Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 24

“Unganisha Moyo Wangu ili Niogope Jina Lako”

“Unganisha Moyo Wangu ili Niogope Jina Lako”

“Unganisha moyo wangu ili niogope jina lako. Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote.”​—ZB. 86:11, 12.

WIMBO 7 Yehova, Nguvu Yetu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kumuogopa Mungu maana yake nini, na juu ya nini ni jambo la maana kwa wale wenye kumupenda Yehova?

WAKRISTO wanamupenda Mungu, lakini pia wanamuogopa. Watu fulani wanaweza kuona kama ile mawazo mbili inapingana. Lakini, hapa hatuzungumuzie woga wenye unafanya mutu atetemeke. Tutazungumuzia aina ya pekee ya woga. Watu wenye kuwa na aina hiyo ya woga wanamuogopa Mungu sana na wanamuheshimia kwelikweli. Hawapendi kumuchukiza Baba yao wa mbinguni kwa sababu hawapendi kuharibu urafiki wao pamoja naye.​—Zb. 111:10; Mez. 8:13.

2. Kulingana na maneno ya Mufalme Daudi yenye kuwa mu Zaburi 86:11, tutazungumuzia mambo gani mbili?

2 Soma Zaburi 86:11. Wakati unafikiria ile maneno, unaweza kuona kama Daudi, mufalme muaminifu, alielewa kama ni jambo la maana kumuogopa Mungu. Sasa, tuzungumuzie namna tunaweza kutumia maneno ya Daudi yenye iliongozwa na roho ya Mungu. Kwanza, tutazungumuzia juu ya nini tunapaswa kuogopa sana jina la Mungu. Pili, tutazungumuzia namna tunaweza kuonyesha kama tunaogopa jina la Mungu mu maisha yetu ya kila siku.

JUU YA NINI TUNAPASWA KUOGOPA SANA JINA LA MUNGU?

3. Ni tukio gani lenye pengine lilimusaidia Musa aendelee kuogopa jina la Mungu?

3 Wazia namna Musa alijisikia wakati alikuwa anashutama katika shimo ndani ya mwamba na kuona utukufu wa Yehova wenye ulipita mbele yake. Kitabu Étude perspicace des Écritures kinasema kama hilo “pengine lilikuwa tukio la kushangaza zaidi lenye mutu alikuwa ameona mbele ya kuja kwa Yesu Kristo.” Musa alisikia maneno yenye kufuata, yenye pengine ilisemwa na malaika: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema na huruma, hakasirike haraka na ni mwenye upendo mwingi mushikamanifu na kweli, mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu kwa maelfu, mwenye kusamehe kosa na uovu na zambi.” (Kut. 33:17-23; 34:5-7) Inawezekana wakati Musa alikuwa anatumia jina Yehova alikuwa anakumbuka ile mambo yenye alionaka. Njo maana kisha wakati fulani, Musa alionya Waisraeli ‘waogope jina hili lenye utukufu na lenye kuogopesha sana.’​—Kum. 28:58.

4. Ni nini inaweza kutusaidia tumuogope Yehova sana?

4 Wakati tunafikiri juu ya jina Yehova, ni muzuri pia tufikiri sana juu ya mwenye jina hilo. Tunapaswa kufikiri juu ya sifa zake, kama vile nguvu zake, hekima yake, haki yake, na upendo wake. Kufikiri juu ya sifa hizo na sifa zingine kunaweza kufanya tumuogope sana.​—Zb. 77:11-15.

5-6. (a) Jina la Mungu liko na maana gani? (b) Kulingana na Kutoka 3:13, 14 na Isaya 64:8, Yehova anafanya mambo itendeke katika njia gani?

5 Tunajua nini kuhusu maana ya jina la Mungu? Watu wengi wenye elimu wanakubali kama, inaonekana jina Yehova linamaanisha “Yeye Anafanya Kuwa.” Maana ya jina la Mungu inatukumbusha kama hakuna kitu chenye kinaweza kumuzuia Yehova kutimiza mapenzi yake, na anaweza kufanya mambo itendeke. Namna gani?

6 Yehova anafanya mambo itendeke kwa kujifanya yeye mwenyewe kuwa kila kitu chenye kinahitajika ili kutimiza kusudi lake. (Soma Kutoka 3:13, 14.) Tumetiwa moyo mara mingi kufikiria sehemu hiyo yenye kushangaza ya utu wa Mungu. Yehova anaweza pia kufanya watumishi wake wenye hawakamilike wakuwe kile kinahitajiwa ili kumutumikia na kutimiza kusudi lake. (Soma Isaya 64:8.) Katika njia hizo, Yehova anafanya mapenzi yake itimie. Hakuna kitu chenye kinaweza kumuzuia kufanya mapenzi yake itimie.​—Isa. 46:10, 11.

