Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 23

Hauko Peke Yako Juu Sikuzote Yehova Iko na Weye

Hauko Peke Yako Juu Sikuzote Yehova Iko na Weye

“Yehova iko karibu na wale wote wenye kumuita.”​—ZB. 145:18.

WIMBO 28 Rafiki ya Yehova Ni Nani?

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni sababu gani zinaweza kufanya watumishi fulani wa Yehova wajisikie kuwa peke yao?

WAKATI fulani wengi kati yetu wanajisikiaka kuwa peke yao. Kwa wamoja, ile hali haikawiake. Lakini kwa wengine, inakawiaka. Tunaweza kujisikia kuwa peke yetu hata wakati tuko na watu wengi. Ni nguvu kwa watu fulani kufanya urafiki mu kutaniko ya mupya. Wengine walikuwa mu familia yenye kufanya mambo mingi pamoja, lakini kisha wao kuhama mbali na watu wa familia yao, ile inafanya wajisikie kuwa peke yao. Na wengine wanajisikia kuwa peke yao juu hawawezi kuzungumuza tena na mutu mwenye walipenda sana mwenye alishakufa. Na Wakristo fulani, zaidi sana wenye wanatoka tu kujifunza kweli, wanajisikia kuwa peke yao wakati watu wa familia yao na marafiki wao wenye hawamuabudu Yehova wanawakatala ao wanawatesa.

2. Tutajibia maulizo gani?

2 Yehova anajua na anaelewa mambo yote yenye inatuhusu. Wakati tunajisikia kuwa peke yetu, Yehova anajua na anapenda kutusaidia tupiganishe ile mawazo. Namna gani Yehova anaweza kutusaidia? Ni mambo gani tunaweza kufanya ili kujisaidia? Na namna gani tunaweza kusaidia wengine mu kutaniko wenye wanajisikia kuwa peke yao? Tuone basi majibu ya ile maulizo.

YEHOVA ANATUHANGAIKIA

Yehova alituma malaika wake ili kumuhakikishia Eliya kama hakukuwa peke yake (Ona fungu la 3)

3. Namna gani Yehova alionyesha kama anamuhangaikia Eliya?

3 Yehova anapenda waabudu wake wote wakuwe na furaha. Iko karibu na kila mumoja wetu, na anajua wakati tunahuzunika ao kuvunjika moyo. (Zb. 145:18, 19) Ona namna Yehova alihangaikia nabii wake Eliya. Ule mwanaume muaminifu aliishi mu kipindi ya nguvu sana mu historia ya Waisraeli. Mu Israeli, watu wenye uwezo na wenye hawakumupenda Yehova, walitesa wale wenye walimuabudu na walipenda zaidi sana kumuua Eliya. (1 Fa. 19:1, 2) Na pengine Eliya aliwaza kama ni yeye tu njo nabii mwenye alikuwa angali muzima; na inawezekana ile ilimuvunja moyo hata zaidi. (1 Fa. 19:10) Bila kukawia, Yehova alifanya jambo fulani ili kumusaidia. Yehova alituma malaika ili kumuhakikishia nabii Eliya kama hakukuwa ye peke na ule malaika alimuambia Eliya kama kulikuwa Waisraeli wengine wengi wenye walikuwa wanamutumikia Yehova kwa uaminifu!​—1 Fa. 19:5, 18.

4. Namna gani Marko 10:29, 30 inaonyesha namna Yehova anahangaikia watumishi wake wenye pengine wanakosa musaada wa wengine?

