Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ufalme Wangu Si Sehemu ya Ulimwengu Huu”

“Ufalme Wangu Si Sehemu ya Ulimwengu Huu”

“Kwa ajili ya hili nimekuja ulimwenguni, ili nitoe ushahidi juu ya ile kweli.”​—YOH. 18:37.

NYIMBO: 15, 74

1, 2. (a) Namna gani ulimwengu unaendelea kugawanyika? (b) Tutajibia maulizo gani katika habari hii?

DADA mumoja wa kusini mwa Ulaya, anasema hivi juu ya maisha yake ya zamani: “Tangu wakati nilikuwa mutoto niliona tu ukosefu wa haki. Kwa hiyo, sikupenda watu wenye kufanya mambo ya politike katika inchi yangu na niliunga mukono mawazo yenye watu wengi waliona kuwa ni yenye musimamo mukali. Kwa kweli, kwa miaka mingi nilikuwa ninafanya urafiki wa kimapenzi na teroriste mumoja.” Ndugu mumoja wa kusini mwa Afrika anaeleza sababu gani alikuwa anatenda kwa jeuri, anasema hivi: “Niliamini kama kabila yangu ilikuwa ya maana zaidi kuliko makabila mengine yote, na nilijiunga na kikundi fulani cha politike. Tulifundishwa kuua maadui wetu kwa kutumia mikuki, hata watu wa kabila letu wenye waliunga mukono vikundi vingine vya politike.” Dada mumoja mwenye kuishi katika Ulaya anasema hivi: “Nilikuwa na ubaguzi, na nilichukia kila mutu mwenye alitoka katika inchi ingine ao mwenye alikuwa katika dini yenye ilikuwa tofauti na dini yangu.”

2 Leo, watu wengi zaidi, wako na tabia kama zile zenye watu hao watatu walikuwa nazo zamani. Vikundi vingi vya politike vinatumia jeuri ili kupata uhuru. Watu wanazoea kubishana juu ya mambo ya politike. Na katika inchi nyingi, watu wanatendea mubaya zaidi na zaidi wale wenye kutoka katika inchi zingine. Kama vile tu Biblia ilitabiri, watu ‘hawataki makubaliano yoyote’ katika siku hizi za mwisho. (2 Tim. 3:1, 3) Namna gani Wakristo wanaweza kuendelea kuwa na umoja hata kama watu katika ulimwengu wanaendelea kugawanyika? Mufano wa Yesu unaweza kutufundisha mambo mengi. Watu wa wakati wake walikuwa wenye kugawanyika pia kwa sababu walishikilia mawazo yenye kuwa tofauti kabisa juu ya mambo ya politike. Katika habari hii, tutapata majibu ya maulizo haya matatu: Sababu gani Yesu alikataa kujiunga na kikundi chochote cha mambo ya politike? Namna gani Yesu alionyesha kama watu wa Mungu hawapaswe kujiingiza katika mambo ya politike? Namna gani Yesu alifundisha kama hatupaswe hata kidogo kutumia jeuri?

YESU ALIUNGA MUKONO WALE WENYE WALIPENDA KUPATA UHURU?

3, 4. (a) Wakati wa Yesu, Wayahudi wengi walipenda nini? (b) Namna gani wanafunzi wa Yesu waliambukizwa na mawazo hayo?

3 Wayahudi wenye Yesu alikuwa anahubiria walipenda kabisa kutoka chini ya Utawala wa Roma. Wazeloti Wayahudi, kikundi cha politike chenye kilikuwa na musimamo mukali, walijikaza sana ili kufanya mawazo hayo yakuwe yenye nguvu zaidi. Wazeloti wengi walifuata mwanaume fulani mwenye aliitwa Yuda wa Galilaya, mwenye aliishi wakati wa Yesu. Yuda alikuwa Masiya wa uongo mwenye alidanganya watu wengi. Mwanahistoria Yosefu alisema kama Yuda alishauria Wayahudi wapiganishe Waroma na aliita wale wenye walikubali kulipa Waroma kodi kuwa “watu wenye kuogopa.” Mwishowe Waroma walimuua Yuda. (Mdo. 5:37) Wazeloti fulani walitumia hata jeuri ili wafikie miradi yao.

