Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uache Sheria na Kanuni za Mungu Zizoeze Zamiri Yako

Uache Sheria na Kanuni za Mungu Zizoeze Zamiri Yako

“Vikumbusho vyako ndivyo ninavyohangaikia [ninafikiria].” ​—ZAB. 119:99.

NYIMBO: 127, 88

1. Ni kitu gani chenye kutufanya tukuwe wa hali ya juu kuliko wanyama?

YEHOVA alipatia wanadamu kitu fulani cha pekee. Kitu hicho ni zamiri yetu. Hilo ni jambo moja lenye linafanya tukuwe viumbe wa hali ya juu kuliko wanyama. Namna gani tunajua kama Adamu na Eva walikuwa na zamiri? Kisha kukosa kumutii Mungu, walijificha ili Mungu asiwaone. Zamiri yao iliwasumbua.

2. Namna gani zamiri yetu iko kama busole? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

2 Zamiri yetu ni uwezo wenye kuwa ndani yetu wa kujua mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa na inaweza kutuongoza katika maisha yetu. Mutu mwenye kuwa na zamiri yenye haizoezwe muzuri iko kama mashua yenye kuwa na busole yenye kuharibika. Upepo na zoruba yenye kuwa katika bahari vinaweza kufanya mashua hiyo iende katika njia ya mubaya. Lakini busole yenye kutumika muzuri inasaidia mutu mwenye kutembeza mashua aendelee kufanya mashua ibakie katika njia yake. Vilevile, ikiwa tunazoeza muzuri zamiri yetu, inaweza kutuongoza muzuri.

3. Ni nini inaweza kutokea ikiwa hatuzoeze muzuri zamiri yetu?

3 Ikiwa zamiri yetu haizoezwe muzuri, haitatuonya ili tusifanye mambo ya mubaya. (1 Tim. 4:1, 2) Inaweza hata kutusadikisha kama “ubaya ni wema.” (Isa. 5:20) Yesu aliambia hivi wanafunzi wake: ‘Saa inakuja wakati ambapo kila mutu anayewaua ninyi atafikiri amemutolea Mungu utumishi mutakatifu.’ (Yoh. 16:2) Wale wenye waliua mwanafunzi Stefano walifikiri hivyo. (Mdo. 6:8, 12; 7:54-60) Kwa miaka mingi watu wengi wa dini wamefanya mambo mengi ya mubaya sana, kama vile kuua, na wamesema kama walifanya hivyo kwa ajili ya Mungu. Lakini kwa kweli, mambo yenye wamefanya yanapinga sheria za Mungu. (Kut. 20:13) Ni wazi kama zamiri yao haijawaongoza muzuri!

4. Tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kama zamiri yetu inatumika muzuri?

4 Kwa hiyo, tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kama zamiri yetu inatumika muzuri? Sheria na kanuni zenye kuwa katika Biblia ziko na ‘faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nizamu katika uadilifu.’ (2 Tim. 3:16) Tunapaswa kujifunza Biblia kwa ukawaida, kufikiri sana juu ya mambo yenye inasema, na kuyatumikisha katika maisha yetu. Ikiwa tunafanya hivyo, tutajifunza kufikiri zaidi na zaidi namna Yehova anafikiri. Kisha, tunaweza kuwa hakika kama zamiri yetu itatuongoza muzuri. Tuzungumuzie basi namna tunaweza kutumia sheria na kanuni za Yehova ili kuzoeza zamiri yetu.

UACHE SHERIA ZA MUNGU ZIKUZOEZE

5, 6. Namna gani sheria za Mungu zinatusaidia?

5 Ikiwa tunapenda sheria za Mungu zitusaidie, tunapaswa kufanya mengi zaidi ya kuzisoma tu na kujua mambo yenye zinasema. Tunapaswa kuzipenda na kuziheshimia. Biblia inatuambia hivi: ‘Muchukie yaliyo mabaya, mupende yaliyo mema.’ (Amo. 5:15) Lakini namna gani tunaweza kufanya hivyo? Tunapaswa kujifunza kuona mambo namna Yehova anayaona. Kwa mufano, fikiria kuwa ni vigumu kwako kupata usingizi, na munganga anakupatia maagizo haya: ukule chakula chenye kujenga mwili, ufanye mazoezi zaidi, na ufanye mabadiliko mengine katika namna yako ya kuishi. Unafuata mashauri hayo na unapata matokeo ya muzuri! Utajisikia namna gani juu ya maagizo ya munganga?

