Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 19

Kuonyesha Upendo na Haki ili Kupiganisha Uovu

Kuonyesha Upendo na Haki ili Kupiganisha Uovu

“Hauko Mungu mwenye anafurahia uovu; hakuna mutu yeyote mubaya mwenye anaweza kukaa pamoja na wewe.”​—ZB. 5:4.

WIMBO 142 Kushikilia Tumaini Letu

KIFUPI CHA HABARI *

1-3. (a) Kulingana na Zaburi 5:4-6, Yehova anaona namna gani uovu? (b) Juu ya nini tunaweza kusema kama kutendea watoto mubaya kingono kunapingana na “sheria ya Kristo”?

YEHOVA MUNGU anachukia aina yote ya uovu. (Soma Zaburi 5:4-6.) Kwa kweli, anachukia sana wakati watoto wanatendewa mubaya kingono: tendo hilo ni la mubaya sana na ni lenye kuchukiza kabisa! Kwa sababu tunamuiga Yehova, sisi Mashahidi wake tunachukia sana matendo ya kutendea watoto mubaya kingono na hatuachilie matendo kama ile katika kutaniko la Kikristo.​—Ro. 12:9; Ebr. 12:15, 16.

2 Matendo yote ya kutendea watoto mubaya kingono inapingana kabisa na “sheria ya Kristo”! (Gal. 6:2) Juu ya nini tunaweza kusema vile? Kama vile tulijifunza katika habari yenye ilitangulia, sheria ya Kristo ni mambo yote yenye Yesu alifundisha kupitia maneno na mufano wake; inategemea upendo na inakazia haki. Kwa sababu Wakristo wa kweli wanaongozwa na sheria hiyo, wanatendea watoto katika njia yenye inawafanya wajisikie kuwa salama na wenye kupendwa kabisa. Lakini, kutendea mutoto mubaya kingono ni tendo la kujifikiria mwenyewe na la kukosa haki, lenye linafanya mutoto asijisikie kuwa salama na asijisikie kuwa anapendwa.

3 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, kutendea watoto mubaya kingono ni tatizo kubwa lenye kuwa mu dunia yote, na Wakristo wa kweli wamepatwa na tatizo hilo. Juu ya nini? “Watu waovu na wajanja” wanaongezeka, na wamoja kati yao wanaweza kujaribu kuingia mu kutaniko. (2 Ti. 3:13) Tena, watu fulani wenye walisema kama wanamutumikia Yehova, wamechochewa na tamaa za mubaya sana na wametendea watoto mubaya kingono. Tuzungumuzie basi juu ya nini kutendea watoto mubaya kingono ni zambi nzito sana. Kisha tutazungumuzia namna wazee wanashugulikia hali za zambi nzito, kutia ndani zambi ya kutendea watoto mubaya kingono, na namna wazazi wanaweza kulinda watoto wao. *

NI ZAMBI NZITO

4-5. Juu ya nini kutendea mutoto mubaya kingono ni kumutendea zambi?

4 Kutendea watoto mubaya kingono kunaleta matokeo ya mubaya kwa wakati murefu. Kunaumiza watoto wenye wametendewa mubaya kingono na kunaumiza wale wenye kuwahangaikia, ni kusema, watu wa familia yao na ndugu na dada zao Wakristo. Kutendea watoto mubaya kingono ni zambi nzito.

5 Ni kumutendea mutoto zambi. Ni zambi kuletea wengine maumivu na mateso. Kama vile tutaona katika habari yenye kufuata, mutu mwenye anatendea mutoto mubaya kingono anamuletea maumivu na mateso; anaumiza mutoto katika njia za mubaya sana. Anafanya mutoto asitumainie mutu, na asijisikie kuwa salama. Watoto wanapaswa kulindwa ili wasitendewe jambo hilo la mubaya sana, na wale wenye wametendewa mubaya kingono wanapaswa kufarijiwa na kusaidiwa.​—1 Te. 5:14.

6-7. Juu ya nini kutendea mutoto mubaya kingono ni kutendea zambi kutaniko na wakubwa wa serikali?

6 Ni kutendea kutaniko zambi. Wakati mutu fulani katika kutaniko anatendea mutoto mubaya kingono, anaharibisha sifa ya kutaniko. (Mt. 5:16; 1 Pe. 2:12) Hilo ni jambo lenye kukosa haki kabisa kuelekea mamilioni ya Wakristo waaminifu wenye wanaendelea ‘kupigania kabisa imani’! (Yud. 3) Haturuhusu watu wenye kufanya mambo maovu wenye hawatubu na wenye kuharibisha sifa ya muzuri ya kutaniko wabakie katika kutaniko.

