Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 21

Usidanganywe na “Hekima ya Ulimwengu Huu”

Usidanganywe na “Hekima ya Ulimwengu Huu”

“Hekima ya ulimwengu huu ni upumbavu kwa Mungu.”​—1 KO. 3:19.

WIMBO 98 Maandiko​—Yaliongozwa na Roho ya Mungu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Neno la Mungu linatupatia nini?

TUNAWEZA kushinda tatizo lolote, kwa sababu tu Yehova ni Mufundishaji wetu Mukubwa. (Isa. 30:20, 21) Neno lake linatupatia kila kitu chenye tuko nacho lazima ili ‘tukuwe na uwezo kamili’ na “vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.” (2 Ti. 3:17) Wakati tunaishi kulingana na mafundisho ya Biblia, tunakuwa wenye hekima zaidi kupita wale wenye kuchochea “hekima ya ulimwengu.”​—1 Ko. 3:19; Zb. 119:97-100.

2. Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Kama vile tutaona, mara mingi hekima ya ulimwengu inavutia tamaa zetu za kimwili. Kwa hiyo, tunaweza kuona kama ni nguvu kuepuka kufikiri na kutenda kama watu wenye kuwa sehemu ya ulimwengu. Njo maana Biblia inasema hivi: “Mufanye angalisho ili mutu yeyote asiwakamate mateka kupitia filozofia na udanganyifu wa bure kulingana na desturi ya wanadamu.” (Kol. 2:8) Katika habari hii, tutajifunza namna mambo mbili ya uongo yenye Shetani anafundisha imefikia kuenea sana. Juu ya kila jambo, tutaona juu ya nini hekima ya ulimwengu ni upumbavu na namna hekima ya Mungu iko ya hali ya juu zaidi kupita kila kitu chenye ulimwengu unatoa.

MAWAZO YA WATU JUU YA KANUNI ZA NGONO IMEBADILIKA

3-4. Ni mabadiliko gani juu ya mawazo ya watu kuhusu ngono yenye ilitokea mu inchi ya Amerika kati ya mwaka wa 1900 na 1930?

3 Kati ya mwaka wa 1900 na 1930, katika inchi ya Amerika, mawazo ya watu juu ya kanuni za ngono ilibadilika sana. Mbele ya pale, watu wengi waliamini kama watu wenye kuoana tu njo wenye walipaswa kufanya ngono na ngono haikukuwa inazungumuziwa mbele ya watu. Lakini kanuni hizo zilivunjwa na mawazo ya kuachilia mambo ilienea.

4 Miaka kuanzia 1920 mupaka 1929 ilifikia kuitwa Miaka ya Raha Sana na ilikuwa na mabadiliko makubwa sana kuhusu namna watu walijiendesha na kuhusu mawazo yao juu ya ngono. Mutu mumoja mwenye kutafuta habari, alisema hivi: “Filme, michezo katika majumba ya maonyesho, nyimbo, vitabu, na matangazo ya biashara, vyote vilianza kuonyesha sana mambo ya ngono.” Katika miaka hiyo, namna za kucheza zilifanya watu wafikirie mambo ya ngono na watu walianza kuvaa bila kiasi. Kama vile Biblia ilikuwa imetabiri juu ya siku za mwisho, watu wangekuwa kabisa “wenye kupenda raha.”​—2 Ti. 3:4.

Watu wa Yehova hawachochewe na kanuni za ulimwengu za mwenendo wenye kupotoka (Picha hii inapatana na fungu la 5) *

5. Watu wa ulimwengu wamekuwa na mawazo gani juu ya kanuni za mwenendo kuanzia miaka ya 1960?

5 Katika miaka ya 1960, mambo kama vile kuishi pamoja bila kuoana, wanaume kulala na wanaume na wanamuke kulala na wanamuke, na kuvunja ndoa kwa vyepesi ilienea sana. Mambo mingi ya kujifurahisha ilianza kuonyesha waziwazi mambo ya ngono. Katika miaka ya hivi karibuni, matokeo ya mubaya ya mwenendo muchafu imeonekana katika njia za mingi. Muandikaji mumoja aliandika kama “kanuni juu ya mambo ya ngono zenye watu wanafuata leo” njo zinafanya familia zivunjike, kukuwe familia za muzazi mumoja, watu wakuwe na maumivu ya moyoni, wakuwe watumwa wa pornografia, na magumu ingine. Magonjwa yenye kuambukizwa kupitia ngono, kama vile SIDA, imeenea sana. Hilo ni jambo moja tu kati ya mambo yenye kuonyesha kama hekima ya ulimwengu ni upumbavu.​—2 Pe. 2:19.

