Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 28

Epuka Kuchochea Mashindano​—Lakini Endeleza Amani

Epuka Kuchochea Mashindano​—Lakini Endeleza Amani

“Tusikuwe tunajisifu, tusichochee mashindano kati yetu, tusisikiliane wivu.”​—GAL. 5:26.

WIMBO 101 Tutumike kwa Umoja

KIFUPI YA HABARI *

1. Roho ya mashindano inaweza kuchochea watu wafanye nini?

MU DUNIA leo, watu wengi wanachochewa na roho ya mashindano. Mufanyabiashara fulani anaweza kutendea wafanyabiashara wengine mambo ya mubaya juu biashara yake ikuwe muzuri zaidi. Muchezaji fulani wa michezo anaweza kuumiza kimakusudi muchezaji wa mu ekipe ingine juu tu ya kupata ushindi. Mwanafunzi fulani mwenye iko anapenda apate fasi ku masomo fulani ya juu na yenye kujulikana sana anaweza hata kuiba examens zenye wanafunzi wanafanyaka juu wakubaliwe kuingia ku ile masomo. Siye Wakristo, tunajua kama matendo ya vile iko mubaya; iko kati ya “matendo ya mwili.” (Gal. 5:19-21) Sasa, inawezekana Mashahidi fulani wa Yehova waanze kuchochea roho ya mashindano mu kutaniko bila hata wao wenyewe kutambua vile? Ile ni ulizo ya maana, juu roho ya mashindano inaweza kuharibu umoja wa familia yetu ya ndugu na dada.

2. Ni mambo gani tutaona mu hii habari?

2 Mu hii habari, tutaona mambo fulani ya mubaya yenye inaweza kutuchochea kuanza kushindana na ndugu zetu. Tutaona pia mifano ya wanaume na wanamuke fulani waaminifu wa zamani wenye hawakuangukia mu mutego wa roho ya mashindano. Kwanza, tuone namna tunaweza kuchunguza nia yetu.

CHUNGUZA NIA YAKO

3. Tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

3 Ni muzuri, mara kwa mara, kuchunguza nia yetu. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Najisikiaka muzuri tu wakati naona kama ninapita mutu fulani? Mu kutaniko, najikazaka kutumika sana juu ionekane kama hakuna mwingine sawa miye, ao ninapita ndugu ao dada fulani? Ao ninafanyaka yangu yote juu tu ninapendaka kumufurahisha Yehova?’ Juu ya nini tunapaswa kujiuliza ile maulizo? Ona mambo yenye Biblia inasema.

4. Sawa vile Wagalatia 6:3, 4 inaonyesha, juu ya nini tunapaswa kuepuka kujilinganisha na wengine?

4 Biblia inatuambia kama tunapaswa kuepuka kujilinganisha na wengine. (Soma Wagalatia 6:3, 4.) Juu ya nini? Sababu moja ni hii: Ikiwa tunawaza kama siye njo tunafanyaka mambo muzuri zaidi kuliko wengine, tunaweza kuwa na kiburi. Na sababu ingine ni hii: Ikiwa tunawaza kama wengine njo wanafanyaka mambo muzuri zaidi kuliko siye, tunaweza kuvunjika moyo. Kufikiri mu zile njia zote mbili haiko muzuri. (Ro. 12:3) Dada Katerina, * mwenye anaishi mu inchi ya Ugiriki, anasema hivi: “Nilikuwa na zoezi ya kujilinganisha na wengine wenye walionekana kuwa na sura ya muzuri zaidi, wenye walipata matokeo ya muzuri mu mahubiri, na wenye walijua kabisa namna ya kupata marafiki. Ile ilifanya nijione kuwa wa bure kabisa.” Tusisahau kama Yehova alituvuta kwake, hapana juu tuko na sura ya muzuri, ao juu tunasemaka muzuri, ao juu tunajulikana sana, lakini ni juu tuko tayari kumupenda na kusikiliza Mwana wake.​—Yoh. 6:44; 1 Ko. 1:26-31.

