Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 24

Unaweza Kuepuka ao Kutoka Katika Mitego ya Shetani!

Unaweza Kuepuka ao Kutoka Katika Mitego ya Shetani!

‘Utoke katika mutego wa Ibilisi.’​—2 TI. 2:26.

WIMBO 36 Tulinde Moyo Wetu

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini tunaweza kusema kama Shetani iko sawa muwindaji?

KUSUDI ya muwindaji inakuwaka kukamata munyama ao kumuua. Anaweza kutumia mitego mbalimbali, na hata mumoja kati ya wafariji wa uongo wa Yobu alionyesha vile. (Yob. 18:8-10) Muwindaji anapaswa kufanya nini juu akamate munyama mu mutego wake? Muwindaji anajikazaka kujua muzuri sana munyama mwenye anapenda kuwinda: Ni wapi ule munyama anazoeaka kuenda? Ni kitu gani anapendaka sana? Ni mutego wa namna gani njo unaweza kumukamata? Shetani iko sawa vile ule muwindaji. Anatuchunguzaka sana juu atujue muzuri. Anakazia uangalifu kwenye tunaendaka na mambo yenye tunapendaka. Kisha kufanya vile, anatumiaka sasa mutego wenye anawaza kama njo unaweza kutukamata, bila siye kutazamia. Lakini Biblia inatuhakikishia kama ikiwa tunakamatwa, tunaweza kutoka mu ile mutego. Tena, Biblia inatuonyesha mambo tunaweza kufanya juu tusiangukie mu mitego ya Shetani.

Kiburi na pupa ni kati ya mitego yenye Shetani anatumia sana (Ona fungu la 2) *

2. Taja mitego mbili kati ya mitego yenye Shetani anatumiaka sana.

2 Kiburi na pupa * iko kati ya mitego yenye Shetani anatumiaka sana. Kwa miaka mingi watu wengi wanaangukiaka sana mu ile mitego mbili ya Shetani. Shetani iko sawa vile muwindaji mwenye anakamata ndege mu wavu ao mu makila. (Zb. 91:3) Hatuna sababu ya kuangukia mu mitego ya Shetani. Juu ya nini? Juu Yehova alishatuonyesha werevu mbalimbali wenye Shetani anatumiaka.​—2 Ko. 2:11.

Mifano fulani yenye kuwa mu Biblia inaweza kutusaidia tujue nini tunaweza kufanya ili kuepuka ao kutoka mu mitego ya Ibilisi (Ona fungu la 3) *

3. Juu ya nini Yehova alitia mu Biblia mifano fulani?

3 Kupitia mifano ya watumishi wake wa zamani, Yehova anatuonyesha hatari ya pupa na kiburi. Tutaona namna Shetani alikamata mu ile mitego watumishi fulani wa Yehova wenye walimutumikia kwa miaka mingi. Ile inamaanisha kama hatuwezi kuepuka kiburi? Jibu ni hapana. Yehova alihakikisha kama ile mifano inaandikwa ili kuwa “onyo kwetu sisi.” (1 Ko. 10:11) Anajua kama tunaweza kujifunza mambo fulani kupitia zile mifano na kuepuka ao kutoka mu mitego ya Ibilisi.

MUTEGO WA KIBURI

Ona fungu la 4

4. Ni nini inaweza kutufikia kama tuko na kiburi?

4 Shetani anapenda tukuwe wenye kiburi sana. Anajua kama, ikiwa tunaacha kiburi itutawale tutakuwa sawa vile yeye na hatutapata uzima wa milele. (Mez. 16:18) Kwa hiyo, mutume Paulo alisema kama ni muzuri mutu “asijivune kwa kiburi na kuhukumiwa kama vile Ibilisi alihukumiwa.” (1 Ti. 3:6, 7) Ile inaweza pia kutufikia ikuwe tulishafanya miaka mingi mu tengenezo ao hapana.