6. Juu ya nini mawazo ya watu wa ulimwengu juu ya ngono njo yenye Shetani anapenda wakuwe nayo?

6 Mawazo ya watu wa ulimwengu juu ya ngono njo yenye Shetani anapenda wakuwe nayo. Kwa kweli, anafurahi wakati anaona namna watu wanatumia mubaya zawadi zenye Mungu alitupatia, ni kusema, zawadi ya ngono na zawadi ya ndoa. (Efe. 2:2) Watu wenye kufanya uasherati wanaonyesha kama hawaone zawadi ya kuzaa yenye Yehova alitupatia kuwa ya maana, na watu hao wanaweza kukosa uzima wa milele.​—1 Ko. 6:9, 10.

MAWAZO YA BIBLIA JUU YA NGONO

7-8. Juu ya nini mawazo ya Biblia juu ya ngono ni ya muzuri zaidi kuliko mawazo ya ulimwengu?

7 Watu wenye kufuata hekima ya ulimwengu huu wanazarau kanuni za Biblia juu ya ngono, wanasema kama haziko zenye kufaa. Watu kama hao wanaweza kuuliza hivi: ‘Juu ya nini Mungu alituumba na tamaa za kufanya ngono na kisha anatuambia tusitimize tamaa hizo?’ Ulizo hilo linategemea mawazo yenye makosa yenye kusema kama wanadamu wanapaswa kutimiza kila tamaa yenye wako nayo. Lakini Biblia inasema jambo lenye kuwa tofauti na hilo. Biblia inafundisha kama Yehova ameheshimisha wanadamu kwa kuwapatia uwezo wa kuzuia tamaa za mubaya. (Kol. 3:5) Zaidi ya hilo, Yehova ametupatia zawadi ya ndoa na katika mupango huo, watu wanaweza kutimiza kwa njia ya heshima tamaa zao za ngono zenye kufaa. (1 Ko. 7:8, 9) Katika mupango wa ndoa, bibi na bwana wanaweza kufurahia ngono bila kujuta na bila kuogopa matokeo ya mubaya yenye inatokana mara mingi na uasherati.

8 Tofauti na hekima ya ulimwengu huu, Biblia inafundisha mawazo yenye kufaa juu ya ngono. Inaonyesha kama ngono inaweza kuleta furaha. (Mez. 5:18, 19) Lakini, Biblia inasema hivi: “Kila mumoja wenu anapaswa kujua namna ya kuzuia mwili wake katika utakatifu na heshima, haiko kwa pupa, tamaa kubwa ya ngono yenye haizuiliwe kama ya watu wa mataifa wenye hawamujue Mungu.”​—1 Te. 4:4, 5.

9. (a) Kati ya mwaka wa 1900 na 1930, namna gani watu wa Yehova walitiwa moyo kufuata hekima ya juu ya Neno la Mungu? (b) Ni shauri gani la hekima lenye kupatikana katika 1 Yohana 2:15, 16? (c) Kama vile Waroma 1:24-27 inaonyesha, ni matendo gani ya mubaya ya ngono yenye tunapaswa kuepuka?

9 Kati ya mwaka wa 1900 na 1930, watu wa Yehova hawakudanganywa na uongo wa wale wenye ‘wameishiwa na ufahamu wote wa mambo yenye kuwa sawa.’ (Efe. 4:19) Walijikaza kushikamana sana na kanuni za Yehova. Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 5, 1926, ulisema kama “mwanaume ao mwanamuke anapaswa kuwa safi katika mawazo na matendo, zaidi sana kuelekea mutu mwenye haiko bibi ao bwana yake.” Hata kama mambo ya mubaya ilikuwa inatendeka katika ulimwengu, watu wa Yehova walifuata hekima ya hali ya juu ya Neno la Mungu. (Soma 1 Yohana 2:15, 16.) Tuko wenye shukrani sana juu tuko na Neno la Mungu! Pia tuko wenye shukrani juu Yehova anatutolea chakula cha kiroho kwa wakati wenye kufaa ili kutusaidia kupinga hekima ya ulimwengu kuhusu kanuni za ngono. *​—Soma Waroma 1:24-27.

