Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kujizuia Ni Sifa ya Maana Sana ili Kukubaliwa na Yehova

Kujizuia Ni Sifa ya Maana Sana ili Kukubaliwa na Yehova

“Wakati binamu yangu alikuwa anaanza kubishana na mimi, nilikuwa namukamata ku shingo na kuanza kumunyonga. Nilipenda kumuua.”​—Paul.

“Ku nyumba, nilikuwa ninakasirika haraka, hata wakati nilichokozwa kidogo tu. Nilikuwa ninavunja-vunja vitu vya mu nyumba, vitu vya watoto vya kuchezea, kila kitu chenye nilipata.”​—Marco.

Wengi kati yetu hawako kama Paul na Marco. Lakini, wakati fulani, sisi wote tunakuwaka na magumu ya kujizuia. Sababu kubwa ni kwamba tuliriti zambi kutoka kwa Adamu, mwanaume wa kwanza. (Ro. 5:12) Watu fulani wako na magumu ya kuzuia kasirani yao, kama vile Paul na Marco. Wengine wanaweza kuona kama ni nguvu kuzuia mawazo yao. Wanaendelea kuogopa sana ao mara mingi wanahangaishwa na mawazo ya mubaya. Na wengine wako na magumu ya kujizuia ili wasifanye uasherati, wasikunywe pombe sana, ao wasitumie dawa za kulewesha.

Wale wenye wanashindwa kuzuia mawazo yao, tamaa zao, na matendo yao wanaweza kuharibu maisha yao. Lakini tunaweza kuepuka jambo hilo lisitufikie. Namna gani? Kwa kukomalisha sifa ya kujizuia. Ili kutusaidia kufanya vile, tuzungumuzie maulizo tatu: (1) Kujizuia maana yake nini? (2) Juu ya nini ni sifa ya lazima? (3) Namna gani tunaweza kukomalisha sifa hiyo yenye kuwa sehemu ya “tunda la roho”? (Gal. 5:22, 23) Kisha, tutazungumuzia mambo yenye kila mumoja wetu anaweza kufanya kama wakati fulani anakosa kuonyesha sifa ya kujizuia.

KUJIZUIA MAANA YAKE NINI?

Mutu mwenye iko na sifa ya kujizuia hatende bila kufikiri. Lakini, anajizuia ili asiseme ao kutenda kwa njia zenye kumuchukiza Mungu.

Kwa kweli, Yesu alionyesha sifa ya kujizuia

Yesu alituonyesha maana ya kujizuia. Biblia inasema hivi: “Wakati alikuwa anatukanwa, hakujibu kwa matukano. Wakati alikuwa anateseka, hakuogopesha watu, lakini alijitia katika mikono ya Ule mwenye anahukumu kwa haki.” (1 Pe. 2:23) Yesu alionyesha sifa ya kujizuia wakati wapinzani wake walimuchekelea na iko ku muti wa mateso. (Mt. 27:39-44) Mbele ya pale, alionyesha sana sifa ya kujizuia wakati viongozi wa dini walimuuliza maulizo mingi ili kumujaribu. (Mt. 22:15-22) Na alionyesha mufano muzuri sana wakati Wayahudi fulani wenye walikuwa na kasirani waliokota majiwe ili kumutupia! Kuliko kulipiza kisasi, ‘Yesu alijificha na akatoka katika hekalu.’​—Yoh. 8:57-59.

Inawezekana tuige mufano wa Yesu? Tunaweza kufanya vile, kwa kiasi fulani. Mutume Petro aliandika hivi: “Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi mufano ili mufuate hatua zake kwa ukaribu.” (1 Pe. 2:21) Hata kama hatukamilike, tunaweza kufuata kwa ukaribu mufano wa Yesu wa kujizuia. Juu ya nini ni lazima tufanye vile?

JUU YA NINI SIFA YA KUJIZUIA NI YA LAZIMA?

Sifa ya kujizuia ni ya lazima ili tukubaliwe na Yehova. Hata kama tumemutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi, tunaweza kupoteza urafiki wetu pamoja naye kama hatuzuie mambo yenye tunafanya na yenye tunasema.

Fikiria mufano wa Musa, mwenye alikuwa “mupole sana kuliko watu wote juu ya uso wa dunia” wakati huo. (Hes. 12:3) Kisha kuvumilia malalamiko ya Waisraeli kwa miaka mingi, Musa alishindwa kujizuia. Alikasirika wakati walilalamika tena juu ya kukosa maji. Alisema na watu kwa ukali hivi: “Musikie, sasa, ninyi waasi! Je, tunapaswa kuwatoshea maji katika mwamba huu?”​—Hes. 20:2-11.

Musa alishindwa kujizuia. Hakumupatia Yehova utukufu kwa ajili ya muujiza huo wa kuwapatia maji. (Zb. 106:32, 33) Njo maana Yehova hakumuruhusu aingie mu Inchi ya Ahadi. (Hes. 20:12) Mupaka siku yenye Musa alikufa, inawezekana aliendelea kuhuzunika juu ya namna alikosaka kujizuia.​—Kum. 3:23-27.

