Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kutenda Kupatana na Milio ya Tarumbeta Leo

Kutenda Kupatana na Milio ya Tarumbeta Leo

SISI wote tunaamini kama Yehova iko anaongoza na kutegemeza watu wake kwa njia ya kiroho katika hizi “siku za mwisho.” (2 Ti. 3:1) Lakini, sisi wote tunapaswa kumutii Yehova. Tunaweza kulinganisha hali yetu na hali ya Waisraeli katika jangwa. Walipaswa kutenda kupatana na milio ya tarumbeta.

Yehova alimuomba Musa atengeneze tarumbeta mbili za feza kwa kutumia nyundo (marteau) ili zitumiwe “kuita mukusanyiko na kuvunja kambi.” (Hes. 10:2) Makuhani walipaswa kupiga tarumbeta kwa njia mbalimbali ili kuonyesha mambo yenye watu walipaswa kufanya. (Hes. 10:3-8) Leo, watu wa Mungu wanapata maagizo katika njia mbalimbali. Fikiria njia tatu zenye zinatukumbusha milio ya tarumbeta ya wakati wa zamani. Njia hizo ni wakati watu wa Mungu leo wanaalikwa kuhuzuria mikusanyiko mikubwa, wakati wazee wenye wamewekwa wanapewa mazoezi, na wakati maagizo kwa makutaniko yote inarekebishwa ao kubadilishwa.

WAKATI TUNAALIKWA KUHUZURIA MIKUSANYIKO MIKUBWA

Wakati Yehova alipenda “mukusanyiko wote” ukutane kwenye muingilio wa hema ya mukutano upande wa mashariki, makuhani walipiga tarumbeta zote mbili. (Hes. 10:3) Makabila yote, yenye ilipiga kambi kuzunguka hema ya mukutano katika migawanyo ine, ilisikia mulio huo. Wale wenye walipiga kambi karibu na hema ya mukutano wangeweza kuja katika dakika kidogo. Wengine walikuwa mbali sana na pengine walikuwa na lazima ya wakati na nguvu mingi ili kufika. Ikuwe walikuwa mbali ao karibu, Yehova alipenda wote wakusanyike na kupata faida.

Leo, hatukusanyike kwenye hema ya mukutano, lakini tunaalikwa kuhuzuria mikusanyiko mikubwa ya watu wa Mungu. Mikusanyiko hiyo mikubwa inatia ndani mikusanyiko ya eneo na matukio ingine ya pekee, kwenye tunapata habari za maana na muongozo. Katika inchi mbalimbali mu dunia yote, watu wa Yehova wanafurahia programu ileile. Kwa hiyo, wale wote wenye wanakubali mwaliko wa kuhuzuria wanakusanyika wakiwa kikundi cha watu wenye furaha. Wamoja wanapaswa kusafiri mbali zaidi kuliko wengine. Lakini, wale wenye wanakubali mualiko wanajionea kama bidii yao haiko ya bure.

Vikundi vyenye kuwa mbali sana na mahali kwenye mikusanyiko hiyo mikubwa inafanywa vinaweza pia kufaidika? Kupitia teknolojia ya sasa, watu wengi wa vikundi hivyo wanaweza kufaidika na programu ileile na hata kujisikia kuwa sehemu ya mikusanyiko mikubwa. Kwa mufano, wakati mujumbe wa makao makubwa alitembelea tawi ya Benini, tawi hiyo ilitumia teknolojia ya sasa ili kusaidia ndugu wa muji wa Arlit, mu inchi ya Niger, katika Jangwa la Sahara wafuate programu hiyo kwa wakati uleule. Watu makumi mbili na moja, wenye kutia ndani ndugu, dada, na watu wenye kupendezwa walikusanyika. Hata kama walikuwa mbali, walijisikia kuwa pamoja na watu 44 131 wenye walihuzuria mukusanyiko huo mukubwa. Ndugu mumoja aliandika hivi: “Tunawashukuru kwa moyo wote kwa kufanya mipango ili sisi pia tufuate programu hii kwa wakati uleule pamoja na ninyi. Ilituonyesha tena kama munatupenda sana.”

WAKATI WAZEE WANAALIKWA ILI KUPATA MAZOEZI ZAIDI

Wakati makuhani Waisraeli walipiga tarumbeta moja tu, “wakubwa peke yao, vichwa vya maelfu,” njo walipaswa kuja kwenye hema ya mukutano. (Hes. 10:4) Pale, Musa alikuwa anawatolea habari na mazoezi kutoka kwa Yehova. Habari hizo na mazoezi yenye walipewa vilikuwa vinawasaidia kutimiza madaraka yao katika makabila yao. Kama ungekuwa kati ya wakubwa hao, kwa kweli, ungefanya mambo yote yenye ungeweza ili ukuwe pale na kupata faida, haiko vile?