7 Ni kutendea wakubwa wa serikali zambi. Wakristo wanapaswa ‘kujitiisha kwa mamlaka zenye kuwa kubwa.’ (Ro. 13:1) Tunaonyesha kama tunajitiisha kwa kuheshimia sheria za inchi. Kama mutu fulani katika kutaniko anavunja sheria yenye kukataza matendo ya mubaya, kama vile kutendea mutoto mubaya kingono, anatendea zambi wakubwa wa serikali. (Linganisha na Matendo 25:8.) Wazee hawaruhusiwe kupatia malipizi watu wenye wamevunja sheria ya inchi, lakini hawalinde mutu mwenye ametendea mutoto mubaya kingono ili asipatwe na malipizi ya serikali. (Ro. 13:4) Mutenda-zambi anavuna kile chenye alipanda.​—Gal. 6:7.

8. Namna gani Yehova anaona zambi zenye mutu anatendea wanadamu wenzake?

8 Zaidi ya yote, ni kumutendea Mungu zambi. (Zb. 51:4) Wakati mwanadamu anatendea mwanadamu mwenzake zambi, anatendea pia Yehova zambi. Fikiria mufano wa Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli. Sheria ilisema kama mutu mwenye aliiba ao kutendea jirani yake kwa udanganyifu alijiendesha kwa njia ya “kukosa uaminifu kwa Yehova.” (Law. 6:2-4) Kwa kweli, wakati mutu fulani katika kutaniko anatendea mutoto mubaya kingono, na kufanya mutoto akose usalama, anakosa uaminifu kwa Mungu. Mutu mwenye alitendea mutoto mubaya kingono anachafua sana jina la Yehova. Njo maana tunapaswa kuelewa kama kutendea mutoto mubaya kingono ni kumutendea Mungu zambi ya mubaya sana, na tunapaswa kuichukia.

9. Ni habari gani zenye kutegemea Maandiko zenye tengenezo la Yehova limetoa kwa miaka mingi, na juu ya nini?

9 Kwa miaka mingi, tengenezo la Yehova limetoa habari za mingi zenye kutegemea Maandiko zenye kuzungumuzia tatizo la kutendea watoto mubaya kingono. Kwa mufano, habari fulani zenye kupatikana katika Munara wa Mulinzi na Amuka! zimezungumuzia namna wale wenye wametendewa mubaya kingono wanaweza kupambana na huzuni ya muda murefu yenye kutokana na jambo lenye liliwafikia, namna wengine wanaweza kuwasaidia na kuwatia moyo, na namna wazazi wanaweza kulinda watoto wao. Wazee wamepata maagizo yenye kutegemea Maandiko yenye kuwa wazi zaidi juu ya namna ya kushugulikia zambi ya kutendea watoto mubaya kingono. Tengenezo linaendelea kuchunguza na kurekebisha namna wazee wa kutaniko wanashugulikia zambi ya kutendea watoto mubaya kingono. Juu ya nini? Ili kuhakikisha kama namna yetu ya kushugulikia tatizo hilo inapatana na sheria ya Kristo.

NAMNA WAZEE WANASHUGULIKIA ZAMBI NZITO

10-12. (a) Wazee wanakumbuka nini wakati wanashugulikia tatizo lolote lenye kuhusu zambi nzito, na wanahangaikia mambo gani? (b) Kulingana na Yakobo 5:14, 15, wazee wanajikaza kufanya nini?

10 Wakati wazee wanashugulikia tatizo lolote lenye kuhusu zambi nzito, wanakumbuka kama sheria ya Kristo inaomba watendee kundi kwa upendo na wafanye mambo yenye Mungu anasema kuwa ni sawa na yenye haki. Kwa hiyo, wako na mambo mingi ya kufikiria wakati wanapata habari kuwa mutu fulani amefanya zambi nzito. Wazee wanahangaikia kwanza kutakasa jina la Mungu. (Law. 22:31, 32; Mt. 6:9) Pia, wanahangaikia sana hali ya muzuri ya kiroho ya ndugu na dada zao katika kutaniko na wanapenda kusaidia mutu yeyote mwenye ametendewa mubaya.

