Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Mu wakati wa Yesu, watu walipaswa kulipa kodi za namna gani?

TANGU zamani, Waisraeli walikuwa na desturi ya kutoa feza ili kutegemeza ibada safi. Lakini, mambo ya kulipa kodi ilifikia kuwa nguvu sana na ikakuwa muzigo kwa Wayahudi wenye waliishi wakati wa Yesu.

Juu ya kutegemeza ibada yenye ilikuwa inafanyika ku tabenakulo na kisha ku hekalu, Wayahudi wote wenye kukomaa walipaswa kulipa nusu ya shekeli (drakma mbili). Mu wakati wa Yesu, ile kodi ilitumiwa kwa ajili ya zabihu na kwa ajili ya kutunza hekalu lenye Herode alijengaka. Wayahudi fulani walimuuliza Petro kuhusu musimamo wa Yesu juu ya ile mambo, na Yesu alisema kama haiko mubaya kulipa kodi. Njo maana, alimuambiaka Petro fasi kwenye angepata feza ya kulipa ile kodi.​—Mt. 17:24-27.

Zamani, watu wa Mungu walipaswa pia kulipa sehemu moja ya kumi ya mazao yenye walipata mu mashamba, na sehemu moja ya kumi ya mapato yao. (Law. 27:30-32; Hes. 18:26-28) Viongozi wa dini walilazimisha sehemu moja ya kumi ilipwe juu ya mimea ya mboga na hata juu ya “munanaa na dili na bizari.” Yesu hakusema kama ni mubaya kulipa sehemu moja ya kumi, lakini alihukumu unafiki wa Waandishi na Wafarisayo.​—Mt. 23:23.

Hata vile mu ile wakati, Waroma njo walikuwa wanatawala na waliwekea watu kodi mingi zenye walipaswa kulipa. Kodi moja ilihusu wale wenye walikuwa na mashamba, na wangeweza kuilipa kwa kutumia feza ao vitu vingine. Inakadiriwa kama kodi yenye wale watu wangepaswa kulipa ingefikia kiasi ya asilimia 20 ao 25 (20-25 %) Kulikuwa pia kodi ya kichwa yenye kila Muyahudi alipaswa kulipa. Siku moja Wafarisayo walimuuliza Yesu juu ya ile kodi. Jibu yenye alileta inaonyesha mawazo yenye tunapaswa kuwa nayo juu ya kulipa kodi. Alisema hivi: “Basi, mumulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”​—Mat. 22:15-22.

Kulikuwa pia kodi ya kulipia vitu vya kuuzisha vyenye viliingia ao kutoka mu eneo fulani. Ile kodi ilikuwa inaombwa ku bandari (ao, port), fasi kwenye kulikuwa vilalo, fasi kwenye barabara zinakutanana, ao ku miingilio ya miji ao soko.

Kodi zenye Waroma walikuwa wanaomba watu zilipita mipaka sana. Kulingana na muhistoria Muroma Tacite, mu utawala wa Tiberio, wakati Yesu alikuwa angali hapa ku dunia, “Siria na Yudea waliomba kodi ipunguzwe juu ilikuwa ilishawalemea sana.”

Kile kilifanya zile kodi zikuwe muzigo zaidi kwa watu ni namna zile kodi ziliombwa. Juu mutu akuwe na haki ya kufanya ile kazi ya kuomba kodi iliomba alipe feza mingi sana. Kisha pale angetafuta watu wenye watamusaidia kuomba kodi juu wote wapate faida. Inaonekana Zakayo alikuwa anatumikisha watu fulani vile. (Lu. 19:1, 2) Haishangaze kuona vile watu walikuwa wanachukia ile hali na hawakufurahia wale watu wenye walikuwa wanalipisha zile kodi.