Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

‘Muache Nuru Yenu Iangaze’ ili Kumutukuza Yehova

‘Muache Nuru Yenu Iangaze’ ili Kumutukuza Yehova

‘Muache nuru yenu iangaze mbele ya watu, ili . . . wamupe utukufu Baba yenu.’​—MT. 5:16.

NYIMBO: 77, 59

1. Tuko na sababu gani ya pekee ya kuwa na furaha?

TUNAFURAHI kusikia namna watu wa Mungu wanaacha nuru yao iangaze! Mwaka jana, watu wa Yehova waliongoza mafunzo ya Biblia zaidi ya 10 000 000. Na mamilioni ya watu wenye kupendezwa walikuja kwenye ukumbusho na walijifunza juu ya zawadi ya zabihu ya ukombozi yenye Yehova alitutolea kwa upendo.​—1 Yoh. 4:9.

2, 3. (a) Ni mambo gani yenye hayatuzuie ‘kuangaza kama mianga’? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Katika dunia yote, Mashahidi wa Yehova wanazungumuza luga nyingi mbalimbali. Lakini hilo halituzuie kumusifu Yehova kama familia moja yenye umoja. (Ufu. 7:9) Hata kama tunazungumuza luga gani ao tunaishi wapi, tunaweza kuangaza “kama mianga katika ulimwengu.”​—Flp. 2:15.

3 Kazi yetu ya kuhubiri, umoja wetu wa Kikristo, na kuona lazima ya kutenda kwa haraka, mambo hayo yote yanamuletea Yehova utukufu. Namna gani tunaweza kuacha nuru yetu iangaze katika njia hizo tatu?​—Soma Mathayo 5:14-16.

USAIDIE WENGINE WAMUABUDU YEHOVA

4, 5. (a) Zaidi ya kufanya kazi ya kuhubiri, namna gani tunaweza kuacha nuru yetu iangaze? (b) Tunapata matokeo gani ya muzuri wakati tunatendea watu kwa wema? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

4 Kuhubiri na kufanya wanafunzi ni njia ya maana ya kuacha nuru yetu iangaze. (Mt. 28:19, 20) Gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 1 Mwezi wa 6, 1925, lilikuwa na habari yenye kichwa “Nuru Katika Giza.” Habari hiyo ilisema kama katika siku za mwisho, hakuna mutu mwenye angekuwa muaminifu kwa Bwana ikiwa hachukue “nafasi ya kuacha nuru yake iangaze.” Kisha ilisema hivi: “Anapaswa kufanya hivyo kwa kuambia watu wa dunia juu ya habari njema, na kwa kujipatanisha na njia za nuru.” Zaidi ya kufanya kazi ya kuhubiri, mwenendo wetu pia unamuletea Yehova utukufu. Watu wengi wanatuangalia wakati tunahubiri. Wakati tunawaonyesha sura ya kicheko na kuwasalimia kwa furaha, hilo linawasaidia wakuwe na mawazo ya muzuri juu yetu na juu ya Mungu mwenye tunaabudu.

5 Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Munapoingia ndani ya nyumba, muwape salamu watu wa nyumba hiyo.’ (Mt. 10:12) Katika eneo kwenye Yesu alihubiri, watu walikuwa na desturi ya kuingiza watu wenye hawajue katika nyumba zao. Katika maeneo mengi leo, watu hawana tena desturi hiyo. Mara nyingi watu wanakuwa na wasiwasi ao wanakasirika wakati wanaona kwenye mulango wao mutu mwenye hawajue. Lakini, ikiwa tunatendea wengine kwa urafiki na wema wanaweza kujisikia muzuri zaidi. Wakati unahubiri mahali pa watu wengi kwa kutumia chombo cha kuwekea vichapo, unaweza kuona kama ikiwa unaonyesha watu sura ya kicheko na kuwasalimia kwa njia ya urafiki, watajisikia huru zaidi kuja na kukamata kichapo. Wanaweza hata kuwa tayari kuzungumuza na sisi!

