MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 5, 2020

Gazeti hili liko na habari za kujifunza tarehe 6/7–2/8/2020.

“Mufalme wa Kaskazini” Katika Wakati wa Mwisho

Habari ya kujifunza ya 19: Tarehe 6-12/7/2020. Tuko tunajionea mambo yenye kuhakikisha kama unabii wa Danieli juu ya “mufalme wa kaskazini” na “mufalme wa kusini” unaendelea kutimia. Juu ya nini tuko hakika na jambo hilo? Na juu ya nini tuko na lazima ya kuelewa mambo yenye unabii huo unazungumuzia?

Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho

Unabii mbalimbali juu ya “mufalme wa kaskazini” na “mufalme wa kusini” unatimia kwa wakati uleule. Namna gani unabii huo unaonyesha kama mupangilio huu wa mambo utafikia mwisho hivi karibuni?

Ni Nani “Mufalme wa Kaskazini” Leo?

Habari ya kujifunza ya 20: Tarehe 13-19/7/2020. Ni nani “mufalme wa kaskazini” leo, na namna gani atafikia mwisho wake ao kuharibiwa? Kujua majibu ya ile maulizo kunaweza kutia nguvu imani yetu na kutusaidia tukuwe tayari kupambana na majaribu yenye itatupata hivi karibuni.

Uko Mwenye Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Zenye Mungu Amekupatia?

Habari ya kujifunza ya 21: Tarehe 20-26/7/2020. Habari hii itatusaidia tukuwe wenye shukrani zaidi kwa Yehova na kwa ajili ya zawadi fulani zenye ametupatia. Itatuonyesha pia namna ya kufikiri na watu wenye wako na mashaka ikiwa Mungu iko.

Onyesha Kama Uko Mwenye Shukrani kwa Ajili ya Zawadi Zenye Hazionekane

Habari ya kujifunza ya 22: Tarehe 27/7–2/8/2020. Katika habari yenye ilitangulia, tulizungumuzia zawadi fulani zenye Mungu ametupatia zenye tunaweza kuona. Habari hii itazungumuzia zawadi zenye hatuwezi kuona na namna tunaweza kuonyesha kama tuko wenye shukrani kwa ajili ya zawadi hizo. Itatusaidia pia tukuwe wenye shukrani zaidi kwa Yehova Mungu, mwenye anatupatia zawadi hizo.