Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sisi Wote Tukuwe na Umoja Kama Vile Yehova na Yesu Wako na Umoja

Sisi Wote Tukuwe na Umoja Kama Vile Yehova na Yesu Wako na Umoja

‘Ninawaombea . . . wote wapate kuwa kitu kimoja, kama vile ambavyo wewe, Baba, uko katika muungano pamoja na mimi.’​—YOH. 17:20, 21.

NYIMBO: 24, 99

1, 2. (a) Yesu aliomba nini katika sala yake ya mwisho pamoja na mitume wake? (b) Sababu gani pengine Yesu alikuwa na mahangaiko juu ya umoja?

WAKATI wa chakula cha mangaribi cha mwisho pamoja na mitume wake, Yesu alikuwa na mahangaiko juu ya umoja. Wakati alikuwa anasali pamoja nao, alisema kama alipenda wanafunzi wake wakuwe mumoja ao wakuwe na umoja, kama vile yeye na Baba yake wako na umoja. (Soma Yohana 17:20, 21.) Ikiwa wanafunzi wa Yesu wangekuwa na umoja, hilo lingehakikishia watu wengine kama Yehova alikuwa ametuma Yesu katika dunia. Watu wangetambua wanafunzi wa kweli wa Yesu kupitia upendo kati yao, na upendo huo ungewafanya wakuwe na umoja zaidi.​—Yoh. 13:34, 35.

2 Tunaweza kuelewa sababu gani usiku huo Yesu alizungumuzia sana umoja. Alikuwa ametambua kama mitume wake hawakukuwa na umoja kabisa-kabisa. Kwa mufano, mitume walibishana juu ya ‘ni nani kati yao alionekana kuwa mukubwa zaidi ya wote,’ kama vile walikuwa wamefanya mbele ya hapo. (Lu. 22:24-27; Mk. 9:33, 34) Wakati mwingine, Yakobo na Yohana walikuwa wamemuomba Yesu awapatie vyeo vya hali ya juu katika Ufalme wa mbinguni, karibu naye.​—Mk. 10:35-40.

3. Pengine ni mambo gani yalizuia wanafunzi wa Yesu kuwa na umoja, na tutajibia maulizo gani?

3 Zaidi ya kupenda kuwa na cheo na mamlaka, kuko jambo lingine lenye lingezuia wanafunzi wa Kristo kuwa na umoja. Wakati wa Yesu, watu walikuwa wamegawanyika kwa sababu ya chuki na ubaguzi. Wanafunzi wa Yesu walipaswa kuachana na mawazo hayo ya mubaya. Katika habari hii, tutajibia maulizo haya: Yesu alitenda namna gani juu ya ubaguzi? Namna gani alisaidia wanafunzi wake wajifunze kutendea wengine bila ubaguzi, ao kwa haki, na kuwa na umoja? Na namna gani mufano wa Yesu na mambo yenye alifundisha yatatusaidia tuendelee kuwa na umoja?

WATU WALIBAGUA YESU NA WANAFUNZI WAKE

4. Yesu alipambana na ubaguzi gani? Toa mufano.

4 Watu walibagua Yesu pia. Wakati Filipo aliambia Nathanaeli kwamba alikuwa amepata Masiya, Nathanaeli alisema hivi: “Je, kitu chochote kilicho chema [kizuri] kinaweza kutoka Nazareti?” (Yoh. 1:46) Pengine Nathanaeli alijua kama Masiya angezaliwa Bethlehemu, kama vile unabii wa Mika 5:2 ulikuwa umesema. Inawezekana alifikiri kama Nazareti ulikuwa muji wa hali ya chini; kwa hiyo, Masiya hangeweza kutokea katika muji huo. Pia, kulikuwa Wayahudi fulani wenye mamlaka wenye walimuzarau Yesu kwa sababu alitoka Galilaya. (Yoh. 7:52) Wayahudi wengi walifikiri kama watu wa Galilaya walikuwa wa hali ya chini. Wayahudi wengine walijaribu kumutukana Yesu kwa kumuita Musamaria. (Yoh. 8:48) Taifa la Wasamaria lilikuwa tofauti na la Wayahudi, na dini yao ilikuwa tofauti pia na dini ya Wayahudi. Wayahudi na Wagalilaya hawakuheshimia kabisa Wasamaria na waliwaepuka.​—Yoh. 4:9.