6. Ni nini inasaidia bibi na bwana fulani wenye kuzeeka waendelee kufanya kazi ya kuhubiri?

6 Bibi na bwana fulani wenye kuzeeka katika inchi ya Uingereza, hawawezi tena kuhubiri nyumba kwa nyumba kama zamani kwa sababu afya yao imeharibika. Kwa hiyo, wanaweka meza yenye kuwa na vichapo inje ya nyumba yao. Wanaishi karibu na masomo; kwa hiyo, wanaweka vichapo vyenye vitafurahisha wazazi wenye wanakuja kukamata watoto wao. Wazazi fulani wamekamata vichapo hivyo, kutia ndani kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1 na la 2. Mara kwa mara dada mumoja painia anajiunga na bibi na bwana hao. Wazazi wanatambua kama painia huyo ni mwenye kuchangamukia watu na kama bibi na bwana hao wanapenda kabisa kusaidia wengine. Muzazi mumoja ameanza hata kujifunza Biblia.

7. Namna gani unaweza kusaidia wakimbizi katika eneo lenu?

7 Hivi karibuni, watu wengi wamelazimika kukimbia inchi yao, na sasa wanaishi kama wakimbizi katika inchi zingine. Unaweza kufanya nini ili kusaidia wakimbizi wenye kuwa katika eneo lenu wajifunze juu ya Yehova? Kwanza, unaweza kujifunza namna ya kuwasalimia katika luga yao. Zaidi ya hilo, kwa kutumia programu ya JW Language, unaweza kujifunza misemo fulani yenye inaweza kuwachochea wakuwe tayari kuzungumuza na wewe. Kisha unaweza kuwaonyesha video na vichapo vyenye kuwa katika luga yao kwenye jw.org.​—Kum. 10:19.

8, 9. (a) Namna gani mikutano yetu ya katikati ya juma inatusaidia? (b) Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao watoe maelezo ya muzuri zaidi kwenye mikutano?

8 Yehova anatupatia mambo yenye tuko nayo lazima kabisa ili tupate matokeo ya muzuri wakati tunahubiri. Kwa mufano, mambo yenye tunajifunza kwenye Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo, yanatusaidia tukuwe na uhakika zaidi wakati tunarudilia watu na kuanzisha mafunzo ya Biblia.

9 Wakati wageni wanakuja kwenye mikutano yetu, mara nyingi wanashangazwa na maelezo yenye watoto wetu wanatoa. Unaweza kufundisha watoto wako kutoa maelezo katika maneno yao wenyewe. Watu fulani walifikia kukubali kweli wakati walisikia namna watoto wanaeleza imani yao kwa njia yenye kuwa mwepesi na kwa moyo wote.​—1 Kor. 14:25.

TUTIE NGUVU UMOJA WETU

10. Namna gani ibada ya familia inaweza kusaidia familia zikuwe na umoja zaidi?

10 Wakati tunajikaza sana ili kusaidia familia yetu itumike pamoja kwa umoja na amani, tunamuletea Yehova utukufu. Kwa mufano, ikiwa wewe ni muzazi, ufanye mipango ya kufanya Ibada ya Familia kwa ukawaida. Familia nyingi zinaangalia JW Télédiffusion pamoja, na kisha wanazungumuzia namna wanaweza kutumikisha mambo yenye wamejifunza. Kumbuka kama muongozo wenye mutoto mudogo iko nao lazima ni tofauti na muongozo wenye kijana iko nao lazima. Fanya nguvu yako yote ili kusaidia kila mutu katika familia yako afaidike kabisa na ibada ya familia.​—Zab. 148:12, 13.

Ni muzuri kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada wenye kuzeeka (Picha hii inapatana na fungu la 11)

11-13. Namna gani tunaweza kusaidia kutaniko letu likuwe na umoja zaidi?