7. Tunaweza kufanya nini ili kumupenda na kumuheshimia zaidi Baba yetu wa mbinguni?

7 Tunaweza kumupenda na kumuheshimia zaidi Baba yetu wa mbinguni kwa kufikiri sana juu ya mambo yenye amefanya na mambo yenye ametuwezesha kufanya. Kwa mufano, wakati tunafikiri sana juu ya vitu vya ajabu vyenye aliumba, tunashangaa sana juu ya mambo yenye amefanya. (Zb. 8:3, 4) Na wakati tunafikiri sana juu ya mambo yenye Yehova ametuwezesha kufanya, tunamuheshimia sana. Jina Yehova ni la ajabu kabisa! Linaonyesha yeye ni nani, mambo yote yenye amefanya, na mambo yote yenye atafanya.​—Zb. 89:7, 8.

“NITATANGAZA JINA LA YEHOVA”

Mafundisho ya Musa ilikuwa yenye kutia moyo. Ilikazia sana jina la Yehova Mungu na sifa zake (Ona fungu la 8) *

8. Kulingana na Kumbukumbu la Torati 32:2, 3, Yehova anapenda tufanye nini kuhusu jina lake?

8 Mbele tu Waisraeli waingie mu Inchi ya Ahadi, Yehova alimufundisha Musa maneno ya wimbo fulani. (Kum. 31:19) Musa pia alipaswa kufundisha watu wimbo huo. (Soma Kumbukumbu la Torati 32:2, 3.) Wakati tunafikiri sana juu ya mustari wa 2 na wa 3, tunaona wazi kama Yehova hapendi jina lake lifichwe, ao lionwe kuwa takatifu sana kwa kiasi ya kwamba halipaswe kutamukwa. Anapenda kila mutu ajue jina lake! Waisraeli walifurahi sana wakati Musa aliwafundisha juu ya Yehova na juu ya jina lake lenye utukufu! Mambo yenye Musa aliwafundisha ilitia nguvu imani yao na iliwatia moyo, kama vile mvua ya kidogo-kidogo inafanya mimea ikomae muzuri. Tunaweza kufanya nini ili namna yetu ya kufundisha ikuwe vile?

9. Tunaweza kufanya nini ili kusaidia kutakasa jina la Yehova?

9 Wakati tunahubiri nyumba kwa nyumba ao mahali pa watu wengi, tunaweza kutumia Biblia ili kuonyesha watu jina la pekee la Mungu, Yehova. Tunaweza kuwatolea vichapo vya muzuri, video za muzuri, na mambo mbalimbali yenye kumutukuza Yehova yenye kuwa ku site yetu ya Enternete. Ku kazi, ku masomo, ao wakati tunasafiri, tunaweza kupata nafasi za kuzungumuza juu ya Mungu wetu mupendwa na juu ya sifa zake. Wakati tunaambia watu wenye tunakutana nao juu ya kusudi la muzuri la Yehova kuhusu wanadamu na dunia, tunawasaidia kujua kama Yehova anawapenda kabisa. Wakati tunaambia wengine kweli juu ya Baba yetu mwenye upendo, tunasaidia kutakasa jina lake. Tunasaidia watu kuelewa kama wamefundishwa mambo mingi ya uongo juu yake. Hakuna mafundisho yenye kutia moyo zaidi kuliko mafundisho ya Biblia yenye tunatolea watu.​—Isa. 65:13, 14.

10. Wakati tunaongoza mafunzo ya Biblia, juu ya nini hatupaswe tu kufundisha wanafunzi sheria na kanuni za Mungu?

10 Wakati tunaongoza mafunzo ya Biblia, tunapenda kusaidia wanafunzi wetu wafikie kujua na kutumia jina la Yehova. Tena, tunapenda kuwasaidia wafikie kumujua Yehova muzuri. Unawaza kama kuwafundisha tu maagizo, kanuni za Mungu, na pia sheria za mwenendo njo itawasaidia? Mwanafunzi muzuri anaweza kujifunza sheria za Mungu, na hata kuzipenda. Lakini, ule mwanafunzi atamutii Yehova kwa sababu anamupenda? Kumbuka kama Eva alijua sheria ya Mungu, lakini, hakupenda kabisa Ule mwenye alitoa sheria hiyo, na Adamu pia hakumupenda. (Mwa. 3:1-6) Kwa hiyo, hatupaswe tu kufundisha watu sheria na kanuni za Mungu za haki.

11. Wakati tunafundisha wanafunzi juu ya sheria na kanuni za Mungu, namna gani tunaweza kuwasaidia wafikie kumupenda Ule mwenye alitoa sheria hizo?

