Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kujilinda Kabisa na Mutego Fulani wa Shetani

Namna ya Kujilinda Kabisa na Mutego Fulani wa Shetani

WAKATI Waisraeli wa zamani walikuwa wanajitayarisha kuvuka Muto Yordani ili kuingia mu inchi yenye Mungu alikuwa amewaahidi, watu fulani walikuja kuwatembelea. Watu hao wenye waliwatembelea walikuwa wanamuke wenye hawakukuwa Waisraeli na waliwaalika ku karamu. Waisraeli wangeona jambo hilo kuwa nafasi ya muzuri sana. Ingefurahisha sana kujifanyia marafiki wapya, kucheza, na kula chakula cha muzuri. Hata kama desturi na tabia za wanamuke hao zilipingana na mambo yenye Sheria ya Mungu iliwaamuru, Waisraeli fulani wangewaza hivi: ‘Hakuna shida. Tutakuwa waangalifu.’

Ni nini ilitokea? Habari yenye iliongozwa na roho ya Mungu inasema hivi: “Watu walianza kufanya uasherati na mabinti wa Moabu.” Kwa kweli, wanamuke hao walipenda wanaume Waisraeli waabudu miungu ya uongo. Na walifanya vile! Njo maana ‘Yehova alikasirikia Israeli.’​—Hes. 25:1-3.

Waisraeli hao walivunja Sheria ya Mungu katika njia mbili: Waliinamia sanamu, na pia walifanya uasherati. Maelfu ya Waisraeli walikufa juu ya kukosa kutii. (Kut. 20:4, 5, 14; Kum. 13:6-9) Ni nini ilifanya tendo hilo likuwe la mubaya zaidi? Ni wakati. Kama wanaume hao hawangevunja Sheria ya Mungu, maelfu ya Waisraeli wangevuka Yordani na kuingia mu Inchi ya Ahadi.​—Hes. 25:5, 9.

Juu ya ile mambo yenye ilitokea, mutume Paulo aliandika hivi: “Mambo hayo yaliwapata ili kuwa mifano, na yaliandikwa ili kuwa onyo kwetu sisi wenye tumefikiwa na miisho ya mipangilio ya mambo.” (1 Ko. 10:7-11) Kwa kweli, Shetani alifurahi kuona kama Waisraeli fulani waliangukia katika zambi nzito na kwa hiyo, hawakustahili kuingia mu Inchi ya Ahadi. Ni jambo la hekima kabisa tufuate onyo hilo, kwa sababu tunajua kama Shetani atafurahi sana ikiwa tunakosa kuingia mu dunia mupya ya Mungu!

MUTEGO HATARI

Shetani anawinda Wakristo kwa kutumia mitego yenye anajua muzuri na yenye imenasa watu wengi. Kama vile tuliona, alitega Waisraeli kwa kutumia uasherati. Katika siku zetu, uasherati unaendelea kuwa mutego hatari. Njia moja kubwa yenye Shetani anatumia ili kutunasa katika mutego huo ni pornografia.

Leo, watu wanaweza kuangalia pornografia bila wengine kujua jambo hilo. Zamani, mutu mwenye alipenda kuangalia pornografia alipaswa kuenda mu jumba la maonyesho ili kuangalia filme zenye hazifae ao alipaswa kuenda mu maduka ya kuuzishia vitabu vya pornografia. Pengine watu wengi hawakukuwa wanaenda kwenye nafasi hizo kwa sababu walisikia haya kuwa watu wengine watawaona. Lakini leo, mutu mwenye iko na uwezo wa kuingia ku Enternete anaweza kuangalia pornografia ku kazi ao hata ndani ya motokari yenye kuegeshwa. Na katika inchi za mingi, mwanaume ao mwanamuke anaweza kuangalia pornografia bila hata kutoka mu nyumba yake.

