Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 22

Fanya Namna Yako ya Kujifunza Ikuwe Muzuri Zaidi!

Fanya Namna Yako ya Kujifunza Ikuwe Muzuri Zaidi!

“Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”​—FLP. 1:10.

WIMBO 35 “Mhakikishe Mambo Muhimu Zaidi”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini ndugu na dada fulani wanashindwa kujifunza?

LEO, inaomba kujikaza sana ili kupata feza za kutusaidia kutimiza mahitaji yetu. Wengi kati ya ndugu zetu wanatumika saa mingi ili kutimizia familia zao mambo ya lazima mu maisha. Wengine wengi wanapitisha saa mingi kila siku ya kazi katika njia ya kuenda ku kazi na kurudia ku nyumba. Wengine wanafanya kazi yenye kuwaomba watumie nguvu mingi ya kimwili ili watimize mahitaji yao. Ku mwisho wa siku, ndugu na dada hao wenye kutumika kwa bidii wanachoka sana! Kwa hiyo, wengi wanajisikia kuwa hawana tena nguvu ya kujifunza.

2. Ni wakati gani unapataka wakati wa kujifunza?

2 Lakini kwa kweli, tunapaswa kutafuta wakati wa kujifunza, kujifunza kabisa Neno la Mungu na vichapo vyetu vya Kikristo. Hilo ni jambo la lazima sana kama tunapenda tukuwe na urafiki muzuri pamoja na Yehova na kupata uzima wa milele. (1 Ti. 4:15) Ndugu na dada fulani wanaamuka asubui kila siku na kujifunza wakati hakuna fujo mu nyumba na wakati akili yao inatulia kisha kupumuzika usiku. Wengine wanatumia dakika kidogo mangaribi wakati hakuna mambo ya kuwakengeusha ili kujifunza mambo ya kiroho na kufikiri sana juu ya mambo yenye wanajifunza.

3-4. Ni mabadiliko gani imefanywa juu ya wingi wa habari zenye kutolewa, na juu ya nini?

3 Pengine unakubali kama ni jambo la maana kupata wakati wa kujifunza. Lakini, tunapaswa kujifunza nini? Unaweza kusema hivi: ‘Kuko habari za mingi za kusoma. Ninashindwa kusoma kila habari.’ Ndugu na dada fulani wako na uwezo wa kusoma vichapo vyote na kuangalia video zote zenye kutegemea Biblia zenye kutolewa, lakini wengine wengi wanashindwa kupata wakati wa kufanya vile. Baraza Lenye Kuongoza linajua jambo hilo. Njo maana, hivi karibuni maagizo ilitolewa ili kupunguza habari zenye kuchapishwa na zenye kutolewa ku Enternete.

4 Kwa mufano, hatuchapishe tena Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova, kwa sababu habari za mingi zenye kutia moyo zinapatikana ku jw.org® na kwenye programu za kila mwezi za JW Télédiffusion. Munara wa Mulinzi gazeti la watu wote na gazeti Amuka! vinachapishwa sasa mara tatu kwa mwaka. Ile mabadiliko haikufanywa ili tupate wakati zaidi wa kufanya mambo yetu ya kimwili. Imefanywa ili kutusaidia kukazia uangalifu “mambo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Tuzungumuzie basi namna unaweza kuchagua mambo ya maana zaidi ya kujifunza na namna funzo lako la pekee la Biblia linaweza kukuletea faida kabisa.

CHAGUA MAMBO YENYE UNAPASWA KUJIFUNZA KWANZA

5-6. Ni vichapo gani vyenye tunapaswa kujifunza kwa uangalifu?

5 Ni mambo gani yenye tunapaswa kujifunza kwanza? Kwa kweli, tunapaswa kutumia wakati kila siku ili kujifunza Neno la Mungu. Sura zenye kupangwa sasa kwenye programu ya usomaji wa Biblia wa kutaniko wa kila juma zimepunguzwa ili tupate wakati zaidi wa kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma na kutafuta habari zaidi. Muradi wetu haupaswe kuwa kusoma tu sura zenye zimepangwa kwenye programu, lakini ni kuruhusu ujumbe wa Biblia uguse moyo wetu na kutufanya tumukaribie Yehova zaidi.​—Zb. 19:14.

