Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 22

Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa

Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa

“Kila mumoja wenu abatizwe.”​—MDO. 2:38.

WIMBO 72 Tutangaze Kweli ya Ufalme

KIFUPI CHA HABARI *

1. Wakati wa mitume, wanaume na wanamuke fulani waliambiwa wafanye nini?

WATU wengi, wanaume na wanamuke wa inchi mbalimbali na wenye walikuwa wanasema luga mbalimbali walikutana fasi moja. Jambo fulani ya kushangaza, ilitokea ile siku. Kulikuwa Wayahudi fulani wenye walikuwa na uwezo wa kuzungumuza na wale watu mu luga zao za kizalikio! Ile ilishangaza sana. Mambo wale Wayahudi walikuwa wanasema na mambo yenye mtume Petro alisema, ilishangaza sana wale watu. Wale wanaume na wale wanamuke, walijifunza kama juu waokolewe, wanapaswa kuonyesha imani katika Yesu Kristo. Ile iIliwagusa sana, tena sana, mupaka wakafikia kuuliza hivi: “Tufanye nini?” Petro akajibu: “Kila mumoja wenu abatizwe.”​—Mdo. 2:37, 38.

Ndugu moja, mwenye kusindikizwa na bibi yake, iko anajifunza Biblia na kijana moja kupitia kitabu Furahia Maisha Milele! (Ona fungu la 2)

2. Ni mambo gani tutaona mu hii habari? (Ona picha kwenye jalada.)

2 Mambo yenye ilitokea ilikuwa ya kushangaza sana. Watu 3 000 hivi, walibatizwa ile siku na wakakuwa wanafunzi wa Kristo. Ile ilikuwa tu mwanzo ya kazi kubwa sana ya kufanya wanafunzi, yenye Yesu aliambia wafuasi wake kufanya. Na wafuasi wake wanaendelea kufanya ile kazi leo. Leo, hatuzungumuzake tu na mutu, na kisha ma saa kidogo anabatizwa. Pengine inaweza kuomba miezi, mwaka ao hata miaka juu mwanafunzi wa Biblia abatizwe. Sawa vile munajua muzuri, haikuwake mwepesi kusaidia mutu afikie kuwa mwanafunzi wa Kristo. Mu hii habari, tutaona mambo yenye unaweza kufanya ili kusaidia mwanafunzi wako wa Biblia afikie kuwa mwanafunzi wa Kristo mwenye kubatizwa.

SAIDIA MWANAFUNZI WAKO WA BIBLIA ATUMIKISHE MAMBO YENYE IKO ANAJIFUNZA

3. Kulingana na Matayo 28:19, 20, mwanafunzi wetu wa Biblia anapaswa kufanya nini juu afikie kubatizwa?

3 Mbele mwanafunzi wa Biblia abatizwe, anapaswa kwanza kutumikisha mambo yenye Biblia inafundisha. (Soma Matayo 28:19, 20.) Wakati mwanafunzi wetu wa Biblia anatumikisha mambo yenye anajifunza, atakuwa sawa vile “mutu mwenye busara” mwenye Yesu alizungumuzia katika mufano wake. Ule mutu alichimba sana ili ajenge nyumba yake juu ya mwamba. (Mt. 7:24, 25; Lu. 6:47, 48) Namna gani tunaweza kusaidia mwanafunzi wetu wa Biblia atumikishe mambo yenye anajifunza? Tuzungumuzie basi mambo tatu.

4. Namna gani tunaweza kusaidia mwanafunzi wetu aendelee kujikaza mupaka afikie kubatizwa? (Ona pia kisanduku “ Saidia Mwanafunzi Apime Kufanya Mambo Fulani na Namna Anaweza Kuitimiza.”)

