Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 26

Unaweza Kusaidia mu Kazi ya Kufanya Wanafunzi?

Unaweza Kusaidia mu Kazi ya Kufanya Wanafunzi?

‘Mungu ndiye . . . anawapatia hamu na pia nguvu za kutenda.’​—FLP. 2:13.

WIMBO 64 Kufanya Kazi ya Mavuno kwa Furaha

KIFUPI YA HABARI *

1. Ni mambo gani Yehova alikufanyia?

NAMNA gani ulifikia kuwa Shahidi wa Yehova? Kwanza, ulisikia “habari njema,” pengine kwa wazazi wako, kwa mufanyakazi ao mwanafunzi mwenzako, ao kupitia mahubiri ya nyumba kwa nyumba. (Mk. 13:10) Kisha, mutu fulani alitumia wakati na nguvu yake mingi juu ya kukufundisha Biblia. Wakati ulikuwa unajifunza, ulifikia kumupenda Yehova na kujua kama anakupenda. Yehova alikuvuta ku kweli, na vile uko sasa mufuasi wa Yesu Kristo, uko na tumaini ya kuishi milele. (Yoh. 6:44) Uko mwenye shukrani kwa Yehova juu alikutumia mutu fulani ili akufundishe kweli na juu anakukubali ukuwe mumoja wa watumishi Wake.

2. Ni mambo gani tutaona mu hii habari?

2 Juu tunajua kweli, tuko na pendeleo ya kusaidia watu wengine wajiunge na siye mu barabara yenye inaongoza ku uzima. Pengine hatukuwake na magumu ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, lakini inawezekana tuko na magumu ya kuanzisha na kuongoza funzo ya Biblia. Ile njo magumu uko nayo? Kama ni vile, tunatumaini kama mapendekezo fulani yenye kuwa mu hii habari itakusaidia. Tutaona nini njo inatuchocheaka kufanya wanafunzi. Tutaona pia magumu yenye inaweza kutuzuia kuongoza funzo ya Biblia. Lakini mbele ya kuizungumuzia, tuone kwanza juu ya nini hatupaswe tu kuwa wahubiri wa habari njema lakini pia walimu.

YESU ALITUAMURU KUHUBIRI NA KUFUNDISHA

3. Juu ya nini tunakuwaka tunahubiri?

3 Wakati Yesu alikuwa hapa ku dunia, alipatia wafuasi wake kazi yenye kuwa na sehemu mbili. Kwanza, aliwaambia wahubiri habari njema kuhusu Ufalme, kisha aliwaonyesha namna ya kufanya vile. (Mt. 10:7; Lu. 8:1) Tena, Yesu alitayarisha wanafunzi wake kwa kuwaambia kama kuko watu wangeitika habari njema na wengine hapana. (Lu. 9:2-5) Aliambia pia wanafunzi wake kama wangetoa “ushahidi kwa mataifa yote.” (Mt. 24:14; Mdo. 1:8) Watu waitike ao hapana, wanafunzi wa Yesu walipaswa kuwahubiria kuhusu Ufalme wa Mungu na mambo yenye ingetimiza.

4. Kama vile Matayo 28:18-20 inaonyesha, zaidi ya kuhubiri juu ya Ufalme ni nini ingine tunapaswa kufanya?

4 Ni nini njo ilikuwa sehemu ya pili ya kazi yenye Yesu alipatia wafuasi wake? Aliwaambia wafundishe watu wenye wanaweza kufikia kuwa wanafunzi wake washike mambo yote yenye aliamuru. Lakini kazi ya kuhubiri na kufundisha ilikuwaka tu ya mu ile wakati, sawa vile watu fulani wanaweza kusema? Hapana, Yesu alionyesha kama ile kazi ya maana sana ingeendelea mupaka leo, ndiyo, “mupaka umalizio wa mupangilio wa mambo.” (Soma Matayo 28:18-20.) Inawezekana Yesu alitoa ile amri wakati alitokea wanafunzi wake zaidi ya 500. (1 Ko. 15:6) Na mu ufunuo wenye alipatia Yohana, Yesu alionyesha waziwazi kama inatazamiwa wanafunzi wake wote wasaidie wengine wamujue Yehova.​—Ufu. 22:17.