6 Ni nini ingine tunapaswa kujifunza kwa uangalifu? Kwa kweli, tunapenda kutayarisha habari ya Funzo la Munara wa Mulinzi na Funzo la Biblia la Kutaniko na habari zingine za kujifunza kwenye mukutano wa katikati ya juma. Tunapaswa pia kusoma kila gazeti Munara wa Mulinzi na Amuka!

7. Tunapaswa kuvunjika moyo ikiwa hatuwezi kusoma ao kuangalia mambo yote yenye kutolewa ku site yetu ya Enternete na ku JW Télédiffusion?

Pengine unaweza kusema hivi: ‘Sawa, halafu mambo yote yenye kutolewa ku site yetu jw.org, na mambo yenye kutolewa ku JW Télédiffusion? Kuko mambo mingi sana!’ Fikiria mufano huu: Vyakula mbalimbali vitamu vinawekwa ku meza mu restora fulani. Watu wenye kuuza chakula mu restora hiyo hawawezi kuonja vyakula vyote vyenye kuwa kwenye meza hiyo. Kwa hiyo, wanachagua kula vyakula fulani. Vilevile, kama hauna uwezo wa kusoma ao kuangalia mambo yote yenye kutolewa kwenye site yetu ya Enternete na ku JW Télédiffusion, usivunjike moyo. Soma ao uangalie mambo yenye unaweza. Tuzungumuzie basi kujifunza maana yake nini na mambo yenye unaweza kufanya ili funzo lako likuletee faida zaidi.

INAOMBA KUJIKAZA ILI KUJIFUNZA!

8. Tunaweza kufanya mambo gani wakati tunatayarisha Munara wa Mulinzi, na kufanya vile kutakuletea faida gani?

8 Kujifunza ni kusoma na kukaza uangalifu juu ya mambo yenye mutu anasoma ili kujua jambo fulani la maana. Haiko kusoma tu mbiombio habari fulani na kutia mistari kwenye majibu. Kwa mufano, wakati unatayarisha Funzo la Munara wa Mulinzi, unapaswa kwanza kusoma kifupi cha habari ku mwanzo wa kila habari. Kisha, ufikiri juu ya kichwa cha habari, pia vichwa vidogo-vidogo na maulizo ya kujikumbusha. Na kisha, usome habari yote polepole na kwa uangalifu. Ukaze uangalifu juu ya musemwa wenye kuonyesha mambo yenye fungu linazungumuzia, kwa kawaida ni musemwa wa kwanza wa kila fungu. Mara mingi, musemwa wa kwanza utakusaidia kujua wazo lenye kuzungumuziwa katika fungu lote. Wakati unaendelea kusoma habari, fikiria namna kila fungu linaunga mukono kichwa kidogo cha habari na wazo kubwa la habari yote. Andika maneno yote yenye haujue maana yake na mambo fulani yenye ungependa kuelewa muzuri kwa kutafuta habari zaidi.

9. (a) Juu ya nini tunapaswa kukazia uangalifu zaidi maandiko wakati tunajifunza Munara wa Mulinzi, na namna gani tunaweza kufanya vile? (b) Kama vile andiko la Yoshua 1:8 linaonyesha, tunapaswa kufanya nini ingine zaidi ya kusoma tu maandiko?

9 Funzo la Munara wa Mulinzi ni funzo la Biblia. Kwa hiyo, kazia uangalifu maandiko, zaidi sana ile yenye itasomwa wakati kutaniko litajifunza ile habari. Ukazie uangalifu namna maneno ao misemwa yenye kuonyesha wazo kubwa katika maandiko inaunga mukono jambo lenye kuzungumuziwa katika fungu. Zaidi ya hilo, utumie wakati ili kufikiri sana juu ya maandiko yenye unasoma, na ufikiri juu ya namna unaweza kuitumia mu maisha yako.​—Soma Yoshua 1:8.

Wazazi, mufundishe watoto wenu namna ya kujifunza (Picha hii inapatana na fungu la 10) *

10. Kulingana na Waebrania 5:14, juu ya nini wazazi wanapaswa kutumia muda fulani wakati wa ibada ya familia ili kufundisha watoto wao namna ya kujifunza na kutafuta habari?