5. Namna gani watu walibagua wanafunzi wa Yesu?

5 Viongozi wa dini ya Wayahudi walizarau pia wanafunzi wa Yesu. Mafarisayo waliwaita “watu waliolaaniwa.” (Yoh. 7:47-49) Mafarisayo waliona kama kila mutu mwenye hakusomea kwenye masomo za dini ya Wayahudi na mwenye hakufuata desturi zao, alikuwa mutu wa bure na wa kawaida. (Mdo. 4:13) Watu walibagua Yesu na wanafunzi wake kwa sababu wakati huo watu walikuwa wanajivunia dini yao, cheo chao, na taifa lao. Ubaguzi huo ulikuwa na matokeo ya mubaya juu ya wanafunzi na namna yao ya kuona wengine. Ili waendelee kuwa na umoja, walipaswa kubadilisha namna yao ya kufikiri.

6. Namna gani tunaweza kuambukizwa na ubaguzi? Toa mufano.

6 Leo, ulimwengu umejaa ubaguzi. Watu wanaweza kutubagua, ao tunaweza kubagua wengine kwa njia fulani. Dada mumoja mwenye kuwa sasa painia katika Australia anasema hivi: “Nilichukia zaidi wazungu wakati nilifikiri sana juu ya namna Waaborijini (wenyeji wa Australia), walitendewa bila haki zamani na hata leo.” Na chuki yake iliongezeka pia kwa sababu watu fulani walikuwa wamemutendea mubaya. Ndugu mumoja katika Kanada anaeleza namna alikuwa anawaza zamani. Anasema hivi: “Nilifikiri kama watu wenye kuzungumuza Kifaransa walikuwa watu wa maana zaidi.” Anasema kama hilo lilifanya asipende watu wenye kuzungumuza Kiingereza.

7. Yesu alitenda namna gani juu ya ubaguzi?

7 Kama wakati wa Yesu, leo mara nyingi mawazo ya ubaguzi ni yenye nguvu sana na haiko mwepesi kuyabadilisha. Yesu alitenda namna gani juu ya mawazo kama hayo? Kwanza, yeye mwenyewe hakuonyesha ubaguzi hata kidogo. Na hakukuwa na upendeleo hata kidogo. Alihubiria matajiri na maskini, Mafarisayo na Wasamaria, na hata wakusanya kodi na watenda zambi. Pili, Yesu alifundisha wanafunzi wake na aliwaonyesha kupitia mufano wake kama hawapaswe kuwa na mawazo ya mubaya juu ya wengine ao kuwaonyesha ubaguzi.

UACHANE NA UBAGUZI KWA KUONYESHA UPENDO NA UNYENYEKEVU

8. Ni kanuni gani yenye kuwa musingi wa umoja wetu? Eleza.

8 Yesu alifundisha kanuni ya maana yenye kuwa musingi wa umoja wetu. Aliambia wanafunzi wake hivi: “Ninyi nyote ni ndugu.” (Soma Mathayo 23:8, 9.) Katika maana fulani, sisi wote tuko ndugu kwa sababu sisi wote ni watoto wa Adamu. (Mdo. 17:26) Yesu alifasiria kama wanafunzi wake walikuwa pia ndugu na dada kwa sababu wote walikubali Yehova kuwa Baba yao wa mbinguni. (Mt. 12:50) Na wote walikuwa wameingia katika familia ya Mungu na waliunganishwa na upendo na imani. Ndiyo sababu mitume waliita Wakristo wengine ndugu na dada zao katika barua zenye waliandikia makutaniko.​—Rom. 1:13; 1 Pet. 2:17; 1 Yoh. 3:13. *​—Ona maelezo ya chini.

9, 10. (a) Sababu gani Wayahudi hawakupaswa kujivunia kabila lao? (b) Namna gani Yesu alifundisha kama ni mubaya kuzarau watu wa kabila ingine? (Ona picha ya kwanza kwenye mwanzo wa habari hii.)

