Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho

Wafalme Wenye Kushindana Katika Wakati wa Mwisho

Unabii fulani wenye kuonyeshwa katika muchoro huu unazungumuzia matukio yenye ilitokea wakati uleule. Unabii huo wote unaonyesha kama tunaishi “wakati wa mwisho.”​—Da. 12:4.

  • Maandiko Ufu. 11:7; 12:13, 17; 13:1-8, 12

    Unabii “Munyama wa pori” ametawala dunia kwa maelfu ya miaka. Katika wakati wa mwisho, kichwa chake cha saba kinaumizwa. Kisha, kichwa chake kinapona na “dunia yote” inafuata ule munyama. Shetani anatumia ule munyama ili “kupigana vita na wale wenye kubakia.”

    Utimizo Kisha Garika, serikali zenye kumupinga Yehova zinatokea. Kisha miaka mingi, wakati wa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, serikali ya Uingereza inakuwa zaifu sana. Inapata nguvu tena wakati inajiunga na Inchi ya Amerika. Zaidi sana wakati wa mwisho, Shetani anatumia serikali zote za dunia ili kutesa watu wa Mungu.

  • Maandiko Da. 11:25-45

    Unabii Mufalme wa kaskazini na mufalme na kusini wanapigania mamlaka wakati wa mwisho.

    Utimizo Ujerumani inapigana na Uingereza na Amerika. Mu mwaka wa 1945, Muungano wa Sovieti na inchi zenye kuunga mukono muungano huo zinakuwa mufalme wa kaskazini. Mu mwaka wa 1991, Muungano wa Sovieti unaanguka, na kisha, serikali ya Urusi na inchi zenye kuiunga mukono zinakuwa mufalme wa kaskazini.

  • Maandiko Isa. 61:1; Mal. 3:1; Lu. 4:18

    Unabii Yehova anatuma “mujumbe” wake ili ‘afungue njia’ mbele Ufalme wa Kimasiya usimamishwe. Ule “mujumbe” anaanza ‘kutangazia wapole habari njema.’

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870, Russell na wenzake wanatumika kwa bidii ili kufasiria watu kweli za Biblia. Katika miaka ya 1880, wanaanza kukazia kama watumishi wa Mungu wanapaswa kuhubiri. Wanachapisha habari kama vile “Wahubiri 1 000 Wanahitajiwa” na “Mumetiwa Mafuta ili Kuhubiri.”

  • Maandiko Mt. 13:24-30, 36-43

    Unabii Mutu fulani anapanda ngano mu shamba. Kisha, adui fulani anapanda magugu mu shamba hilo. Magugu inakomaa na kufunika ngano. Wakati wa mavuno, magugu inatenganishwa na ngano.

    Utimizo Kuanzia mwaka wa 1870, tofauti kati ya Wakristo wa kweli na Wakristo wa uongo inaanza kuonekana wazi zaidi na zaidi. Katika wakati wa mwisho, Wakristo wa kweli wanakusanywa na kutenganishwa na Wakristo wa uongo.

  • Maandiko Da. 2:31-33, 41-43

    Unabii Vikanyangio vya chuma na udongo vya sanamu ya munyama yenye kutengenezwa na metali mbalimbali.

    Utimizo Udongo unafananisha watu wa kawaida, wenye Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inatawala, wenye wanapinga serikali hiyo. Watu hao wanafanya serikali hiyo ikuwe zaifu na ishindwe kutawala kwa mamlaka yenye kuwa nguvu kama chuma.

  • Maandiko Mt. 13:30; 24:14, 45; 28:19, 20

    Unabii “Ngano” inakusanywa mu “depo” na “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anawekwa juu ya “watumishi wa nyumbani.” Kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” inaanza kufanywa katika “dunia yote yenye kuikaliwa na watu.”

    Utimizo Mu mwaka wa 1919, mutumwa muaminifu anawekwa ili asimamie watu wa Mungu. Kuanzia wakati huo, Wanafunzi wa Biblia wanahubiri kwa bidii sana. Leo, Mashahidi wa Yehova wanahubiri mu inchi zaidi ya 200 na wanachapisha vichapo vyenye kutegemea Biblia mu luga zaidi ya 1 000.