WATU WAMEKUWA WENYE KUJIPENDA WENYEWE

10-11. Biblia ilionya kama ni nini ingetokea katika siku za mwisho?

10 Biblia ilionya kama katika siku za mwisho, watu wangekuwa “wenye kujipenda wenyewe.” (2 Ti. 3:1, 2) Hatushangae kuona kama ulimwengu umechochea watu wakuwe na mawazo ya kujipenda wenyewe. Kitabu kimoja kinasema kama katika miaka ya 1970, “vitabu vyenye kufundisha namna ya kujisaidia mwenyewe viliongezeka sana.” Vitabu fulani “vilitia moyo wasomaji wajijue na wakubali namna wako na wafurahie namna wako.” Fikiria kwa mufano maneno fulani yenye kupatikana katika kitabu kimoja, yenye kusema hivi: “Upende mutu mwenye sura ya muzuri zaidi, mwenye kufurahisha zaidi, na wa maana zaidi, ni kusema, wewe mwenyewe.” Kitabu hicho kinasema kama mutu anapaswa kuamua yeye mwenyewe namna ya kujiendesha, na kufanya mambo yote yenye anaona kuwa ni sawa na yenye kufaa.

11 Umekwisha kusikia mawazo kama ile? Shetani alimuchochea Eva afanye jambo kama hilo. Alimuambia kama ‘angekuwa kama Mungu; akijua mema na mabaya.’ (Mwa. 3:5) Leo, watu wengi wanajifikiria sana wao wenyewe mupaka wanawaza kama hakuna mutu mwenye anaweza kuwaambia mambo yenye kuwa sawa na mambo yenye kuwa makosa, hata Mungu hawezi kufanya vile. Kwa mufano, ile mawazo imeonekana zaidi sana katika namna watu wanaona ndoa.

Mukristo anatanguliza mahitaji ya wengine, zaidi sana mahitaji ya bibi yake (Picha hii inapatana na fungu la 12) *

12. Watu wa ulimwengu wanachochea mawazo gani juu ya ndoa?

12 Biblia inaomba bibi na bwana waheshimiane na waheshimie naziri zao za ndoa. Inatia moyo bibi na bwana wakuwe na azimio la kushikamana na mupango wa ndoa; inasema hivi: “Mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na atashikamana na bibi yake, nao watakuwa mwili mumoja.” (Mwa. 2:24) Lakini, wale wenye kuchochewa na hekima ya ulimwengu wako na mawazo yenye kuwa tofauti na ile, wanasema kama kila mutu katika ndoa anapaswa kutanguliza mahitaji yake mwenyewe. Kitabu kimoja chenye kuzungumuzia mambo ya kuvunja ndoa kinasema kama “katika sherehe fulani, maneno ‘kwa muda wote wenye sisi wawili tutaishi pamoja,’ yenye inazoea kutumiwa katika naziri ya ndoa, imebadilishwa na naziri yenye kuwa na mipaka, na imekuwa ‘kwa muda wote wenye sisi wawili tutapendana.’” Ile mawazo ya kukosa kukamata ndoa kwa uzito imefanya familia za mingi zivunjike na imeleta maumivu mingi ya moyoni. Kwa kweli, mawazo ya ulimwengu yenye kushushia ndoa heshima ni mafundisho ya upumbavu.

13. Ni sababu gani moja yenye kufanya Yehova achukie watu wenye kiburi?

13 Biblia inasema hivi: “Kila mutu mwenye kiburi katika moyo ni chukizo kwa Yehova.” (Mez. 16:5) Juu ya nini Yehova anachukia watu wenye kiburi? Sababu moja ni kwamba wale wenye kukomalisha na kuchochea mawazo ya kujipenda wenyewe kupita kiasi wanaonyesha kiburi kama Shetani. Wazia jambo hili: Shetani aliamini kama Yesu, mutu mwenye Mungu alitumia ili kuumba vitu vyote, alipaswa kuinama na kumuabudu! (Mt. 4:8, 9; Kol. 1:15, 16) Watu wenye kuwa na ile mawazo ya kujiona kuwa wa maana kupita kiasi, wanaonyesha kabisa kama hekima ya ulimwengu ni upumbavu kwa Mungu.

