Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Upole​—Unatuletea Faida Gani?

Upole​—Unatuletea Faida Gani?

Dada mumoja mwenye kuitwa Sara * anasema hivi: “Niko mutu mwenye haya na sijitumainie sana. Kwa hiyo, sijisikie muzuri wakati niko pamoja na watu wenye kujitumainia sana na wenye kulazimisha wengine wafuate mawazo yao. Lakini ninajisikia muzuri wakati niko pamoja na mutu mwenye kuwa mupole na munyenyekevu. Ninaweza kuambia mutu wa vile namna ninajisikia, na kuzungumuza naye juu ya magumu yangu. Marafiki wangu wa sana ni watu wapole na wanyenyekevu.”

Maneno ya Sara inaonyesha kama, ikiwa tuko wapole, watu wengine watapenda kuwa marafiki wetu. Sifa ya upole inamufurahisha pia Yehova. Neno lake linatushauria hivi: “Muvae . . . upole.” (Kol. 3:12) Upole maana yake nini? Namna gani Yesu alionyesha upole? Na namna gani sifa ya upole inaweza kutusaidia tukuwe na furaha zaidi katika maisha?

UPOLE MAANA YAKE NINI?

Upole ni sifa yenye mutu anakuwa nayo wakati iko mutu mwenye kupenda amani. Mutu mupole anatendea wengine muzuri na anaendelea kuwa mutulivu wakati mambo yenye kukasirisha inamufikia.

Kama mutu iko mupole, ile haimaanishe kama iko muzaifu. Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “upole” lilitumiwa ili kuzungumuzia farasi wa pori mwenye amefugwa. Farasi huyo angali na nguvu, lakini amezoezwa kuzuia nguvu yake. Vilevile, wakati tunaonyesha sifa ya upole, tunazuia uzaifu wetu na tunaendelea kuishi kwa amani pamoja na wengine.

Pengine tunaweza kuwaza hivi: ‘Mimi siko mutu mupole.’ Tunaishi katika ulimwengu kwenye watu wengi sana ni wakali na wenye kukosa uvumilivu, njo maana inaweza kuwa nguvu sana kuonyesha sifa ya upole. (Ro. 7:19) Kwa kweli, inaomba kujikaza sana ili kuonyesha sifa ya upole, lakini, roho takatifu ya Yehova itatusaidia tuendelee kujikaza ili kuwa wapole. (Gal. 5:22, 23) Juu ya nini tunapaswa kujikaza kukomalisha sifa ya upole?

Upole ni sifa yenye inavutia watu. Kama vile Sara, mwenye tulizungumuzia, alisema, tunafurahiaka kuwa pamoja na mutu mwenye iko na tabia ya upole. Yesu njo mutu mwenye alionyesha mufano muzuri sana wa upole na wema. (2 Ko. 10:1) Hata watoto wenye hawakukuwa wanamujua Yesu muzuri, walipenda kuwa pamoja naye​—Mk. 10:13-16.

Sifa ya upole inatusaidia na inasaidia watu wenye kutuzunguka. Kama tuko wapole, hatukwazike haraka-haraka ao kutenda kwa kasirani. (Mez. 16:32) Kwa hiyo, hatutajisikia kuwa wenye hatia kwa sababu tumekwaza watu wengine, zaidi sana watu wenye tunapenda. Na wakati tuko wapole, tutajizuia na kwa hiyo, hatutafanya wengine wateseke kwa kuwakwaza.

MUFANO MUKAMILIFU WA UPOLE

Hata kama Yesu alikuwa na madaraka mazito na mambo mingi ya kufanya, alikuwa mupole kwa watu wote. Watu wengi wa wakati wake walikuwa wanapambana na matatizo na walikuwa wamelemewa na mizigo, na walikuwa na lazima ya mutu wa kuwapumuzisha. Kwa kweli, walijisikia muzuri sana wakati Yesu aliwaambia hivi: “Mukuje kwangu, . . . kwa maana mimi ni mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo”!​—Mt. 11:28, 29.