Habari hiyo inatufundisha nini? Hata kama tumekuwa katika kweli kwa miaka mingi, hatupaswe hata kidogo kusema bila heshima na wale wenye wanatukasirisha ao wenye wanapaswa kurekebishwa. (Efe. 4:32; Kol. 3:12) Kwa kweli, wakati tunaendelea kukomaa, inaweza kuwa nguvu zaidi kwetu kuonyesha uvumilivu wakati fulani. Lakini, tumukumbuke Musa. Hatupendi hata kidogo miaka yote yenye tumemutumikia Yehova kwa uaminifu ikuwe ya bure kwa sababu ya kukosa kujizuia. Tunaweza kufanya nini ili kukomalisha sifa hiyo ya lazima?

NAMNA YA KUKOMALISHA SIFA YA KUJIZUIA

Sali ili kupata roho takatifu. Sababu gani? Kwa sababu kujizuia ni sehemu ya tunda la roho ya Mungu, na Yehova anapatiaka roho yake wale wenye wanamuomba. (Lu. 11:13) Kupitia roho yake takatifu, Yehova anaweza kutupatia nguvu yenye tuko nayo lazima. (Flp. 4:13) Anaweza pia kutusaidia tukomalishe sehemu zingine za tunda la roho, kama vile upendo, wenye unafanya ikuwe mwepesi kwetu kuonyesha sifa ya kujizuia.​—1 Ko. 13:5.

Epuka kila kitu chenye kinafanya ikuwe nguvu kwako kuonyesha sifa ya kujizuia

Epuka kila kitu chenye kinaweza kufanya ikuwe nguvu kwako kuonyesha sifa ya kujizuia. Kwa mufano, epuka mambo ya kujifurahisha na site za Enternete zenye kuonyesha mwenendo mubaya. (Efe. 5:3, 4) Kwa kweli, tunapaswa kuepuka kila kitu chenye kinaweza kutushawishi tufanye mambo ya mubaya. (Mez. 22:3; 1 Ko. 6:12) Kwa mufano, ikiwa mutu anashawishiwaka kwa vyepesi kufanya mambo machafu ya ngono, inaweza kuwa muzuri aepuke vitabu na filme za mapenzi.

Pengine inaweza kuwa nguvu kwetu kutumia shauri hilo. Lakini, kama tunajikaza sana, Yehova atatupatia nguvu yenye tuko nayo lazima ili tuweze kujizuia. (2 Pe. 1:5-8) Atatusaidia kuzuia mawazo, maneno, na matendo yetu. Tuko hakika na jambo hilo kwa sababu Paul na Marco, wenye tulizungumuzia, wote wawili walijifunza kuzuia kasirani yao. Fikiria pia mufano wa ndugu mwenye alikuwa anakasirika mara mingi wakati alikuwa anatembeza motokari, hata alikuwa anabishana na watu wengine wenye kutembeza motokari. Alifanya nini juu ya hali hiyo? Anasema hivi: “Nilisali sana kila siku. Nilijifunza habari zenye kuzungumuzia sifa ya kujizuia na niliweka mu akili maandiko fulani yenye kusaidia. Hata kama nimejikaza kufanya vile kwa miaka mingi, ninaendelea kujikumbusha kila asubui kama ninapenda kubakia kimya. Na wakati ninaenda mahali fulani, ninatoka mbele ya wakati ili nisikuwe haraka.”

WAKATI TUNASHINDWA KUONYESHA SIFA YA KUJIZUIA

Wakati fulani, tutashindwa kuonyesha sifa ya kujizuia. Kama jambo hilo linatokea, tunaweza kusikia haya sana kumukaribia Yehova katika sala. Lakini ni wakati huo njo tunapaswa kusali sana. Kwa hiyo, sali kwa Yehova palepale. Umuombe musamaha, tafuta musaada wake, na uazimie kuepuka kufanya makosa ileile. (Zb. 51:9-11) Yehova hatazarau sala yako yenye kutoka mu moyo ya kumuomba rehema. (Zb. 102:17) Mutume Yohana anatukumbusha kama damu ya Mwana wa Mungu “inatusafisha kutoka katika zambi yote.” (1 Yo. 1:7; 2:1; Zb. 86:5) Kumbuka kama Yehova anaambia watumishi wake wasamehe tena na tena. Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama atatusamehe sisi pia tena na tena.​—Mt. 18:21, 22; Kol. 3:13.

Yehova hakufurahi wakati Musa alipoteza sifa ya kujizuia kwa wakati fulani katika jangwa. Lakini, Yehova alimusamehe. Na Neno la Mungu linaonyesha kama Musa alikuwa mwanaume muaminifu sana mwenye tunapaswa kuiga. (Kum. 34:10; Ebr. 11:24-28) Yehova hakumuruhusu Musa aingie mu Inchi ya Ahadi, lakini atamuruhusu aingie mu Paradiso hapa ku dunia na atamupatia tumaini la kuishi milele. Tunaweza pia kuwa na tumaini hilo kama tunaendelea kujikaza ili kuonyesha sifa hiyo ya lazima ya kujizuia.​—1 Ko. 9:25.