5. Mu 1 Wakorinto 3:6-9, ni mufano gani Paulo alitumia ili kuonyesha uhusiano kati ya kuhubiri na kufundisha?

5 Mutume Paulo alilinganisha kazi ya kufanya wanafunzi na kazi ya kulima shamba, ili kuonyesha kama tunapaswa kufanya mingi zaidi kuliko tu kupanda mbegu. Alikumbusha Wakorinto hivi: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji . . . Ninyi ni shamba la Mungu lenye linalimwa.” (Soma 1 Wakorinto 3:6-9.) Tukiwa wafanyakazi mu “shamba la Mungu,” hatufanye tu kazi ya kupanda mbegu lakini tunazimwangia pia maji na kila mara tunachunguza ili kuona kama ziko zinakomala. (Yoh. 4:35) Hata vile, tunatambua kama ni Mungu njo iko anazikomalisha.

6. Kazi yetu ya kufundisha inatia ndani nini?

6 Tuko tunatafuta watu wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele.” (Mdo. 13:48) Juu wakuwe wanafunzi, tunapaswa kuwasaidia (1) kuelewa, (2) kukubali, na (3) kutumikisha mambo yenye wanajifunza mu Biblia. (Yoh. 17:3; Kol. 2:6, 7; 1 Te. 2:13) Siye wote mu kutaniko tunaweza kusaidia wanafunzi wa Biblia kwa kuonyesha kama tunawapenda na kufanya wasijisikie kuwa peke yao wakati wanakusanyika. (Yoh. 13:35) Ule mwenye iko anaongoza funzo ya Biblia anapaswa kutumia sana wakati na nguvu yake ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia aachane na tabia ao mambo yenye alikuwa anaamini, yenye ilikuwa ‘ilishatia mizizi kabisa.’ (2 Ko. 10:4, 5) Itaomba pengine miezi ya mingi ili kumusaidia mutu afanye ile mambo yote na afikie kubatizwa. Lakini kufanya vile kunaleta matokeo ya muzuri.

UPENDO NJO UNATUCHOCHEAKA KUFANYA WANAFUNZI

7. Ni nini njo inatuchocheaka kuhubiri na kufanya wanafunzi?

7 Juu ya nini tunahubiri na kufanya wanafunzi? Kwanza, ni juu tunamupenda Yehova. Wakati unafanya yako yote ili kutii amri ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, unaonyesha kama unamupenda Mungu. (1 Yo. 5:3) Waza kidogo: Kumupenda Yehova njo kumekuchochea kuhubiri nyumba kwa nyumba. Lakini ilikuwa mwepesi kutii ile amri? Pengine hapana. Uliogopaka wakati, kwa mara ya kwanza, ulikuwa karibu kupiga hodi ku mulango? Inawezekana! Lakini ulijua kama njo kazi yenye Yesu anapenda ufanye, na ulitii. Na inawezekana, kisha wakati fulani, ilianza kuwa mwepesi kwako kuhubiri. Sasa, tuseme nini juu ya kuongoza funzo ya Biblia? Unaogopa wakati unasikia tu ile maneno? Pengine. Lakini, wakati unamuomba Yehova akusaidie ushinde woga na akupatie uhodari wa kuanzisha funzo ya Biblia, atakusaidia. Atakupatia nguvu ya kutimiza tamaa yako ya kufanya wanafunzi.

