Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna Tunavua na Kuepuka Kabisa Utu wa Zamani

Namna Tunavua na Kuepuka Kabisa Utu wa Zamani

‘Muvue utu wa zamani pamoja na mazoea yake.’​KOL. 3:9.

NYIMBO: 83, 129

1, 2. Watu wamesema nini juu ya Mashahidi wa Yehova?

WATU wengi wamejionea sifa za pekee zenye watu wa Yehova wanaonyesha. Kwa mufano, juu ya ndugu na dada zetu katika Ujerumani wakati wa utawala wa Wanazi, mwandishi Anton Gill, aliandika hivi: “Wanazi walichukia sana Mashahidi wa Yehova. . . . Kufikia mwaka 1939, Mashahidi 6 000 walikuwa katika [kambi za mateso].” Mwandishi huyo aliongezea kuwa hata kama Mashahidi walipata mateso makali, walionyesha kuwa ni “wenye kutumainika na wenye kutulia,” walionyesha pia “ushikamanifu na umoja.”

2 Hivi karibuni, watu katika Afrika ya Kusini walijionea sifa kama hizo zenye kupendeza kati ya watu wa Mungu. Wakati fulani, Mashahidi wenye kuwa na rangi tofauti ya ngozi katika inchi hiyo hawangeweza kukusanyika pamoja kwa uhuru. Hata hivyo, Siku ya Yenga, tarehe 18 Mwezi wa 12, 2011, ilipendeza kuona ndugu na dada zaidi ya 78 000 wa rangi tofauti ya ngozi wa Afrika ya Kusini na wengine kutoka katika inchi zingine za karibu-karibu wanakusanyika katika uwanja mukubwa wa Johannesburg ili kufurahia programu moja ya kiroho. Mutu mumoja kati ya watu wenye kusimamia uwanja huo, alisema hivi juu ya watu wenye walikusanyika: “Hawa ndio watu wenye tabia ya muzuri zaidi wenye nimekwisha kuona katika uwanja huu. Wote wanavaa muzuri. Na mumesafisha muzuri sana uwanja huu. Lakini, zaidi ya yote, hamuna ubaguzi kabisa.”

3. Nini inafanya familia yetu ya ndugu na dada ikuwe ya pekee?

3 Mambo hayo yenye watu wenye hawako Mashahidi wanasema yanaonyesha kuwa familia yetu ya ndugu na dada wa ulimwenguni pote ni ya pekee kabisa. (1 Pet. 5:9) Lakini, ni nini inafanya tukuwe tofauti na matengenezo mengine yote? Kwa musaada wa Neno la Mungu na roho yake takatifu, tunajikaza sana ‘kuvua utu wa zamani.’ Kisha kuvua utu huo, ‘tunavaa utu mupya.’​—Kol. 3:9, 10.

4. Tutazungumuzia nini katika habari hii, na sababu gani?

4 Tunapaswa kuvua utu wa zamani, lakini pia tunapaswa kuuepuka kabisa. Katika habari hii, tutazungumuzia namna gani tunaweza kuvua utu wa zamani, sababu gani ni jambo la haraka kufanya hivyo, na sababu gani inawezekana kufanya mabadiliko hata kama tumezoea sana kufanya mambo ya mubaya. Pia tutazungumuzia mambo yenye wale wenye wamefanya miaka mingi katika kweli wanaweza kufanya ili waepuke kabisa utu wa zamani. Sababu gani tuko na lazima ya vikumbusho hivyo? Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu fulani wenye walikuwa wanamutumikia Yehova wameacha kuwa waangalifu na wamerudilia matendo yao ya zamani. Ndio sababu, sisi wote tunapaswa kukamata kwa uzito onyo hili: ‘Kwa hiyo yeye anayefikiri kuwa amesimama na ajihazari [akuwe muangalifu] kwamba asianguke.’​—1 Kor. 10:12.

‘MUUE’ TAMAA YOYOTE “KWA HABARI YA UASHERATI”

5. (a) Sababu gani ni jambo la haraka kuvua utu wa zamani? Toa mufano. (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Andiko la Wakolosai 3:5-9, linataja matendo gani yenye kuonyesha utu wa zamani?

5 Utafanya nini ikiwa nguo yako inachafuka, na pengine hata inaanza kunuka mubaya? Utavua nguo hiyo chafu haraka kabisa. Vilevile, tunapaswa kutenda haraka ili kutii amri ya kuachana na tabia zenye Mungu anachukia. Tunapenda kutii agizo hili lenye kuwa wazi lenye Paulo alipatia Wakristo wa siku zake: ‘Muondolee mbali mambo haya yote kutoka kwenu.’ Kati ya matendo ya mubaya yenye Paulo alitaja, tuzungumuzie basi matendo mbili, ni kusema, uasherati na uchafu.​—Soma Wakolosai 3:5-9.