6 Vilevile, Muumbaji wetu ametupatia sheria za kutulinda ili tusipate matokeo ya mubaya ya zambi na ili kufanya maisha yetu yakuwe ya muzuri zaidi. Kwa mufano, Biblia inatufundisha kama hatupaswe kusema uongo, kutenda kwa udanganyifu, kufanya uasherati, na kutenda kwa jeuri, ao kuzungumuza kwa njia yoyote na mashetani. (Soma Methali 6:16-19; Ufu. 21:8) Wakati tunajionea matokeo ya muzuri ya kumutii Yehova, tunamupenda zaidi na tunapendezwa zaidi na sheria zake.

7. Namna gani habari zenye kuwa katika Biblia zinatusaidia?

7 Haiko lazima tujionee katika maisha yetu matokeo ya mubaya ya kuvunja sheria za Mungu ili tujifunze mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. Tunaweza kujifunza mambo fulani kwa kuchunguza mifano fulani ya watu wenye walifanya makosa zamani. Mifano hiyo iko katika Biblia. Methali 1:5 inasema hivi: ‘Mutu mwenye hekima anasikiliza na kupata mafundisho zaidi.’ Mafundisho hayo yanatoka kwa Mungu na ni mafundisho ya muzuri zaidi! Kwa mufano, fikiria namna Daudi aliteseka sana wakati alikosa kumutii Mungu na kufanya uzinifu na Bath-sheba. (2 Sam. 12:7-14) Wakati unasoma habari hiyo, ujiulize hivi: ‘Namna gani Daudi angeepuka matatizo hayo? Ningefanya nini katika hali kama hiyo? Ikiwa ninajaribiwa kufanya mambo ya uasherati, nitakuwa kama Daudi ao kama Yosefu?’ (Mwa. 39:11-15) Ikiwa tunafikiria kwa uangalifu matokeo ya mubaya sana ya zambi, ‘tutachukia yaliyo mabaya’ zaidi na zaidi.

8, 9. (a) Zamiri yetu inatusaidia kufanya nini? (b) Namna gani kanuni za Yehova zinasaidia zamiri yetu?

8 Tunaepuka kabisa mambo yenye Mungu anachukia. Lakini tunapaswa kufanya nini ikiwa tuko katika hali fulani na Biblia haitoe sheria yenye kuwa wazi juu ya hali hiyo? Namna gani tutajua jambo lenye Mungu anapenda tufanye? Ikiwa tumeruhusu Biblia izoeze zamiri yetu, tutakamata uamuzi wenye hekima.

9 Kwa sababu Yehova anatupenda, ametutolea kanuni zenye zinaweza kuongoza zamiri yetu. Yehova anasema hivi: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake.” (Isa. 48:17, 18) Wakati tunafikiri sana juu ya kanuni za Biblia na kuziacha ziguse moyo wetu, tunaweza kurekebisha na kuongoza muzuri zamiri yetu. Kwa kawaida, hilo linatusaidia kukamata maamuzi yenye hekima.

UACHE KANUNI ZA MUNGU ZIKUONGOZE

10. Kanuni ni nini, na namna gani Yesu alitumia kanuni wakati alikuwa anafundisha?

10 Kanuni ni kweli ya musingi yenye kuongoza mawazo yetu na kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri. Kujua muzuri kanuni za Yehova kunatusaidia kuelewa namna anafikiri na sababu gani anatupatia sheria fulani. Yesu alitumia kanuni ili kufundisha wanafunzi wake kama mawazo na matendo yetu yako na matokeo. Kwa mufano, alifundisha kama hasira inaweza kuongoza mutu kwenye jeuri na kama mawazo machafu yanaweza kuongoza kwenye uzinifu. (Mt. 5:21, 22, 27, 28) Ikiwa tunaacha kanuni za Yehova zituongoze, zamiri yetu itazoezwa muzuri, na tutakamata maamuzi yenye kumuletea Mungu utukufu.​—1 Kor. 10:31.