5. Mufano wa ndugu Hyun unakufundisha nini?

5 Ulizo ingine yenye tunaweza kujiuliza njo hii: ‘Najulikana kuwa mutu mwenye anafanyaka amani, ao mara mingi ninakosanaka-kosanaka tu na wengine?’ Ona mambo yenye ndugu Hyun, mwenye anaishi mu Korea ya Kusini, alijionea. Wakati fulani, alikuwa anaona wale wenye walikuwa na madaraka fulani sawa vile walikuwa wanapenda kuonekana kuwa wazuri zaidi kumushinda. Anasema hivi: “Nilikuwa nasema wale ndugu mubaya, na mara mingi sikukubaliana na mambo yenye walikuwa wanasema.” Ile ilikuwa na matokeo gani? Anasema tena hivi: “Ile tabia yangu iligawanya kutaniko.” Marafiki fulani wa ndugu Hyun walimusaidia aelewe kama ile haikukuwa tabia ya muzuri. Hyun alifanya mabadiliko, na leo iko muzee muzuri mu kutaniko. Tukiona kama tunaanza kuwa na muelekeo fulani wa roho ya mashindano kuliko kuendeleza amani, tusibakie tu vile, tunapaswa kubadilika haraka sana.

USIJISIFU NA USISIKILIE WENGINE WIVU

6. Kulingana na Wagalatia 5:26, ni mambo gani inaweza kuchochea roho ya mashindano?

6 Soma Wagalatia 5:26. Ni mambo gani inaweza kutuchochea kuwa na roho ya mashindano? Ya kwanza ni kujisifu. Mutu wa kujisifu-sifu anakuwaka na kiburi na anajihangaikiaka tu yeye peke. Ya pili ni wivu. Mutu mwenye iko na wivu anapendaka kitu yenye mutu mwingine iko nayo, na anapenda hata ule mutu naye aikose. Kwa kweli, wivu ni aina fulani ya chuki. Tunapenda kabisa kuepuka ile mambo mbili sawa vile tunaweza kuepuka ugonjwa wa kuambukiza!

7. Leta mufano wenye kuonyesha matokeo ya mubaya ya kujisifu na kusikilia wengine wivu?

7 Kujisifu na wivu iko sawa vile uchafu wenye uko mu carburant yenye inatumiwa mu avion. Ni kweli kama avion inaweza kupanda juu, lakini ile uchafu yenye iko mu carburant italeta shida sana, na kufanya motere zisitumike muzuri ao hata kufanya avion ianguke. Vilevile, mutu anaweza kumutumikia Yehova kwa muda fulani. Lakini kama iko anajisifu na iko na wivu, ataanguka. (Mez. 16:18) Ataacha kumutumikia Yehova na atajiletea magumu na kuletea wengine magumu. Sasa, tunaweza kufanya nini juu tusijisifu na tusisikilie wengine wivu?

8. Namna gani tunaweza kupiganisha roho ya kujisifu?

8 Tunaweza kupiganisha roho ya kujisifu kama tunatia mu akili hii shauri yenye mutume Paulo alipatia Wafilipi: “Musifanye jambo lolote kwa ugomvi ao kwa kutafuta sifa, lakini kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi.” (Flp. 2:3) Kama tunaona wengine kuwa wazuri zaidi kuliko siye, hatutashindana na wale wenye wako na vipaji ao uwezo wenye hatuna. Kuliko kufanya vile, tutafurahi, zaidi sana kama wako wanatumia uwezo wao mu utumishi wa Yehova ili kumusifu. Tena, kama wale ndugu na dada wenye kuwa na uwezo fulani wanafuata shauri ya Paulo, watakazia sifa za muzuri zenye tuko nazo. Ile itasaidia kuendeleza amani na umoja mu kutaniko.

9. Namna gani tunaweza kuepuka kuwa na wivu?

9 Tunaweza kuepuka kuwa na wivu kwa kuonyesha sifa ya kiasi, ni kusema, kutambua mipaka yetu. Kama tuko wenye kiasi, hatutajaribu kuonyesha kama tuko na vipaji ao uwezo zaidi kuliko wengine. Lakini, tutatafuta njo kuiga mambo ya muzuri kwa wale wenye kuwa na uwezo zaidi kuliko siye. Kwa mufano, waza ndugu fulani anatoaka hotuba za muzuri sana mu kutaniko. Tunaweza kumuuliza atuonyeshe namna anatayarishaka hotuba zake. Kama dada fulani anapikaka muzuri sana chakula, tunaweza kumuuliza siri yake ni nini, yenye inaweza kutusaidia na siye tukuwe tunapika muzuri zaidi chakula. Na kama kijana Mukristo iko na magumu ya kupata marafiki, anaweza kuomba shauri kwa ule mwenye hakuwake na ile magumu. Kama tunafanya vile tutaepuka wivu, lakini tutakomalisha uwezo wetu.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MIFANO FULANI YA BIBLIA

Juu alikuwa munyenyekevu, Gideoni alilinda amani na Waefraimu (Ona fungu ya 10-12)