4 Saidia mwanafunzi apime kufanya mambo fulani. Juu ya nini unapaswa kufanya vile? Fikiria hii mufano: Waza, uko unapanga kufanya safari ya murefu sana, pengine unaweza kufikiria fasi fulani za muzuri kwenye unaweza kusimama. Kufanya vile, kutakusaidia usione kama safari iko murefu sana. Ni vile pia, kama mwanafunzi wa Biblia anajiwekea miradi ya mufupi-mufupi, na anaifikia, ile itamusaidia afikie kuona kama anaweza kufikia muradi wa kubatizwa. Tumia sehemu “Pima kufanya hivi” yenye kuwa mu kitabu Furahia Maisha Milele! ili kusaidia mwanafunzi wako afanye maendeleo. Ku mwisho wa kila somo, zungumuzia na mwanafunzi wako namna sehemu “Pima kufanya hivi” inaweza kumusaidia atumikishe mambo yenye ametoka kujifunza. Ukiwaza kama kuko jambo ingine yenye mwanafunzi anaweza kupima kufanya, uiandike ku sehemu “Mambo ingine.” Kila mara, tumia ile sehemu wakati muko munajifunza ili kujikumbusha pamoja na mwanafunzi wako miradi ya mufupi-mufupi na miradi ingine ya muda murefu yenye anaweza kufikia.

5. Kama vile Marko 10:17-22 inaonyesha, Yesu aliambia tajiri moja afanye nini, na juu ya nini?

5 Saidia mwanafunzi afanye mabadiliko. (Soma Marko 10:17-22.) Yesu alijua kama ingekuwa nguvu kwa tajiri moja kuuzisha mali zake. (Mk. 10:23) Lakini, alimuambia afanye ile badiliko kubwa sana. Juu ya nini? Juu Yesu alimupenda. Wakati fulani, nasiye pia tunaweza kujizuia kutia moyo mwanafunzi wetu wa Biblia atumikishe mambo yenye iko anajifunza, juu tu tunawaza kama haiko tayari kufanya mabadiliko yenye anapaswa kufanya. Kusema kweli, inaomba wakati juu watu wabadilishe matendo yao ya mubaya, na wavale utu mupya. (Kol. 3:9, 10) Lakini, tukiambia mwanafunzi wetu bila kuchelewa mambo yenye anapaswa kufanya, ni vile pia ataanza kufanya mabadiliko. Kama tunaongea naye juu ya ile jambo, tutaonyesha kama tunamuhangaikia.​—Zb. 141:5; Mez. 27:17.

6. Juu ya nini tunapaswa kutumia maulizo ya maoni?

6 Ulizo ya maoni ni ulizo yenye tunaulizaka mwanafunzi juu ya kujua mawazo yake ao maoni yake kuhusu jambo fulani. Tumia ulizo ya vile ili kujua mambo yenye mwanafunzi wako anaelewa na yenye anaamini, kama unafanya vile kwa ukawaida, itakuwa mwepesi kuzungumuzia mambo yenye inaweza kuwa nguvu kwake kuitika. Kitabu Furahia Maisha milele! iko na maulizo mingi ya maoni. Kwa mufano, mu somo ya 4 muko hii ulizo: “Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati unatumikisha jina lake?” Na mu somo ya 9 muko hii ulizo: “Unapenda kusali juu ya mambo gani fulani?” Ku mwanzo, mwanafunzi wako anaweza kukuwa na lazima ya wakati, juu ajibie ile maulizo ya maoni. Unaweza kumusaidia kwa kufikiri sana naye juu ya Maandiko na juu ya picha zenye kuwa mu ile kitabu.

7. Namna gani tunaweza kutumia muzuri mifano ya watu mbalimbali?

7 Kisha mwanafunzi wako kuelewa mambo yenye anapaswa kufanya, zungumuzia mifano ya watu mbalimbali yenye inaweza kumusaidia. Kwa mufano, kama mwanafunzi wako hakusanyikake kwa ukawaida ku mikutano, unaweza kumuonyesha video Yehova Alinihangaikia yenye kuwa mu sehemu “Habari Zingine” ya somo ya 14. Mu somo za mingi zenye kuwa mu kitabu Furahia Maisha milele! utapata mambo fulani yenye kuwa mu sehemu “Tujifunze mambo mingi zaidi” ao mu sehemu “Habari Zingine.” * Ukuwe muangalifu, usilinganishe mwanafunzi wako na mutu mwingine kwa kusema hivi: “Kama yeye anaweza kufanya, na weye pia unaweza kufanya.” Uache mwanafunzi ye peke afikie kusema vile. Kuliko kufanya vile, unaweza kuonyesha wazi mambo makubwa, yenye ilisaidia ule mutu mwenye kuzungumuziwa mu video atumikishe mafundisho ya Biblia. Pengine unaweza kufanya vile kwa kutaja andiko moja ao jambo fulani yenye ilizungumuziwa mu video. Na kama inawezekana, ukazie namna Yehova alimusaidia ule mutu mwenye kuzungumziwa mu video.

8. Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wako wa Biblia amupende Yehova?

8 Saidia mwanafunzi wako wa Biblia amupende Yehova. Namna gani? Tumia nafasi mbalimbali ili kumusaidia mwanafunzi wako ajifunze mingi zaidi juu ya sifa za Yehova. Musaidie amuone Yehova kuwa Mungu mwenye furaha na mwenye anategemeza wale wote wenye wanamupenda. (1 Ti. 1:11; Ebr. 11:6) Onyesha mwanafunzi wako faida yenye atapata kwa kutumikisha mambo yenye anajifunza, na umufasirie aone kama faida zenye anapata zinaonyesha kuwa Yehova anamupenda. (Isa. 48:17, 18) Ile itasaidia mwanafunzi wako achochewe kufanya mabadiliko yenye anapaswa kufanya kadiri upendo wake kwa Yehova unaendelea kuongezeka.​—1 Yo. 5:3.

SAIDIA MWANAFUNZI WAKO AJUANE NA NDUGU NA DADA

9. Kulingana na Marko 10:29, 30, ni nini mutu anaweza kuacha ili afikie kuwa mwanafuzi mwenye kubatizwa?

9 Juu afikie kubatizwa, mwanafunzi wa Biblia anapaswa kujiima mambo fulani. Sawa vile tajiri mwenye tulishazungumuzia, wanafunzi fulani wa Biblia wanapaswa kuacha vitu fulani vya kimwili. Kama kazi yao inapingana na kanuni za Biblia, pengine wanaweza hata kuiacha na kutafuta ingine. Wengi wanaweza kuacha marafiki wao wenye hawamupendi Yehova. Na wengine wanaweza kuachwa na watu wa familia yao wenye wanachukiaka Mashahidi wa Yehova. Yesu alisema kama, inaweza kuwa nguvu kwa watu fulani kukubali ile hali. Lakini aliahidi kama hataacha wale wenye wanamufuata. Atawabariki sana kwa kuwapatia familia ya kiroho. (Soma Marko 10:29, 30.) Namna gani unaweza kusaidia mwanafunzi wako wa Biblia afaidike na hii zawadi ya muzuri sana?

10. Mufano wa Manuel umekufundisha nini?

10 Fanya urafiki pamoja na mwanafunzi wako. Ni jambo ya maana sana kuonyesha mwanafunzi wako kama unamuhangaikia. Juu ya nini? Ona mufano wa Manuel, mwenye kuishi Meksiko. Anakumbuka wakati alikuwa mwanafunzi wa Biblia, anasema hivi: “Kila mara mbele tuanze kujifunza, mwalimu wangu alikuwa ananiuliza kama nilikuwa muzuri. Alinisaidia nijisikie huru na ile ilifanya nifikie kumuambia mambo yote. Nilijisikia kama ananihangaikia kabisa.”

11. Ni faida gani wanafunzi wetu wa Biblia wanaweza kupata saa yenye tunapitisha wakati pamoja nao?

11 Pitisha wakati pamoja na wanafunzi wako sawa vile Yesu alipitisha wakati pamoja na wafuasi wake. (Yoh. 3:22) Kama inawezekana, alika mwanafunzi wako mwenye kufanya maendeleo ku nyumba, ili mutumie pamoja café, chakula ao kuona pamoja programu ya mwezi ya JW Télédiffusion. Pengine mwanafunzi wako atafurahia wakati unamualika siku yenye anajisikia kuwa ye peke juu marafiki wake na watu wa familia yake wako wanafanya sikukuu fulani ya kidini ao ya kitaifa. Kazibwa, mwenye anaishi Uganda, anasema hivi: “Nawaza, nilijifunza mambo mingi zaidi kuhusu Yehova saa yenye nilipitisha wakati na mwalimu wangu wa Biblia kuliko wakati wenye tulitumia ili kujifunza. Niliona kwa kiasi gani Yehova anahangaikia watu wake na namna wako na furaha. Ile njo nilipenda mu maisha yangu.”