Namna gani tunaweza kuonyesha sifa ya upole kama Yesu? Tunajifunza Neno la Mungu ili kujua namna Yesu alikuwa anatendea watu na namna alitenda katika hali ngumu. Kwa hiyo, wakati tunapambana na hali zenye kufanya ikuwe nguvu kwetu kuonyesha sifa ya upole, tunajikaza kutenda kama Yesu. (1 Pe. 2:21) Fikiria mambo tatu yenye ilimusaidia Yesu akuwe mupole.

Yesu alikuwa munyenyekevu kabisa. Yesu alisema kama alikuwa “mwenye tabia ya upole na munyenyekevu katika moyo.” (Mt. 11:29) Biblia inataja sifa hizo mbili pamoja kwa sababu sifa ya upole inapatana sana na sifa ya unyenyekevu. (Efe. 4:1-3) Juu ya nini?

Unyenyekevu unatusaidia tuepuke kujiona kuwa watu wa maana ao kukasirika mbio-mbio. Yesu alitenda namna gani wakati watu walimuchambua bila haki kwamba alikuwa “mutu mulafi” na “mwenye anazoea kunywa divai”? Kupitia namna yake ya kuishi, alionyesha kama mambo yenye walisema mubaya juu yake haikukuwa kweli, na kwa sababu alikuwa munyenyekevu alionyesha kwa upole kama “hekima inaonekana kuwa yenye haki kupitia kazi zake.”​—Mt. 11:19.

Kama mutu anakusema mubaya juu ya rangi yako ya ngozi, juu uko mwanaume ao mwanamuke, ao juu ya mahali kwenye ulitoka, ujikaze sana kujibu kwa upole. Peter, muzee mumoja wa kutaniko mu inchi ya Afrika ya Kusini, anasema hivi: “Wakati ninakasirika juu ya mambo yenye mutu fulani anasema, ninajiuliza hivi: ‘Yesu angetenda namna gani katika hali hii?’” Anasema tena hivi: “Nimejifunza kama sipaswe kujiona kuwa mutu wa maana sana.”

Yesu alielewa uzaifu wa wanadamu. Wanafunzi wa Yesu walikuwa na nia ya kufanya mambo ya muzuri, lakini wakati fulani hali yao ya kukosa kukamilika iliwazuia kufanya mambo yenye walikusudia kufanya. Kwa mufano, usiku wenye ulitangulia kifo cha Yesu, Petro, Yakobo, na Yohana walishindwa kukesha pamoja na Yesu, kama vile alikuwa amewaomba wafanye. Yesu alitambua kama “kwa kweli, roho inataka lakini mwili ni muzaifu.” (Mt. 26:40, 41) Yesu hakuwakasirikia kwa sababu alielewa kama hawakukuwa wakamilifu.

Mandy ni dada mwenye alikuwa anachambua-chambua wengine, lakini leo anajikaza sana kufuata mufano wa Yesu wa upole. Anasema hivi: “Ninajikaza kuelewa kama wanadamu wote hawakamilike na ninajikaza kuona sifa za muzuri za wengine, kama vile Yehova anafanyaka.” Yesu alielewa uzaifu wa wanadamu; jambo hilo haliwezi kukusaidia pia kutendea wengine kwa upole?

Yesu aliacha mambo katika mikono ya Mungu. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, alivumilia kutendewa bila haki. Watu walimuelewa mubaya, walimuzarau, na kumutesa. Lakini, aliendelea kuonyesha tabia ya upole kwa sababu “alijitia katika mikono ya Ule mwenye anahukumu kwa haki.” (1 Pe. 2:23) Yesu alijua kama Baba yake wa mbinguni angemusaidia kuvumilia na kama angemaliza ukosefu wa haki kwa wakati wenye kufaa.

Kama tunatendewa bila haki na tunajaribu kutenda kwa ukali, tunaweza kufanya hali ikuwe mubaya zaidi. Njo maana maandiko inatukumbusha kama “kasirani ya mwanadamu haitokeze haki ya Mungu.” (Yak. 1:20) Hata wakati tuko na sababu ya kukasirika, hali yetu ya kukosa kukamilika inaweza kutufanya tutende kwa njia ya mubaya.