5. Kulingana na Muhubiri 7:16, 20, ni nini inaweza kuonyesha kama mutu fulani iko na kiburi?

5 Kiburi ni aina ya uchoyo. Shetani anajaribu kutufanya tukuwe wachoyo. Anapenda tukaze akili yetu hapana juu ya Yehova lakini juu yetu siye wenyewe, zaidi sana wakati tuko tunapambana na magumu. Kwa mufano, wamekushitaki mambo ya uongo ao wamekutendea kwa njia yenye haiko ya haki? Shetani angependa ukasirikie Yehova na ndugu na dada zako. Shetani anapenda tuwaze kama njia moja tu ya muzuri ya kumaliza magumu yetu ni kujifanyia mambo vile tunapenda kuliko kufuata muongozo wa Yehova wenye anatupatia mu Neno lake Biblia.​—Soma Muhubiri 7:16, 20.

6. Mufano wa dada moja wa Pays-bas unakufundisha nini?

6 Fikiria mufano wa dada moja, mwenye anaishi mu inchi ya Pays-bas, mwenye alikasirika sana juu wengine walimukosea. Aliamua kama hangeendelea kuvumilia tena ile hali. Anasema hivi: “Nilijisikia kuwa miye peke kabisa na niliona kama siwezi kuwasamehe. Nilimuambia bwana yangu kama tunapaswa kuhamia mu kutaniko ingine.” Kisha, wakati aliangalia programu ya JW Télédiffusion® ya Mwezi wa 3, 2016, alipata mapendekezo ya muzuri sana, kuhusu namna ya kutenda wakati wengine wanakukosea. Ule dada anasema hivi: “Nilipaswa kwanza kufikiri na kukubali kwa unyenyekevu wote kama na miye nakuwaka na makosa yangu, kuliko kuanza kuwaza kama ndugu na dada njo wanapaswa kubadilika, hapana miye. Ile programu ya JW Télédiffusion® ilinisaidia kukaza akili yangu juu ya Yehova na juu ya Mamlaka yake Makubwa Zaidi.” Unaona wazo yenye kuwa hapa? Kama uko na magumu fulani, kaza akili yako juu ya Yehova. Umuombe akusaidie uone wengine sawa vile yeye anawaonaka. Baba yako wa mbinguni anaona makosa yenye wanafanya lakini iko tayari kuwasamehe. Anapenda na weye ufanye vile.​—1 Yo. 4:20.

Ona fungu la 7

7. Ni nini ilimufikia Mufalme Uzia?

7 Juu Mufalme Uzia wa Yuda alikuwa na kiburi, alikatala kufuata mashauri na alifanya mambo yenye hakuruhusiwa kufanya. Uzia alifanya mambo mingi muzuri. Alipata ushindi mu vita mingi, alijenga miji mingi na alikuwa na mashamba mingi sana. “Mungu wa kweli alimufanya apate matokeo ya muzuri.” (2 Ny. 26:3-7, 10) Biblia inasema hivi: “Hata hivyo, wakati tu alikuwa na nguvu, moyo wake ukakuwa na majivuno na kufikia kuleta uharibifu wake mwenyewe.” Tayari Yehova alikuwa alishaamuru kama ni makuhani tu njo waliruhusiwa kutoa uvumba ku hekalu. Lakini, siku moja, kwa kiburi, Mufalme Uzia alienda ku hekalu na akatoa uvumba. Ile haikumufurahisha Yehova na akamupiga ukoma Uzia, Mufalme mwenye kiburi. Uzia alibakia mwenye ukoma maisha yake yote.​—2 Ny. 26:16-21.