Haiko ile tu. Vyombo kama vile telefone za hali ya juu ao tablete, vimefanya ikuwe mwepesi sana kuangalia pornografia. Wakati watu wanatembea mu njia ao wakati wako mu bisi ao mu treni, wanaweza kuangalia picha chafu ku telefone ao ku tablete yao.

Kwa sababu imekuwa mwepesi sana kwa watu kuangalia pornografia na kuficha jambo hilo, leo pornografia inaleta matokeo ya mubaya sana kupita zamani. Watu wengi wenye kuangalia pornografia wanaharibu ndoa zao, zamiri yao, na wanajishushia heshima. Jambo la mubaya zaidi, wanaweza kuharibu urafiki wao pamoja na Mungu. Unaweza kuwa hakika kama pornografia inaletea matokeo ya mubaya wale wenye kuiangalia. Katika hali za mingi, pornografia inaletea watu matokeo ya mubaya sana na ile matokeo inaweza kuendelea kwa wakati murefu, na wakati fulani mutu hawezi kumaliza kabisa ile matokeo ya mubaya.

Lakini, tunapaswa kujua kama Yehova anatulinda ili tusinaswe na mutego huo wa Shetani. Kama tunapenda Yehova atulinde, tunapaswa kufanya jambo lenye Waisraeli wa zamani walishindwa kufanya, ni kusema, ‘kumutii [Yehova] kabisa.’ (Kut. 19:5) Tunapaswa kujua kama Mungu anachukia sana pornografia. Juu ya nini tunasema vile?

CHUKIA PORNOGRAFIA KAMA VILE YEHOVA ANAICHUKIA

Fikiria jambo hili: Sheria zenye Mungu alipatia taifa la Israeli zilikuwa tofauti na sheria za mataifa ingine yote ya wakati ule. Sheria hizo zilikuwa kama ukuta; zililinda Waisraeli ili wasichochewe na watu wenye waliwazunguka na pia mazoea yao ya mubaya. (Kum. 4:6-8) Sheria hizo zilionyesha wazi kweli hii ya maana: Yehova anachukia uasherati.

Yehova alitaja mambo machafu yenye mataifa yenye ilizunguka Waisraeli ilikuwa inafanya na aliwaambia hivi: “Hamupaswe kufanya mambo yenye wanafanya katika inchi ya Kanaani, kwenye ninawapeleka. . . . Inchi hiyo haiko safi, na nitaleta azabu juu ya inchi hiyo kwa sababu ya kosa lake.” Mungu mutakatifu wa Israeli aliona maisha ya Wakanaani kuwa machafu sana mupaka akaona inchi yao kuwa chafu.​—Law. 18:3, 25.

Hata kama Yehova alipatia Wakanaani azabu ao malipizi, watu wengine waliendelea kufanya uasherati. Miaka zaidi ya 1 500 kisha pale, Paulo alizungumuzia mataifa yenye Wakristo walikuwa wanaishi katikati yake kuwa ‘ilishiwa na ufahamu wote wa mambo yenye kuwa sawa.’ Kwa kweli, ‘walijitoa wenyewe katika mwenendo mupotovu wa bila haya ili kufanya kwa pupa kila namna ya ukosefu wa usafi.’ (Efe. 4:17-19) Leo pia, watu wengi wako na mwenendo mupotovu na hawana haya juu ya mwenendo huo. Kwa kadiri inawezekana, Wakristo wa kweli wanapaswa kuepuka kuangalia mambo machafu ya watu wa ulimwengu huu.

Pornografia inamukosea Mungu heshima kabisa. Alituumba sisi wanadamu kwa mufano wake na sura yake na alitupatia uwezo wa kujua ikiwa jambo fulani liko sawa ao haliko sawa. Mungu alionyesha hekima kwa kutupatia sheria juu ya ngono. Alikusudia ngono iletee bibi na bwana furaha katika ndoa. (Mwa. 1:26-28; Mez. 5:18, 19) Lakini wale wenye wanatengeneza ao kuchochea mambo ya pornografia wanafanya nini? Wanazarau kabisa kanuni za Mungu za mwenendo. Kwa kweli, watu wenye wanachochea pornografia wanamukosea Yehova heshima. Mungu atahukumu watu wenye wanazarau kanuni zake kwa kutengeneza ao kuchochea mambo machafu.​—Ro. 1:24-27.