10 Kwa kweli, wazazi wanapenda watoto wao wafurahie Ibada ya Familia ya kila juma. Lakini, hata kama sikuzote wazazi wanapaswa kupanga jambo fulani lenye watafanya wakati wa ibada ya familia, haiko lazima waone kuwa kila juma wanapaswa kupanga mambo fulani ya pekee ao miradi fulani yenye kufurahisha. Hata kama wakati wa Ibada ya Familia unaweza kutumiwa ili kuangalia programu ya kila mwezi ya JW Télédiffusion, ao ili kufanya jambo fulani la pekee wakati fulani, kama vile kutengeneza safina ya Noa, ni jambo la maana pia kufundisha watoto namna ya kujifunza. Kwa mufano, wako na lazima ya kujifunza namna ya kutayarisha mikutano ya kutaniko, ao namna ya kutafuta habari juu ya tatizo fulani lenye lilitokezwa ku masomo. (Soma Waebrania 5:14.) Kama wanatumia wakati fulani ili kujifunza habari fulani ya Biblia ku nyumba, itakuwa mwepesi zaidi kwao kukaza akili juu ya habari zenye kuzungumuziwa ku mikutano ya kutaniko, na mikusanyiko, zenye wakati fulani hazina sehemu ya video. Kwa kweli, wakati wa kutumia ili kujifunza utategemea miaka na hali ya watoto.

11. Juu ya nini ni jambo la maana tufundishe wanafunzi wetu wa Biblia namna ya kujifunza kwa uangalifu wao wenyewe?

11 Wanafunzi wetu wa Biblia wako pia na lazima ya kujua namna ya kujifunza. Wakati wanaanza kujifunza Biblia, tunafurahi ikiwa wanatia kistari kwenye majibu ili kutayarisha funzo lao la Biblia ao mikutano ya kutaniko. Lakini, tunapaswa kufundisha wanafunzi wetu wa Biblia namna ya kutafuta habari na namna ya kujifunza kwa uangalifu wao wenyewe. Kama tunafanya vile, wakati watapata magumu, watajua wao wenyewe namna ya kupata mashauri yenye kufaa kwa kutafuta habari katika vichapo vyetu, hawataomba mara moja wengine katika kutaniko musaada.

UKUWE NA MURADI FULANI WAKATI UNAJIFUNZA

12. Tunaweza kuwa na miradi gani wakati tunajifunza?

12 Kama haupendake kujifunza, unaweza kuwaza kama hakuna siku utafurahiaka kujifunza. Lakini unaweza kufurahia kujifunza. Uanze kwa kutumia wakati mufupi ili kujifunza, na pole kwa pole uongeze wakati wenye unatumia ili kujifunza. Fikiria muradi wako wakati unajifunza. Kwa kweli, muradi wetu wa maana zaidi ni kumukaribia Yehova zaidi. Muradi wenye tunaweza kufikia bila kukawia unaweza kuwa kujibu ulizo lenye mutu fulani aliuliza ao kutafuta habari juu ya tatizo fulani lenye tuko nalo.

13. (a) Kijana anaweza kufanya mambo gani ili aweze kutetea imani yake ku masomo? Fasiria. (b) Namna gani unaweza kutumia shauri lenye kuwa mu Wakolosai 4:6?

13 Kwa mufano, uko mwanafunzi kijana? Pengine wanafunzi wenzako wote wanaamini fundisho la mageuzi. Unapenda kutetea kweli ya Biblia, lakini pengine unajisikia kuwa hauna uwezo wa kufanya vile. Kwa hiyo, unapaswa kujifunza juu ya jambo hilo! Unaweza kuwa na kusudi mbili: (1) kuwa hakika zaidi kama Mungu aliumba vitu vyote na (2) kukomalisha ufundi wako wa kutetea kweli. (Ro. 1:20; 1 Pe. 3:15) Unaweza kwanza kujiuliza hivi: ‘Wanafunzi wenzangu wametumia mawazo gani ili kutetea fundisho la mageuzi?’ Kisha, utafute habari kwa uangalifu katika vichapo vyetu. Kutetea mambo yenye unaamini haitakuwa nguvu kama vile unawazia. Watu wengi wanaamini mageuzi juu tu mutu fulani mwenye wanaheshimia aliwaambia kuwa fundisho hilo ni la kweli. Kama unapata tu wazo moja ao mawazo mbili ya kuzungumuzia, unaweza kusaidia mutu fulani mwenye anapenda kabisa kujua kweli.​—Soma Wakolosai 4:6.