11 Hata kama uko kijana, unaweza kusaidia kufanya kila mutu katika kutaniko ajione kuwa wa maana. Njia moja ni kwa kufanya urafiki pamoja na ndugu na dada wenye kuzeeka. Uwaulize ni nini imewasaidia waendelee kumutumikia Yehova kwa miaka mingi. Wanaweza kukufundisha mambo mengi ya maana sana. Hilo litawatia moyo na litakutia moyo wewe pia! Na sisi wote, iwe tuko vijana ao wazee, tunaweza kusaidia wageni wajisikie kuwa wamekaribishwa kwenye Jumba la Ufalme. Unaweza kuwasalimia, kuwaonyesha sura ya kicheko, kuwasaidia wapate nafasi ya kukaa, na kuwatambulisha kwa wengine. Uwasaidie wajisikie kuwa nyumbani.

12 Ikiwa unapewa mugao wa kuongoza mukutano kwa ajili ya mahubiri, unaweza kusaidia wale wenye kuzeeka wafanye nuru yao iendelee kuangaza. Hakikisha kama unawapatia eneo lenye kufaa. Upange vijana wahubiri pamoja na wale wenye kuzeeka. Mara nyingi ndugu na dada wenye kuzeeka na wale wenye kuwa na matatizo ya afya wanavunjika moyo kwa sababu hawawezi kuhubiri sana kama zamani. Lakini watajisikia muzuri zaidi wakati wanajua kama unawahangaikia na unaelewa hali yao. Hata iwe wako na miaka ngapi ao wamefanya miaka ngapi katika kweli, ikiwa unawatendea kwa wema hilo linaweza kuwatia moyo waendelee kuhubiri kwa bidii.​— Law. 19:32.

13 Waisraeli walifurahia kumuabudu Yehova pamoja. Muandikaji mumoja wa zaburi alisema hivi: “Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza ndugu kukaa pamoja kwa umoja!” (Soma Zaburi 133:1, 2.) Alilinganisha umoja huo na mafuta ya kupakaa yenye kuregeza ngozi na yenye kuwa na harufu ya muzuri. Vilevile tunaweza kusaidia ndugu na dada zetu wajisikie muzuri kwa kuwatendea kwa upendo na kuwahangaikia. Hilo linafanya kutaniko likuwe na umoja zaidi. Unaweza kujikaza kujua muzuri zaidi ndugu na dada katika kutaniko lako?​—2 Kor. 6:11-13.

14. Namna gani unaweza kuacha nuru yako iangaze katika eneo kwenye unaishi?

14 Nuru yako inaweza kuangaza hata kama unaishi wapi. Wema wako unaweza kuchochea majirani wako wakuwe tayari kujifunza mengi zaidi juu ya Yehova. Ujiulize hivi: ‘Majirani wangu wako na mawazo gani juu yangu? Nyumba yangu na kiwanja changu viko safi? Vinafanya mahali kwenye ninaishi kuonekane muzuri? Ninasaidia majirani wangu?’ Uliza Mashahidi wengine namna wema wao na mufano wao muzuri vimekuwa na matokeo ya muzuri juu ya watu wa jamaa yao, majirani wao, wafanyakazi wenzao, ao wanafunzi wenzao.​—Efe. 5:9.

ENDELEA KUKESHA

15. Sababu gani tunapaswa kuendelea kukesha?

15 Ikiwa tunapenda nuru yetu iendelee kuangaza, tunapaswa kutambua wakati wenye tunaishi. Yesu aliambia mara nyingi wanafunzi wake hivi: ‘Muendelee kukesha.’ (Mt. 24:42; 25:13; 26:41) Ikiwa tunafikiri kama ‘ziki kubwa’ ingali mbali, hatutatumia kila nafasi yenye kujitokeza ili kusaidia wengine wajifunze juu ya Yehova. (Mt. 24:21) Kuliko kuangaza zaidi, nuru yetu itapunguka pole kwa pole na inaweza hata kupotea.

16, 17. Unaweza kufanya nini ili uendelee kuona kama ni jambo la lazima kutenda kwa haraka?