11 Zaidi ya hilo, kama mutenda-zambi ni mutu fulani katika kutaniko, wazee wanahangaikia kusaidia mutu huyo arudilie urafiki wake pamoja na Mungu, kama inawezekana. (Soma Yakobo 5:14, 15.) Mukristo mwenye anafanya zambi nzito ili kutimiza tamaa yake ya mubaya, iko mugonjwa kiroho. Hilo linamaanisha kama hana tena urafiki muzuri pamoja na Yehova. * Kwa njia fulani, wazee ni wanganga wa kiroho. Wanajikaza ‘kuponyesha ule mugonjwa [ni kusema, ule mutenda-zambi].’ Mashauri yenye kutegemea Maandiko yenye wanamutolea, inaweza kumusaidia akuwe tena na urafiki muzuri pamoja na Mungu, lakini hilo linawezekana kama tu anatubu kweli-kweli.​—Mdo. 3:19; 2 Ko. 2:5-10.

12 Ni wazi kwamba, wazee wako na daraka kubwa. Wanahangaikia sana kundi lenye Mungu amewapatia. (1 Pe. 5:1-3) Wanapenda ndugu na dada zao wajisikie kuwa salama katika kutaniko. Njo maana, wanatenda bila kukawia wakati wanapata habari kuwa mutu fulani amefanya zambi nzito, kutia ndani zambi ya kutendea watoto mubaya kingono. Fikiria maulizo yenye kupatikana ku mwanzo wa  fungu la 13,  15, na  17.

13-14. Je, wazee wanatii sheria za inchi zenye kuomba kujulisha wakubwa wa serikali shitaka la kutendea mutoto mubaya kingono? Fasiria.

 13 Je, wazee wanatii sheria za inchi zenye kuomba kujulisha wakubwa wa serikali shitaka la kutendea mutoto mubaya kingono? Ndiyo. Katika inchi kwenye sheria kama hizo zinapatikana, wazee wanajikaza kutii sheria zenye kuomba kujulisha wakubwa wa serikali mashitaka ya kutendea watoto mubaya kingono. (Ro. 13:1) Sheria kama hizo hazipingane na sheria ya Mungu. (Mdo. 5:28, 29) Kwa hiyo, wakati wazee wanapata shitaka fulani, wanatafuta muongozo bila kukawia kwenye biro ya tawi juu ya namna wanaweza kutii sheria zenye kuhusu kujulisha jambo hilo.

14 Wazee wanahakikishia wale wenye wametendewa mubaya kingono na pia wazazi wao na wengine wenye wanajua jambo hilo kama wako huru kujulisha wakubwa wa serikali shitaka la kutendea mutoto mubaya kingono. Halafu kama mutu mwenye kushitakiwa iko katika kutaniko na kisha ile mambo inajulikana katika eneo? Mukristo mwenye alijulisha jambo hilo anapaswa kuwaza kama amechafua jina la Mungu? Hapana. Mutu mwenye alitendea mutoto mubaya kingono njo mwenye anachafua jina la Mungu.

15-16. (a) Kulingana na 1 Timoteo 5:19, juu ya nini inaomba kuwe mashahidi wawili hivi mbele wazee waunde halmashauri ya hukumu? (b) Wazee wanafanya nini wakati wanapata habari kwamba mutu fulani katika kutaniko anashitakiwa kuwa ametendea mutoto mubaya kingono?

 15 Katika kutaniko, juu ya nini kunapaswa kuwa mashahidi wawili hivi mbele wazee waunde halmashauri ya hukumu? Kwa sababu Biblia inasema kama kufanya vile ni kutenda kwa haki. Kama mutu hakubali kuwa alifanya zambi nzito, inaomba kuwe mashahidi wawili ili kuhakikisha ile mashitaka na wazee wanaruhusiwa kuunda halmashauri ya hukumu. (Kum. 19:15; Mt. 18:16; soma 1 Timoteo 5:19.) Je, hilo linamaanisha kama inaomba kuwe mashahidi wawili mbele ya kujulisha wakubwa wa serikali shitaka la kutendea mubaya mutoto kingono? Hapana. Wazee ao watu wengine hawana lazima ya mashahidi wawili ili kujulisha shitaka la kosa kubwa kwa wakubwa wa serikali.