9 Kisha Yesu kuambia wanafunzi wake kama walipaswa kujiona kuwa ndugu na dada, alikazia kama walipaswa kuwa wanyenyekevu. (Soma Mathayo 23:11, 12.) Kama vile tumekwisha kuona, wakati fulani majivuno yaligawanya mitume. Na wakati wa Yesu, watu walijivunia sana taifa lao. Wayahudi wengi walijiona kuwa walikuwa wa maana kuliko watu wengine, kwa sababu walikuwa watoto wa Abrahamu. Lakini Yohana Mubatizaji aliwaambia hivi: ‘Mungu ana nguvu za kumuinulia Abrahamu watoto kutoka katika majiwe haya.’​—Lu. 3:8.

10 Yesu alifundisha kama haiko muzuri watu wajivunie kabila lao. Alionyesha wazi jambo hilo wakati mwandishi mumoja alimuuliza hivi: “Ni nani kwa kweli aliye jirani yangu?” Ili kujibia ulizo hilo, Yesu alieleza habari fulani. Mwanaume fulani Muyahudi alipigwa na wezi na kuachwa kwenye barabara. Hata kama Wayahudi fulani walipita karibu na mwanaume huyo, hawakumusaidia. Lakini Musamaria fulani alimusikilia Muyahudi huyo huruma na akamuhangaikia. Yesu alimalizia habari yake kwa kuambia mwandishi huyo kama alipaswa kuwa kama Musamaria huyo. (Lu. 10:25-37) Yesu alionyesha kama Musamaria angeweza kufundisha Wayahudi maana ya kupenda jirani yao.

11. Sababu gani wanafunzi wa Yesu hawakupaswa kuwa na ubaguzi, na namna gani Yesu aliwasaidia kuelewa jambo hilo?

11 Mbele Yesu aende mbinguni aliambia wanafunzi wake wahubiri katika ‘Yudea yote na Samaria na mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Mdo. 1:8) Ili kufanya hivyo, Wanafunzi wa Yesu walipaswa kuachana na majivuno na ubaguzi wao. Mara nyingi Yesu alizungumuzia sifa za muzuri za watu wa mataifa mengine, na hilo lilitayarisha wanafunzi wake kuhubiria watu wa mataifa yote. Kwa mufano, alisifu ofisa mumoja wa jeshi mwenye hakukuwa Muyahudi mwenye alikuwa na imani kubwa. (Mt. 8:5-10) Katika muji wake wa Nazareti, Yesu alifasiria namna Yehova alisaidia watu wa mataifa mengine, kama vile mujane wa Foenike kutoka Zarefathi na Naamani wa Siria mwenye alikuwa na ukoma. (Lu. 4:25-27) Yesu alihubiria pia mwanamuke Musamaria na hata alifanya siku mbili katika muji wa Wasamaria kwa sababu watu walipendezwa na ujumbe wake.​—Yoh. 4:21-24, 40.

WAKRISTO WA KWANZA-KWANZA WALIPASWA KUPIGANISHA UBAGUZI

12, 13. (a) Namna gani mitume walitenda wakati Yesu alifundisha mwanamuke Musamaria? (Ona picha ya pili kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Ni nini inaonyesha kama Yakobo na Yohana hawakuelewa kabisa jambo lenye Yesu alikuwa anajaribu kuwafundisha?

12 Haikukuwa mwepesi kwa mitume kuachana na ubaguzi wao. Walishangaa kuona Yesu alikuwa tayari kufundisha mwanamuke Musamaria. (Yoh. 4:9, 27) Sababu gani? Kwa sababu viongozi wa dini ya Wayahudi hawangezungumuza na mwanamuke mahali pa watu wengi, na zaidi sana mwanamuke kama huyo Musamaria mwenye alikuwa na tabia ya mubaya. Mitume waliambia Yesu akule chakula, lakini Yesu alikuwa amefurahia sana kuzungumuza na mwanamuke huyo, na aliona kama kula haikukuwa jambo la maana kwake. Mungu alipenda afanye kazi ya kuhubiri, na kufanya mambo yenye Baba yake alipenda, hata kuhubiria mwanamuke Musamaria, ilikuwa kama chakula kwake.​—Yoh. 4:31-34.

