Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 30

Endelea Kutembea Katika Kweli

Endelea Kutembea Katika Kweli

“Sina furaha kubwa kuliko hii: nisikie kama watoto wangu wanaendelea kutembea katika kweli.”​—3 YO. 4.

WIMBO 54 “Hii Ndiyo Njia”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kama vile 3 Yohana 3, 4 inaonyesha, ni nini inafanya tukuwe na furaha?

WAZIA namna mutume Yohana alifurahi sana wakati alisikia kama watu wenye alisaidia kujifunza kweli walikuwa wanaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. Walikuwa na magumu mingi, na Yohana alifanya yake yote ili kutia nguvu imani ya wale Wakristo waaminifu, wenye yeye aliona kuwa watoto wake wa kiroho. Ni vile pia tunajisikia wakati watoto wetu, ikuwe wa kiroho ao wenye tulizaa kabisa, wanatoa maisha yao kwa Yehova na wanaendelea kumutumikia.​—Soma 3 Yohana 3, 4.

2. Barua zenye Yohana aliandika zilikuwa na kusudi gani?

2 Mu mwaka wa 98 K.K.Y., inawezekana Yohana alikuwa anaishi Efeso ao karibu na Efeso. Pengine alienda Efeso kisha kutoka katika kisiwa cha Patmo, kwenye alikuwa anafungwa. Ni karibu na ile kipindi, njo Yehova alitumia roho yake ili kumuongoza Yohana aandike barua tatu. Zile barua zilikuwa na kusudi la kutia moyo Wakristo waaminifu waendelee kulinda imani yao na waendelee kutembea katika kweli.

3. Tutazungumuzia maulizo gani?

Yohana njo alikuwa mutume wa mwisho mwenye alikuwa angali muzima, na alihangaishwa na hali ya mubaya yenye walimu wa uongo walileta mu makutaniko. * (1 Yo. 2:18, 19, 26) Wale waasi-imani walikuwa wanasema kama walimujua Yehova Mungu, lakini hawakukuwa wanatii sheria zake. Tuchunguze basi shauri lenye kuongozwa na roho lenye Yohana alitoa. Wakati tuko tunachunguza shauri hilo, tutajibia hii maulizo tatu: Kutembea katika kweli maana yake nini? Ni magumu gani yenye tunapambana nayo? Na namna gani tunaweza kusaidiana ili kubakia katika kweli?

KUTEMBEA KATIKA KWELI MAANA YAKE NINI?

4. Kulingana na 1 Yohana 2:3-6 na 2 Yohana 4, 6, kutembea katika kweli kunatia ndani nini?

4 Ili kutembea katika kweli, tunapaswa kujua kweli yenye kuwa katika Neno la Mungu, Biblia. Tena, tunapaswa “kushika amri [za Yehova],” ni kusema, tunapaswa kuzitii. (Soma 1 Yohana 2:3-6; 2 Yohana 4, 6.) Yesu alituachia mufano muzuri sana wa kumutii Yehova. Njo maana, njia moja ya muzuri ya kumutii Yehova ni kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu.​—Yoh. 8:29; 1 Pe. 2:21.

5. Tunapaswa kuwa hakika na mambo gani?

5 Ili kuendelea kutembea katika kweli, tunapaswa kuwa hakika kabisa kama Yehova ni Mungu wa kweli, na kama mambo yote yenye anatuambia katika Neno lake Biblia ni ya kweli. Tunapaswa pia kuwa hakika kama Yesu njo Masiya mwenye aliahidiwa. Leo, watu wengi wako na mashaka kama Yesu amechaguliwa ili kuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Yohana alionya kama kulikuwa “wadanganyifu wengi,” wenye wangepotosha wale wenye imani yao haikukuwa nguvu kabisa ili kutetea kweli kuhusu Yehova na Yesu. (2 Yo. 7-11) Yohana aliandika hivi: “Ni nani mwenye kuwa muongo kama haiko ule mwenye anakana kwamba Yesu ndiye Kristo?” (1 Yo. 2:22) Njia moja tu yenye inaweza kutusaidia ili tusidanganywe ni kujifunza Neno la Mungu. Ni kwa kufanya vile tu njo tunaweza kufikia kumujua Yehova na Yesu. (Yoh. 17:3) Na ni kwa kufanya vile tu njo tunaweza kuwa hakika kama mambo yenye tunaamini ni ya kweli.

NI MAGUMU GANI YENYE TUNAPAMBANA NAYO?