Dada mumoja mu inchi ya Ujerumani mwenye kuitwa Cathy alikuwa anawaza hivi: ‘Kama haujitetee, hakuna mutu mwenye atakutetea.’ Lakini wakati alijifunza kumutegemea Yehova, alibadilisha mawazo yake. Anasema hivi: “Sione tena kama ni lazima kujitetea. Niko tayari kuonyesha sifa ya upole, kwa sababu ninajua kama Yehova anaona mambo yote.” Kama umekwisha kutendewa bila haki, kufuata mufano wa Yesu wa kumutegemea Mungu kutakusaidia uendelee kuwa mupole.

“WENYE FURAHA NI WALE WENYE TABIA YA UPOLE”

Namna gani upole unatusaidia katika hali ngumu kama hizi?

Yesu alionyesha kama, ikiwa tunapenda kuwa wenye furaha, tunapaswa kuwa wapole. Alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye tabia ya upole.” (Mt. 5:5) Ona namna sifa ya upole inasaidia katika hali zenye kufuata.

Upole unasaidia kumaliza matatizo katika ndoa. Ndugu Robert, wa Australia anasema hivi: “Nimemuambia bibi yangu maneno mingi yenye kuumiza yenye sikukusudia kusema. Lakini, wakati mutu anasema maneno makali kwa sababu ya kasirani, hawezi kuirudisha. Nilijisikia mubaya sana wakati niliona namna nilimuumiza sana.”

“Sisi wote tunajikwaa mara nyingi” katika kusema, na maneno yenye tunasema bila kufikiri inaweza kuvuruga amani katika ndoa. (Yak. 3:2) Kama hali hiyo inatokea, upole unatusaidia kuendelea kutulia na kuzuia ulimi wetu.​—Mez. 17:27.

Robert alijikaza sana ili kuwa na sifa ya utulivu na kujizuia. Kufanya vile kumemusaidia namna gani? Anasema hivi: “Leo, kama tunakosa kuelewana, ninajikaza sana kusikiliza kwa uangalifu, kusema kwa upole, na ninajikaza sana ili nisikasirike. Uhusiano wangu pamoja na bibi yangu umekuwa muzuri zaidi.”

Upole unatusaidia kusikilizana na watu wengine. Watu wenye kukasirika haraka-haraka hawana marafiki wengi. Lakini, upole unatusaidia “kuendeleza . . . kifungo chenye kuunganisha cha amani.” (Efe. 4:2, 3) Cathy, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Upole umenisaidia nifurahie kuwa na watu wengine, hata kama ni nguvu kusikilizana na watu fulani.”

Upole unatusaidia kuwa na amani ya moyo. Biblia inaonyesha kama kuko upatano kati ya “hekima yenye inatoka juu” na upole na amani. (Yak. 3:13, 17) Mutu mupole iko na “moyo mutulivu.” (Mez. 14:30) Martin, mwenye amejikaza sana ili kukomalisha sifa ya upole, anasema hivi: “Sasa silazimishe tena wengine wafuate mawazo yangu, na niko na amani ya moyo na furaha zaidi.”

Kwa kweli, inaweza kuomba tujikaze sana ili kukomalisha sifa ya upole. Ndugu mumoja anasema hivi: “Kusema kweli, mupaka leo ninasikiaka kasirani sana wakati fulani.” Lakini Yehova, mwenye anatutia moyo tujikaze kuendelea kuwa wapole, atatusaidia. (Isa. 41:10; 1 Ti. 6:11) Anaweza ‘kumaliza mazoezi yetu’; anaweza ‘kutufanya kuwa imara.’ (1 Pe. 5:10) Kisha wakati fulani, tunaweza kuiga “upole na fazili za Kristo” kama vile mutume Paulo alifanya.​—2 Ko. 10:1.

^ fu. 2 Majina fulani imebadilishwa.