8. Kulingana na 1 Wakorinto 4:6, 7, ni nini inaweza kutusaidia tuepuke kuwa na kiburi?

8 Je inawezekana na siye tukuwe na kiburi na tufanye zambi sawa vile Uzia? Fikiria mufano wa José. Alikuwa mufanyabiashara mwenye alikuwa na matokeo ya muzuri mu kazi yake na alikuwa muzee mwenye aliheshimiwa sana mu kutaniko. Alikuwa anatoa hotuba ku mikusanyiko ya muzunguko na ya eneo na waangalizi wa muzunguko walikuwa wanamuona kila mara juu ya kupata mashauri fulani. Anasema hivi: “Nilitegemea uwezo wangu na uzoefu wangu, sikumutegemea sana Yehova na niliwaza kama nilikuwa nguvu sana. Njo maana sikukuwa tena nasikiliza mashauri na maonyo ya Yehova.” Siku moja José alifanya zambi nzito na akatengwa. Lakini kisha miaka mingi, alifikia kurudishwa. Sasa anasema hivi: “Yehova amenifundisha kama jambo ya maana haiko kuwa na cheo lakini ni kufanya mambo yenye anatuomba tufanye.” Kwa hiyo, tusisahau kama uwezo wenye tuko nao na mapendeleo yenye tuko nayo mu kutaniko inatoka kwa Yehova. (Soma 1 Wakorinto 4:6, 7.) Kama tuko na kiburi Yehova hatatutumia.

MUTEGO WA PUPA

Ona fungu la 9

9. Juu ya pupa Shetani na Eva walifanya nini?

9 Wakati unasikia neno pupa, pengine Shetani Ibilisi njo anakuya mu akili yako. Mbele akuwe Shetani, alikuwa na madaraka mingi mbinguni wakati alikuwa malaika wa Yehova. Lakini alipenda zaidi ya ile. Alipenda ibada yenye Yehova tu njo anastahili kupewa. Shetani anapenda tukuwe sawa yeye, njo maana anajaribu kutufanya tuwaze kama mambo yenye tuko nayo haitoshe inaomba zaidi ya ile yenye tuko nayo. Alianza kufanya vile na Eva. Kwa upendo Yehova alipatia Eva na bwana yake chakula mingi sana​—“matunda ya kila muti wa bustani” isipokuwa muti moja tu. (Mwa. 2:16) Lakini, Shetani alimudanganya Eva kwa kumufanya afikiri kama alikuwa na lazima ya kula matunda ya muti wenye ulikatazwa. Eva hakutosheka na yenye alikuwa nayo; alipenda zaidi ya ile. Na tunajua kwenye mambo iliishia. Eva alifanya zambi na ku mwisho akakufa.​—Mwa. 3:6, 19.

Ona fungu la 10

10. Namna gani Daudi alifikia kuanguka mu mutego wa pupa?

10 Pupa ilifanya Mufalme Daudi asahau mambo yote yenye Yehova alimupatia, ni kusema, utajiri, kujulikana, na ushindi mbalimbali juu ya maadui wake. Daudi alimushukuru Mungu kwa zile zawadi zenye alimupatia na alisema kama “zilikuwa nyingi sana kusimulia!” (Zb. 40:5) Lakini, hata vile, alisahau ile mambo yote yenye Yehova alikuwa amemupatia. Hakutosheka na mambo alikuwa nayo, alipenda zaidi ya ile. Hata kama Daudi alikuwa na bibi wengi, alifikia kutamani bibi ya mutu mwingine. Ule mwanamuke alikuwa Bat-sheba na bwana yake alikuwa Uria Muhiti. Daudi alifanya uzinifu pamoja na Bat-sheba na akapata mimba. Lakini Daudi hakuishia pale, alienda mbali zaidi, akakamata mipango ili Uria auawe! (2 Sa. 11:2-15) Daudi alikuwa anawaza nini? Aliwaza kama Yehova hangemuona? Ijapokuwa alimutumikia Yehova kwa miaka mingi alifikia kuwa mutu wa pupa na ile ilimuletea mateso mingi. Lakini, jambo ya kufurahisha, Daudi alifikia kukubali kosa yake na akatubu. Alimushukuru sana Yehova juu alimusamehe!​—2 Sa. 12:7-13.

11. Kulingana na Waefeso 5:3, 4, ni nini inaweza kutusaidia tupiganishe pupa?

11 Mufano wa Daudi unatufundisha nini? Tunaelewa kama ikiwa tuko wenye shukrani juu ya mambo yenye Yehova ametupatia, ile itatusaidia tupiganishe pupa. (Soma Waefeso 5:3, 4.) Tunapaswa kutosheka na mambo yenye tuko nayo. Wakati tunaanza kujifunza Biblia pamoja na mutu fulani ni muzuri kumuambia afikirie hata jambo moja yenye Yehova amemupatia na tumutie moyo amushukuru juu ya ile. Kama kila siku anasali juu ya jambo moja, wakati juma itaisha atakuwa amesali juu ya mambo saba tofauti. (1 Te. 5:18) Na weye unafanyaka vile? Kama unafikiri sana juu ya mambo yote yenye Yehova alishakufanyia, ile itakusaidia ukuwe mwenye shukrani. Na wakati uko mwenye shukrani, unatosheka. Na wakati unatosheka, pupa yote inakimbia.