4 Yehova anajua kama wakati tunachagua kumutumikia, wamoja kati yetu wanaweza kupoteza musaada kutoka kwa watu wa familia yao, na marafiki wao wenye hawamutumikie Yehova. Pengine, juu alikuwa na woga, mutume Petro alimuuliza Yesu hivi: “Tumeacha vitu vyote na tumekufuata, basi tutapata nini?” (Mt. 19:27) Kwa upole Yesu aliambia wanafunzi wake kama wangepata familia kubwa ya kiroho. (Soma Marko 10:29, 30.) Na Yehova, kichwa ya familia yetu ya kiroho, anaahidi kama atategemeza wale wote wenye wanapenda kumutumikia. (Zb. 9:10) Ona mambo fulani yenye unaweza kufanya juu upate musaada wa Yehova ili kupiganisha hali ya kujisikia kuwa peke yako.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA KAMA UNAJISIKIA KUWA PEKE YAKO

5. Kufikiria namna Yehova iko anakusaidia, kunaleta faida gani?

5 Fikiria namna Yehova iko anakusaidia. (Zb. 55:22) Ile itakusaidia uendelee kuwa na maoni ya muzuri kuhusu hali yako. Dada Carol, * mwenye hajaolewa na mwenye watu wa familia yake hawako Mashahidi, anasema hivi: “Wakati nakumbuka na kufikiri sana juu ya namna Yehova alinisaidia mu magumu yangu, ile inanisaidia sana nisijisikie kuwa peke yangu. Na ile inanihakikishia kama Yehova ataendelea kunisaidia.”

6. Namna gani 1 Petro 5:9, 10 inaweza kutia moyo wale wenye wanajisikia kuwa peke yao?

6 Fikiria namna Yehova iko anasaidia ndugu na dada wenye wanajisikia kuwa peke yao. (Soma 1 Petro 5:9, 10.) Hiroshi, mwenye watu wa familia yake hawako Mashahidi wa Yehova na mwenye amemutumikia Yehova kwa miaka mingi, anasema hivi: “Mu kutaniko ni mwepesi kuona kama kila mutu iko na magumu yake. Kujua kama siye wote tunajikaza kumutumikia Yehova kunaweza kutia moyo wale wenye watu wa familia yao hawako Mashahidi wa Yehova.”

7. Sala inaweza kukusaidia namna gani?

7 Endelea kuwa na programu ya muzuri ya kiroho. Ile inatia ndani kumuambia Yehova namna unajisikia. (1 Pe. 5:7) Wakati Massiel, dada mumoja kijana, aliamua kujifunza kweli, watu wa familia yake walimukatala. Ile ilifanya ajisikie kuwa peke yake. Anasema hivi: “Jambo moja ya maana sana yenye ilinisaidia nipiganishe hali ya kujisikia kuwa peke yangu, ni kusali sana kwa Yehova. Alikuwa Baba kabisa kwangu, na nilikuwa nasali kwake mara mingi kila siku; nilikuwa namumwangia moyo wangu.”

Kusikiliza usomaji wa Biblia na wa vichapo vingine vyenye kutegemea Biblia, kunaweza kusaidia watu wenye kuwa peke yao wasijisikie kuwa peke yao (Ona fungu la 8) *

8. Kusoma Neno la Mungu na kufikiri sana juu ya mambo yenye unasoma kunakusaidia namna gani?

8 Usome Neno la Mungu kwa ukawaida na ufikiri sana kuhusu habari zenye kuonyesha kama Yehova anakupenda. Bianca, dada mumoja mwenye alipaswa kuvumilia maneno ya mubaya kutoka kwa watu wa familia yake, anasema hivi: “Kusoma na kufikiri sana juu ya habari zenye kuwa mu Biblia na habari za watumishi wa Yehova wenye walikutana na magumu sawa yangu, inanisaidia sana.” Wakristo fulani wanatia mu kichwa Maandiko yenye inawaletea faida sana, kama vile Zaburi 27:10 na Isaya 41:10. Na wengine wanasikiliza usomaji wenye ulirekodiwa wa Biblia ao wa kichapo fulani ya funzo ili kutayarisha mikutano. Ile inawasaidia wasijisikie kuwa peke yao.

