Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Sifa zenye kutajwa katika Wagalatia 5:22, 23 njo sehemu zote za “tunda la roho”?

Mistari hiyo inataja sifa kenda zenye Mukristo anapaswa kukomalisha: “Tunda la roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, fazili, wema, imani, upole, kujizuia.” Lakini, haiko zile tu njo sifa za muzuri zenye roho ya Mungu inaweza kutusaidia kukomalisha.

Ona mambo yenye mutume Paulo aliandika katika mistari yenye kutangulia: “Matendo ya mwili . . . ni uasherati, uchafu, mwenendo mupotovu wa bila haya, ibada ya sanamu, kupashana habari na pepo wachafu, uadui, mizozo, wivu, milipuko ya kasirani, magomvi, migawanyiko, mazehebu, kutamani, ulevi, karamu za kupitisha mipaka, na mambo kama hayo.” (Gal. 5:19-21) Kwa hiyo, Paulo hakutaja mambo yote yenye kuwa kati ya “matendo ya mwili.” Angeweza kutaja mambo ingine kama ile yenye inazungumuziwa mu Wakolosai 3:5. Ni vile pia kuhusu sifa zenye kutajwa katika Wagalatia 5:22, 23, Paulo hakutaja sifa zote zenye roho takatifu inaweza kutusaidia kukomalisha.

Tunaelewa jambo hilo wakati tunalinganisha sifa za tunda la roho na mambo yenye Paulo aliandikia kutaniko la Efeso. Alisema hivi: “Tunda la mwangaza ni kila namna ya wema, na haki, na kweli.” (Efe. 5: 8, 9) Kwa kweli, “wema,” pamoja na haki na kweli, ni sehemu ya “tunda la mwangaza,” lakini “wema” ni sehemu ya “tunda la roho” pia.

Vilevile, Paulo alimutia Timoteo moyo ‘afuatilie haki, ushikamanifu kwa Mungu, imani, upendo, uvumilivu, na upole,’ sifa sita za muzuri. (1 Ti. 6:11) Sifa ine tu kati ya sifa hizo (imani, upendo, upole, na uvumilivu) njo zenye zinatajwa kuwa sehemu za “tunda la roho.” Lakini, Timoteo alikuwa na lazima ya musaada wa roho takatifu ili kukomalisha pia sifa zingine zenye kutajwa: haki na ushikamanifu kwa Mungu.​—Linganisha na Wakolosai 3:12; 2 Petro 1:5-7.

Kwa hiyo, andiko la Wagalatia 5:22, 23 halitaje sifa zote zenye Mukristo anapaswa kukomalisha. Roho takatifu ya Mungu inaweza kutusaidia kukomalisha zile sifa kenda zenye zinatajwa kuwa “tunda la roho.” Lakini, kuko sifa zingine zenye tunapaswa kukomalisha ili tukuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho na “kuvaa utu mupya wenye uliumbwa kupatana na mapenzi ya Mungu katika haki ya kweli, na ushikamanifu.”​—Efe. 4:24.