16 Tunapaswa kuendelea kukesha wakati huu kuliko wakati mwingine wowote wenye umepita. Hali za ulimwengu huu zinaendelea kuharibika zaidi. Lakini tunajua kama mwisho utakuja wakati uleule wenye Yehova ameweka. (Mt. 24:42-44) Mbele wakati huo ufike, tunapaswa kungojea na kukaza akili yetu juu ya wakati wetu wenye kuja. Soma Biblia kila siku, na usiache hata kidogo kusali kwa Yehova. (1 Pet. 4:7) Ujifunze mambo fulani kupitia mifano ya ndugu na dada wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi. Kwa mufano unaweza kusoma habari juu ya maisha ya watu, kama vile habari yenye kichwa, “Nilishika Upindo wa Nguo ya Muyahudi kwa Miaka Zaidi ya 70,” yenye ilitolewa katika gazeti Munara wa Mulinzi la tarehe 15 Mwezi wa 4, 2012, ukurasa wa 18-21.

17 Uendelee kuwa na mambo mengi ya kufanya katika utumishi wa Yehova. Ufanyie watu mambo ya muzuri, na upitishe wakati pamoja na ndugu na dada zako. Kisha utakuwa na furaha, na itaonekana kuwa wakati inapita haraka. (Efe. 5:16) Watumishi wa Yehova wamefanya mambo mengi kwa miaka mia moja yenye imepita. Na leo, tuko na mambo mengi zaidi ya kufanya kuliko wakati mwingine wowote. Kazi ya Yehova imeongezeka sana kuliko namna tungewazia. Nuru yetu inaangaza kabisa!

Wakati wazee wanatutembelea, tunaweza kufaidika na hekima ya Mungu (Picha hii inapatana na fungu la 18, 19)

18, 19. Namna gani wazee wanaweza kutusaidia tumutumikie Yehova kwa bidii? Toa mufano.

18 Hata kama tunafanya makosa mengi, Yehova anaturuhusu tumutumikie. Ili kutusaidia anatutolea “zawadi katika wanadamu,” ni kusema, wazee wa kutaniko. (Soma Waefeso 4:8, 11, 12.) Kwa hiyo, wakati wazee wanakutembelea, tumia nafasi yenye unapitisha pamoja nao ili kujifunza mambo fulani kupitia hekima yao na mashauri yao.

19 Kwa mufano, bibi na bwana fulani katika Uingereza walikuwa na matatizo katika ndoa yao, na waliomba wazee musaada. Bibi aliona kama bwana yake hakukuwa anatimiza daraka lake la kichwa cha familia katika mambo ya kiroho. Bwana aliona kama hakukuwa mwalimu muzuri na alikubali kama hakukuwa anafanya ibada ya familia kwa ukawaida. Wazee walisaidia bibi na bwana hao wafikirie mufano wa Yesu. Walitia bwana moyo aige mufano wa Yesu mwenye alihangaikia wanafunzi wake. Walitia moyo bibi avumilie bwana yake. Waliwatolea pia mapendekezo juu ya namna wanaweza kufanya ibada ya familia pamoja na watoto wao wawili. (Efe. 5:21-29) Bwana alijikaza sana kutimiza muzuri daraka lake la kichwa cha familia. Wazee walimutia moyo asichoke na aendelee kutegemea roho ya Yehova. Upendo na wema wenye wazee walionyesha vilisaidia kabisa familia hiyo!

20. Kuacha nuru yako iangaze kutaleta matokeo gani?

20 ‘Mwenye furaha ni kila mutu anayemuogopa Yehova. Anayetembea katika njia zake.’ (Zab. 128:1) Utakuwa na furaha wakati utaacha nuru yako iangaze. Kwa hiyo, ufundishe wengine juu ya Mungu, ujikaze kusaidia umoja ukuwe katika familia yako na katika kutaniko lenu, na uendelee kukesha. Wengine wataona mufano wako muzuri na watakuwa tayari kumutukuza Baba yetu, Yehova.​—Mt. 5:16.