8. Kulingana na Marko 6:34, ni nini ingine inaweza kutuchochea kufundisha wengine?

8 Pili, kupenda majirani wetu kunatuchocheaka pia kufundisha watu kweli. Siku moja, Yesu na wanafunzi wake walikuwa walishachoka juu walikuwa wamehubiri sana. Walikuwa na lazima ya kupumuzika kidogo, lakini watu wengi wakawapata. Juu aliwasikilia huruma, Yesu akaanza kuwafundisha mambo mingi.” (Soma Marko 6:34.) Aliwafundisha hata kama alikuwa alishachoka. Juu ya nini? Alijitia pa nafasi ya wale watu. Aliona mateso yao​—walikuwa na lazima ya kupata tumaini—​na alipenda kuwasaidia. Leo, watu wengi pia wako mu hali ya vile. Sura yao isikudanganye. Wako sawa vile kondoo wenye walishapotea, wenye wako na lazima ya musaada, juu hawana muchungaji wa kuwaongoza. Paulo alisema kama watu wa vile wako sawa vile hawana Mungu wala tumaini. (Efe. 2:12) Wako mu “barabara yenye kuongoza kwenye uharibifu”! (Mt. 7:13) Wakati tunaona hali ya mubaya ya kiroho ya watu wa mu eneo yetu, upendo na huruma itatuchochea kuwasaidia. Na njia ya muzuri sana ya kuwasaidia ni kuanza kujifunza nao Biblia.

9. Kulingana na Wafilipi 2:13, namna gani Yehova anaweza kukusaidia?

Pengine uko unajizuia kuanzisha funzo ya Biblia, juu unawaza kama itakuomba wakati mingi ili kutayarisha mambo ya kujifunza na mwanafunzi. Kama ni vile, ambia Yehova namna uko unajisikia. Umuombe akupatie hamu ya kupata na kuongoza funzo ya Biblia. (Soma Wafilipi 2:13.) Mutume Yohana anatuhakikishia kama Yehova atajibia sala zenye zinalingana na mapenzi Yake. (1 Yo. 5:14, 15) Kwa hiyo, ukuwe hakika kama Yehova atakupatia hamu ya kushiriki mu kazi ya kufanya wanafunzi.

NAMNA YA KUSHINDA MAGUMU INGINE

10-11. Ni nini inaweza kutuzuia kuongoza funzo ya Biblia?

10 Tunakamata kwa uzito kazi yetu ya kufundisha hata kama kuko magumu mingi yenye inaweza kutuzuia kufanya mingi zaidi kuliko vile tungependa mu kazi ya kufanya wanafunzi. Tuzungumuzie magumu fulani na tuone namna tunaweza kuishinda.

11 Kujisikia kama hali yetu inatuwekea mipaka. Kwa mufano, wahubiri fulani walishazeeka ao wako na magumu ya afya. Ile njo magumu uko nayo? Kama ni vile, ona mambo fulani yenye tumejifunza mu kipindi ya Coronavirus. Tumevumbula kama tunaweza kuongoza mafunzo ya Biblia mu njia ya kielektroniki na kupata matokeo ya muzuri! Ndiyo, unaweza kuongoza funzo na uko tu kwako, mu nyumba. Lakini kuko faida ingine. Watu fulani wanaweza kupenda kujifunza Biblia, lakini hawana wakati saa yenye ndugu ao dada zetu walipanga kuhubiri. Lakini, wale watu wanaweza kuwa na wakati asubui sana, ao usiku sana. Je, unaweza kujipatanisha na wakati yao ili kuwapata? Yesu alifundishaka Nikodemo usiku, na ile njo ilikuwaka wakati ya muzuri sana kwa Nikodemo.​—Yoh. 3:1, 2.