11 Sheria na kanuni za Yehova ni za muzuri kwetu. (Zb. 119:97, 111, 112) Lakini, wanafunzi wetu wataziona pia vile kama tu wanaelewa kuwa Yehova anatupatia sheria hizo kwa sababu anatupenda. Kwa hiyo, tunaweza kuuliza wanafunzi wetu hivi: “Unawaza ni juu ya nini Mungu anaomba watumishi wake wafanye hivi ao wasifanye vile? Ile inatufundisha nini juu yake?” Kama tunasaidia wanafunzi wetu wafikiri juu ya Yehova na kupenda kabisa jina lake lenye utukufu, tunaweza kabisa kugusa moyo wao. Wanafunzi wetu watafikia kupenda sheria na pia watapenda Ule mwenye alitoa sheria hizo. (Zb. 119:68) Watakuwa na imani yenye nguvu na watakuwa na uwezo wa kuvumilia majaribu makali yenye inaweza kuwafikia.​—1 Ko. 3:12-15.

“TUTATEMBEA KATIKA JINA LA YEHOVA”

Wakati fulani Daudi aliacha moyo wake ugawanyike (Ona fungu la 12)

12. Wakati fulani, namna gani Daudi alishindwa kuendelea kuwa na moyo wenye haugawanyike, na jambo hilo lilileta matokeo gani?

12 Maneno ya maana yenye kuwa mu Zaburi 86:11 ni “unganisha moyo wangu.” Mufalme Daudi aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika ile maneno. Katika maisha yake, aliona kama ni mwepesi kabisa kuacha moyo wetu ugawanyike. Wakati fulani, alikuwa ku sehemu ya juu ya nyumba yake na akaona bibi wa mwanaume mwingine iko anaoga. Wakati huo, moyo wa Daudi ulikuwa kamili ao wenye kugawanyika? Alijua sheria ya Yehova yenye ilisema hivi: “Haupaswe kutamani bibi ya mwenzako.” (Kut. 20:17) Lakini, inaonekana kuwa aliendelea kuangalia ule mwanamuke. Moyo wake uligawanyika kati ya tamaa yake kumuelekea ule mwanamuke, Bat-sheba, na nia yake ya kumufurahisha Yehova. Hata kama Daudi alikuwa amemupenda Yehova na kumuogopa kwa wakati murefu, alishindwa kuzuia tamaa yake. Katika hali hiyo, Daudi alifanya mambo ya mubaya. Alichafua jina la Yehova. Pia, Daudi aliletea matokeo ya mubaya sana watu wenye hawakukuwa na kosa, hata watu wa familia yake mwenyewe.​—2 Sa. 11:1-5, 14-17; 12:7-12.

13. Ni nini inatuonyesha kama moyo wa Daudi uliunganishwa tena?

13 Yehova alimupatia Daudi nizamu, na kisha Daudi akakuwa tena na urafiki muzuri pamoja na Yehova. (2 Sa. 12:13; Zb. 51:2-4, 17) Daudi alikumbuka huzuni na matatizo yenye ilitokea wakati aliacha moyo wake ugawanyike. Maneno yake yenye kuwa mu Zaburi 86:11 inaweza pia kutafsiriwa hivi: “Unipatie moyo wenye haugawanyike.” Yehova alimusaidia Daudi akuwe tena na moyo kamili, ao wenye haugawanyike? Ndiyo, kwa sababu kisha wakati fulani Neno la Yehova lilionyesha kama Daudi alikuwa mwanaume mwenye “moyo . . . kamili kumuelekea Yehova Mungu wake.”​—1 Fa. 11:4; 15:3.

14. Tunapaswa kujiuliza nini, na juu ya nini?

14 Mufano wa Daudi unatutia moyo na pia unatuonya. Namna aliangukia katika zambi nzito ni onyo kwa watumishi wa Mungu leo. Ikuwe umeanza kumutumikia Yehova hivi karibuni ao umemutumikia kwa miaka mingi, ni muzuri ujiulize hivi: ‘Niko napinga majaribu yenye Shetani iko anatumia ili kugawanya moyo wangu?’

Shetani atatumia kila njia ili kujaribu kugawanya moyo wako. Usimuruhusu afanye vile! (Ona fungu la 15-16) *

15. Namna gani kumuogopa Mungu kunaweza kutulinda wakati tunaona picha zenye zinaweza kuchochea tamaa ya ngono?

15 Kwa mufano, kama unaona picha ku televizyo ao ku Enternete, yenye inaweza kuchochea tamaa ya ngono, unafanyaka namna gani? Inaweza kuwa mwepesi kuwaza kama ile picha ao filme haionyeshe kabisa mambo ya pornografia. Lakini, pengine ni njia yenye Shetani anatumia ili kugawanya moyo wako. (2 Ko. 2:11) Picha hiyo inaweza kufananishwa na shoka yenye mutu anatumia ili kupasua kipande kikubwa cha muti. Kwanza, mutu anapiga sehemu ya makali ya shoka ndani ya kipande cha muti. Wakati anaingiza shoka ndani kabisa, kile kipande cha muti kinapasuka. Picha yenye kuchochea tamaa ya ngono inaweza kuwa kama ile sehemu ya makali ya shoka. Kitu fulani cha kidogo na chenye kinaonekana kuwa hakina hatari kinaweza kugawanya moyo wa mutu na kumuongoza afanye zambi na kuvunja uaminifu-mushikamanifu wake. Kwa hiyo, kataa kabisa kuingiza jambo lolote la mubaya mu moyo wako! Endelea kufanya moyo wako ukuwe kamili ili kuogopa jina la Yehova!

