatia. Yehova anafurahi sana wakati anaona tunajikaza sana ili ‘kuendelea kuzaa matunda mengi’!

^ fu. 17 Wakati alikuwa anazungumuza na mitume wake, Yesu aliwakumbusha mara nyingi kama Yehova angejibia sala zao.​—Yoh. 14:13; 15:7, 16; 16:23.