9. Kukusanyika kunaweza kukuletea faida gani?

9 Ujikaze kukusanyika kwa ukawaida. Kufanya vile kutakutia moyo na kutafanya ujuane na ndugu na dada. (Ebr. 10:24, 25) Massiel, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Hata kama nilikuwa nasikia haya sana niliamua kukusanyika kwa ukawaida na kutoa maelezo. Ile ilinisaidia nijisikie kuwa karibu na ndugu na dada mu kutaniko.”

10. Juu ya nini ni jambo ya maana kufanya urafiki pamoja na Wakristo waaminifu?

10 Ufanye urafiki pamoja na Wakristo waaminifu. Tafuta marafiki mu kutaniko wenye unaweza kujifunza mambo fulani kutoka kwao, ikuwe wanakupita miaka ao hapana, na hata kama wako na desturi tofauti na yako. Biblia inatukumbusha kama “wazee ndio wenye kuwa na hekima.” (Yob. 12:12) Lakini, watu wakubwa wanaweza pia kujifunza mambo mingi kwa vijana waaminifu. Hata kama Daudi alikuwa mudogo kwa Yonatani, ile haikuwazuia wasikuwe marafiki wa karibu sana. (1 Sa. 18:1) Daudi na Yonatani walisaidiana ili kumutumikia Yehova hata wakati walikuwa na magumu mingi. (1 Sa. 23:16-18) Irina, dada mumoja mwenye watu wa familia yake hawako Mashaidi wa Yehova, anasema hivi: “Ndugu na dada zetu wanaweza kabisa kufikia kuwa sawa vile wazazi wetu wa kiroho ao watu wa familia yetu. Yehova anaweza kuwatumikisha juu wakuwe familia yenye tuko nayo lazima.”

11. Tunapaswa kufanya nini juu tukuwe na urafiki wa karibu sana na wengine?

11 Haiko mwepesi kufanya urafiki na watu wengine zaidi sana kama uko mutu wa haya. Ratna, dada mumoja mwenye kuwa na haya mwenye alijifunza kweli ijapokuwa upinzani, anasema hivi: “Nilipaswa kukubali kama niko na lazima ya musaada wa ndugu na dada mu kutaniko.” Inaweza kuwa nguvu kuambia mutu mwengine namna uko unajisikia. Lakini wakati unafanya vile, ule mutu anaweza kufikia kuwa rafiki yako wa karibu. Marafiki wenye uko nao wanapenda kukutia moyo na kukutegemeza. Njo maana unapaswa kuwaambia vile unajisikia juu wajue namna wanaweza kukusaidia.

12. Namna gani mahubiri inaweza kukusaidia upate marafiki wazuri?

12 Moja kati ya njia ya muzuri zaidi ya kupata marafiki, ni kuhubiri nao. Carol, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Nilipata marafiki wazuri sana saa nilipitisha wakati pamoja na dada mu mahubiri na mu mambo ingine ya kiroho. Yehova amenitegemeza kwa miaka mingi kupitia wale marafiki.” Kila mara inakuwaka muzuri sana wakati tunafanya urafiki na Wakristo waaminifu. Yehova anatumia wale marafiki juu ya kutusaidia tupiganishe mawazo yenye kutuhangaisha, sawa vile kujisikia kuwa peke yetu.​—Mez. 17:17.

SAIDIA WENGINE WAJISIKIE SAWA VILE WAKO MU FAMILIA YETU

13. Kila mutu mu kutaniko iko na daraka gani?

13 Kila mutu iko na daraka ya kusaidia kutaniko iendelee kuwa fasi ya amani na kwenye watu wanaonyeshana upendo, juu mutu yeyote asijikie kuwa peke yake. (Yoh. 13:35) Mambo yenye tunafanya na yenye tunasema inaweza kutia wengine moyo sana. Ona jambo yenye dada mumoja alisema: “Wakati nilijifunza kweli, kutaniko njo ilikuwa familia yangu. Singefikia kuwa Shahidi wa Yehova kama ndugu na dada hawangenisaidia.” Ni mambo gani unaweza kufanya ili kusaidia ndugu ao dada fulani asijisikie kuwa peke yake mu kutaniko, juu watu wa familia yake hawako Mashahidi wa Yehova?