MAWAZO YA BIBLIA JUU YA KUJIONA KUWA WA MAANA

14. Namna gani Waroma 12:3 inatusaidia kuwa na mawazo yenye kusawazika juu ya sisi wenyewe?

14 Biblia inatusaidia tukuwe na mawazo yenye kusawazika juu ya sisi wenyewe. Inaonyesha kama haiko mubaya kujipenda kwa kadiri fulani. Yesu alisema hivi: “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe,” hilo linaonyesha kama tunapaswa kuhangaikia mahitaji yetu kwa kiasi chenye kufaa. (Mt. 19:19) Hata hivyo, Biblia haifundishe kama tunapaswa kujipandisha juu ya wengine. Lakini, inasema hivi: “Musifanye jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kutafuta sifa, lakini kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi.”​—Flp. 2:3; soma Waroma 12:3.

15. Juu ya nini unaona kama mashauri ya Biblia juu ya kujiona kuwa wa maana ni yenye kufaa?

15 Leo, watu wengi wenye wanaonwa kuwa wenye hekima wanazarau shauri la Biblia kuhusu kujiona kuwa mutu wa maana. Wanaweza kusema kama kuona wengine kuwa wazuri zaidi kuliko wewe kunaweza kukufanya ukuwe muzaifu, na kama wengine wanaweza kukuonea. Lakini, mawazo yenye kuchochewa na ulimwengu wa Shetani ya kujipenda mwenyewe imeleta matokeo gani? Umejionea nini? Je, watu wenye kujipenda wenyewe wako na furaha? Wako na familia zenye kuwa na furaha? Wako na marafiki wa kweli? Wako na urafiki wa sana pamoja na Mungu? Kulingana na mambo yenye umejionea, ni nini inaleta matokeo ya muzuri zaidi, kufuata hekima ya ulimwengu huu ao kufuata hekima yenye kuwa katika Neno la Mungu?

16-17. Tuko wenye shukrani juu ya jambo gani, na juu ya nini?

16 Watu wenye kufuata mashauri ya wale wenye ulimwengu unaona kuwa wenye hekima, wako kama mutu mwenye kusafiri mwenye anauliza musafiri mwenzake amuonyeshe njia wakati wote wawili wamepotea. Yesu alisema hivi juu ya watu “wenye hekima” wa siku zake: “Wao ni viongozi vipofu. Basi, kama kipofu anamuongoza kipofu, wote wawili wataanguka ndani ya shimo.” (Mt. 15:14) Kwa kweli, hekima ya ulimwengu huu ni upumbavu kwa Mungu.

Watumishi wa Mungu wanakumbuka kwa furaha maisha yenye walipitisha katika kazi ya Yehova (Picha hii inapatana na fungu la 17) *

17 Mashauri yenye hekima ya Biblia imeonekana sikuzote kuwa yenye “faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kurekebisha, kwa kutia nizamu katika haki.” (2 Ti. 3:16, maelezo ya chini) Tuko wenye shukrani sana kwa sababu, kupitia tengenezo lake, Yehova ametulinda ili tusichochewe na hekima ya ulimwengu huu! (Efe. 4:14) Chakula cha kiroho chenye ametupatia kinatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tushikamane na kanuni za Neno lake. Tuko na pendeleo kubwa la kuongozwa na hekima yenye kutegemeka yenye kupatikana katika Biblia!

WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”

^ fu. 5 Habari hii itatusaidia tukuwe hakika zaidi kama Yehova tu njo mwenye anatoa mwongozo wenye kutegemeka. Pia, itaonyesha kama kufuata hekima ya ulimwengu kunaleta matokeo ya mubaya sana, lakini kutumia hekima ya Neno la Mungu kunaleta faida.

^ fu. 9 Kwa mufano, ona kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1, sura ya 24-26, na Buku la 2, sura ya 4-5.

^ fu. 50 MAFASIRIO YA PICHA: Tunaona mambo fulani yenye bibi na bwana wenye kuwa Mashahidi wamefanya mu maisha yao kadiri wakati unaendelea kupita. Ndugu huyo na bibi yake wanahubiri ku mwisho-mwisho wa miaka ya 1960.

^ fu. 52 MAFASIRIO YA PICHA: Katika miaka ya 1980, bwana anahangaikia bibi yake wakati iko mugonjwa na mutoto wao mudogo mwanamuke anaangalia.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Leo, bibi na bwana hao wanakumbuka kwa furaha mambo yenye walifanya katika kazi ya Yehova. Mutoto wao mwanamuke mwenye alishakomaa na familia yake wanafurahi pamoja na wazazi wake.