KOMALISHA TAMAA YAKO YA KUJIFUNZA

14-16. (a) Unaweza kufanya nini ili uelewe muzuri kitabu fulani cha Biblia chenye haujue muzuri? (b) Kwa kutumia maandiko yenye kutajwa, fasiria namna unaweza kuelewa muzuri kitabu cha Amosi. (Ona pia kisanduku “ Fanya Habari za Biblia Zionekane Kuwa za Kweli Kwako!”)

14 Wazia jambo hili: kwenye programu ya mukutano wa kutaniko wenye kuja tunaombwa kuchunguza kitabu kimoja kati ya vitabu vyenye vinaitwa manabii wadogo, pengine nabii mwenye haujue muzuri. Pengine jambo lenye unapaswa kwanza kufanya ni kukomalisha tamaa ya kujua mengi zaidi juu ya mambo yenye ule nabii aliandika. Namna gani unaweza kufanya vile?

15 Kwanza, ujiulize hivi: ‘Ninajua mambo gani juu ya muandikaji wa kitabu hicho? Alikuwa nani, aliishi wapi, alikuwa anafanya kazi gani?’ Kujua mambo fulani juu ya muandikaji kunaweza kutusaidia kuelewa juu ya nini alitumia maneno fulani ao mifano fulani. Wakati unasoma Biblia, tafuta misemwa yenye kuonyesha utu wa muandikaji.

16 Kisha, utaona kuwa ni muzuri kujua kitabu hicho kiliandikwa wakati gani. Unaweza kufanya vile kwa vyepesi kwa kuangalia muchoro “Oroza ya Vitabu vya Biblia” kwenye kurasa za mwisho za Biblia​Tafsiri ya Ulimwengu Mupya. Tena, unaweza kuangalia muchoro wenye kuonyesha manabii na wafalme mu Nyongeza A6. Kama kitabu cha Biblia chenye uko unajifunza ni kitabu cha unabii, itakuwa muzuri utafute kujua hali zilikuwa namna gani wakati kitabu hicho kiliandikwa. Nabii alipenda kusaidia watu waache tabia ao mazoea gani? Ni nani waliishi katika kipindi kimoja naye? Ili kuelewa hali muzuri, inaweza kuwa jambo la lazima kuchunguza vitabu vingine vya Biblia. Kwa mufano, ili kuelewa zaidi mambo yenye ilikuwa inatendeka wakati wa nabii Amosi, utapata habari zaidi kama unasoma mistari fulani katika kitabu cha 2 Wafalme na 2 Mambo ya Nyakati, vyenye kuonyeshwa mu referanse za katikati za Amosi 1:1. Tena, unaweza kusoma kitabu cha Hosea, mwenye inawezekana aliishi katika kipindi kimoja na Amosi. Vitabu hivyo vyote vitakusaidia kuelewa muzuri maisha ilikuwa namna gani wakati wa Amosi.​—2 Fa. 14:25-28; 2 Ny. 26:1-15; Ho. 1:1-11; Amo. 1:1.

KAZIA UANGALIFU MAMBO YA KIDOGO-KIDOGO

17-18. Kwa kutumia mifano yenye kuwa katika mafungu ao mufano wako mwenyewe, onyesha namna kukazia uangalifu mambo yenye kuonekana kuwa ya kidogo-kidogo kunaweza kukufanya ufurahie funzo la Biblia.

17 Wakati unasoma Biblia, ni muzuri ukuwe na tamaa ya kujua mambo mingi zaidi. Kwa mufano, wazia unasoma sura ya 12 ya unabii wa Zekaria, yenye inatabiri kifo cha Masiya. (Zek. 12:10) Wakati unafika ku mustari wa 12, unasoma kama “familia ya nyumba ya Natani” ingelia na kuhuzunika sana juu ya kifo cha Masiya. Kuliko kupita haraka bila kukazia uangalifu jambo hilo la kidogo, uache kwanza kusoma na ujiulize hivi: ‘Kuko upatano gani kati ya nyumba ya Natani na Masiya? Kuko njia fulani ya kunisaidia kupata habari zaidi?’ Tafuta habari zaidi. Referanse ya katikati inakutuma ku andiko la 2 Samweli 5:13, 14, lenye kusema kama Natani alikuwa kati ya wana wa Mufalme Daudi. Referanse ya pili ya katikati inakutuma ku andiko la Luka 3:23, 31, lenye kuonyesha kama Yesu alikuwa muzao wa moja kwa moja wa Natani kupitia Maria. (Ona Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 8, 2017, uku. 32 fu. 4.) Bila kukawia, unafurahia ile habari! Ulijua kama Biblia ilitabiri kuwa Yesu angetokea katika familia ya Daudi. (Mt. 22:42) Lakini Daudi alikuwa na wana zaidi ya 20. Hauone kama ni jambo la kushangaza kabisa kuona kama Zekaria alionyesha kama nyumba ya Natani ingekuwa na sababu ya kuhuzunika juu ya kifo cha Yesu?