4 Wayahudi wengi walikuwa wanangojea kwa hamu kuja kwa Masiya. Walifikiri kama Masiya angewakomboa kutoka katika Utawala wa Waroma na angefanya Israeli ikuwe tena taifa kubwa. (Lu. 2:38; 3:15) Watu wengi waliamini kama Masiya angeanzisha ufalme duniani katika Israeli. Wakati hilo lingefanyika, Wayahudi wote wenye walikuwa wanaishi mahali mbalimbali katika dunia wangerudia katika Israeli. Wakati fulani hata Yohana Mubatizaji aliuliza Yesu hivi: ‘Je, wewe ndiye Yule Anayekuja, au tumutarajie [tumungojee] mwingine?’ (Mt. 11:2, 3) Pengine Yohana alijiuliza ikiwa mutu mwingine angekuja kuweka huru Wayahudi. Pia, kisha kufufuliwa kwa Yesu, wanafunzi wake wawili walikutana naye katika barabara ya kuenda Emau. Walisema kwamba walitumainia kama Yesu ndiye mwenye angeweka Israeli huru. (Soma Luka 24:21.) Muda mufupi kisha hapo, mitume waliuliza Yesu hivi: “Bwana, je, unarudishia Israeli ufalme wakati huu?”​—Mdo. 1:6.

5. (a) Sababu gani watu wa Galilaya walipenda Yesu akuwe mufalme wao? (b) Namna gani Yesu aliwasaidia kubadilisha mawazo yao?

5 Wayahudi walitumainia kama Masiya angemaliza magumu yao. Pengine ndiyo sababu watu wa Galilaya walipenda Yesu akuwe mufalme wao. Inawezekana walifikiri kama angekuwa mutawala muzuri sana. Alikuwa musemaji muzuri, angeweza kuponyesha wagonjwa, na angetolea hata chakula watu wenye walikuwa na njaa. Kisha Yesu kutolea chakula wanaume 5 000 hivi, watu walishangaa sana. Yesu alitambua jambo lenye walitaka kufanya. Biblia inasema hivi: ‘Yesu, akijua walikuwa karibu kuja kumukamata wamufanye kuwa mufalme, akaondoka tena kuenda mulimani akiwa peke yake.’ (Yoh. 6:10-15) Siku yenye ilifuata, pengine watu walikuwa wametulia. kisha Yesu aliwafasiria kama hakukuja ili kuwatolea vitu vya kimwili vyenye walikuwa navyo lazima, lakini alikuja ili kuwafundisha juu ya Ufalme wa Mungu. Aliwaambia hivi: ‘Mufanye kazi, si kwa ajili ya chakula ambacho kinaharibika, bali kwa ajili ya chakula ambacho kinadumu kufikia uzima wa milele.’​—Yoh. 6:25-27.

6. Namna gani Yesu alionyesha wazi kwamba hakupenda kupata mamlaka katika mambo ya politike katika dunia? (Ona picha ya kwanza kwenye mwanzo wa habari hii.)

6 Muda mufupi mbele ya kifo chake, Yesu alitambua kama wanafunzi wake fulani waliamini kama angekuwa mufalme na angeanza kutawala katika Yerusalemu. Kwa hiyo, Yesu aliwaelezea mufano wa mina ili kuwasaidia waelewe kama jambo hilo halingetokea. Mufano huo ulizungumuzia ‘mutu fulani wa ukoo mashuhuri,’ ni kusema Yesu, mwenye angeenda kwa muda murefu. (Lu. 19:11-13, 15) Pia, Yesu aliambia waziwazi kiongozi Muroma Pontio Pilato kama hakujiingiza katika mambo ya politike ya ulimwengu. Pilato alimuuliza Yesu hivi: ‘Je, wewe ndiye mufalme wa Wayahudi?’ (Yoh. 18:33) Pengine Pilato aliogopa kwamba Yesu angefanya watu waasi Utawala wa Roma. Lakini Yesu alijibia hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.” (Yoh. 18:36) Yesu alikataa kujiingiza katika mambo ya politike, kwa sababu Ufalme wake ungekuwa mbinguni. Alisema kama kazi yake katika dunia ilikuwa ‘kutoa ushahidi juu ya ile kweli.’​—Soma Yohana 18:37.