Lakini tuseme nini juu ya watu wenye wanasoma ao kuangalia pornografia kwa makusudi? Watu fulani wanaweza kuwaza kama pornografia ni namna ya kujifurahisha yenye haina hatari yoyote. Lakini kwa kweli, wanaunga mukono wale wenye wanazarau kanuni za Yehova. Pengine hawakukuwa na kusudi hilo wakati walianza kuangalia pornografia. Hata hivyo, ni wazi kama waabudu wa Mungu wa kweli wanapaswa kuchukia sana pornografia. Biblia inaonya hivi: “Enyi wenye kumupenda Yehova, muchukie mambo ya mubaya.”​—Zb. 97:10.

Hata wale wenye wanapenda kuepuka kuangalia pornografia wanaweza kuona kama ni vigumu kufanya vile. Hatukamilike, na inaweza kuomba tupigane ili kupinga tamaa chafu za ngono. Tena, moyo wetu wenye haukamilike unaweza kujaribu kutafuta njia ya kutetea kama haiko mubaya kuangalia pornografia. (Yer. 17:9) Lakini, watu wengi wenye wamekuwa Wakristo wameshinda vita hiyo. Kujua vile kunaweza kukufanya ukuwe hakika kama na wewe unaweza kushinda vita hiyo. Ona namna Neno la Mungu linaweza kukusaidia ili uepuke mutego wa Shetani wa pornografia.

USIENDELEE KUWAZA JUU YA TAMAA ZA MUBAYA

Kama vile tulisema, Waisraeli wengi waliacha tamaa za mubaya ziwaongoze kufanya jambo lenye lilileta matokeo ya mubaya sana. Jambo kama hilo linaweza kutokea leo. Yakobo, ndugu-nusu wa Yesu, alieleza hatari hiyo kwa kusema hivi: ‘Kila mutu . . . anavutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe. Kisha tamaa, wakati imepata mimba, inazaa zambi.’ (Yak. 1:14, 15) Wakati tamaa ya mubaya inakomaa kwa kiasi fulani ndani ya moyo wa mutu fulani, inawezekana kabisa mutu huyo afanye zambi. Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza ili kuachana na mawazo machafu, hatupaswe kuendelea kuifikiria.

Kama unaendelea kuwaza juu ya mambo machafu, fanya jambo fulani bila kukawia. Yesu alisema hivi: “Basi, kama mukono wako ao muguu wako unakufanya ukwazike, uukate na kuutupa mbali na wewe. . . . Tena, kama jicho lako linafanya ukwazike, lingoe na kulitupa mbali na wewe.” (Mt. 18:8, 9) Yesu hakusema kama tunapaswa kukata viungo vya mwili wetu. Alitumia maneno ya mufano yenye kuonyesha kama tuko na lazima ya kuachana na mambo yenye kufanya tujikwae na kisha tunapaswa kufanya haraka sana mabadiliko yenye kuombwa. Namna gani tunaweza kutumia ile mashauri juu ya pornografia?

Kama unaona mambo ya pornografia bila kutazamia, usiwaze hivi: ‘Haitanifanya kitu.’ Angalia pembeni mara moja. Funga televizyo bila kukawia. Funga ordinatere, tablette ao telefone yako palepale. Waza juu ya jambo fulani la muzuri. Kufanya vile kutakusaidia uongoze mawazo yako kuliko kuacha tamaa za mubaya zikuongoze.

TUTAFANYA NINI KAMA TUNAENDELEA KUWAZA JUU YA MAMBO YA PORNOGRAFIA YENYE TULIONAKA ZAMANI?