6. Ni magumu gani kijana mumoja Mukristo alipambana nayo?

6 Wakristo wote wanapaswa kuwa waangalifu ili wasidanganywe na filozofia za wanadamu. (1 Yo. 2:26) Zaidi sana vijana Wakristo wanapaswa kufungua macho ili wasiangukie mu ile mutego. Alexia, * dada wa miaka 25, mwenye kuishi katika inchi ya Ufaransa, anasema hivi: “Wakati nilikuwa mudogo, mawazo ya hii ulimwengu kama vile, fundisho la mageuzi na filozofia za wanadamu, ilinivuruga akili. Kisha wakati fulani, ile mafundisho ilianza kunivutia. Lakini niliona kama haingekuwa muzuri nifanye sawa vile sijue mambo yenye Biblia inafundisha na kuanza kuamini kila kitu walikuwa wanatufundisha ku masomo.” Alexia alijifunza kitabu La vie: comment est-elle apparue ? Évolution ou création ? Kisha tu majuma fulani, mashaka yote ilipotea. Anasema hivi: “Nilijihakikishia mimi mwenyewe kama Biblia iko na kweli. Na nilifikia kuona kama kuishi kulingana na kanuni za Biblia njo kunaleta furaha na amani.”

7. Tunapaswa kuepuka nini, na juu ya nini?

7 Wakristo wote, vijana na wenye kukomaa, wanapaswa kuepuka kuwa na maisha ya unafiki. Yohana alionyesha kama hatuwezi kuwa tunatembea katika kweli, na wakati uleule tuko na mwenendo mubaya. (1 Yo. 1:6) Kama tunapenda Mungu aendelee kutukubali, tunapaswa kukumbuka kila mara kama iko anaona kila kitu chenye tunafanya. Ni kusema, hakuna zambi yenye tunaweza kuficha, sababu Yehova anaonaka kila kitu.​—Ebr. 4:13.

8. Tunapaswa kukataa jambo gani?

8 Tunapaswa kukataa maoni ya ulimwengu kuhusu zambi. Mutume Yohana aliandika hivi: “Kama tunasema, ‘Hatuna zambi,’ tunajidanganya sisi wenyewe.” (1 Yo. 1:8) Katika wakati wa Yohana, waasi-imani walikuwa wanasema kama inawezekana mutu afanye mambo yenye Mungu anakataza na wakati uleule akuwe rafiki yake. Leo, tunaishi kati ya watu wenye kuwa na mawazo ileile. Watu wengi wanasema kama wanamuamini Mungu, lakini hawakubaliane na mawazo ya Yehova kuhusu zambi, zaidi sana kama inahusu mambo ya ngono. Mambo yenye Yehova anaona kuwa ni zambi, wao wanaona kama kila mutu iko na uhuru wa kuifanya kama anapenda.

Vijana, mujikaze kujua sababu yenye inafanya Yehova aone jambo fulani kuwa sawa ao hapana. Kufanya vile kutawasaidia kujua namna ya kutetea imani yenu (Ona fungu la 9) *

9. Namna gani kufuata mambo yenye Biblia inasema kumesaidia sana vijana?

9 Ni nguvu, zaidi sana kwa vijana Wakristo, kuwa na maoni ya muzuri juu ya ngono wakati wanafunzi wenzao ao watu wenye kutumika pamoja nao hawakubaliane na mambo yenye Biblia inasema. Ile hali ilimufikia Aleksandar. Anasema hivi: “Ku masomo, vijana fulani wanamuke walinikaza ili nifanye nao ngono. Waliniambia kama, juu sikukuwa na rafiki mwanamuke, iko saa tu ninakuwaka na tabia ya kulala na wanaume wenzangu.” Ile hali inaweza pia kukupata. Lakini kumbuka kama, wakati unafanya mambo yenye Biblia inasema, unajiheshimisha mwenyewe, unatunza afya na akili yako, na pia unalinda urafiki wako pamoja na Yehova. Na kila mara, wakati unashinda jaribu fulani, inakuwa mwepesi kwako kufanya mambo yenye kuwa sawa. Usisahau kama, maoni yenye kupotoka ya ulimwengu huu kuhusu ngono inatoka kwa Shetani. Kwa hiyo, wakati unakataa kufuata ile maoni, ‘unashinda ule muovu.’​—1 Yo. 2:14.

