Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 31

“Hatuache”!

“Hatuache”!

“Kwa hiyo, hatuache.”​—2 KO. 4:16.

WIMBO 128 Kuvumilia Mpaka Mwisho

KIFUPI CHA HABARI *

1. Wakristo wanapaswa kufanya nini ili wakimbie mbio ya uzima mupaka mwisho?

WAKRISTO wako katika mbio ya uzima. Ikuwe tumeanza tu kukimbia ao tumekimbia kwa miaka mingi, tunapaswa kuendelea kukimbia mupaka tuvuke mustari wa mwisho. Shauri lenye mutume Paulo alitolea Wakristo wa Filipi linaweza kututia moyo ili tukimbie mupaka mwisho. Wakristo fulani wa kutaniko la Filipi walikuwa wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi wakati walipata barua ya Paulo. Walikuwa wanakimbia muzuri, lakini Paulo aliwakumbusha kama walipaswa kuendelea kukimbia kwa uvumilivu. Alipenda waige mufano wenye alionyesha wa “kujikaza kuelekea muradi.”​—Flp. 3:14.

2. Juu ya nini shauri lenye Paulo alipatia Wafilipi lilitolewa kwa wakati wenye kufaa?

2 Paulo alitolea Wafilipi shauri hilo kwa wakati wenye kufaa. Watu wa muji wa Filipi walipinga ndugu na dada wa kutaniko la Filipi tangu tu wakati lilianza. Katika mwaka wa 50 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Paulo na Sila walitii mualiko wa Mungu wa ‘kuvuka kuingia Makedonia.’ Kwa hiyo, walienda Filipi ili kuhubiri habari njema. (Mdo. 16:9) Kule, walikuta mwanamuke mwenye kuitwa Lidia, mwenye “alikuwa anasikiliza, na Yehova akafungua wazi moyo wake” ili akubali habari njema. (Mdo. 16:14) Bila kukawia, alibatizwa pamoja na watu wa nyumba yake. Lakini, Ibilisi hakulala usingizi. Wanaume wa muji wakaleta Paulo na Sila mbele ya waamuzi wa raia na kuwashitaki kwa uongo kama walikuwa wanaleta muvurugo. Kwa hiyo, Paulo na Sila walipigwa, walitiwa katika gereza, na kisha waliwaomba watoke katika muji. (Mdo. 16:16-40) Je, waliacha? Hapana! Na ndugu na dada wa kutaniko hilo la mupya walifanya nini? Jambo la muzuri ni kwamba wao pia walivumilia! Kwa kweli, mufano muzuri wenye Paulo na Sila waliwaonyesha uliwatia moyo sana.

3. Paulo alijua nini, na tutazungumuzia maulizo gani?

3 Paulo aliazimia kama hataacha kumutumikia Yehova. (2 Ko. 4:16) Lakini, alijua kama ili afike ku mwisho wa mbio yake, alipaswa kukaza akili juu ya muradi wake. Mufano wa Paulo unaweza kutufundisha nini? Ni mifano gani ya Wakristo waaminifu wa leo yenye kuonyesha kama tunaweza kuvumilia hata kama tuko na magumu? Na namna gani tumaini letu juu ya wakati wenye kuja linaweza kutusaidia tuazimie kabisa kukimbia mbio ya uzima mupaka mwisho?

NAMNA MUFANO WA PAULO UNAWEZA KUTUSAIDIA

4. Paulo alifanya nini ili aendelee kufanya mambo mingi katika kazi ya Yehova hata kama alikuwa mufungwa?

4 Fikiria namna Paulo alijikaza wakati aliandikia Wafilipi. Alikuwa anafungwa mu nyumba kule Roma. Hakuruhusiwa kuenda kuhubiri. Lakini aliendelea kuhubiria watu wenye walikuwa wanamutembelea na kuandikia barua makutaniko yenye ilikuwa mbali. Leo vilevile, Wakristo wengi wenye hawawezi kutoka mu nyumba zao wanatumia kila nafasi yenye wanapata ili kuhubiria habari njema wale wenye wanakuja kuwatembelea. Pia wanaandika barua zenye kutia moyo na kuzitumia watu wenye haiwezekane kuonana nao.

