Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Angekubaliwa na Mungu

Angekubaliwa na Mungu

TUNAMUTUMIKIA Yehova na tunapenda atukubali na kutubariki. Lakini namna gani tunaweza kukubaliwa na Mungu? Wakati wa zamani, watu fulani wenye walikuwa wamefanya zambi nzito walikubaliwa tena na Mungu. Wengine walikuwa na sifa za muzuri lakini mwishowe Mungu hakuwakubali tena. Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: “Yehova anatafuta nini ndani ya kila mumoja wetu?” Mufano wa Rehoboamu, mufalme wa Yuda, unaweza kutusaidia kupata jibu.

MWANZO MUBAYA

Sulemani, baba ya Rehoboamu, alikuwa mufalme wa Israeli kwa miaka 40. (1 Fal. 11:42) Kisha baba yake kufa, Rehoboamu alifanya safari ya kutoka Yerusalemu na kuenda Shekemu ili akuwe mufalme. (2 Nya. 10:1) Aliogopa kuwa mufalme mupya wa Israeli? Sulemani alijulikana kwa sababu ya hekima yake nyingi. Bila kukawia, Rehoboamu angepaswa kuonyesha kama alikuwa na hekima kabisa ili kushugulikia tatizo kubwa.

Waisraeli waliona kama waliteswa na walituma wajumbe ili wamuambie Rehoboamu mambo yenye walipenda afanye, walisema hivi: ‘Baba yako aliifanya nira yetu kuwa ngumu; na sasa wewe ufanye ule utumishi mugumu wa baba yako na ile nira nzito aliyoweka juu yetu kuwa rahisi, nasi tutakutumikia.’​—2 Nya. 10:3, 4.

Rehoboamu alipaswa kukamata uamuzi muzito. Ikiwa angefanya mambo yenye watu waliomba, yeye na familia yake na wale wenye waliishi katika nyumba ya mufalme wangelazimika kuishi bila vitu fulani vya hali ya juu vyenye walikuwa wamezoea. Lakini, ikiwa angekataa ombi la watu, wangeweza kumuasi. Alifanya nini? Alizungumuza kwanza na wanaume wazee wenye walitumika pamoja na baba yake. Walimuambia asikilize watu. Lakini, kisha Rehoboamu alizungumuza na vijana wa miaka yake na aliamua kutendea watu kwa ukali. Aliambia watu hivi: ‘Nitaifanya nira yenu ikuwe nzito zaidi, nami nitaizidisha. Baba yangu aliwatia ninyi adabu kwa fimbo, lakini mimi nitawatia adabu kwa mijeledi.’​—2 Nya. 10:6-14.

Hilo linaweza kutufundisha nini? Leo tuko na ndugu na dada wengi wenye kukomaa wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi na wenye wanaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. Tukuwe basi na hekima na kuwasikiliza.​—Ayu. 12:12.

‘WALITII NENO LA YEHOVA’

Kisha, Rehoboamu alikusanya jeshi lake ili kupigana na makabila yenye yaliasi. Lakini, Yehova alituma nabii Shemaya ili awaambia hivi: ‘Musipande kuenda kupigana na ndugu zenu wana wa Israeli. Murudi kila mumoja nyumbani kwake, kwa maana jambo hili limetokea kwa muongozo wangu.’​—1 Fal. 12:21-24. *

Ilikuwa mwepesi kwa Rehoboamu kumusikiliza Yehova? Watu wangefikiri nini juu ya mufalme wao mupya? Alikuwa amesema kama angewatia adabu “kwa mijeledi,” lakini sasa hangefanya kitu juu ya uasi huo mubaya sana! (Linganisha na 2 Mambo ya Nyakati 13:7.) Lakini, hata kama watu walifikiri mambo gani juu yake, mufalme na jeshi lake ‘walitii neno la Yehova, wakarudi nyumbani kulingana na neno la Yehova.’

Hilo linatufundisha nini? Sikuzote ni jambo la hekima kumutii Mungu hata kama watu wanatucheka kwa sababu ya kufanya hivyo. Mungu atatubariki sikuzote ikiwa tunamutii.​—Kum. 28:2.

Rehoboamu alibarikiwa kwa sababu alitii? Ndiyo. Rehoboamu aliendelea kutawala makabila ya Yuda na Benyamini, na aliamua kujenga miji ya mupya katika maeneo hayo. Alifanya pia miji fulani ikuwe yenye nguvu “kwa kiwango kikubwa sana.” (2 Nya. 11:5-12) Na jambo la maana zaidi ni kwamba kwa wakati fulani alitii sheria za Yehova. Kwa sababu katika Ufalme wa makabila kumi watu walianza kuabudu sanamu, watu wengi walifanya safari ya kuenda Yerusalemu ili kuunga mukono Rehoboamu na ibada ya kweli. (2 Nya. 11:16, 17) Kwa hiyo, kwa sababu Rehoboamu alimutii Yehova, ufalme wake ulifikia kuwa wenye nguvu zaidi.