10. Gideoni alipambana na magumu gani?

10 Ona mambo yenye ilitokea kati ya Gideoni, mwenye alikuwa wa kabila ya Manase, na wanaume wa kabila ya Efraimu. Kwa musaada wa Yehova, Gideoni na wanaume wake 300 walipata ushindi wa ajabu sana wenye ungefanya wakuwe na kiburi sana. Wale wanaume wa Efraimu walikuja kuona Gideoni, hapana juu ya kumupongeza, lakini juu ya kumulaumu. Inaonekana walikasirika sana juu tangu mwanzo Gideoni hakuwaomba wajiunge naye ili kupigana na maadui wa Mungu. Walihangaikia sana kuheshimisha kabila yao, mupaka wakasahau jambo ya maana sana yenye Gideoni alikuwa amefanya, ni kusema, kuheshimisha jina ya Mungu na kulinda watu wake.​—Amu. 8:1.

11. Gideoni aliambia nini wanaume wa Efraimu?

11 Kwa unyenyekevu, Gideoni aliambia hivi wanaume wa Efraimu: “Nimefanya nini nikilinganishwa na ninyi?” Kisha akawapatia mufano fulani wenye kuonyesha namna Yehova aliwabariki. Ile ikafanya wale wanaume ‘wapoe.’ (Amu. 8:2, 3) Gideoni alionyesha unyenyekevu ili kulinda amani kati ya watu wa Mungu.

12. Mufano wa Waefraimu na wa Gideoni unatufundisha nini?

12 Hii habari inatufundisha nini? Kuhusu Waefraimu, tunaona kama tunapaswa kukaza akili yetu zaidi juu ya kulinda sifa ya Yehova kuliko yetu. Kama uko kichwa ya familia ao muzee, unaweza kujifunza jambo fulani kupitia mufano wa Gideoni. Kama mutu fulani anakwazika juu ya mambo tulifanya, tunapaswa kujikaza kuelewa sababu yenye ilifanya akwazike. Tunapaswa pia kumupongeza juu ya mambo ya muzuri yenye amefanya. Ile inaomba tukuwe wanyenyekevu, zaidi sana kama inaonekana waziwazi kuwa yeye njo iko na kosa. Jambo ya maana zaidi ni kulinda amani kati yetu na ndugu zetu kuliko kuonyesha kama siye njo tuko na sheria.

Juu Hana alikuwa hakika kama Yehova angetengeneza mambo, alipata tena amani ya moyo (Ona fungu ya 13-14)

13. Hana alipambana na hali gani, na aliishinda namna gani?

13 Fikiria pia mufano wa Hana. Alikuwa bibi ya Mulawi mumoja mwenye aliitwa Elkana. Elkana alimupenda sana Hana. Lakini alikuwa na bibi mwingine, Penina. Hata vile, Elkana alimupenda zaidi Hana kuliko Penina; ijapokuwa ile yote, “Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakukuwa na watoto.” Ile ilifanya Penina akuwe anamuchokoza Hana “bila kuacha ili kumukasirisha.” Hana alijisikia namna gani? Alihuzunika sana! “Alikuwa analia na hakukuwa anakula.” (1 Sa. 1:2, 6, 7) Hakuna kwenye Biblia inaonyesha kama Hana alijaribu kulipiza kisasi mu njia fulani. Lakini, alimumwangia Yehova moyo wake na alikuwa hakika kama angetengeneza mambo. Je, Penina alibadilikaka? Biblia haiseme kitu juu ya ile. Lakini, tunajua kama Hana alipata tena amani ya moyo, ndiyo, “uso wake haukukuwa tena na huzuni.”​—1 Sa. 1:10, 18.

14. Mufano wa Hana unatufundisha nini?

14 Mufano wa Hana unatufundisha nini? Kama mutu fulani anajaribu kushindana na weye mu njia fulani, kumbuka kama unaweza kufanya hali ikuwe muzuri ao hapana. Haulazimike kuangukia mu mutego wa mashindano. Kuliko kurudisha ubaya kwa ubaya, jaribu kufanya amani na ule mutu. (Ro. 12:17-21) Hata kama habadilike, weye utaendelea kuwa na amani ya moyo.

Juu Apolo na Paulo walitambua kama Yehova njo alikuwa anabariki kazi, hakuna mwenye alisikilia mwenzake wivu (Ona fungu ya 15-18)

15. Apolo na Paulo walifanana mu mambo gani?

15 Tumalizie sasa na mufano wa mwanafunzi Apolo na wa mutume Paulo, na tuone mambo yenye tunaweza kujifunza. Wote wawili walijua muzuri sana Maandiko, walijulikana sana, na walikuwa walimu wazuri sana. Na wote walisaidia kufanya wanafunzi wengi. Lakini hakuna mwenye alisikilia mwenzake wivu.