Leo, wazee wa makutaniko hawako “wakubwa”; na hawako mabwana juu ya kundi la Mungu lenye wanachunga. (1 Pe. 5:1-3) Lakini, kwa kweli wanafanya mambo yote yenye wanaweza ili kuchunga kundi. Kwa hiyo, wako tayari kukubali wakati wanaalikwa ili kupewa mazoezi zaidi, kwa mufano ku Masomo ya Huduma ya Ufalme. Kwenye ile masomo, wazee wanajifunza namna ya kushugulikia muzuri zaidi mambo ya kutaniko. Mazoezi yenye wanapata kwenye masomo hiyo inasaidia wazee na hata watu wote mu kutaniko wakuwe na hali ya muzuri zaidi ya kiroho. Hata kama haujahuzuriaka ile masomo, unaweza kupata faida kwa sababu wale wenye walihuzuria wanatumia mambo yenye walijifunza ili kusaidia kutaniko.

WAKATI TUNAOMBWA KUFANYA MABADILIKO

Wakati fulani, makuhani Waisraeli walipiga tarumbeta kwa mulio wenye kubadilika-badilika. Mulio huo ulionyesha kama Yehova alipenda kambi yote ihame. (Hes. 10:5, 6) Wakati watu walihamisha kambi, walifanya vile kwa njia yenye kupangwa muzuri, lakini ilikuwa kazi ya nguvu sana kwa kila mutu. Wakati fulani, pengine Waisraeli fulani walisita kuhamia nafasi ingine. Juu ya nini?

Pengine wamoja waliwaza kama mulio wa kuhama haukuwa unakawia kuja na ulikuja bila kutazamia. “Wakati fulani wingu hilo lilisimama tu kuanzia mangaribi mupaka asubui.” Wakati mwingine, iliomba “siku mbili, mwezi mumoja, ao wakati murefu zaidi” mbele wahame. (Hes. 9:21, 22) Na kambi ilihama mara ngapi? Hesabu sura ya 33 inataja nafasi 40 hivi kwenye Waisraeli walipiga kambi.

Wakati fulani, Waisraeli wamoja walipata nafasi yenye ilikuwa na kivuli. Walikuwa wanafurahi sana kupata kivuli katika lile “jangwa lote kubwa na lenye kuogopesha.” (Kum. 1:19) Kwa hiyo, Waisraeli wangeshawishiwa kuwaza kama wangehamia nafasi ya mubaya sana.

Wakati makabila ilianza kuhama, Waisraeli fulani walipaswa kuonyesha uvumilivu ili wachunge wakati wao wa kuondoka. Wote walikuwa wanasikia mulio wa tarumbeta wenye kubadilika-badilika, lakini wote hawakukuwa wanaenda kwa wakati uleule. Ule mulio ulionyesha makabila yenye ilipiga kambi upande wa mangaribi, ni kusema, Yuda, Isakari, na Zabuloni, kama walipaswa kuondoka. (Hes. 2:3-7; 10:5, 6) Kisha wao kuondoka, makuhani walikuwa wanapiga mulio wa tarumbeta wenye kubadilika-badilika kwa mara ya pili ili kuonyesha mugawanyo wa makabila tatu yenye ilipiga kambi upande wa kusini kama walipaswa kuondoka. Makuhani waliendelea kufanya vile mupaka wakati kambi yote iliondoka.

Pengine wakati fulani haukufurahia mabadiliko fulani yenye ilifanywa katika tengenezo. Pengine uliona kama mabadiliko imekuwa mingi sana na pengine haukutazamia kama itatokea. Ao pengine ulikuwa umezoea namna mambo fulani ilikuwa inafanywa na haukupenda kukuwe mabadiliko. Hata sababu ikuwe nini, inawezekana uliona kuwa ni vigumu kwako kukuwa muvumilivu ili ufikie kuzoea ile mabadiliko. Lakini, kama tunajikaza sana ili kujipatanisha na ile mabadiliko, kwa kweli tutaona kama Yehova iko anatubariki.

Katika siku za Musa, Yehova aliongoza mamilioni ya wanaume, wanamuke, na watoto katika jangwa. Bila musaada na muongozo wake, hawangeweza kuokoka. Leo, Yehova anatuongoza katika hizi siku za mwisho zenye kuwa hatari. Anatusaidia tuendelee kuwa nguvu kiroho! Kwa hiyo, sisi wote tuazimie kutenda kupatana na milio mbalimbali ya tarumbeta, kama vile Waisraeli waaminifu walifanya!