6, 7. (a) Namna gani maneno ya Paulo yanaonyesha kuwa inaomba kujikaza sana ili kuvua utu wa zamani? (b) Sakura alikuwa na maisha ya namna gani, na ni nini ilimupatia nguvu ya kuachana na maisha hayo?

6 Uasherati. Neno lenye lilitumiwa katika Biblia ili kutafsiri neno “uasherati” linatia ndani ngono kati ya watu wawili wenye hawajaoana kulingana na sheria na wanaume kulala na wanaume na wanawake kulala na wanawake. Paulo aliambia Wakristo wenzake ‘waue viungo vya mwili’ wao, ni kusema, waondoe kabisa tamaa yoyote yenye kuhusu “uasherati.” Maneno ya Paulo yanaonyesha wazi kama tunapaswa kujikaza sana ili kuachana kabisa na tamaa za mubaya kama hizo. Hata hivyo, inawezekana kushinda tamaa za mubaya.

7 Fikiria mambo yenye yalimufikia Sakura * wa Japani. Wakati alikuwa anakomaa, alikuwa anajisikia kuwa peke yake na kuwa mutu wa bure. Wakati alikuwa na miaka 15, alianza kufanya uasherati na watu mbalimbali ili kumaliza hali yake ya kujisikia kuwa peke yake. Anasema hivi kwa huzuni: “Matokeo ni kwamba nilitosha mimba mara tatu.” Anaeleza hivi: “Mwanzoni, nilijisikia kuwa salama wakati nilikuwa ninafanya uasherati, kwa sababu nilifikiri kuwa watu walikuwa na lazima yangu na walinipenda. Lakini, kadiri niliendelea kufanya uasherati, nilijisikia zaidi kuwa siko salama.” Sakura aliendelea na maisha hayo mupaka wakati alikuwa na miaka 23. Kisha akaanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Sakura alipenda mambo yenye alikuwa anajifunza, na Yehova amemusaidia kuacha kusumbuliwa na zamiri na kujiona kuwa hafae na kuepuka kabisa matendo ya uasherati. Sasa Sakura ni painia wa kawaida na hajisikie tena kuwa peke yake. Lakini, anasema hivi: “Niko na furaha kabisa kwa sababu Yehova ananionyesha upendo wake kila siku.”

KUACHANA NA MATENDO MACHAFU

8. Ni mambo gani yenye yanaweza kufanya Mungu atuone kuwa watu wachafu?

8 Uchafu. Neno lenye lilitumiwa katika Biblia ili kutafsiri neno “uchafu” ni neno lenye kuzungumuzia mambo mengi zaidi ya zambi za uasherati. Linaweza kuzungumuzia tabia hatari ya kuvuta tumbako ao kusema maneno machafu ili kufanya mizaha. (2 Kor. 7:1; Efe. 5:3, 4) Linatia ndani pia matendo machafu yenye mutu anafanya wakati iko peke yake, kama vile kusoma vitabu vyenye kuamusha tamaa ya ngono ao kuangalia pornografia; matendo hayo yanaweza kuchochea mutu akuwe na tabia chafu ya kugusa-gusa viungo vyake vya uzazi ili kutimiza tamaa ya ngono.​—Kol. 3:5. *

9. Mutu mwenye kukomalisha “hamu ya ngono” anaweza kupatwa na matokeo gani?

9 Watu wenye wanazoea kuangalia pornografia, wanakomalisha “hamu ya ngono” yenye inaweza kuwafanya wakuwe mutumwa wa ngono. Uchunguzi unaonyesha kuwa watu wenye walikubali kuwa hawawezi kuzuia tamaa yao ya kuangalia pornografia wanaonyesha alama kama za watu wenye kuwa watumwa wa pombe ao wa dawa za kulewesha. Ndiyo sababu tabia ya kuangalia pornografia iko na matokeo ya mubaya, kama vile mutu kusumbuliwa sana na zamiri, kushindwa kutumika muzuri kwenye kazi, kukosa furaha katika maisha ya familia, kuvunjika kwa ndoa, na kujiua. Wakati alieneza mwaka mumoja kisha kutoka katika utumwa wa kuangalia pornografia, mwanaume mumoja aliandika hivi: “Nimekuwa tena na hali ya kujiheshimia yenye nilikuwa nimepoteza.”