Mukristo mwenye kukomaa kiroho anaheshimia zamiri ya wengine (Picha hizi zinapatana na fungu la 11, 12)

11. Namna gani zamiri ya mutu mumoja inaweza kuwa tofauti na ya mwingine?

11 Wakristo wawili wenye kuwa na zamiri yenye kuzoezwa muzuri na Biblia, wanaweza kuchukua maamuzi tofauti juu ya mambo fulani. Kwa mufano, inaweza kuwa juu ya kunywa pombe ao hapana. Biblia haiseme kama ni mubaya kunywa pombe, lakini inatuonya kama hatupaswe kunywa sana ao kulewa. (Met. 20:1; 1 Tim. 3:8) Hilo linamaanisha kama ikiwa tu Mukristo hakunywe pombe sana, hana lazima ya kufikiria jambo lingine lolote wakati anakamata uamuzi wake? Hapana. Hata kama zamiri yake inamuruhusu kunywa pombe, anapaswa kufikiria pia zamiri za wengine.

12. Namna gani maneno yenye kuwa katika Waroma 14:21 yanatusaidia kuheshimia zamiri za wengine?

12 Paulo alionyesha kama tunapaswa kufikiria zamiri za wengine wakati aliandika hivi: ‘Ni vema kutokula nyama ao kunywa divai ao kufanya jambo lolote ambalo ndugu yako anakwazika juu yake.’ (Rom. 14:21) Kwa hiyo, hata kama tuko na haki ya kunywa pombe, tutakuwa tayari kuachana na haki hiyo ikiwa tunajua kama kunywa pombe kutakwaza zamiri ya Mukristo mwengine. Pengine ndugu fulani alikuwa anakunywa sana pombe zamani, kisha akajifunza kweli na akaamua kama hatakunywa tena pombe hata kidogo. Hatuwezi kupenda kufanya jambo lolote lenye linaweza kufanya ndugu huyo arudilie tabia yake ya zamani. (1 Kor. 6:9, 10) Ikiwa ndugu huyo anatutembelea nyumbani kwetu, tutamukaza akunywe pombe hata kama anakataa? Hapana kabisa!

13. Namna gani Timotheo aliheshimia zamiri za wengine ili kuwasaidia wakubali habari njema?

13 Wakati Timotheo alikuwa kijana, alikubali kutahiriwa hata kama kufanya hivyo kulimuletea maumivu. Alijua kama kutahiriwa kulikuwa jambo la maana kwa Wayahudi wenye angehubiria. Kama Paulo, Timotheo hakupenda kukwaza mutu yeyote. (Mdo. 16:3; 1 Kor. 9:19-23) Uko pia tayari kujinyima mambo fulani ili kusaidia wengine?

“TUSONGE MBELE KUELEKEA UKOMAVU”

14, 15. (a) Namna gani tunafikia kukomaa kiroho? (b) Namna gani Wakristo wenye kukomaa kiroho wanatendea wengine?

14 Tunapaswa kuwa tayari ‘kuacha fundisho la musingi juu ya Kristo’ na ‘kusonga mbele kuelekea ukomavu.’ (Ebr. 6:1) Hata kama tumefanya miaka mingi katika kweli, hilo halimaanishe kama tuko Wakristo wenye kukomaa kiroho. Inaomba kujikaza ili kukomaa kiroho. Tunapaswa kuendelea kuongeza ujuzi na uelewaji wetu. Kwa hiyo, tunapaswa kusoma Biblia kila siku. (Zab. 1:1-3) Kadiri unaendelea kusoma Biblia kila siku, utaelewa muzuri zaidi sheria za Yehova na kanuni zake.