16 Wakati wazee wanapata habari kwamba mutu fulani katika kutaniko anashitakiwa kuwa ametendea mutoto mubaya kingono, wanajikaza kutii sheria zozote za inchi zenye kuomba kujulisha jambo hilo, na kisha wanachunguza ikiwa halmashauri ya hukumu inapaswa kuundwa. Kama ule mutu anakataa ile mashitaka, wazee wanasikiliza ushuhuda wa watu wenye pengine wanajua jambo lenye lilitokea. Wazee wanaunda halmashauri ya hukumu ikiwa watu wawili hivi wanahakikisha ile mashitaka, ni kusema, mutu mwenye kushitaki na mutu mwingine mwenye anaweza kushuhudia kuwa tendo hilo ao matendo mengine ya kutendea watoto mubaya kingono imefanywa na mutu mwenye kushitakiwa. * Kama hakuna shahidi wa pili hilo halimaanishe kama mutu mwenye kushitaki anasema uongo. Hata kama hakuna mashahidi wawili wenye wanaweza kuhakikisha kama zambi nzito imefanywa, wazee wanaelewa kama pengine zambi nzito imefanywa yenye inaumiza sana wengine. Wazee wanaendelea kufariji na kutegemeza mutu yeyote mwenye anaweza kuwa ameumizwa. Zaidi ya hilo, wazee wanaendelea kuwa waangalifu ili kulinda kutaniko juu ya hatari yoyote yenye inaweza kuletwa na mutu huyo mwenye pengine ametendea mutoto mubaya kingono.​—Mdo. 20:28.

17-18. Fasiria daraka la halmashauri ya hukumu.

 17 Halmashauri ya hukumu iko na daraka gani? Neno “hukumu” halimaanishe kama wazee wanaamua ikiwa mutu mwenye alitendea mutoto mubaya kingono anapaswa kupewa malipizi na wakubwa wa serikali kwa sababu ya kuvunja sheria. Daraka la wazee haiko kuhakikisha kama watu wanatii sheria; wanaachia wakubwa wa serikali washugulikie mambo yenye kuhusu kuvunja sheria. (Ro. 13:2-4; Tit. 3:1) Lakini wazee wanahukumu, ao kuamua ikiwa ule mutu anaweza kubakia katika kutaniko.

18 Wakati wazee wako katika halmashauri ya hukumu, daraka lao ni kushugulikia mambo ya kiroho. Kwa kutumia Maandiko, wanaamua ikiwa ule mutu mwenye alitendea mutoto mubaya kingono anatubu ao hapana. Kama hatubu, anatengwa na kutaniko, na tangazo linafanywa katika kutaniko. (1 Ko. 5:11-13) Kama anatubu, anaweza kubakia katika kutaniko. Lakini, wazee watamuambia kama inawezekana hatapataka mapendeleo yoyote katika kutaniko ao kutumikia madaraka yoyote katika kutaniko. Ili kuhangaikia usalama wa watoto, wazee wanaweza kuonya wazazi kwa siri kwamba wanapaswa kuwa waangalifu wakati watoto wao wako karibu na mutu huyo. Wakati wazee wanachukua hatua kama hizo, wanapaswa kuwa waangalifu ili wasifunue ni nani wenye walitendewa mubaya na mutu huyo.

NAMNA YA KULINDA WATOTO WAKO

Wazazi wanaelezea watoto wao habari zenye kufaa juu ya ngono ili kuwalinda wasitendewe mubaya kingono. Ili kufanya vile, wazazi wanatumia habari zenye tengenezo la Mungu limetutolea. (Picha hii inapatana na fungu la 19-22)

19-22. Wazazi wanaweza kufanya nini ili kulinda watoto wao? (Ona picha ku jalada ya gazeti hili.)

19 Ni nani wenye kuwa na daraka la kulinda watoto ili wasitendewe mubaya? Ni wazazi. * Watoto wako ni zawadi kutoka kwa Mungu, “uriti kutoka kwa Yehova.” (Zb. 127:3) Ni daraka lako kulinda zawadi hiyo. Unaweza kufanya nini ili kulinda watoto wako wasitendewe mubaya kingono?

20 Kwanza, tafuta habari juu ya tatizo la kutendea watoto mubaya kingono. Ujifunze ni watu wa namna gani njo wanatendeaka watoto mubaya kingono na ufundi wenye wanatumia ili kuwadanganya. Ukuwe muangalifu juu ya hatari zenye zinaweza kutokea. (Mez. 22:3; 24:3) Ukumbuke kama, mara mingi mutu mwenye kutendea mutoto mubaya kingono ni mutu mwenye mutoto anajua tayari na anamutumainia.