10. Ni nini ilimusaidia Ribeiro atoke katika utumwa wa pornografia?

10 Watu wengi wanapaswa kuendelea kupigana sana ili kuepuka pornografia. Lakini, mambo yenye yalimufikia Ribeiro wa Brazili, yanaonyesha kuwa inawezekana kushinda pigano hilo. Ribeiro aliondoka nyumbani kwao wakati alikuwa kijana, na kisha akaanza kutumika nafasi moja ya kushugulikia karatasi zenye zimekwisha kutumiwa ili kutengeneza vitu vingine; ilikuwa mwepesi kwake kuona mambo ya pornografia nafasi hiyo. Anaeleza hivi: “Pole kwa pole, nilifikia kuwa mutumwa. Hali iliharibika sana mupaka singeweza tena kungoja mwanamuke mwenye tulikuwa tunaishi naye aondoke ili niangalie video za pornografia.” Kisha, siku moja wakati alikuwa kwenye kazi, Ribeiro aliona furushi ya vitabu vyenye walipaswa kushugulikia, na akaona kitabu chenye kichwa Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Alichukua kitabu hicho na kukisoma. Mambo yenye alijifunza yalimuchochea ajifunze Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, lakini ilimuomba muda murefu ili aachane na tabia yake ya mubaya. Ni nini ilifikia kumusaidia? Anasema hivi: “Kupitia sala, kujifunza Biblia, na kutafakari juu ya mambo yenye nilikuwa ninajifunza, nilipendezwa zaidi na sifa za Mungu mupaka upendo wangu kwa Yehova ukakuwa wenye nguvu zaidi kuliko tamaa yangu ya kuangalia pornografia.” Kwa musaada wa nguvu ya Neno la Mungu na roho yake takatifu, Ribeiro alivua utu wake wa zamani, akabatizwa, na sasa yeye ni muzee wa kutaniko.

11. Mutu anapaswa kufanya nini ili kujiepusha na pornografia?

11 Ona kwamba, zaidi ya kujifunza Biblia, Ribeiro alipaswa kufanya mengi ili apate ushindi katika pigano lake. Alipaswa kuruhusu ujumbe wa Biblia uguse moyo wake pole kwa pole. Kupitia sala, na kutafakari, upendo wake kwa Mungu ukakuwa wenye nguvu zaidi kuliko tamaa yake ya kuangalia pornografia. Kutia nguvu upendo wetu kwa Yehova na kuchukia mambo mabaya ndiyo njia ya muzuri zaidi ya kujiepusha na pornografia.​—Soma Zaburi 97:10.

EPUKA KABISA HASIRA, MATUKANO, NA UWONGO

12. Ni nini ilimusaidia Stephen aepuke kabisa hasira na matukano?

12 Watu wenye kukasirika haraka, mara nyingi wanaonyesha hasira yao kwa kutumia matukano ao matusi. Kwa kweli, tabia kama hiyo haiwezi kufanya familia ikuwe na furaha. Stephen, baba mumoja wa Australia, anaeleza hivi: “Nilikuwa ninazoea kutukana watu na mara nyingi niliwaka hasira kwa sababu ya mambo madogo-madogo. Mimi na bibi yangu tulitengana mara tatu na tulikuwa tunafanya mipango ya kuvunja ndoa yetu.” Kisha, Mashahidi wa Yehova wakaanza kujifunza Biblia na Stephen na bibi yake. Matokeo yalikuwa gani wakati Stephen alianza kutumikisha mashauri ya Biblia? Anasema hivi: “Maisha yetu ya familia yakakuwa ya muzuri zaidi. Kwa musaada wa Yehova, sasa mimi ni mwenye amani na mutulivu kabisa, lakini zamani nilikuwa kama bombe ya hasira yenye ilikuwa tayari kulipuka ikiwa inachokozwa tu kidogo.” Leo, Stephen ni mutumishi wa huduma, na bibi yake amefanya miaka fulani katika kazi ya upainia. Wazee wa kutaniko la Stephen wanasema hivi: “Stephen ni ndugu mutulivu, mwenye kutumika kwa bidii, na munyenyekevu.” Hakuna siku wamemuona akiwa mwenye hasira. Stephen anaona kuwa alifanya mabadiliko hayo kwa nguvu zake mwenyewe? Anasema hivi: “Singepata baraka hizo za muzuri katika maisha yangu ikiwa ningekataa musaada wa Yehova ili kubadilisha kabisa utu wangu.”

13. Sababu gani hasira ni hatari sana, na Biblia inatoa onyo gani?

13 Biblia inatuonya tuepuke hasira, matukano, na malalamiko. (Efe. 4:31) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, mara nyingi tabia kama hizo zinatokeza jeuri. Watu wa ulimwengu wanaweza kuona kuwa ni jambo la kawaida kuwa na hasira, lakini tabia hiyo inamukosea Muumbaji wetu heshima. Wengi walipaswa kuacha tabia hizo za mubaya ili waweze kuvaa utu mupya.​—Soma Zaburi 37:8-11.