5. Kulingana na maneno ya Paulo mu Wafilipi 3:12-14, ni nini ilimusaidia Paulo akaze akili juu ya muradi wake?

5 Paulo hakuacha mambo yenye alitimiza zamani ao makosa yake ya zamani vimukengeushe. Kwa kweli, alisema kama ilikuwa lazima ‘kusahau mambo ya nyuma’ ili ‘kujinyoosha kuelekea mambo yenye kuwa mbele,’ ni kusema, kufikia mwisho wa mbio yake. (Soma Wafilipi 3:12-14.) Paulo alifanya nini ili asikengeuke? Jambo la kwanza, hata kama Paulo alitimiza mambo ya ajabu katika dini ya Wayahudi, aliona ile mambo kuwa “takataka nyingi.” (Flp. 3:3-8) Jambo la pili, hata kama zamiri yake ilikuwa inamusumbua kwa sababu alitesa Wakristo zamani, hakuacha jambo hilo limuzuie kumutumikia Yehova. Na jambo la tatu, hakuona kama mambo yote ya muzuri yenye alikuwa amemufanyia Yehova ilikuwa inatosha na kama hakupaswa tena kufanya zaidi. Paulo alipata matokeo ya muzuri katika kazi ya kuhubiri hata kama alifungwa, alipigwa fimbo, alipigwa majiwe, alivunjikiwa mashua, na kukosa chakula na nguo. (2 Ko. 11:23-27) Lakini, hata kama alikuwa ametimiza mambo mingi zamani na kuteseka, Paulo alijua kama alipaswa kujikaza, ni kusema, kuendelea kumutumikia Yehova. Na sisi tunapaswa kufanya vile.

6. Ni mambo gani fulani ya nyuma yenye tunapaswa kusahau?

6 Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Paulo wa “kusahau mambo ya nyuma”? Wamoja kati yetu wanapaswa kujikaza ili zamiri yao isiendelee kuwasumbua juu ya makosa yenye walifanya zamani. Kama uko katika hali hiyo, unaweza kufanya mupango wa kujifunza habari zenye kuzungumuzia bei ya ukombozi ya Kristo. Kama tunajifunza, tunafikiri sana, na kusali juu ya habari hiyo yenye kutia moyo, hilo linaweza kutusaidia sana ili zamiri yetu isiendelee kutusumbua juu ya zambi zenye Yehova amekwisha kusamehe. Tunaweza hata kuacha kujilaumu juu ya zambi zenye Yehova amekwisha kusamehe. Fikiria jambo lingine lenye mufano wa mutume Paulo unaweza kutufundisha. Pengine wamoja kati yetu waliacha kazi ya mushahara muzuri ili watie faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza. Kama ni vile, je, tunaweza kusahau mambo ya nyuma kwa kuacha kutamani vitu vya kimwili vyenye pengine tungepataka? (Hes. 11:4-6; Muh. 7:10) “Mambo ya nyuma” inaweza kutia ndani hata mambo yenye tulitimiza katika kazi ya Yehova ao majaribu yenye tulivumilia zamani. Kwa kweli, wakati tunafikiria namna Yehova ametubariki na kututegemeza kwa miaka mingi, hilo linaweza kutusaidia tumukaribie Baba yetu zaidi. Lakini, hatupaswe kuwaza kama mambo yenye tumefanya kwa ajili ya Yehova inatosha.​—1 Ko. 15:58.

Katika mbio yetu ya uzima, tunapaswa kuepuka mambo ya kukengeusha na kukaza akili yetu juu ya muradi wetu (Picha hii inapatana na fungu la 7)

7. Kulingana na 1 Wakorinto 9:24-27, tunapaswa kufanya nini ili tupate ushindi katika mbio yetu ya uzima? Leta mufano.

7 Paulo alielewa muzuri maneno ya Yesu yenye kusema hivi: “Mujikaze sana.” (Lu. 13:23, 24) Paulo alijua kama, ili kumuiga Kristo, alipaswa kujikaza sana mupaka mwisho. Njo maana alilinganisha Mukristo na mutu mwenye kukimbia katika mashindano ya mbio. (Soma 1 Wakorinto 9:24-27.) Mukimbiaji mwenye iko katika mashindano ya mbio anapaswa kukaza akili juu ya mustari wa mwisho na anaepuka mambo ya kukengeusha. Kwa mufano, mukimbiaji anaweza kukimbia mu barabara yenye kuwa na maduka na mambo ingine yenye inaweza kumukengeusha. Unawaza kama mukimbiaji anaweza kusimama na kuanza kuangalia kupitia madirisha vitu vyenye kuwa mu duka? Hawezi kufanya vile kama anapenda kupata ushindi! Katika mbio ya uzima, sisi pia tunapaswa kuepuka mambo ya kukengeusha. Kama tunaendelea kukaza akili juu ya muradi wetu na kujikaza sana kama vile Paulo alifanya, tutapata zawadi!

