MUNARA WA MULINZI—GAZETI YA FUNZO Mwezi wa 6, 2020

Gazeti hili liko na habari za kujifunza tarehe 3-30/8/2020.

“Jina Lako Litakaswe”

Habari ya kujifunza ya 23: Tarehe 3-9/8/2020. Ni jambo gani la maana lenye linahusu wanadamu na malaika? Juu ya nini jambo hilo ni la maana sana, na namna gani linatuhusu? Kuelewa majibu ya ile maulizo na maulizo ingine kutatusaidia kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova.

“Unganisha Moyo Wangu ili Niogope Jina Lako”

Habari ya kujifunza ya 24: Tarehe 10-16/8/2020. Katika habari hii, tutazungumuzia maneno fulani yenye Mufalme Daudi alisema mu sala yake yenye kuwa mu Zaburi 86:11, 12. Kuogopa jina la Yehova maana yake nini? Ni sababu gani fulani zenye kufanya tuogope sana jina hilo kubwa? Na namna gani kumuogopa Mungu kunaweza kutulinda ili tusishindwe wakati tunapata majaribu?

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Sifa zenye kutajwa katika Wagalatia 5:22, 23 njo sehemu zote za “tunda la roho”?

“Mimi Mwenyewe, Nitatafuta Kondoo Wangu”

Habari ya kujifunza ya 25: Tarehe 17-23/8/2020. Juu ya nini watu fulani wenye wamemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi wanaachaka kutaniko? Mungu anajisikia namna gani juu yao? Habari hii itajibu ile maulizo. Inazungumuzia pia mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia namna Yehova alisaidia watu fulani wa zamani wenye waliacha kumutumikia kwa wakati fulani.

“Munirudilie”

Habari ya kujifunza ya 26: Tarehe 24-30/8/2020. Yehova anapenda wale wenye wameacha kutaniko wamurudilie. Tunaweza kufanya mambo mingi ili kutia moyo wale wenye wanapenda kukubali mwaliko huu wa Yehova: “Munirudilie.” Katika habari hii, tutazungumuzia namna tunaweza kuwasaidia wamurudilie Yehova.