21 Pili, ukuwe unazungumuza waziwazi na watoto wako na uwatie moyo wakuwe wanazungumuza na wewe waziwazi. (Kum. 6:6, 7) Maana yake, unapaswa kusikiliza watoto wako kwa uangalifu. (Yak. 1:19) Ukumbuke kama mara mingi watoto wenye wametendewa mubaya kingono wanaogopa kueleza jambo hilo. Wanaweza kuogopa kama watu hawatawaamini, ao wanaweza kuogopa kwa sababu mutu mwenye aliwatendea mubaya aliwaambia kama atawafanyia jambo fulani la mubaya kama wanaambia mutu yeyote. Kama unawaza kuwa watoto wako wamepatwa na jambo fulani, uwaulize maulizo kwa uvumilivu ili kuwasaidia wajieleze na usikilize majibu yao.

22 Tatu, ufundishe watoto wako. Kulingana na miaka yao, uwaambie mambo yenye wako na lazima ya kujua juu ya ngono. Uwafundishe mambo yenye wanaweza kusema ao kufanya kama mutu fulani anajaribu kuwagusa mu njia yenye haifae. Utumie habari zenye tengenezo la Mungu limetoa juu ya namna ya kulinda watoto wako.​—Ona kisanduku “ Ujifundishe Wewe Mwenyewe na Ufundishe Watoto Wako.”

23. Tuko na mawazo gani juu ya kutendea watoto mubaya kingono, na habari yenye kufuata itajibu ulizo gani?

23 Sisi Mashahidi wa Yehova, tunaona kuwa kutendea watoto mubaya kingono ni zambi nzito na ni tendo la mubaya sana. Kwa sababu tunaongozwa na sheria ya Kristo, sisi Mashahidi wa Yehova hatulinde watu wenye kutendea watoto mubaya kingono ili wasipatwe na matokeo ya zambi zao. Lakini, tunaweza kufanya nini ili kusaidia wale wenye wametendewa mubaya kingono? Habari yenye kufuata itajibu ulizo hilo.

WIMBO 103 Wachungaji—Zawadi Katika Wanadamu

^ fu. 5 Habari hii itazungumuzia namna watoto wanaweza kulindwa ili wasitendewe mubaya kingono. Tutajifunza namna wazee wanalinda kutaniko na namna wazazi wanaweza kulinda watoto wao.

^ fu. 3 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Tendo la kutendea mutoto mubaya kingono linafanyika wakati mutu muzima anatumia mutoto ili kutimiza tamaa zake za ngono. Linaweza kutia ndani ngono; ngono ya mudomo ao ngono ya mukundu; kugusa-gusa viungo vya uzazi, maziba, ao matako yake; ao kufanya matendo ingine machafu. Ni jambo la maana tujue kama mutoto mwenye ametendewa mubaya kingono, ameumizwa, ametendewa mubaya, na mutoto huyo hana kosa. Hata kama mara mingi ni watoto wanamuke njo wanatendewa mubaya kingono, watoto wengi wanaume pia wanatendewa mubaya kingono. Hata kama wengi kati ya wale wenye kutendea watoto mubaya kingono ni wanaume, wanamuke fulani wanatendea pia watoto mubaya kingono.

^ fu. 11 Kuwa mugonjwa kiroho hakumupatie mutu sababu ya kufanya zambi nzito. Mutenda-zambi anapaswa kukubali matokeo ya maamuzi na matendo yake ya mubaya na atatoa hesabu kwa Yehova.​—Ro. 14:12.

^ fu. 16 Wazee hawapaswe hata kidogo kuomba mutoto akuwe pale wakati wanazungumuza na mutu mwenye anashitakiwa kuwa alimutendea mubaya kingono. Muzazi ao mutu mwingine mwenye mutoto anatumainia na mwenye mutoto iko tayari kuzungumuza naye anaweza kuambia wazee mambo yenye mutoto anasema kuwa ilitokea. Kwa kufanya vile, mutoto hataumia tena zaidi katika moyo wake.

^ fu. 19 Mambo yenye kusemwa kwa ajili ya wazazi inahusu pia wale wenye wako na daraka la kukomalisha watoto wenye hawako watoto wao.