Ona fungu la 12

12. Juu alikuwa na pupa Yuda Iskariote alifanya nini?

12 Juu Yuda Iskariote alikuwa mwenye pupa alifanya jambo ya mubaya sana na alimusaliti Yesu. Lakini ile haionyesha kama tangu zamani alikuwa mutu mubaya. (Lu. 6:13, 16) Yesu alimuchaguaka ili akuwe mutume wake. Inaonekana Yesu alimutumainia Yuda juu ni yeye njo alikuwa anachunga sanduku la feza. Yesu na mitume wake walitumia ile feza juu ya kutimiza mahitaji yao wakati walikuwa wanafanya kazi ya kuhubiri. Leo, tunaweza kusema kama ile feza ilikuwa sawa vile feza yenye kutolewa juu ya kazi ya ulimwenguni. Lakini kisha wakati fulani Yuda akaanza kuiba, hata kama alikuwa alishasikia Yesu iko anaonya watu mara mingi juu ya hatari ya kuwa na pupa. (Mk. 7:22, 23; Lu. 11:39; 12:15) Lakini Yuda alifanya sawa vile mwenye hakusikia kitu.

13. Ni wakati gani pupa yenye Yuda alikuwa nayo ilionekana wazi?

13 Siku kidogo mbele Yesu auawe, kuko jambo fulani yenye ilitokea yenye ilionyesha waziwazi pupa ya Yuda. Siku moja Simoni mwenye ukoma alialika watu fulani kwake. Kati ya wale watu kulikuwa Yesu, wanafunzi wake, Maria na dada yake Marta. Wakati walikuwa wanakula, Maria alisimama akakamata mafuta yenye marashi na kuimwanga ku kichwa ya Yesu. Ile mafuta ilikuwa ya bei sana. Yuda na wanafunzi wengine walikwazika sana. Pengine wanafunzi wengine waliwaza kama kuliko kutumia feza juu ya kuuza ile mafuta, pengine ile feza ingetumiwa juu ya kazi ya mahubiri. Lakini Yuda yeye, hakukwazika juu ya ile sababu. “Alikuwa mwizi,” na alipenda kuiba feza zenye zilikuwa katika sanduku la feza. Sababu Yuda alikuwa na pupa alimusaliti Yesu kwa feza yenye ililingana na bei ya mutumwa.​—Yoh. 12:2-6; Mt. 26:6-16; Lu. 22:3-6.

14. Bwana moja na bibi yake walifanya nini juu ya kuonyesha kama walifuata shauri yenye kuwa mu Luka 16:13?

14 Yesu alikumbusha wafuasi wake hii kweli ya musingi: “Hamuwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.” (Soma Luka 16:13.) Na ile ni kweli hata leo. Fikiria namna bibi na bwana fulani wenye kuwa mu inchi ya Romania walitumikisha ile maneno ya Yesu. Walipata kazi ya muda mu inchi yenye ilikuwa tajiri sana. Wanasema hivi: “Tulikuwa na deni kubwa ku banke yenye tulipaswa kurudisha. Ku mwanzo tuliona hii kazi kuwa baraka kutoka kwa Yehova.” Lakini kusema kweli kulikuwa mutego. Kama wangekubali ile kazi hawangekuwa tena na wakati ya kumutumikia Yehova. Kisha kusoma habari “Dumisha Ushikamanifu Ukiwa na Moyo Kamili” yenye kuwa mu Munara wa mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 8, 2008, walikamata uamuzi fulani. Wanasema hivi: “Ikiwa kutafuta feza zaidi njo ingekuwa kusudi yetu ya kuenda kutumikia mu ile inchi, ile ingefanya urafiki wetu na Yehova ukuwe pa nafasi ya pili. Kusema kweli kungefanya pia hali yetu ya kiroho iharibike.” Njo maana walikatala ile kazi. Ni nini ilitokea? Bwana alipata kazi ingine mu inchi yao, yenye iliwatimizia mahitaji yao. Bibi anasema hivi: “Mukono wa Yehova haukuwake mufupi.” Ule bwana na bibi yake wako na furaha juu walichagua Yehova kuwa Bwana wao, hapana utajiri.

