Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Ni wakati gani Yesu alifikia kuwa Kuhani Mukubwa, na je, kuko tofauti kati ya wakati agano jipya lilikubaliwa na wakati lilizinduliwa?

Ushuhuda unaonyesha kama Yesu alifikia kuwa Kuhani Mukubwa wakati alibatizwa katika mwaka wa 29 K.K.Y. Tunajua vile namna gani? Wakati Yesu alibatizwa, alionyesha kama alikuwa tayari kutoa uzima wake kwenye mazabahu ya mufano, yenye inafananisha “mapenzi” ya Mungu. (Gal. 1:4; Ebr. 10:5-10) Kwa kuwa mazabahu ni sehemu ya maana ya hekalu, inawezekana hekalu la kiroho pia lilianza wakati Yesu alibatizwa. Hekalu kubwa la kiroho la Yehova linafananisha mupango wa Yehova wenye unategemea zabihu ya ukombozi ya Yesu, wenye unatuwezesha kumutolea Yehova ibada safi.​—Mt. 3:16, 17; Ebr. 5:4-6.

Juu hekalu kubwa la kiroho lilikuwa limewekwa, iliomba kukuwe kuhani mukubwa. Njo maana, Yehova alimutia Yesu mafuta “kwa roho takatifu na nguvu.” (Mdo. 10:37, 38; Mk. 1:9-11) Lakini, ni jambo gani linatuhakikishia kama Yesu alichaguliwa kuwa Kuhani Mukubwa mbele akufe na afufuliwe? Mufano wa Haruni na makuhani wengine wenye walikuja kisha yeye, wenye walitumika chini ya Sheria ya Musa, utatusaidia kupata jibu.

Kulingana na Sheria, ni kuhani mukubwa tu njo aliruhusiwa kuingia katika Patakatifu Zaidi mu tabenakulo, na kisha, katika Patakatifu Zaidi mu hekalu. Pazia njo ilitenganisha Patakatifu Zaidi na Patakatifu. Kuhani mukubwa alikuwa anaingia kupitia ile pazia, mara moja tu kwa mwaka, katika Siku ya Kufunika Zambi. (Ebr. 9:1-3, 6, 7) Kama vile tu Haruni na makuhani wengine wenye walikuja kisha yeye walikuwa wanachaguliwa na kuwekwa kuwa makuhani wakubwa mbele ya kuingia “kupitia lile pazia [la kwelikweli]” la tabenakulo, Yesu pia aliwekwa kuwa Kuhani Mukubwa wa hekalu kubwa la kiroho la Yehova mbele akufe na kisha alipita “kupitia lile pazia, ni kusema, mwili wake,” ili kuingia mbinguni. (Ebr. 10:20) Njo maana, mutume Paulo alisema kama, kwanza Yesu alikuja “akiwa kuhani mukubwa” na kisha akapita “katika hema kubwa na kamilifu zaidi yenye haikutengenezwa kwa mikono,” na kuingia “mbinguni kwenyewe.”​—Ebr. 9:11, 24.

Hakuna tofauti kati ya wakati agano jipya lilikubaliwa na wakati lilizinduliwa. Juu ya nini tunasema vile? Juu wakati Yesu alipanda mbinguni na kumutolea Mungu bei ya uzima wake mukamilifu kwa ajili yetu, alianzisha hatua ya kwanza kati ya hatua tatu zenye zilifanya agano jipya likubaliwe kulingana na sheria. Hatua zilezile njo zilizindua agano jipya, ni kusema, zilifanya agano jipya lianze kufanya kazi. Zile hatua zilikuwa nini?

Kwanza, Yesu alijionyesha mwenyewe mbele ya Yehova; kisha, Yesu alitoa samani ya zabihu yake kwa Yehova; na ku mwisho, Yehova alikubali samani ya damu yenye Yesu alimwanga. Agano jipya lilianza kufanya kazi wakati tu zile hatua zote zilitimizwa.

Biblia haionyeshe kabisa wakati wenye Yehova alikubali samani ya zabihu ya Yesu. Kwa hiyo, hatuwezi kusema ni wakati gani kabisa agano jipya lilikubaliwa na kuanza kufanya kazi. Lakini, tunajua kama Yesu alipanda mbinguni siku kumi mbele ya Pentekoste. (Mdo. 1:3) Ni wakati fulani mu kile kipindi kifupi, njo alitoa samani ya zabihu yake kwa Yehova, na Yehova aliikubali. (Ebr. 9:12) Ushuhuda wa jambo hilo ulionekana wazi wakati wa Pentekoste. (Mdo. 2:1-4, 32, 33) Ni wazi kama wakati huo agano jipya lilikuwa limewekwa na kuanza kufanya kazi.

Kwa kifupi, agano jipya lilikubaliwa na kuzinduliwa kisha Yehova kukubali samani ya damu yenye Yesu alimwanga. Kisha pale, agano hilo lilianza kufanya kazi. Mupatanishi wa agano hilo ni Yesu, mwenye kuwa na kazi ya Kuhani Mukubwa.​—Ebr. 7:25; 8:1-3, 6; 9:13-15.