Wakati unasindikizwa na wahubiri mbalimbali kwenye funzo lako la Biblia, itakuwa mwepesi kwa mwanafunzi kukusanyika (Ona fungu la 12) *

12. Juu ya nini tunapaswa kuambia wahubiri mbalimbali watusindikize ku funzo letu la Biblia?

12 Ambia wahubiri mbalimbali wakusindikize ku funzo lako la Biblia. Wakati fulani, pengine tunaonaka kama ni mwepesi kuenda siye peke ao kuenda na muhubiri uleule ili kuongoza funzo letu la Biblia. Hata kama tunaweza kuona kuwa ni mwepesi kufanya vile, kuenda na wahubiri mbalimbali kutamusaidia mwanafunzi wetu wa Biblia. Dimitrii, mwenye anaishi Moldavie, anasema hivi: “Kila muhubiri mwenye alisindikiza mwalimu wangu, alikuwa na namna yake ya kufasiria mambo. Na ile ilinisaidia nijue namna ya kutumikisha mambo yenye niko najifunza mu njia zingine na ilinisaidia pia nisisikie haya sana wakati nilikusanyika kwa mara ya kwanza, juu tayari nilikuwa nilishajuana na ndugu na dada wengi.”

13. Juu ya nini tunapaswa kusaidia mwanafunzi wetu wa Biblia akusanyike?

13 Saidia mwanafunzi wako wa Biblia akusanyike. Juu ya nini? Ni juu Yehova anaomba waabudu wake wakusanyike pamoja. Na ile ni sehemu ya ibada yetu. (Ebr. 10:24, 25) Zaidi ya ile, ndugu na dada zetu ni familia yetu ya kiroho. Wakati tuko ku mikutano pamoja nao ni sawa vile tuko pamoja ku nyumba na tunatumia chakula fulani ya muzuri. Wakati unasaidia mwanafunzi wako wa Biblia akusanyike, ile ni njia moja ya maana zaidi yenye itamusaidia afikie kubatizwa. Lakini, pengine inaweza kuwa nguvu kwake kuanza kukusanyika. Namna gani kitabu Furahia Maisha Milele! inaweza kusaidia mwanafunzi wako wa Biblia apiganishe matatizo yoyote yenye inamuzuia akusanyike?

14. Namna gani tunaweza kuchochea mwanafunzi wetu wa Biblia akusanyike?

14 Tumia somo ya 10 ya kitabu Furahia Maisha Milele! ili kuchochea mwanafunzi wako akusanyike. Mbele kitabu itoke, waliomba wahubiri fulani wapime ile somo mu mahubiri. Kisha kuipima, walisema kama walipata matokeo ya muzuri na ile somo ilisaidia wanafunzi wao wa Biblia waanze kukusanyika. Lakini, hatuseme kama inaomba tu kuchunga mupaka wakati mutafika ku somo ya 10 njo ualike mwanafunzi wako wa Biblia ku mikutano. Usikawie-kawie ili kumualika, na uendelee kufanya vile kila mara. Kila mwanafunzi wa Biblia anakuwaka na magumu yake. Njo maana ujikaze kujua mambo yenye mwanafunzi wako iko nayo lazima, na ile itakusaidia ujue ni musaada gani unaweza kumutolea. Usivunjike moyo kama mwanafunzi wako anakawa juu aanze kukusanyika. Ukuwe muvumilivu, lakini uendelee kumualika.

SAIDIA MWANAFUNZI WAKO WA BIBLIA APIGANISHE WOGA WAKE

15. Pengine mwanafunzi wetu wa Biblia anaweza kuwa na woga gani?

15 Unakumbuka wakati ulisikia woga kidogo juu ya kuwa Shahidi wa Yehova? Pengine ulijisikia hautawezaka kuhubiri nyumba kwa nyumba. Ao pengine, uliogopa watu wa familia yako ao marafiki wenye pengine wangekupinga. Kama ni vile, unaweza kuelewa namna mwanafunzi wako wa Biblia anajisikia. Yesu alisema kama, watu fulani wanaweza kuwa na ule woga. Njo maana, Yesu aliambia wafuasi wake wasiache woga uwafanye waache kumutumikia Yehova. (Mt. 10:16, 17, 27, 28) Namna gani Yesu alisaidia wafuasi wake wapiganishe woga wenye walikuwa nao? Na namna gani unaweza kufuata mufano wake?