18 Fikiria mufano mwingine. Katika sura ya kwanza ya kitabu cha Luka, tunasoma kama malaika Gabrieli alimutembelea Maria na akamuambia hivi juu ya mutoto mwenye angezaa: “Huyo atakuwa mukubwa na ataitwa Mwana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi; na Yehova Mungu atamupatia kiti cha ufalme cha Daudi baba yake, na atatawala akiwa Mufalme juu ya nyumba ya Yakobo milele.” (Lu. 1:32, 33) Tunaweza kuwa na muelekeo wa kukazia uangalifu sehemu ya kwanza ya ujumbe wa Gabrieli, yenye kusema kama Yesu angeitwa “Mwana wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi.” Lakini Gabrieli alitabiri pia kama Yesu ‘angetawala akiwa Mufalme.’ Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza ikiwa Maria alielewa ile maneno namna gani. Je, aliwaza kama maneno ya Gabrieli ilimaanisha kuwa Yesu angekamata nafasi ya Mufalme Herode, ao nafasi ya mumoja kati ya wale wenye wangetawala Israeli kisha Herode? Kama Yesu angekuwa mufalme, Maria angekuwa mama ya mufalme, na familia yake ingeishi katika nyumba ya kifalme. Lakini, Biblia haiseme kama Maria alizungumuza na Gabrieli juu ya jambo kama hilo; na hakuna nafasi kwenye Biblia inasema kuwa Maria aliomba apewe cheo fulani cha juu katika Ufalme, kama vile wanafunzi wawili wa Yesu walifanya. (Mt. 20:20-23) Jambo hilo la kidogo linatuhakikishia hata zaidi kuwa Maria alikuwa mwanamuke munyenyekevu sana!

19-20. Kama vile Yakobo 1:22-25 na 4:8 inaonyesha, tuko na miradi gani wakati tunajifunza?

19 Tukumbuke basi kama muradi wetu wa maana zaidi wakati tunajifunza Neno la Mungu na vichapo vyetu vya Kikristo ni kumukaribia Yehova zaidi. Pia, tunapenda kuona muzuri zaidi sisi ni ‘watu wa namna gani’ na ni mabadiliko gani tunapaswa kufanya ili kumufurahisha Mungu. (Soma Yakobo 1:22-25; 4:8.) Kwa hiyo, kila wakati mbele ya kuanza kujifunza, tunapaswa kumuomba Yehova roho yake. Tunapaswa kumuomba atusaidie ili habari yenye tutajifunza ituletee faida kabisa na tujione namna anatuona.

20 Sisi wote tukuwe basi kama mutu wa Mungu mwenye muandikaji mumoja wa zaburi anasema hivi juu yake: “Anapendezwa na sheria ya Yehova, na anasoma sheria Yake kwa sauti ya chini muchana na usiku. . . . Kila jambo lenye anafanya litafanikiwa.”​—Zb. 1:2, 3.

WIMBO 88 Nijulishe Njia Zako

^ fu. 5 Yehova anatupatia kwa ukarimu mambo mingi ya kuangalia, ya kusoma, na kujifunza. Habari hii itakusaidia kuchagua habari za kujifunza, na inatoa mapendekezo yenye kufaa juu ya mambo yenye unaweza kufanya ili funzo lako likuletee faida zaidi.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Wazazi wanaonyesha watoto wao namna ya kutayarisha Funzo la Munara wa Mulinzi la kila juma.

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mumoja anatafuta habari juu ya muandikaji wa kitabu cha Biblia mwenye kuitwa Amosi. Picha zenye kuwa nyuma yake zinaonyesha mambo yenye ndugu anaona katika akili wakati anasoma habari za Biblia na kufikiri sana juu ya zile habari.