14. Inawezekana mutu mwenye hasira akuwe mutu mupole?

14 Fikiri mufano wa Hans, mwenye kuwa muzee katika kutaniko moja katika Austria (Autriche). Muratibu wa baraza la wazee wa kutaniko la Hans alisema hivi: “Yeye ni mumoja kati ya ndugu wapole zaidi.” Lakini zamani Hans hakukuwa mupole. Wakati alikuwa kijana, alianza kunywa sana pombe, na kwa hiyo akakuwa mukali sana. Siku moja, kwa sababu ya ulevi, hasira yake iliwaka na akaua rafiki yake mwanamuke; kwa hiyo, alihukumiwa kufungwa miaka 20 katika gereza. Mwanzoni, maisha katika gereza hayakubadilisha tabia ya ukali ya Hans. Kisha wakati fulani, mama yake alifanya mipango ili muzee mumoja aende kuzungumuza naye katika gereza, na Hans akaanza kujifunza Biblia. Anasema hivi: “Ilikuwa vigumu kwangu kuvua utu wangu wa zamani. Maandiko ya Biblia yenye yalinitia moyo ni Isaya 55:7, lenye kusema hivi: ‘Mutu mwovu aiache njia yake,’ na 1 Wakorintho 6:11, lenye kusema hivi juu ya wale wenye walikuwa wameachana na matendo ya zambi: ‘Na bado wengine wenu mulikuwa hivyo.’ Kwa miaka mingi, Yehova alinivumilia na kunisaidia kupitia roho yake takatifu ili nivae utu mupya.” Kisha kufanya miaka 17 na nusu katika gereza, Hans alifunguliwa na tayari alikuwa Mukristo mwenye kubatizwa. Anasema hivi: “Niko mwenye shukrani kwa huruma na musamaha mukubwa wa Yehova.”

15. Watu wanazoea kufanya nini, lakini Biblia inasema nini juu ya jambo hilo?

15 Zaidi ya matukano, tabia ya kusema uwongo ni sehemu pia ya utu wa zamani. Kwa mufano, watu wanazoea kudanganya juu ya kodi yenye wanapaswa kulipa ao kudanganya ili kuepuka matokeo ya zambi zao. Lakini, Yehova ni “Mungu wa ukweli.” (Zab. 31:5) Kwa hiyo, anaomba ‘kila mumoja’ wa watumishi wake ‘aseme kweli’ pamoja na jirani yake na asiseme “uwongo.” (Efe. 4:25; Kol. 3:9) Kwa hiyo, tunapaswa kusema kweli hata kama hilo linaweza kutufanya tusikie haya ao ni vigumu kufanya hivyo.​—Met. 6:16-19.

NAMNA WALIPATA USHINDI

16. Tunapaswa kufanya nini ili tuweze kuvua utu wa zamani?

16 Mutu hawezi kuvua utu wa zamani kwa nguvu zake mwenyewe. Watu wenye kuzungumuziwa katika habari hii, ni kusema, Sakura, Ribeiro, Stephen, na Hans, walipaswa kujikaza sana ili kuachana kabisa na matendo yao ya mubaya. Walipata ushindi kwa kuacha nguvu ya Neno la Mungu na roho yake takatifu viguse akili na mioyo yao. (Lu. 11:13; Ebr. 4:12) Ili tufaidike na nguvu hiyo, tunapaswa kusoma Biblia kila siku, kutafakari juu ya mambo tunasoma, na kusali kila mara ili Mungu atupatie hekima na nguvu ya kutumikisha mashauri ya Biblia. (Yos. 1:8; Zab. 119:97; 1 Tes. 5:17) Tunafaidika pia na Neno la Mungu na roho yake takatifu wakati tunatayarisha na kuhuzuria mikutano. (Ebr. 10:24, 25) Pia, tunapaswa kutumia muzuri njia mbalimbali zenye tengenezo la Yehova linatumia leo ili kutolea watu wa Mungu chakula cha kiroho katika dunia yote.​—Lu. 12:42.

Tunapaswa kufanya nini ili tuweze kuvua utu wa zamani? (Picha hizi zinapatana na fungu la 16)

17. Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Tumezungumuzia tabia fulani za mubaya zenye Wakristo wanapaswa kuachana nazo na kuepuka kabisa. Lakini inaomba tu kufanya hivyo ili tukubaliwe na Mungu? Hapana. Tunapaswa pia kuvaa utu mupya. Katika habari yenye kufuata, tutazungumuzia sifa mbalimbali za utu mupya zenye tunapaswa kuonyesha wakati wote.