Unakaza akili juu ya matatizo yenye kuwa katika ulimwengu ao juu ya Ufalme wa Mungu? (Picha hizi zinapatana na fungu la 7)

7. Sababu gani inaweza kuwa vigumu kuepuka kuunga mukono vikundi vya politike hata katika moyo wetu?

7 Yesu alielewa mugawo wake. Wakati sisi pia tunaelewa mugawo wetu, tutaepuka kuunga mukono kikundi chochote cha politike hata katika moyo wetu. Haiko mwepesi kufanya hivyo kila wakati. Mwangalizi mumoja mwenye kusafiri anasema kama watu wa eneo lake wanaendelea kuwa na musimamo mukali zaidi na zaidi. Wanajivunia sana taifa lao na wanaamini kama maisha yao yangekuwa ya muzuri zaidi ikiwa watu wa taifa lao ndio wangewaongoza. Anaongezea hivi: “Jambo la kufurahisha ni kwamba, ndugu wamelinda umoja wao wa Kikristo kwa kukaza akili juu ya kazi ya kuhubiri habari njema juu ya Ufalme. Wanatumainia Mungu amalize ukosefu wa haki na magumu mengine yenye tunapambana nayo.”

NAMNA GANI YESU HAKUJIINGIZA KATIKA MAMBO YA POLITIKE?

8. Namna gani Wayahudi wengi walitendewa bila haki wakati wa Yesu?

8 Wakati watu wanaona ukosefu wa haki wenye unafanyika mahali penye wanaishi, mara nyingi wanajiingiza zaidi katika mambo ya politike. Wakati wa Yesu kulipa kodi ao taxe ilikuwa tatizo lenye lilifanya watu wengi wajiingize katika mambo ya politike. Kwa kweli, Yuda wa Galilaya aliasi Utawala wa Roma kwa sababu Waroma walikuwa wanaandikisha watu ili kuhakikisha kama wangelipa kodi. Na kulikuwa kodi za mingi zenye watu walipaswa kulipa kama vile, kulipia mali, kiwanja, na nyumba. Pia watu wenye walikuwa wanalipisha kodi walikuwa wadanganyifu sana, na hilo lilifanya mambo yakuwe mubaya zaidi. Wakati fulani walikuwa wanalipa wakubwa wa serikali ili wapate cheo na kisha walitumia mamlaka yao ili kupata feza nyingi. Zakayo, mukubwa wa wakusanya kodi katika Yeriko, alifikia kuwa tajiri kwa sababu aliomba watu walipe feza nyingi.​—Lu. 19:2, 8.

9, 10. (a) Namna gani maadui wa Yesu walijaribu kumuchochea ajiingize katika jambo fulani la politike? (b) Jibu la Yesu linatufundisha nini? (Ona picha ya pili kwenye mwanzo wa habari hii.)

9 Maadui wa Yesu walijaribu kumuchochea ajiingize katika mambo ya kulipa kodi. Walimuuliza juu ya “kodi” ya dinari moja yenye kila Muyahudi alipaswa kulipa. (Soma Mathayo 22:16-18.) Wayahudi walichukia kabisa kodi hiyo kwa sababu iliwakumbusha kama serikali ya Waroma ilikuwa inawatawala. “Wafuasi wa chama cha Herode,” ni kusema, wale wenye waliunga mukono mawazo ya politike ya Herode, walitazamia kama Yesu angesema kama hawangepaswa kulipa kodi ili wamushitaki kama alikuwa adui wa Utawala wa Roma. Lakini ikiwa Yesu angesema kama walipaswa kulipa kodi, watu wangeacha kumufuata. Kwa hiyo, Yesu alifanya nini?

10 Yesu alikuwa muangalifu ili asiunge mukono upande wowote katika mambo ya kulipa kodi. Alisema hivi: ‘Mumulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.’ (Mt. 22:21) Yesu alijua kama watu wengi wenye walilipisha kodi walikuwa wadanganyifu lakini hakukazia jambo hilo. Hata hivyo, alikazia jambo lenye lingemaliza kabisa matatizo ya wanadamu, ni kusema, Ufalme wa Mungu. Yesu alituachia mufano wa kuiga. Hatupaswe kuunga mukono wazo fulani la mambo ya politike hata kama upande mumoja unaonekana kuwa sawa na wenye haki na upande mwingine unaonekana kuwa wenye makosa na wenye kukosa haki. Wakristo wanakaza akili juu ya Ufalme wa Mungu na juu ya mambo yenye Mungu anasema kama ni yenye kuwa sawa. Kwa hiyo, hatushikilie mawazo fulani juu ya ukosefu wa haki ao kusema mambo yenye kupinga ukosefu huo wa haki.​—Mt. 6:33.