10. Namna gani 1 Yohana 1:9 inatusaidia kuendelea kumutumikia Yehova tukiwa na zamiri safi?

10 Tunajua kama Yehova iko na haki ya kutuonyesha jambo lenye anaona kuwa ni zambi. Na tunajikaza sana ili tusifanye zambi. Lakini wakati tunafanya zambi, tunaungama zambi zetu kwa Yehova kupitia sala. (Soma 1 Yohana 1:9.) Na kama tunafanya zambi nzito, tunatafuta musaada wa wazee, wenye Yehova aliweka ili kutuhangaikia kiroho. (Yak. 5:14-16) Lakini, hatupaswe kuendelea kuhangaika kwa sababu ya zambi yenye tulifanyaka zamani. Juu ya nini? Juu, Baba yetu mwenye upendo alitoa zabihu ya bei ya ukombozi ya Mwana wake ili zambi zetu zisamehewe. Wakati Yehova anasema kama anakuwaka anasamehe wale wenye wanatubu kikweli, ni vile anafanyaka kabisa. Kwa hiyo, hakuna kitu kinaweza kutuzuia kuendelea kumutumikia Yehova tukiwa na zamiri safi.​—1 Yo. 2:1, 2, 12; 3:19, 20.

11. Namna gani tunaweza kulinda akili yetu juu isipotoshwe na mafundisho yenye inaweza kuregeza imani yetu?

11 Tunapaswa kukataa mafundisho ya waasi-imani. Tangu kutaniko la Kikristo lianze, Ibilisi ametumia watu wengi ili kudanganya watumishi waaminifu wa Mungu kwa kuwafanya wakuwe na mashaka. Kwa hiyo, ni muzuri kujua tofauti kati ya habari za kweli na habari za uongo. * Maadui wetu wanaweza kutumia Enternete ao site za Enternete za kupashana habari, ili kuregeza imani yetu kwa Yehova na upendo wenye tuko nao kwa ndugu na dada zetu. Ukumbuke kama zile habari za uongo zinatoka kwa Shetani, kwa hiyo uzikatae!​—1 Yo. 4:1, 6; Ufu. 12:9.

12. Juu ya nini tunapaswa kutia nguvu imani yetu katika kweli zenye tumejifunza?

12 Ili kupinga majaribu ya Shetani, tunapaswa kutia nguvu tumaini letu katika Yesu na katika daraka lenye iko nalo mu kutimizwa kwa mapenzi ya Mungu. Tunapaswa pia kutumainia njia moja tu yenye Yehova iko anatumia leo ili kuongoza tengenezo lake. (Mt. 24:45-47) Tunatia nguvu tumaini letu kwa kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida. Tukifanya vile, imani yetu itakuwa kama muti wenye mizizi yake inaingia chini sana ndani ya udongo. Paulo alizungumuzia jambo lenye kufanana na hilo wakati aliandikia kutaniko la Kolosai. Alisema hivi: “Kama vile mumepokea Kristo Yesu mwenye ni Bwana, muendelee kutembea katika umoja naye, mukiwa mumetia mizizi na kujengwa katika yeye na kufanywa imara katika imani.” (Kol. 2:6, 7) Wakati Mukristo anatia nguvu imani yake, hakuna kitu chenye Shetani ao watu wake wanaweza kufanya ili kumutikisa.​—2 Yo. 8, 9.

13. Tunapaswa kutazamia nini, na juu ya nini?

13 Tunapaswa kutazamia kama ulimwengu utatuchukia. (1 Yo. 3:13) Yohana anatukumbusha kama “ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za ule muovu.” (1 Yo. 5:19) Kadiri mupangilio huu wa mambo unakaribia mwisho wake, kasirani ya Shetani inaendelea kuongezeka pia. (Ufu. 12:12) Zaidi ya kutumia njia zenye haziko za moja kwa moja ili kutushambulia, kama vile uasherati ao habari za uongo za waasi-imani, Shetani anatumia pia njia za moja kwa moja, kama vile mateso makali. Shetani anajua kama anabakia tu na kipindi kifupi cha wakati ili kujaribu kusimamisha kazi yetu ya kuhubiri ao kuvunja imani yetu. Njo maana, hatushangae kuona kama kazi yetu imekatazwa katika inchi fulani. Lakini, ndugu na dada zetu wenye kuwa katika zile inchi wanaendelea kuvumilia. Mufano wao unatuhakikishia kama, hata Shetani afanye nini, tunaweza kumushinda!

TUSAIDIANE ILI KUENDELEA KUBAKIA KATIKA KWELI

14. Ni mu njia gani tunaweza kusaidia ndugu na dada zetu waendelee kubakia katika kweli?

14 Ili kusaidia ndugu na dada zetu waendelee kubakia katika kweli, tunapaswa kuwaonyesha huruma. (1 Yo. 3:10, 11, 16-18) Tunapaswa kupendana, hapana tu wakati mambo iko muzuri, lakini pia wakati magumu inatokea. Kwa mufano, unajua mutu mwenye alifisha mupendwa wake, na iko na lazima ya kutiwa moyo ao kusaidiwa mu njia fulani? Ao kuko ndugu na dada zetu fulani wenye wamepatwa na musiba wa asili na wako na lazima ya kujengewa tena Majumba yao ya Ufalme ao nyumba zao? Tunaonyesha kama tuko na upendo na huruma kwa ndugu na dada zetu, hapana tu kupitia maneno yetu, lakini pia kupitia matendo yetu.