12. Ni mambo gani inatuhakikishia kama tunaweza kuwa walimu wazuri?

12 Kuwaza kama hatuna uwezo wa kuongoza funzo ya Biblia. Pengine unaweza kuwaza kama inaomba kuwa na ujuzi sana ao ufundi kabisa sawa vile wa mwalimu mbele ya kuanza kuongoza funzo ya Biblia. Kama njo vile uko unawaza, ona mambo tatu yenye itakusaidia ukuwe hakika kama unaweza kuongoza funzo. Kwanza, Yehova anaona kama unastahili kufundisha wengine. (2 Ko. 3:5) Pili, Yesu, mwenye iko na “mamlaka yote mbinguni na duniani,” amekupatia ruhusa ya kufundisha. (Mt. 28:18) Na tatu, unaweza kutegemea musaada kutoka kwa wengine. Mambo yenye Yesu alikuwa anasema ilitegemea mambo yenye Baba yake alimufundishaka, na weye unaweza kufanya vile. (Yoh. 8:28; 12:49) Zaidi ya ile, unaweza kuomba mwangalizi wa kikundi yenu ya mahubiri, painia, ao muhubiri mwingine mwenye uzoefu akuonyeshe namna ya kuanzisha na kuongoza funzo ya Biblia. Njia moja ya kukusaidia, ni kusindikiza mumoja kati ya wale wahubiri ku funzo yake ya Biblia.

13. Juu ya nini tunapaswa kujikaza kuzoea njia za mupya za kujifunza na watu?

13 Kuwaza kama ni nguvu kuzoea njia za mupya ao vyombo vya mupya. Namna yetu ya kuongoza mafunzo ya Biblia ilishabadilika. Kitabu yetu ya funzo Furahia Maisha Milele! yenye tuko tunatumia sana, inaomba kujitayarisha muzuri na kujifunza na mwanafunzi tofauti kabisa na vile tulikuwaka tunafanya zamani. Tunasoma tu mafungu kidogo, lakini tunazungumuza sana na mwanafunzi. Na wakati tuko tunamufundisha, tunatumia sana video na vyombo vya kielektroniki, sawa vile JW Library®. Kama haujue muzuri namna ya kutumia vile vyombo, omba mutu fulani akuonyeshe namna ya kuvitumia. Mutu anajisikiaka muzuri kama iko anafanya kitu fulani mu njia yenye anazoea kukifanya. Haikuwake mwepesi kuzoea namna ya mupya ya kufanya mambo. Lakini kwa musaada wa Yehova na wa wengine, utaona kama ni mwepesi kuzoea na hata kufurahia zaidi kujifunza na watu. Kama vile ndugu moja painia alisemaka, hii njia mupya ya kujifunza na watu “inafurahisha mwalimu na mwanafunzi.”

14. Tunapaswa kukumbuka nini wakati tunahubiri mu eneo kwenye watu hawapendezwe, na namna gani 1 Wakorinto 3:6, 7 inatutia moyo?

14 Pengine tunaishi mu eneo kwenye haiko mwepesi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Watu wanaweza kuonekana kama hawapendezwe na ujumbe wetu ao hata kuupinga. Ni nini inaweza kutusaidia tukuwe hakika kama kuko watu fulani wanaweza kupendezwa? Tusisahau kama hali ya watu mu hii dunia inaweza kubadilika haraka. Wale wenye hawakukuwa wanapendezwa jana, wanaweza kupendezwa leo na kutambua kama wako na uhitaji wa kiroho. (Mt. 5:3) Watu wengine wenye zamani walikuwa wanakatala vichapo vyetu, kisha masiku fulani walifikia kukubali funzo ya Biblia. Tunajua pia kama Yehova njo Bwana wa mavuno. (Mt. 9:38) Anapenda siye tuendelee kupanda na kumwangia maji, lakini Yeye njo iko na daraka ya kukomalisha. (1 Ko. 3:6, 7) Na inatia moyo kukumbuka kama, hata ikiwa kwa sasa hatuna funzo ya Biblia, Yehova anatubariki hapana juu ya matokeo yenye tunapata, lakini juu ya bidii yenye tunaonyesha! *

PATA FURAHA KATIKA KAZI YA KUFANYA WANAFUNZI

Ona namna kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha inaweza kubadilisha maisha ya mutu (Ona fungu ya 15-17) *

15. Yehova anajisikiaka namna gani wakati mutu fulani anakubali kujifunza Biblia na anatumikisha mambo yenye iko anajifunza?