11. Namna gani tunaweza kusaidia wengine wapate haki ya kweli?

11 Mashahidi wengi wa Yehova wameweza kuachana na mawazo yenye musimamo mukali yenye walikuwa nayo zamani juu ya mambo ya politike. Kwa mufano, mbele ya kujifunza Biblia, dada mumoja katika inchi ya Uingereza alijifunza elimu ya jamii ao soshiolojia kwenye masomo ya juu na akaanza kuwa na musimamo mukali katika mambo ya politike. Anasema hivi: “Nilipenda kutetea haki za watu weusi, kwa sababu ya mambo mengi ya ukosefu wa haki yenye tulikuwa tumetendewa. Hata kama nilikuwa ninapata ushindi katika mabishano, mwishowe nilikuwa ninajisikia tu kuwa mwenye kuvunjika moyo. Sikutambua kama mambo yenye yanafanya watu watendewe bila haki kwa sababu ya rangi yao ya ngozi, yalipaswa kuondolewa kabisa katika mioyo ya watu. Lakini, wakati nilianza kujifunza Biblia, nilitambua kama nilipaswa kwanza kuondoa mambo hayo ndani ya moyo wangu mwenyewe.” Na dada muzungu ndiye alimusaidia abadilishe mambo yenye yalikuwa katika moyo wake. Anaongezea hivi: “Sasa ninamutumikia Yehova na niko painia wa kawaida katika kutaniko la luga ya ishara, na ninajifunza kuhubiria watu wa namna zote.”

“RUDISHA UPANGA WAKO MAHALI PAKE”

12. Yesu aliambia wanafunzi wake waepuke “chachu” ya aina gani?

12 Wakati wa Yesu, mara nyingi viongozi wa dini waliunga mukono vikundi vya mambo ya politike. Kwa mufano, kitabu kimoja kinasema kama Wayahudi walikuwa wamegawanyika katika vikundi vya dini vyenye vilikuwa kama vikundi mbalimbali vya politike. (Daily Life in Palestine at the Time of Christ) Kwa hiyo, Yesu alionya wanafunzi wake hivi: ‘Muendelee kufungua macho yenu, mujihazari [mukuwe waangalifu] na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.’ (Mk. 8:15) Wakati Yesu alitaja Herode, pengine alikuwa anazungumuzia chama cha wafuasi wa herode. Kikundi kingine, ni kusema, Mafarisayo walipenda Wayahudi wapate uhuru kutoka katika Utawala wa Roma. Kulingana na habari ya Mathayo, Yesu alionya pia wanafunzi wake juu ya Masadukayo. Masadukayo walipenda Waroma waendelee kutawala kwa sababu hilo liliwasaidia wakuwe na mamlaka yenye nguvu. Yesu alionya wanafunzi wake waepuke “chachu,” ao mafundisho ya vikundi hivyo vitatu. (Mt. 16:6, 12) Na inafurahisha kujua kama Yesu alitolea wanafunzi wake onyo hilo muda mufupi kisha watu kujaribu kumufanya kuwa mufalme.

13, 14. (a) Namna gani mabishano juu ya mambo ya dini na mambo ya politike yalileta jeuri na ukosefu wa haki? (b) Sababu gani haiko muzuri hata kidogo kutenda kwa jeuri, hata wakati tunatendewa bila haki? (Ona picha ya tatu kwenye mwanzo wa habari hii.)

13 Wakati dini zinajiingiza katika mambo ya politike, mara nyingi hilo linaleta jeuri. Yesu alifundisha wanafunzi wake wasijiingize hata kidogo katika mambo ya politike. Hiyo ni sababu moja yenye ilifanya makuhani wakubwa na Mafarisayo watafute kumuua Yesu. Waliogopa kwamba watu wangemusikiliza na kuacha kuwafuata. Ikiwa jambo hilo lingetokea, wangepoteza mamlaka yao katika mambo ya dini na ya politike. Walisema hivi: ‘Tukimuacha hivyo, hao wote watamuamini, na Waroma watakuja na kuondolea mbali mahali petu na taifa letu pia.’ (Yoh. 11:48) Kwa hiyo, Kuhani Mukubwa Kayafa alifanya mupango ili kumuua Yesu.​—Yoh. 11:49-53; 18:14.