13 Yakobo na Yohana hawakuelewa somo hilo la maana. Wakati wanafunzi walikuwa wanasafiri pamoja na Yesu katika Samaria, walitafuta mahali pa kulala usiku katika kijiji fulani cha Samaria. Lakini Wasamaria hawakuwaruhusu kulala huko. Yakobo na Yohana walikasirika sana mupaka wakauliza Yesu ikiwa anapenda waombe moto ushuke kutoka mbinguni ili kuharibu kijiji chote. Yesu aliwatolea mashauri makali. (Lu. 9:51-56) Pengine Yakobo na Yohana hawangekasirika sana hivyo ikiwa jambo hilo lingefanyika katika muji wao wa Galilaya. Pengine walikasirika kwa sababu walikuwa na ubaguzi. Kisha, wakati Yohana alikuwa anahubiria Wasamaria na wengi wakasikiliza, pengine alisikia haya juu ya mambo yenye alikuwa amesema mbele ya hapo.​—Mdo. 8:14, 25.

14. Namna gani tatizo la ubaguzi lilimalizwa?

14 Muda mufupi kisha Pentekoste ya mwaka wa 33, kulikuwa tatizo la ubaguzi katika kutaniko. Wakati ndugu walipatia chakula wajane wenye walikuwa na lazima ya musaada, hawakuhangaikia wajane wenye walikuwa wanazungumuza Kigiriki. (Mdo. 6:1) Pengine hilo lilitokea kwa sababu ya ubaguzi wa luga. Mitume walimaliza tatizo hilo haraka. Walichagua ndugu saba wenye kukomaa kiroho ili wagawanye chakula bila ubaguzi. Ndugu hao wote walikuwa na majina ya Kigiriki, pengine hilo lilifariji wajane wenye walikuwa wamekwazika.

15. Namna gani Petro alijifunza kutendea watu wote bila ubaguzi? (Ona picha ya tatu kwenye mwanzo wa habari hii.)

15 Katika mwaka wa 36, wanafunzi wa Yesu walianza kuhubiria watu wa mataifa yote. Mbele ya hapo mutume Petro alizoea kupitisha wakati pamoja na Wayahudi tu. Kisha Mungu alionyesha wazi kama Wakristo hawapaswe kuwa na ubaguzi, na Petro alihubiria Kornelio, askari Muroma. (Soma Matendo 10:28, 34, 35.) Kisha hapo, Petro alianza kupitisha wakati pamoja na Wakristo wenye hawakukuwa Wayahudi na alikula chakula pamoja nao. Lakini, kisha kupita miaka fulani, wakati alikuwa katika muji wa Antiokia, Petro aliacha kula chakula pamoja na Wakristo wenye hawakukuwa Wayahudi. (Gal. 2:11-14) Paulo alimurekebisha Petro, na Petro alikubali mashauri hayo. Namna gani tunajua jambo hilo? Wakati Petro aliandika barua yake ya kwanza kwa Wakristo Wayahudi na wenye hawakukuwa Wayahudi katika Asia Ndogo, alionyesha kama ni jambo la maana sana kupenda ndugu zetu wote.​—1 Pet. 1:1; 2:17.

16. Ni nini ilitambulisha Wakristo wa kwanza-kwanza?

16 Kwa kweli, mufano wa Yesu ulisaidia mitume wajifunze kupenda “watu wa namna zote.” (Yoh. 12:32; 1 Tim. 4:10) Hata kama ilikamata wakati, walibadilisha namna yao ya kuona watu. Kwa kweli, Wakristo wa kwanza-kwanza walifikia kujulikana kuwa watu wenye kupendana. Katika mwaka wa 200 hivi, mwandikaji Tertullian alionyesha kama watu walisema hivi juu ya Wakristo: “Wanapendana,” na “wako tayari kufa kwa ajili ya wenzao.” Kwa sababu Wakristo hao walivaa ‘utu mupya’ walijifunza kuona watu wote kuwa sawasawa, namna Mungu anawaona.​—Kol. 3:10, 11.