Utafanya nini kama umeachana na tabia ya kuangalia pornografia, lakini wakati fulani unaendelea kukumbuka mambo yenye ulionaka? Picha ao mawazo ya pornografia inaweza kubakia katika akili ya mutu kwa wakati murefu. Inaweza kutokea wakati wowote. Kama hilo linakufikia, unaweza kushawishiwa kufanya jambo fulani chafu, kama vile kugusa-gusa viungo vyako vya uzazi ili kutimiza tamaa ya ngono. Kwa hiyo, ujue kama mawazo kama ile inaweza kutokea wakati wowote, na ukuwe tayari kuipiganisha.

Uazimie zaidi kupatanisha mawazo na matendo yako kulingana na mapenzi ya Mungu. Ukuwe kama mutume Paulo, mwenye alikuwa tayari ‘kupiga-piga mwili [wake] na kuuongoza kama mutumwa.’ (1 Ko. 9:27) Usiache tamaa za mubaya zikutawale. ‘Ugeuzwe kwa kufanya upya akili yako, ili ujihakikishie wewe mwenyewe mapenzi ya Mungu yenye kuwa mema na yenye kukubalika na makamilifu.’ (Ro. 12:2) Kumbuka jambo hili: Kuwaza na kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu kunaleta furaha zaidi kuliko kutii tamaa za zambi.

Kuwaza na kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu kunaleta furaha zaidi kuliko kutii tamaa za zambi

Ujikaze kuweka maandiko fulani ya Biblia katika akili yako. Kisha, kama mawazo ya mubaya inaingia katika akili yako, ujikaze kuwaza juu ya ile maandiko. Maandiko kama vile Zaburi 119:37; Isaya 52:11; Matayo 5:28; Waefeso 5:3; Wakolosai 3:5; na 1 Watesalonike 4:4-8 itakusaidia kuona pornografia kama vile Yehova anaiona na kuelewa mambo yenye anapenda ufanye.

Utafanya nini kama wakati fulani unashindwa kuzuia tamaa ya kuona ao kuwaza mambo machafu? Umuige kabisa Yesu, Mufano wetu. (1 Pe. 2:21) Kisha Yesu kubatizwa, Shetani aliendelea kumujaribu. Yesu alifanya nini? Aliendelea kumupinga. Yesu alitaja maandiko mara mingi ili kupinga vishawishi vya Shetani. Alisema hivi: “Toka mbele yangu, Shetani!” na Shetani akamuacha. Yesu hakuacha hata kidogo kumupinga Ibilisi, na wewe usiache. (Mt. 4:1-11) Shetani na ulimwengu wake wataendelea kujaribu kujaza mawazo machafu katika akili yako, lakini usiache kuipiganisha. Unaweza kushinda vita juu ya pornografia. Yehova anaweza kukusaidia kumushinda adui yako.

USALI KWA YEHOVA, NA UMUTII

Umutegemee kabisa Yehova kupitia sala. Paulo alisema hivi: “Maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.” (Flp. 4:6, 7) Mungu atakupatia amani yake ili kukusaidia kupinga mambo ya mubaya. Kama unamukaribia Yehova, naye ‘atakukaribia.’​—Yak. 4:8.

Tutalindwa na mitego ya Shetani kama tunaendelea kuwa na urafiki wa muzuri pamoja na Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote. Yesu alisema hivi: “Mutawala wa ulimwengu [Shetani] anakuja, na hana uwezo juu yangu.” (Yoh. 14:30) Juu ya nini Yesu alikuwa hakika na jambo hilo? Mbele ya pale, alikuwa amesema hivi: “Ule mwenye alinituma iko pamoja na mimi; hakuniacha peke yangu, kwa sababu sikuzote ninafanya mambo yenye kumupendeza.” (Yoh. 8:29) Kama unafanya mambo yenye kumupendeza Yehova, na wewe hatakuacha hata kidogo. Uepuke mutego wa pornografia, na Shetani hataweza kukunasa.