16. Namna gani tunaweza kuzoeza mwanafunzi wetu ahubiri?

16 Pole kwa pole, zoeza mwanafunzi wako ahubiri. Pengine wanafunzi wa Yesu walisikia woga wakati aliwatuma kuhubiri. Lakini Yesu aliwasaidia kwa kuwaambia fasi kwenye wangehubiri na mambo yenye wangehubiri. (Mt. 10:5-7) Namna gani unaweza kuiga Yesu? Saidia mwanafunzi wako ajue fasi kwenye anaweza kuhubiri. Kwa mufano, unaweza kumuuliza kama anajua mutu fulani mwenye angependa kujifunza kweli ya musingi ya Biblia. Kisha, umusaidie kutayarisha mambo yenye atasema kwa kumuonyesha njia moja ya mwepesi ya kuhubiri ile kweli. Kama inafaa, unaweza kumuzoeza kwa kutumia sehemu yenye kuwa chini ya kichwa “Watu Fulani Wanasemaka” na “Kama Mutu Anauliza” yenye kupatikana mu kitabu Furahia Maisha Milele! Wakati unafanya vile, ujikaze kuzoeza mwanafunzi wako atumie Biblia ili kutoa majibu ya mwepesi na yenye busara.

17. Namna gani tunaweza kutumia Matayo 10:19, 20, 29-31 ili kusaidia mwanafunzi wetu wa Biblia amutegemee Yehova?

17 Saidia mwanafunzi wako amutegemee Yehova. Yesu aliambia wanafunzi wake kama Yehova atawasaidia juu anawapenda. (Soma Matayo 10:19, 20, 29-31.) Kumbusha mwanafunzi wako kama Yehova atamusaidia pia. Unaweza kumusaidia amutegemee Yehova kwa kusali naye kuhusu miradi yake. Franciszek, mwenye anaishi Polandi, anasema hivi: “Kila mara mwalimu wangu wa Biblia alikuwa anataja miradi yangu mu sala zake. Wakati niliona Yehova anajibia sala za mwalimu wangu, mara moja nilianza kusali. Nilijionea musaada wa Yehova wakati nilipaswa kuomba ruhusa ili kuhuzuria ku mikutano na ku mikusanyiko.”

18. Yehova anajisikia namna gani kuhusu kazi yenye walimu Wakristo wanafanya?

18 Yehova anahangaikia kabisa wanafunzi wetu wa Biblia. Anajua namna walimu Wakristo wanajikaza sana ili kusaidia watu wamukaribie na anawapenda sana juu ya ile kazi yenye wanafanya. (Isa. 52:7) Kwa sasa kama hauko unaongoza funzo la Biblia, unaweza kuendelea kusaidia wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo na wafikie kubatizwa, kwa kusindikiza wahubiri wengine ku mafunzo yao.

WIMBO 60 Tuwafundishe ili Wapate Uzima wa Milele

^ fu. 5 Mu hii habari, tutaona namna gani Yesu alisaidia watu wafikie kuwa wanafunzi wake, na namna tunaweza kumuiga. Tutaona pia namna tunaweza kutumia sehemu fulani za kitabu ya mupya yenye kichwa Furahia Maisha Milele! Hii kitabu, imetayarishwa ili kusaidia wanafunzi wetu wa Biblia, wafanye maendeleo na wafikie kubatizwa.

^ fu. 7 Unaweza pia kupata habari zaidi mu kitabu (1) Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova, chini ya kichwa “Biblia” kwenye sehemu “Iko na Mashauri ya Lazima sana” na katika habari “‘Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu’ (yenye inatokaka mu Munara wa Mulinzi)” ao (2) mu JW Library® kwenye sehemu “Kuulizwa Maulizo na Ushuhuda.”

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu moja na bibi yake wako wanajifunza Biblia na kijana moja. Na wakati ingine, ndugu mbalimbali wanamusindikiza ku funzo lake la Biblia.