NAMNA YA KUENDELEA KUMUTUMIKIA YEHOVA HATA KAMA TUKO NA MAGUMU

8. Ni magumu gani tatu yenye tutazungumuzia?

8 Tuzungumuzie sasa magumu tatu yenye inaweza kutuvunja moyo. Jambo la kwanza, wakati mambo yenye tunangojea inakawia kufika. Jambo la pili, wakati tunakuwa wazaifu kwa sababu ya uzee. Jambo la tatu, wakati tuko na majaribu yenye kuendelea kwa wakati murefu. Mifano ya watu wenye walivumilia ile magumu inaweza kutufundisha mambo mingi.​—Flp. 3:17.

9. Kama mambo yenye tunangojea inakawia kufika, hilo linaweza kuwa na matokeo gani juu yetu?

9 Wakati mambo yenye tunangojea inakawia kufika. Kwa kawaida, tunangojea sana mambo ya muzuri yenye Yehova ametuahidi. Kwa kweli, wakati Habakuki, nabii wa Yehova, alisema kama alipenda sana Yehova amalize mambo ya mubaya katika Yuda, Yehova alimuambia ‘aendelee kungojea.’ (Hab. 2:3) Lakini, wakati mambo yenye tunangojea inaonekana kuwa inakawia, hilo linaweza kufanya tupunguze bidii yetu. Tunaweza hata kuvunjika moyo. (Mez. 13:12) Jambo hilo lilitokea ku mwanzo wa miaka ya 1900. Wakati huo, Wakristo wengi watiwa-mafuta walitumaini kama wataenda mbinguni mu mwaka wa 1914. Wakati jambo hilo halikufanyika, ndugu na dada waaminifu walitenda namna gani?

Mambo yenye Royal Spatz na bibi yake Pearl walitumaini haikutimia mu mwaka wa 1914, lakini waliendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi (Picha hii inapatana na fungu la 10)

10. Bwana mumoja na bibi yake walitenda namna gani wakati mambo yenye walingojea ilikawia kufika?

10 Fikiria mufano wa Wakristo wawili waaminifu wenye walishinda ile magumu. Ndugu Royal Spatz alibatizwa mu mwaka wa 1908 wakati alikuwa na miaka 20. Alikuwa hakika kabisa kama alikuwa karibu kuenda mbinguni. Njo maana, wakati alichumbia dada mumoja mwenye kuitwa Pearl mu mwaka wa 1911, alimuambia hivi: “Unajua jambo lenye litafanyika mu mwaka wa 1914. Kama tutaoana, itakuwa muzuri zaidi tufanye vile haraka!” Je, bwana huyo na bibi yake waliacha mbio yao ya uzima juu hawakuenda mbinguni mu mwaka wa 1914? Hapana, kwa sababu walikaza akili yao juu ya kufanya mapenzi ya Mungu kwa uaminifu, haiko juu ya kuenda mbinguni. Waliazimia kukimbia kwa uvumilivu mbio yao ya uzima. Royal na Pearl waliendelea kuwa wenye bidii na waaminifu mupaka mwisho wa maisha yao ku dunia miaka mingi kisha pale. Kwa kweli, unangojea kwa hamu Yehova atakase jina lake na kutetea mamlaka yake makubwa zaidi na kutimiza ahadi zake zote. Ukuwe hakika kama ile mambo itatimia kwa wakati wenye Yehova ameweka. Mupaka wakati huo ufike, tuendelee basi kumutumikia Mungu wetu, tusivunjike moyo ao kupunguza bidii yetu hata kidogo wakati mambo yenye tunangojea inakawia kufika.

Hata wakati wa uzee, Arthur Secord alipenda sana kumutumikia Yehova kwa uwezo wake wote (Picha hii inapatana na fungu la 11)

11-12. Juu ya nini tunaweza kuendelea kumutumikia Yehova hata kama hatuna tena nguvu kama zamani? Leta mufano.