  • Maandiko Da. 12:11; Ufu. 13:11, 14, 15

    Unabii Munyama wa pori mwenye pembe mbili anaambia watu wafanye “sanamu ya munyama wa pori,” na anapatia “pumuzi ile sanamu.”

    Utimizo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika inaanzisha Ushirika wa Mataifa. Mataifa ingine inaunga mukono ushirika huo. Kisha, mufalme wa kaskazini anajiunga pia na Ushirika wa Mataifa, lakini ni kuanzia tu mwaka wa 1926 mupaka mwaka wa 1933. Watu waliamini kama Ushirika wa Mataifa njo utaleta amani mu dunia, jambo lenye Ufalme wa Mungu tu njo unaweza kufanya. Na wanaamini vile pia kuhusu Umoja wa Mataifa wenye ulianzishwa kisha.

  • Maandiko Da. 8:23, 24

    Unabii Mufalme mwenye kuonekana kuwa mukali analeta “uharibifu kwa njia ya ajabu.”

    Utimizo Serikali Kubwa ya Ulimwengu ya Uingereza na Amerika imeua watu wengi na kuleta uharibifu mukubwa. Kwa mufano, wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Inchi ya Amerika ilileta uharibifu mukubwa sana kuliko uharibifu wowote wenye ulikuwa umekwisha kutokea wakati iliangusha bombe mbili za atomu juu ya taifa lenye lilikuwa adui wa Uingereza na Amerika.

  • Maandiko Da. 11:31; Ufu. 17:3, 7-11

    Unabii Munyama “mwenye rangi nyekundu yenye kungaa” mwenye kuwa na pembe kumi anatoka mu abiso na yeye njo mufalme wa munane. Kitabu cha Danieli kinaita ule mufalme kuwa “chukizo lenye linaleta uharibifu.”

    Utimizo Ushirika wa Mataifa unaacha kufanya kazi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Kisha vita hiyo, Umoja wa Mataifa ‘unasimamishwa’ ao unaundwa. Watu waliamini kama Umoja wa Mataifa njo utaleta amani mu dunia, jambo lenye Ufalme wa Mungu njo unaweza kufanya. Ni vile pia waliamini kuhusu Ushirika wa Mataifa wenye ulikuwa mbele yake. Umoja wa Mataifa utashambulia dini.

  • Maandiko 1 Te. 5:3; Ufu. 17:16

    Unabii Mataifa inatangaza “amani na usalama,” na “zile pembe kumi” na “ule munyama wa pori” wanashambulia “ule kahaba” na kumuharibu. Kisha, mataifa yote inaharibiwa.

    Utimizo Mataifa itasema kama imeleta amani na usalama mu dunia. Kisha, mataifa yenye kuunga mukono Umoja wa Mataifa itaharibu matengenezo ya dini za uongo. Tukio hilo litakuwa mwanzo wa taabu kubwa. Ile taabu itamalizika wakati Yesu ataharibu ulimwengu wote wa Shetani ku Armagedoni.

  • Maandiko Eze. 38:11, 14-17; Mt. 24:31

    Unabii Gogu anashambulia inchi ya watu wa Mungu. Kisha, malaika wanakusanya wale “wenye kuchaguliwa.”

    Utimizo Mufalme wa kaskazini na serikali zingine za dunia, wanashambulia watu wa Mungu. Wakati fulani kisha shambulizi hilo kuanza, mabaki ya watiwa-mafuta wanapelekwa mbinguni.

  • Maandiko Eze. 38:18-23; Da. 2:34, 35, 44, 45; Ufu. 6:2; 16:14, 16; 17:14; 19:20

    Unabii “Ule mwenye kukaa” juu ya “farasi mweupe” anakamilisha “ushindi wake” kwa kuharibu Gogu na jeshi lake. “Ule munyama wa pori” ‘anatupwa ndani ya ziwa la moto,’ na ile sanamu kubwa inapondwa-pondwa.

    Utimizo Yesu, Mufalme mwenye kutawala Ufalme wa Mungu, anakuja kuokoa watu wa Mungu. Yeye na watawala wenzake 144 000 na majeshi yake ya malaika, wanaharibu muungano wa mataifa. Huo utakuwa mwisho wa ulimwengu wa Shetani.