17. Namna gani tunaweza kuachana na mawazo yoyote ya ubaguzi? Toa mufano.

17 Leo pia, inaweza kutuomba wakati ili tuachane kabisa na mawazo yoyote ya ubaguzi. Dada mumoja katika Ufaransa anaeleza namna imekuwa vigumu kwake kufanya hivyo. Anasema hivi: “Yehova amenifundisha maana ya upendo, maana ya kutolea wengine, na maana ya kupenda watu wa namna zote. Lakini, ningali ninajifunza kuacha kubagua wengine, na haiko mwepesi sikuzote. Ndiyo sababu ninaendelea kusali juu ya jambo hilo.” Dada mumoja katika Uhispania anafasiria kama wakati fulani anapaswa kupiganisha mawazo ya mubaya juu ya kikundi fulani cha watu. Anasema hivi: “Mara nyingi ninaweza kufanya hivyo. Lakini ninajua kama ninapaswa kuendelea kupigana. Ninamushukuru Yehova kwa sababu niko na furaha ya kuwa katika familia yenye umoja.” Sisi wote tunapaswa kuchunguza kwa uangalifu mawazo yetu. Sisi pia tunapaswa kuachana na mawazo fulani ya ubaguzi?

WAKATI UPENDO UNAKOMAA, UBAGUZI UNAPOTEA

18, 19. (a) Sababu gani tunapaswa kukaribisha kila mutu? (b) Namna gani tunaweza kufanya hivyo?

18 Ni muzuri tukumbuke kama zamani sisi wote tulikuwa mbali na Mungu. (Efe. 2:12) Lakini kwa upendo, Yehova alituvuta kwake. (Hos. 11:4; Yoh. 6:44) Na Kristo alitukaribisha. Na alituwezesha kuwa katika familia ya Mungu. (Soma Waroma 15:7.) Hata kama hatukamilike Yesu ametukubali kwa upendo, kwa hiyo, hatupaswe hata kidogo kufikiria kukataa mutu yeyote!

Tuko na umoja na tunapendana kwa sababu tunatafuta “hekima inayotoka juu” (Picha hii inapatana na fungu la 19)

19 Kadiri tunakaribia mwisho wa ulimwengu huu muovu, watu watagawanyika zaidi, watakuwa na ubaguzi zaidi, na watakuwa na chuki zaidi. (Gal. 5:19-21; 2 Tim. 3:13) Lakini kwa sababu sisi ni watu wa Yehova, tunatafuta “hekima inayotoka juu,” yenye inatusaidia tusikuwe na ubaguzi na tuendeleze amani. (Yak. 3:17, 18) Tunafurahia kufanya urafiki na watu wa inchi zingine, kukubali namna yao ya kufanya mambo, na pengine hata kujifunza luga yao. Wakati tunafanya hivyo, tunafurahia amani ‘kama muto’ na haki “kama mawimbi ya bahari.”​—Isa. 48:17, 18.

20. Ni nini inatokea wakati upendo unabadilisha namna tunawaza na namna tunajisikia?

20 Wakati dada wa Australia mwenye tulizungumuzia alijifunza Biblia, mawazo yote yenye nguvu ya ubaguzi yenye alikuwa nayo na chuki yake, vilipotea polepole. Upendo ulibadilisha namna alifikiri na namna alijisikia katika moyo wake. Ndugu wa Kanada mwenye tumekwisha kutaja mwenye kuzungumuza Kifaransa, anasema kama sasa anatambua kama mara nyingi watu wanachukia wengine kwa sababu tu hawawajue. Alijifunza kama “sifa za watu hazitegemee mahali kwenye walizaliwa.” Alioa hata dada mwenye kuzungumuza Kiingereza! Mifano hiyo inaonyesha kama upendo unamaliza ubaguzi. Upendo unatuunganisha katika muungano wenye hauwezi kuvunjwa.​—Kol. 3:14.

^ fu. 8 Neno “ndugu” linaweza kutia ndani dada katika kutaniko. Paulo aliandikia barua “ndugu” katika Roma, lakini ni wazi kama ilihusu pia dada kwa sababu alitaja majina ya dada fulani. (Rom. 16:3, 6, 12) Kwa miaka mingi, gazeti Munara wa Mulinzi limeita Wakristo katika kutaniko ‘ndugu na dada.’