REHOBOAMU ANATENDA ZAMBI NA ANATUBU

Wakati ufalme wa Rehoboamu ulikuwa wenye nguvu, alifanya jambo fulani la mubaya. Aliacha kutii sheria za Yehova na akaanza kuabudu miungu ya uongo! Sababu gani? Mama yake mwenye alikuwa Muamoni alichochea uamuzi wake? (1 Fal. 14:21) Hatujue, lakini taifa lote lilifuata mufano wake mubaya. Kwa hiyo, Yehova aliruhusu Mufalme Shishaki wa Misri akamate miji mingi ya Ufalme wa Yuda. Jambo hilo lilitokea hata kama Rehoboamu alikuwa amefanya miji hiyo ikuwe yenye nguvu!​—1 Fal. 14:22-24; 2 Nya. 12:1-4.

Hali iliharibika zaidi wakati Shishaki na jeshi lake walikuja kushambulia Yerusalemu, kwenye Rehoboamu alikuwa anatawala. Wakati huo, nabii Shemaya alipatia Rehoboamu na wakubwa wake ujumbe huu kutoka kwa Mungu: ‘Ninyi mumeniacha mimi, nami pia nimewaacha ninyi mukononi mwa Shishaki.’ Rehoboamu alitenda namna gani juu ya nizamu hiyo? Alitenda muzuri sana! Biblia inasema hivi: “Wakubwa wa Israeli na mufalme wakajinyenyekeza na kusema: ‘Yehova ni muadilifu.’” Kwa hiyo, Yehova akamuokoa Rehoboamu na Yerusalemu haikuharibiwa tena.​—2 Nya. 12:5-7, 12.

Kisha hapo, Rehoboamu akaendelea kutawala ufalme wa Yuda. Mbele akufe, alipatia wana wake zawadi nyingi. Pengine alipenda kuhakikisha kama hawataasi ndugu yao Abiya, mwenye angekuwa mufalme mupya. (2 Nya. 11:21-23) Kwa kufanya hivyo, Rehoboamu alitenda kwa hekima zaidi kuliko wakati alikuwa kijana.

REHOBOAMU ALIKUWA MUTU MUZURI AO MUBAYA?

Hata kama Rehoboamu alifanya mambo fulani ya muzuri, Biblia inasema hivi juu ya utawala wake: “Alifanya yaliyokuwa mabaya.” Sababu gani? Kwa sababu ‘hakuwa ameufanya imara moyo wake ili kumutafuta Yehova.’ Kwa hiyo, Yehova hakumufurahia.​—2 Nya. 12:14.

Tofauti na Daudi, Rehoboamu hakukuwa na urafiki wenye nguvu pamoja na Yehova

Maisha ya Rehoboamu yanaweza kutufundisha nini? Wakati fulani alimutii Mungu. Na alifanyia watu wa Yehova mambo fulani ya muzuri. Lakini hakukuwa na urafiki wa sana pamoja na Yehova, hakukuwa na tamaa yenye nguvu ya kumupendeza. Kwa hiyo, aliacha kufanya mambo ya muzuri na akaanza kuabudu miungu ya uongo. Unaweza kujiuliza hivi: ‘Wakati Rehoboamu alikubali Yehova amurekebishe, ilikuwa kwa sababu alihuzunika kabisa juu ya makosa yake na alitaka kumupendeza? Ao ni kwa sababu wengine walimuambia kuwa alipaswa kufanya hivyo?’ (2 Nya. 11:3, 4; 12:6) Kisha alifikia tena kufanya mambo ya mubaya katika maisha yake. Alikuwa tofauti kabisa na tate (nkambo) yake Mufalme Daudi! Ni kweli kwamba Daudi alifanya makosa. Lakini, Daudi alitubu kwa moyo wake wote zambi zenye alikuwa amefanya. Na alipenda Yehova na ibada ya kweli katika maisha yake yote.​—1 Fal. 14:8; Zab. 51:1, 17; 63:1.

Habari hii yenye kuwa katika Biblia inaweza kutufundisha mambo mengi. Wakati watu wanatimiza mahitaji ya familia zao na wanatendea wengine mambo ya muzuri, wanastahili pongezi. Lakini ili Yehova atukubali tunapaswa kumuabudu katika njia yenye kumupendeza, na tunapaswa kuwa na urafiki wenye nguvu pamoja naye.

Ili kufikia muradi huo, tunapaswa kuwa na upendo wenye nguvu kwa Yehova. Kama tu vile tunafanya moto uendelee kuwaka kwa kuongeza kuni, tunafanya upendo wetu kwa Mungu uendelee kuongezeka kwa kujifunza neno lake kwa ukawaida, kutafakari juu ya Neno hilo, na kuendelea kusali. (Zab. 1:2; Rom. 12:12) Na upendo huo utatuchochea kumupendeza Yehova katika mambo yote yenye tunafanya. Utatuchochea pia kuhuzunika kabisa wakati tunafanya makosa na kuomba Yehova atusamehe. Ikiwa tunafanya hivyo, hatutakuwa kama Rehoboamu lakini tutabakia waaminifu kwa ibada ya kweli.​—Yuda 20, 21.

^ fu. 9 Kwa sababu Sulemani hakukuwa muaminifu, Mungu alikuwa amesema kama ufalme ungegawanyika mara mbili.​—1 Fal. 11:31.