16. Wakati tunapata vishawishi, ni muzuri tujiulize maulizo gani?

16 Zaidi ya picha zenye kuchochea tamaa ya ngono, Shetani anatumia mambo ingine mingi ili kutushawishi tufanye mambo ya mubaya. Wakati tunajikuta mbele ya ile mambo, tunafanyaka namna gani? Ni mwepesi kuwaza kama ile mambo haiko ya mubaya kabisa. Kwa mufano, tunaweza kuwaza hivi: ‘Hata kama ninafanya hivi sitatengwa, maana yake haiko jambo nzito sana.’ Ile mawazo ni ya mubaya kabisa. Ni muzuri tujiulize maulizo kama vile: ‘Shetani anajaribu kutumia jambo hili ili kugawanya moyo wangu? Kama ninashindwa na tamaa za mubaya, nitachafua jina la Yehova? Kufanya hivi kutanisaidia nimukaribie Mungu wangu, ao kutaharibu urafiki wangu pamoja naye?’ Fikiri sana juu ya ile maulizo. Umuombe Mungu hekima ili ujibu ile maulizo bila kujidanganya. (Yak. 1:5) Kufanya vile kunaweza kukulinda kabisa. Kunaweza kukusaidia upinge kabisa vishawishi, kama vile Yesu alifanya wakati alisema hivi: “Toka mbele yangu, Shetani!”​—Mt. 4:10.

17. Juu ya nini haiko muzuri kuwa na moyo wenye kugawanyika? Leta mufano.

17 Haiko muzuri kuwa na moyo wenye kugawanyika. Wazia timu fulani ya wachezaji wa kabumbu wenye hawasikilizane. Wamoja wanapenda kujiletea tu utukufu, wengine kidogo hawapendi kufuata sheria za michezo, na wengine wanazarau mutu wa kuwazoeza. Ni vigumu kwa timu hiyo kupata ushindi katika muchezo. Lakini, inawezekana kabisa kuwa timu yenye iko na umoja itapata ushindi. Moyo wako unaweza kuwa kama ile timu yenye imepata ushindi ikiwa unaacha mawazo yako, tamaa zako, na namna unajisikia vikuwe na upatano wakati unamutumikia Yehova. Kumbuka kama Shetani anapenda kugawanya moyo wako. Anapenda mawazo yako, tamaa zako, na namna unajisikia mu moyo visipatane na kanuni za Yehova. Lakini, moyo wako unapaswa kuwa kamili ili uweze kumutumikia Yehova. (Mt. 22:36-38) Usimuruhusu hata kidogo Shetani agawanye moyo wako!

18. Kulingana na maneno ya Mika 4:5, unaazimia kufanya nini?

18 Sali kwa Yehova kama vile Daudi alifanya. Alisali hivi: “Unganisha moyo wangu ili niogope jina lako.” Ujikaze sana kuendelea kuishi kupatana na maneno ya ile sala. Kila siku, uazimie kukamata maamuzi yenye inaonyesha kama unaogopa sana jina la Yehova, ikuwe maamuzi makubwa ao ya kidogo. Ukifanya vile, kwa sababu uko Shahidi wa Yehova, utaletea utukufu jina la Yehova. (Mez. 27:11) Na sisi wote tutaweza kusema kama nabii Mika mwenye alisema hivi: “Tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu milele na milele.”​—Mik. 4:5.

WIMBO 41 Tafadhali Sikiliza Sala Yangu

^ fu. 5 Katika habari hii, tutazungumuzia maneno fulani yenye Mufalme Daudi alisema mu sala yake yenye kuwa mu Zaburi 86:11, 12. Kuogopa jina la Yehova maana yake nini? Ni sababu gani fulani zenye kufanya tuogope sana jina hilo kubwa? Na namna gani kumuogopa Mungu kunaweza kutulinda ili tusishindwe wakati tunapata majaribu?

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Musa alifundisha watu wa Mungu wimbo wenye ulimutukuza Yehova.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Eva hakuzuia tamaa za mubaya. Tofauti na yeye, tunakataa picha ao habari zenye zinaweza kuchochea tamaa za mubaya na kutufanya tuchafue jina la Mungu.