14. Namna gani tunaweza kufanya urafiki na wapya?

14 Ujikaze kufanya urafiki na wapya. Unaweza kuanza kufanya vile kwa kukaribisha kwa furaha wapya wenye wanakuya mu kutaniko. (Ro. 15:7) Lakini, tusiishie tu ku salamu. Tunapaswa kufanya urafiki wetu pamoja nao ukuwe nguvu sana na uendelee kuwa vile. Njo maana uwatendee kwa upole na uonyeshe kabisa kama unawahangaikia. Ujikaze pia kujua magumu yenye wako wanapata, bila kutaka kujua-jua mambo yao ya kipekee. Wamoja kati yao wanaweza kuwa na magumu ya kufasiria waziwazi mambo yenye iko mu moyo wao. Njo maana ukuwe muangalifu, usiwakaze waseme. Kuliko kufanya vile, tumia maulizo kwa busara, na uwasikilize kwa uvumilivu wakati wako wanajieleza. Kwa mufano, unaweza kuwauliza namna gani walifikia kupata kweli.

15. Namna gani Wakristo wakomavu wanaweza kusaidia wengine mu kutaniko?

15 Kila mutu mu kutaniko ataendelea kukomaa kiroho wakati Wakristo wakomavu, zaidi sana wazee, wanamuonyesha kama wanamuhangaikia. Melissa, mwenye alikomalishwa na mama yake katika kweli, anasema hivi: “Siwezi kusahau hata kidogo namna ndugu walinisaidia kama baba zangu wa kiroho, kwa miaka yote hii. Kila mara wakati niko na lazima ya kusema kitu fulani, niko na mutu mwenye iko pale kwa ajili ya kunisikiliza.” Mauricio, ndugu kijana mwenye alijisikia kuwa peke yake wakati mwalimu wake wa Biblia aliacha kweli, anasema hivi: “Wazee walionyesha kama wananihangaikia sana, na ile ilinisaidia sana. Kila mara walikuwa nazungumuza na miye. Tulihubiri nao, tulizungumuzia mali mbalimbali za kiroho zenye walipata mu funzo lao la kipekee, na hata tulicheza nao pamoja.” Mupaka leo, Melissa na Mauricio wameendelea na utumishi wa wakati wote.

Kuko mutu fulani mu kutaniko yenu mwenye atafurahia sana upitishe wakati naye? (Ona fungo la 16-19) *

16-17. Ni mu njia gani ingine tunaweza kusaidia wengine?

16 Usaidie wengine. (Gal. 6:10) Leo, mwenye ni misionere mu inchi fulani mbali na familia yake, anasema hivi: “Mara mingi, kile mutu anakuwaka nayo lazima ni kutendewa muzuri mu wakati yenye kufaa. Nakumbuka siku moja nilifanyaka aksida na gari, kisha nikarudia ku nyumba. Kusema kweli, ile hali ilinihangaisha sana mu akili. Lakini kisha pale, bwana fulani na bibi yake, walinialika kwao juu ya kutumia nao chakula. Sikumbuke kama tulikulaka nini ile siku, lakini nakumbuka kama walinisikiliza kwa upole. Na ku mwisho, nilijisikia muzuri zaidi!”