11 Wakati tunakuwa wazaifu kwa sababu ya uzee. Mukimbiaji iko na lazima ya nguvu za kimwili ili akimbie muzuri. Lakini haiko lazima sisi tukuwe na nguvu za kimwili ili tuendelee katika mbio yetu ya Kikristo. Kwa kweli, ndugu na dada wenye nguvu yao ya kimwili imepunguka wangali wanapenda sana kumutumikia Yehova kwa nguvu yao yote. (2 Ko. 4:16) Kwa mufano, Ndugu Arthur Secord * alikuwa na miaka 88 na alikuwa muzaifu kisha kutumikia ku Beteli kwa miaka 55. Munganga mumoja alikaribia kitanda chake ili kumutimizia mahitaji yake. Alimuangalia na akasema hivi kwa upendo: “Ndugu Secord, umefanya mambo mingi mu kazi ya Yehova.” Lakini Arthur, hakukuwa anakaza akili juu ya mambo yenye alifanya zamani. Alimuangalia, akaonyesha sura ya kicheko, na akasema hivi: “Aksanti. Lakini haiko mambo yenye tumefanya njo ya maana. Ni mambo yenye tunafanya leo na kuendelea.”

12 Pengine umemutumikia Yehova kwa miaka mingi na sasa unaona kama afya yako inakuzuia kufanya mambo mingi kama zamani. Kama ni vile, usivunjike moyo. Ukuwe hakika kama Yehova anafurahia kazi yenye ulifanya kwa uaminifu zamani. (Ebr. 6:10) Na ukumbuke kama haiko mambo mingi yenye tunafanya katika utumishi wa Yehova njo inaonyesha kama tunamupenda kwa nafsi yote. Lakini, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova kwa nafsi yetu yote wakati tunaendelea kuwa na furaha na tumaini na wakati tunafanya nguvu yetu yote katika utumishi wake. (Kol. 3:23) Yehova anaelewa mipaka yetu na hatuombe tufanye mambo mingi kuliko ile yenye tunaweza kufanya.​—Mk. 12:43, 44.

Anatoly Melnik na bibi yake Lidiya walivumilia kwa uaminifu hata kama walipata majaribu mingi (Picha hii inapatana na fungu la 13)

13. Namna gani mufano wa Anatoly na Lidiya unatutia moyo tuendelee kumutumikia Yehova hata kama tuko na majaribu mingi?

13 Wakati tuko na majaribu yenye kuendelea kwa wakati murefu. Watumishi fulani wa Yehova wamevumilia majaribu na mateso kwa miaka mingi. Kwa mufano, Anatoly Melnik * alikuwa tu na miaka 12 wakati baba yake alikamatwa, alifungwa, na kupelekwa Siberia umbali wa kilometre zaidi ya 7 000 na familia yake yenye ilikuwa inaishi katika inchi ya Moldova. Kisha mwaka moja, Anatoly, mama yake, na wazazi wa mama yake, nao pia walipelekwa Siberia. Kisha wakati fulani, waliweza kuhuzuria mikutano katika kijiji kingine, lakini walipaswa kutembea kilometre 30 katika teluji na kuvumilia baridi kali. Kisha, Ndugu Melnik alifanya miaka tatu katika gereza, mbali na bibi yake, Lidiya, na mutoto wao mwanamuke wa mwaka moja. Hata kama Anatoly na familia yake walipata majaribu kwa miaka mingi, waliendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu. Leo Anatoly iko na miaka 82 na anatumikia katika Halmashauri ya Tawi la Asia ya Kati. Kama vile Anatoly na Lidiya, tuendelee kufanya nguvu yetu yote katika kazi ya Yehova, na kuendelea kuvumilia kama vile tulifanya zamani.​—Gal. 6:9.

TUENDELEE KUKAZA AKILI JUU YA TUMAINI LETU LA WAKATI WENYE KUJA

14. Paulo alielewa kama anapaswa kufanya nini ili afikie muradi wake?

14 Paulo alikuwa hakika kama angefikia mwisho wa mbio yake na kufikia muradi wake. Kwa sababu alikuwa Mukristo mutiwa-mafuta, alikuwa na tumaini la kupata “zawadi ya mwito wa Mungu wa kuenda juu.” Lakini, ili afikie muradi wake, alielewa kama alipaswa kuendelea “kujikaza.” (Flp. 3:14) Paulo alitumia mufano wenye kupendeza ili kusaidia Wafilipi wakaze akili juu ya muradi wao.