15. Kama vile inaonyeshwa katika 1 Yohana 4:7, 8, ni jambo gani lenye tunapaswa kufanya?

15 Wakati tuko na upendo kati yetu, tunaonyesha kama tunamuiga Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo. (Soma 1 Yohana 4:7, 8.) Njia moja ya lazima yenye tunaonyesha kama tuko na upendo ni kusameheana. Kwa mufano, mutu fulani anaweza kutukosea na kisha anaomba musamaha. Kama tuko na upendo, tutamusamehe na hatutakumbuka tena kosa lenye alifanya. (Kol. 3:13) Ndugu mumoja mwenye kuitwa Aldo alihuzunika sana wakati ndugu fulani mwenye aliheshimia alisema jambo fulani lenye halikukuwa la muzuri kuhusu watu wa kabila yake. Aldo anasema hivi: “Nilisali sana Yehova anisaidie ili nisikuwe na mawazo ya mubaya juu ya ule ndugu.” Lakini, Aldo alifanya jambo lingine. Alimuambia ule ndugu kama alipenda kuhubiri naye. Wakati walikuwa wanahubiri, Aldo alimuambia kama mambo yenye alisemaka ilimukwaza. Aldo anasema hivi: “Wakati ule ndugu alisikia mambo yenye nilimuambia, aliniomba musamaha. Kupitia tu namna yake ya kusema, niliona kama alihuzunika sana, sana kabisa. Kisha pale, tukakuwa marafiki wa karibu sana.”

16-17. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

16 Mutume Yohana alipenda sana ndugu na dada na alipenda wakuwe na imani yenye nguvu. Upendo wake unaonekana mu mashauri yenye aliwatolea katika barua tatu zenye kuongozwa na roho. Tunafurahi sana kujua kama, wanaume na wanamuke wengine wenye wako kama Yohana, watatawala pamoja na Kristo mbinguni!​—1 Yo. 2:27.

17 Tusisahau hata kidogo mashauri yenye tumezungumuzia. Tuazimie basi kuendelea kutembea katika kweli, na kumutii Yehova mu kila jambo katika maisha yetu. Ujifunze Neno lake, na ulitumainie. Endelea kuwa na imani yenye nguvu katika Yesu. Kataa filozofia za wanadamu na mafundisho ya waasi-imani. Epuka zambi na maisha ya unafiki. Uishi kulingana na kanuni za juu za mwenendo zenye Yehova anatupatia. Na pia saidia ndugu zako waendelee kuwa nguvu kiroho kwa kuwasamehe kama wanakukosea, na pia kwa kuwasaidia kama wako na lazima ya jambo fulani. Tukifanya vile, hata kama tunapambana na magumu, tutaendelea kutembea katika kweli.

WIMBO 49 Kufurahisha Moyo wa Yehova

^ fu. 5 Tunaishi mu dunia yenye kutawaliwa na Shetani, baba ya uongo. Kwa hiyo, haiko mwepesi kwetu kuendelea kutembea katika kweli. Wakristo wenye waliishi ku mwisho wa karne ya kwanza, walikuwa pia na ile magumu. Juu ya kusaidia wale Wakristo wa zamani na sisi pia, Yehova alimuongoza mutume Yohana aandike barua tatu. Habari zenye kupatikana katika zile barua tatu zitatusaidia tutambue magumu yenye inaweza kutuzuia kuendelea kutembea katika kweli na namna tunaweza kupambana nayo.

^ fu. 6 Majina fulani imebadilishwa.

^ fu. 11 Ona habari ya funzo yenye kichwa “Unajua Ukweli wa Mambo?” katika Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 8, 2018.

^ fu. 59 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati iko ku masomo, dada mumoja anaona na kusikia mambo mingi kuhusu matendo ya wanaume kulala na wanaume na wanamuke kulala na wanamuke. (Mu desturi fulani, rangi za upinde wa mvua ni alama ya matendo ya wanaume kulala na wanaume na wanamuke kulala na wanamuke.) Kisha, anatafuta habari mu vichapo ili kutia nguvu imani yake. Ile inamusaidia kukamata uamuzi wa muzuri.