17 Siye wote tunafurahiaka saa tunapitisha wakati pamoja na Mashahidi wengine na kuzungumuzia hotuba zenye tulisikia ku mikusanyiko ya muzunguko ao ya eneo. Lakini, Carol, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Najisikiaka kuwa peke yangu zaidi sana ku mikusanyiko ya muzunguko na ya eneo.” Juu ya nini? Anasema hivi: “Hata kama kunakuwaka ndugu na dada wengi, mara mingi wanakuwaka pamoja na familia zao na wakati nawaona najisikiaka kuwa peke yangu sana.” Kwa wengine, ni nguvu sana kuenda ku mikusanyiko ya muzunguko na ya eneo kisha tu kufisha bibi ao bwana. Unajua mutu mwenye iko na magumu ya vile? Juu ya nini usimualike siku ingine, wakati mutakuwa na programu fulani ya kiroho, ili akuwe pale pamoja na familia yako?

18. Namna gani unaweza kutumikisha 2 Wakorinto 6:11-13 wakati unapenda kuonyesha mutu fulani ukarimu?

18 Mupitishe wakati pamoja. Ujikaze kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada mbalimbali, zaidi sana wale wenye pengine wanajisikia kuwa peke yao. Tunapenda “kufungua mioyo yetu wazi,” zaidi sana kwa wale wenye kujisikia kuwa peke yao. (Soma 2 Wakorinto 6:11-13.) Melissa, mwenye tulishataja, anasema hivi: “Siku zote tulikuwa wenye furaha sana wakati ndugu na dada walitualika ku nyumba zao ili kupitisha wakati pamoja na familia yao ao kuenda fasi fulani.” Mu kutaniko yenu, kuko ndugu ao dada fulani mwenye ungependa kuonyesha ukarimu?

19. Ni mu hali gani inaweza kuwa muzuri zaidi kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu?

19 Kunakuwaka saa yenye Wakristo fulani wanaweza kufurahia sana kupitisha wakati na siye. Wamoja wanaweza kuona kama ni nguvu sana kupitisha wakati pamoja na watu wa jamaa yao, wenye hawako Mashahidi wa Yehova, wakati wa sikukuu fulani. Wengine, wanakuwaka na huzuni sana tarehe fulani, sawa vile siku yenye mupendwa wao alikufa. Saa yenye tunajikaza kupitisha wakati pamoja na ndugu na dada zetu wenye kuwa mu ile hali, tunaonyesha kama “tunawahangaikia sana.”​—Flp. 2:20.

20. Namna gani maneno ya Yesu yenye kuwa mu Matayo 12:48-50 inaweza kutusaidia wakati tunajisikia kuwa peke yetu?

20 Kuko sababu mingi zenye zinaweza kufanya wakati fulani Mukristo ajisikie kuwa peke yake. Lakini, tusisahau hata kidogo kama Yehova anajua na anaelewa muzuri vile tunajisikia. Mara mingi, anatumia ndugu na dada zetu juu ya kutupatia musaada wenye tuko nao lazima. (Soma Matayo 12:48-50.) Wakati tunafanya yetu yote ili kutegemeza ndugu na dada, tunaonyesha kama tuko wenye shukrani kwa Yehova kwa ajili ya ule mupango wa upendo wenye amekamata. Hata kama wakati fulani tunaweza kujisikia kuwa peke yetu, tujue kama hatuko peke yetu juu sikuzote Yehova iko na siye!

WIMBO 46 Aksanti Yehova

^ fu. 5 Wakati fulani unajisikiaka kuwa peke yako? Kama ni vile, ukuwe hakika kama Yehova anajua namna unajisikia, anapenda kukusaidia na iko tayari kukutolea musaada wenye uko nao lazima. Mu hii habari, tutazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya ili kupiganisha hali ya kujisikia kuwa peke yako. Tutajifunza pia namna tunaweza kutia moyo ndugu na dada wenye wanajisikia kuwa peke yao.

^ fu. 5 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA Ndugu moja mwenye alifisha bibi iko anasikiliza usomaji wenye ulirekodiwa wa Biblia na wa kichapo fulani ya funzo.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA Ndugu moja na mutoto yake mwanamuke wanatembelea ndugu moja muzee-muzee wa mu kutaniko na wanamuletea chakula.