15. Namna gani Paulo alitumia mufano wa uraia ili kutia moyo Wakristo Wafilipi waendelee “kujikaza”?

15 Paulo alikumbusha Wafilipi kama walikuwa raia wa mbinguni. (Flp. 3:20) Juu ya nini ilikuwa muzuri wakumbuke vile? Katika siku hizo, watu walipenda kabisa kuwa raia wa Roma kwa sababu kuwa raia wa Roma kuliwaletea faida za mingi. * Lakini, Wakristo watiwa-mafuta walikuwa na uraia wa muzuri zaidi, wenye ungewaletea faida kubwa zaidi. Kuwa raia wa serikali ya mbinguni kulikuwa na faida kubwa kuliko kuwa raia wa Roma! Njo maana, Paulo alitia moyo Wafilipi “wajiendeshe kama wanainchi [ao, raia] kwa njia yenye inastahili habari njema juu ya Kristo.” (Flp. 1:27, maelezo ya chini) Leo, Wakristo watiwa-mafuta wanatuonyesha mufano muzuri wakati wanajikaza ili kufikia muradi wao wa kupata uzima wa milele mbinguni.

16. Ikuwe tuko na tumaini la kuishi mbinguni ao ku dunia, tunapaswa kuendelea kufanya nini kulingana na Wafilipi 4:6, 7?

16 Ikuwe tuko na tumaini la kuishi mbinguni ao ku dunia paradiso, tunapaswa kuendelea kujikaza ili kufikia muradi wetu. Hata tukuwe katika hali gani, tunapaswa kuepuka kuangalia mambo ya nyuma; na hatupaswe kuacha jambo lolote litufanye tuache kumutumikia Yehova. (Flp. 3:16) Mambo yenye tunangojea inaweza kuonekana kuwa inakawia kufika, ao pengine nguvu zetu za kimwili ziko zinapunguka. Pengine tumevumilia majaribu na mateso kwa miaka mingi. Hata ukuwe mu hali gani, ‘usihangaike juu ya jambo lolote.’ Lakini, umulilie Mungu katika sala na kumujulisha maombi yako, na atakupatia amani yenye kupita jambo lolote lenye unaweza kuwazia.​—Soma Wafilipi 4:6, 7.

17. Tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

17 Kama vile mukimbiaji anajikazaka sana wakati anataka kufika ku mustari wa mwisho, tuendelee kukaza akili yetu juu ya muradi wetu wa kumaliza mbio yetu ya uzima. Kwa kadiri nguvu yetu na hali zetu zinaruhusu, tujikaze sana na kuendelea mbele ili tupate mambo ya muzuri yenye Mungu ametuahidi. Tunaweza kufanya nini ili tuendelee kukimbia kwa uvumilivu? Habari yenye kufuata itatusaidia tujue mambo yenye tunapaswa kutia pa nafasi ya kwanza na namna tunaweza ‘kuhakikisha mambo ya maana zaidi.’​—Flp. 1:9, 10.

WIMBO 79 Wafundishe Kusimama Imara

^ fu. 5 Hata kama tumemutumikia Yehova kwa miaka mingi, tunapenda tuendelee kufanya mabadiliko ili tukuwe Wakristo wenye kukomaa kiroho. Mutume Paulo alitia moyo waamini wenzake wasiache hata kidogo! Barua yenye aliandikia Wafilipi iko na maneno yenye kutia moyo yenye inaweza kutusaidia tukimbie kwa uvumilivu mbio yetu ya uzima. Habari hii itatuonyesha namna gani tunaweza kutumia ile maneno ya Paulo yenye iliongozwa na roho ya Mungu.

^ fu. 11 Ona habari juu ya maisha ya Ndugu Secord, La part que j’ai prise à l’extension du vrai culte,” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, 1966 (katika Kifaransa).

^ fu. 13 Ona habari juu ya maisha ya Ndugu Melnik, “Nilifundishwa Kumpenda Mungu Tangu Utotoni,” katika Amuka! ya tarehe 22 Mwezi wa 10, 2004.

^ fu. 15 Kwa sababu muji wa Filipi uliongozwa na utawala wa Roma, wakaaji wa muji huo walikuwa na uraia wa Roma. Kwa hiyo, ndugu na dada katika Filipi walielewa muzuri mufano huo.