15 Ni sheria gani yenye kuwa ya maana zaidi kwa Wakristo? Ni sheria ya upendo. Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukiwa na upendo kati yenu wenyewe.’ (Yoh. 13:35) Upendo unaitwa “sheria ya kifalme” na “utimizo wa sheria.” (Yak. 2:8; Rom. 13:10) Hatushangae kuona kama upendo ni jambo la maana sana, kwa sababu Biblia inasema kama “Mungu ni upendo.” (1 Yoh. 4:8) Upendo wa Mungu hauonekane tu katika namna anajisikia. Anaonyesha pia upendo wake kupitia matendo. Yohana aliandikia hivi: ‘Kwa hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwa habari yetu, kwa sababu Mungu alimutuma Mwana wake muzaliwa-pekee kuja ulimwenguni ili tupate uzima kupitia yeye.’ (1 Yoh. 4:9) Wakati tunapenda Yehova, Yesu, ndugu na dada zetu, na watu wengine, tunaonyesha kama sisi ni Wakristo wenye kukomaa kiroho.​—Mt. 22:37-39.

Kadiri tunafikiri juu ya kanuni za Biblia, zamiri yetu inakuwa kiongozi mwenye kutumainika zaidi (Picha hii inapatana na fungu la 16)

16. Kadiri tunaendelea kukomaa kiroho, sababu gani tunapendezwa na kanuni zaidi na zaidi?

16 Kadiri tunaendelea kukomaa kiroho, tunapendezwa na kanuni zaidi na zaidi. Kwa kawaida Sheria zinatumiwa katika hali fulani ya pekee, lakini kanuni zinatumiwa katika hali nyingi tofauti. Kwa mufano, mutoto mudogo haelewe kuwa ni hatari sana kufanya urafiki pamoja na watu wabaya; kwa hiyo, wazazi wake wanapaswa kumuwekea sheria mbalimbali ili kumulinda. (1 Kor. 15:33) Lakini, kadiri mutoto anakomaa anajifunza namna ya kufikiri juu ya kanuni za Biblia. Kanuni hizo zitamusaidia kuchagua marafiki wazuri. (Soma 1 Wakorintho 13:11; 14:20.) Kadiri tunafikiri zaidi juu ya kanuni za Biblia, zamiri yetu inakuwa yenye kutumainika zaidi. Tunaelewa muzuri zaidi mambo yenye Mungu anapenda tufanye katika hali yoyote.

17. Ni nini inaweza kutusaidia kukamata maamuzi ya muzuri?

17 Tuko na kila kitu chenye tuko nacho lazima ili kutusaidia tukamate maamuzi yenye kumupendeza Yehova. Biblia iko na sheria na kanuni zenye zinatusaidia kuwa na ‘uwezo kamili, tukiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’ (2 Tim. 3:16, 17) Kanuni za Biblia zinatusaidia kuelewa namna Yehova anafikiri. Lakini inaomba kujikaza ili kuzipata. (Efe. 5:17) Ili kutusaidia, tunaweza kutumia vyombo kama vile, Index des publications des Témoins de Jéhovah, kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova, Watchtower Library, Watchtower MAKTABA KWENYE ENTERNETE, na programu JW Library. Ikiwa tunatumia vyombo hivyo, tutafaidika na funzo letu la pekee na funzo letu la familia.

ZAMIRI YENYE KUZOEZWA NA BIBLIA INALETA BARAKA

18. Tutapata faida gani ikiwa tunatumikisha sheria na kanuni za Yehova katika maisha yetu?

18 Maisha yetu yanakuwa ya muzuri zaidi wakati tunatumikisha sheria na kanuni za Yehova! Andiko la Zaburi 119:97-100 linasema hivi: ‘Jinsi ninavyoipenda sheria yako! Ndiyo ninayoihangaikia muchana kutwa. Amri yako inanifanya kuwa na hekima kuliko adui zangu, kwa sababu ni yangu mupaka wakati usio na kipimo. Nimepata kuwa na ufahamu kuliko walimu wangu wote, kwa sababu vikumbusho vyako ndivyo ninavyohangaikia. Ninajiendesha kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee, kwa sababu nimeyashika maagizo yako.’ Wakati tunachukua wakati wa kufikiri sana juu ya sheria na kanuni za Mungu, tutatenda kwa hekima zaidi na kwa uelewaji zaidi. Na ikiwa tunatumia sheria na kanuni zake ili kuzoeza zamiri yetu, tutafikia “kipimo cha kimo ambacho ni cha ujazo wa Kristo.”​—Efe. 4:13.