16. Apolo alikuwa mutu wa namna gani?

16 Apolo alikuwa “muzaliwa wa Aleksandria,” kwenye watu walikuwa wanaenda ili kupata elimu. Inaonekana Apolo alikuwa musemaji muzuri, na “alikuwa anajua sana Maandiko.” (Mdo. 18:24) Wakati alienda Korinto, watu fulani mu kutaniko walionyesha waziwazi kama walimupenda zaidi kuliko ndugu wengine, kutia ndani Paulo. (1 Ko. 1:12, 13) Je, Apolo aliunga mukono ile roho ya kuleta migawanyiko? Hatuwazie kama alifanya vile. Juu wakati fulani kisha Apolo kutoka Korinto, Paulo alimuomba arudie tena kule. (1 Ko. 16:12) Paulo hangemuombaka Apolo afanye vile kama angeonaka kuwa iko naleta migawanyiko mu kutaniko. Ni wazi kama, Apolo alitumia muzuri zawadi yenye alikuwa nayo ili kutangaza habari njema na kutia nguvu ndugu zake. Tunaweza pia kuwa hakika kama Apolo alikuwa mwanaume munyenyekevu. Kwa mufano, hakuna kwenye Biblia inaonyesha kama alikwazika wakati Akila na Prisila ‘walimufasiria njia ya Mungu sawasawa kabisa.’​—Mdo. 18:24-28.

17. Namna gani Paulo aliendeleza amani?

17 Mutume Paulo alijua kazi ya muzuri yenye Apolo alikuwa anafanya. Lakini Paulo hakuwaza kama watu wataona Apolo kuwa muzuri zaidi kumushinda. Tunaona unyenyekevu, kiasi, na usawaziko wa Paulo mu shauri yenye alipatia kutaniko ya Korinto. Kuliko kufurahia wakati watu walikuwa wanasema “mimi ni wa Paulo,” aliacha sifa yote imuendee Yehova Mungu na Yesu Kristo.​—1 Ko. 3:3-6.

18. Kulingana na 1 Wakorinto 4:6, 7, mufano wa Apolo na Paulo unatufundisha nini?

18 Mufano wa Apolo na Paulo unatufundisha nini? Tunaweza kujitoa sana mu kazi ya Yehova, na kusaidia watu wengi wafanye maendeleo na wafikie kubatizwa. Lakini tunatambua kama ile yote inawezekana tu kwa musaada wa Yehova. Lakini, tunajifunza tena kama kuwa na madaraka mingi kunatupatia nafasi zaidi ya kusaidia kuendeleza amani mu kutaniko. Tuko wenye shukrani sana wakati ndugu wenye kuwa na madaraka wanasaidia kuendeleza umoja na amani kwa kutupatia mashauri yenye kutegemea Biblia. Pia kuliko kujionyesha kuwa wa maana, wanatusaidia kumutii Kristo Yesu na kufuata mufano wake!​—Soma 1 Wakorinto 4:6, 7.

19. Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini? (Ona kisanduku “ Epuka Kuchochea Mashindano.”)

19 Kila mumoja wetu iko na uwezo fulani wenye Yehova amemupatia. Tunaweza kutumia ile uwezo ili “kutumikiana.” (1 Pe. 4:10) Tunaweza kuwaza kama mambo yenye tuko tunafanya ni ya kidogo. Lakini ile matendo kidogo-kidogo yenye kusaidia kuendeleza umoja iko sawa vile brike moja-moja yenye inatumiwa ili kujenga nyumba. Kwa hiyo, kila mumoja wetu afanye yake yote ili kutosha ndani yake alama yoyote ya roho ya mashindano. Tuazimie basi kuendeleza umoja na amani mu kutaniko.​—Efe. 4:3.

WIMBO 80 Uonje na Uone Vile Yehova Ni Mwema

^ fu. 5 Kama chungu ya udongo iko na mipasuko ya kidogo-kidogo ndani yake, ile inaweza kufanya ivunjike. Vilevile, roho ya mashindano inaweza kufanya kutaniko ikuwe zaifu. Kama kutaniko haiko nguvu na haina umoja, haiwezi kuwa fasi ya amani ili kumuabudu Mungu. Hii habari itaonyesha juu ya nini tunapaswa kuepuka roho ya mashindano na pia nini njo tunaweza kufanya ili kuendeleza amani mu kutaniko.

^ fu. 4 Majina imebadilishwa.