EPUKA MITEGO YA SHETANI

15. Ni nini inatuhakikishia kama tunaweza kutoka mu mitego ya Shetani?

15 Tunaweza kufanya nini ikiwa tunatambua kama tulishaangukia mu mutego wa kiburi ao wa pupa? Tunaweza kutoka mu ile mutego. Paulo alisema kama wale wenye ‘wamekamatwa [na Ibilisi] wakiwa wazima’ wanaweza kutoka katika mutego wake. (2 Ti. 2:26) Zaidi ya ile, kisha kusikiliza karipio kutoka kwa Natani, Daudi alitubu na akajikaza ili kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova. Usisahau kama,Yehova iko na nguvu sana kuliko Shetani. Kwa hiyo, kama tunakubali musaada wa Yehova tunaweza kutoka mu mutego wowote wa Shetani.

16. Nini njo inaweza kutusaidia tuepuke mitego ya Shetani?

16 Kusema kweli, haiombe tu kutoka mu mitego ya Shetani. Tunapaswa pia kuiepuka. Tunaweza kufanya vile tu kwa musaada wa Yehova. Lakini tusiwaze kama siye hatuwezi kuwa na kiburi ao na pupa! Hata watumishi fulani wa Yehova waliangukia mu ile mitego. Njo maana umuombe Yehova kila siku akusaidie uchunguze mawazo yako na matendo yako. (Zb. 139:23, 24) Ujikaze sana juu usiangukie mu mutego wa pupa ao wa kiburi!

17. Ni nini itapata hivi karibuni Shetani, adui wetu mukubwa?

17 Shetani amekuwa muwindaji wa miaka mingi sana. Lakini hivi karibuni atafungwa na ataharibiwa milele. (Ufu. 20:1-3, 10) Tunachunga ile siku kwa hamu sana. Lakini mbele ile siku ifike, fungula macho juu usiangukie mu mitego ya Shetani. Usiruhusu hata kidogo kiburi ao pupa vikutawale. Uazimie “kumupinga Ibilisi, naye atakukimbia.”​—Yak. 4:7.

WIMBO 127 Ninapaswa Kuwa Mutu wa Namna Gani?

^ fu. 5 Shetani iko sawa vile muwindaji mwenye iko na ufundi sana. Anajaribu kutumia mitego mbalimbali juu ya kutukamata, ikuwe tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi ao hapana. Mu hii habari tutaona namna Shetani anatumia mitego mbili, ni kusema, kiburi na pupa ili kuharibu urafiki wetu pamoja na Mungu. Tena tutaona mifano ya watu fulani wenye waliangukia mu ile mitego na tutaona namna gani tunaweza kuepuka ile mitego.

^ fu. 2 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Hii habari inazungumuzia kiburi na pupa. Mutu mwenye iko na kiburi ni mutu mwenye anajiona kuwa wa maana sana kuliko wengine, na mutu mwenye pupa ni mutu mwenye iko na tamaa kubwa sana ya kupenda kupata makuta mingi, mamlaka mingi, ya kupenda kufanya uasherati, ao ya kupenda kufanya mambo ingine sawa ile.

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu mumoja anakatala kwa kiburi muongozo wenye hekima wenye wanamupatia. Dada moja mwenye tayari iko na vitu mingi, lakini anapenda tena kupata vingine.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Mufalme Uzia na kiumbe moja wa kiroho wa Mungu waliangukia mu mutego wa kiburi. Pupa ilimuchochea Eva akule tunda ya muti yenye ilikatazwa; Daudi iko anafanya uzinifu na Bat-sheba; Yuda iko anaiba feza.