15 Yehova anafurahi wakati mutu fulani anakubali kweli yenye kuwa mu Biblia na anaitangazia wengine. (Mez. 23:15, 16) Yehova anafurahi sana kuona mambo yenye iko inafanyika leo! Kwa mufano, hata kama kulikuwa Coronavirus mu mwaka wa utumishi wa 2020, mafunzo ya Biblia 7 705 765 iliongozwa, na ile ilisaidia watu 241 994 watoe maisha yao kwa Yehova na kubatizwa. Hawa wanafunzi wapya nao wataongoza mafunzo ya Biblia na kufanya wanafunzi wengi zaidi. (Lu. 6:40) Hakuna shaka, wakati tunashiriki mu kazi ya kufanya wanafunzi tunamufurahisha Yehova.

16. Ni muradi gani wa muzuri unaweza kujiwekea?

16 Kufanya wanafunzi haiko kazi ya mwepesi, lakini kwa musaada wa Yehova tunaweza kufundisha hawa wanafunzi wapya wamupende Baba yetu wa mbinguni. Unaweza kujiwekea muradi wa kuanzisha na kuongoza hata funzo moja tu? Unaweza kushangala kuona matokeo utapata kama unatumia kila nafasi yenye inajitokeza ili kuomba watu waanze kujifunza Biblia na weye. Ukuwe hakika kama Yehova atabariki bidii yako.

17. Utapata nini kama unajikaza kuongoza funzo ya Biblia?

17 Ni pendeleo kabisa kuhubiri na kufundisha wengine Biblia! Kusema kweli, hii kazi inatuleteaka furaha ya mingi sana. Mutume Paulo, mwenye alisaidia Watesalonike wengi wafikie kuwa wanafunzi, alionyesha vile alijisikia kwa kusema hivi: “Ni nini tumaini letu ao shangwe ao taji la furaha kubwa mbele ya Bwana wetu Yesu wakati wa kuwapo kwake? Je, kwa kweli haiko ninyi? Hakika, ninyi ndio utukufu wetu na furaha yetu.” (1 Te. 2:19, 20; Mdo. 17:1-4) Wengi wanajisikia vile leo. Dada Stéphanie pamoja na bwana yake, amesaidia watu wengi wafikie kubatizwa. Dada Stéphanie anasema hivi: “Hakuna furaha yenye inapita ile ya kusaidia watu watoe maisha yao kwa Yehova.”

WIMBO 57 Tuhubirie Watu Wote

^ fu. 5 Yehova hakutupatia tu pendeleo ya kuhubiria watu lakini pia ya kuwafundisha kushika mambo yote yenye Yesu aliamuru. Ni nini inatuchocheaka kufundisha wengine? Ni magumu gani tunapataka mu kazi ya kuhubiri na ya kufanya wanafunzi? Na nini njo inaweza kutusaidia kupambana na ile magumu? Hii habari itajibia ile maulizo.

^ fu. 14 Ili kupata maelezo zaidi kuhusu daraka yetu katika kazi ya kufanya wanafunzi, ona habari “Namna Kutaniko Linaweza Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa,” yenye ilitolewa mu Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 3, 2021.

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Ona namna funzo ya Biblia inaweza kubadilisha maisha ya mutu: Ku mwanzo mwanaume moja anaonekana sawa vile hamujue hata Mungu na kama maisha yake haina kusudi. Kisha anakutana na Mashahidi wa Yehova wenye wako mu mahubiri, na anakubali funzo. Mambo anajifunza inamusaidia atoe maisha yake kwa Yehova na abatizwe. Kisha wakati, na yeye anaanza kufanya wanafunzi. Ku mwisho, wote wanafurahia maisha mu Paradiso.