14 Kayafa alingojea wakati wa usiku na kisha akatuma maaskari ili waende kumukamata Yesu. Lakini, Yesu alijua mupango huo wa kumuua. Kwa hiyo, wakati wa chakula chake cha mwisho pamoja na mitume wake aliwaambia walete mipanga. Angetumia mipanga hiyo mbili ili kuwafundisha somo la maana. (Lu. 22:36-38) Kisha, usiku huo, kikundi cha watu kilikuja kumukamata Yesu na Petro akakasirika sana kwa sababu ya ukosefu huo wa haki; kwa hiyo, akachukua upanga na kushambulia mwanaume mumoja kati ya wanaume hao. (Yoh. 18:10) Lakini Yesu akaambia Petro hivi: “Rudisha upanga wako mahali pake, kwa maana wale wote wanaouchukua upanga wataangamia kwa upanga.” (Mt. 26:52, 53) Yesu alifundisha wanafunzi wake somo gani la maana sana? Aliwafundisha kama hawapaswe kuwa sehemu ya ulimwengu. Yesu alikuwa amesali juu ya jambo hilo mbele ya hapo usiku huo. (Soma Yohana 17:16.) Mungu tu ndiye iko na haki ya kupiganisha ukosefu wa haki.

15, 16. (a) Namna gani Neno la Mungu limesaidia Wakristo waepuke mambo yenye kugawanya watu? (b) Yehova anaona tofauti gani wakati anaangalia ulimwengu wa leo?

15 Dada wa kusini mwa Ulaya mwenye tumekwisha kuzungumuzia alijifunza pia somo hilo. Anasema hivi: “Nimeona kama jeuri hailete haki. Niliona kama mara nyingi wale wenye kutenda kwa jeuri wanafikia kufa. Na wengine wengi wanakuwa na hasira. Nilifurahi kujifunza katika Biblia kama Mungu tu ndiye anaweza kuleta haki ya kweli katika dunia. Huo ndio ujumbe wenye nimehubiri kwa miaka 25 yenye imepita.” Ndugu wa kusini mwa Afrika mwenye tulizungumuzia alibadilisha mikuki yake kuwa “upanga wa roho,” ni kusema, Neno la Mungu. (Efe. 6:17) Sasa anahubiri ujumbe wa amani kwa watu wote, hata wakuwe wa kabila gani. Na wakati dada wa Ulaya ya kati mwenye tulizungumuzia alikuwa Shahidi wa Yehova, aliolewa na ndugu wa kabila lenye alikuwa anachukia zamani. Wote watatu walifanya mabadiliko hayo kwa sababu walipenda kuwa kama Kristo.

16 Ni jambo la maana sana kufanya mabadiliko hayo! Biblia inasema kama wanadamu wako kama bahari yenye upepo na zoruba yenye haitulie hata kidogo. (Isa. 17:12; 57:20, 21; Ufu. 13:1) Mambo ya politike yanachochea watu, yanawagawanya, na kuleta jeuri. Lakini sisi tuko na amani na umoja. Wakati Yehova anaona namna watu wako katika ulimwengu, anafurahi sana kuona namna watu wake wako na umoja kabisa.​—Soma Sefania 3:17.

17. (a) Tunaweza kuendeleza umoja katika njia gani tatu? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Katika habari hii tumejifunza kama tunaweza kuendeleza umoja katika njia tatu: (1) Tunaamini kama Ufalme wa Mungu utamaliza ukosefu wote wa haki, (2) hatujiingize hata kidogo katika mambo ya politike, na (3) tunaepuka jeuri. Lakini jambo lingine lenye linaweza kutia umoja wetu katika hatari ni ubaguzi. Katika habari yenye kufuata tutajifunza namna tunaweza kuachana na ubaguzi, kama vile Wakristo wa kwanza-kwanza walifanya.