Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 32

Muache Upendo Wenu Ukuwe Mwingi

Muache Upendo Wenu Ukuwe Mwingi

“Hili ndilo ninaendelea kusali, kwamba upendo wenu ukuwe mwingi zaidi na zaidi.”​—FLP. 1:9.

WIMBO 106 Kusitawisha Sifa ya Upendo

KIFUPI CHA HABARI *

1. Ni nani wenye walisaidia kuanzisha kutaniko la Filipi?

WAKATI mutume Paulo, Sila, Luka, na Timoteo walifika mu muji wa Filipi wenye ulitawaliwa na Waroma, walipata watu wengi wenye walifurahia ujumbe wa Ufalme. Ndugu hao ine wenye bidii walisaidia kuanzisha kutaniko, na wanafunzi wote walianza kukutana pamoja, pengine mu nyumba ya mwanamuke mumoja mwenye aliamini mwenye aliitwa Lidia. Mwanamuke huyo alikuwa na roho ya kukaribisha wageni.​—Mdo. 16:40.

2. Bila kukawia, kutaniko hilo lilipata magumu gani?

2 Bila kukawia, kutaniko hilo mupya lilipata magumu. Shetani alichochea watu wenye hawakukuwa wanapenda kweli ili wapinge sana kazi ya kuhubiri ya Wakristo hao washikamanifu. Paulo na Sila walikamatwa, walipigwa fimbo, na kufungwa katika gereza. Kisha wao kufunguliwa, walitembelea wanafunzi hao wapya na kuwatia moyo. Kisha, Paulo, Sila, na Timoteo walitoka mu muji huo lakini inawezekana Luka alibakia kule. Ndugu na dada hao wapya wangefanya nini sasa? Yehova aliwasaidia kupitia roho yake; kwa hiyo waliendelea kufanya kazi ya Yehova kwa bidii. (Flp. 2:12) Paulo alikuwa na sababu ya muzuri ya kujivunia Wakristo hao!

3. Kulingana na Wafilipi 1:9-11, Paulo alisali juu ya mambo gani?

3 Miaka kumi hivi kisha kuanzishwa kwa kutaniko hilo la Filipi, Paulo aliandikia ndugu na dada wa kutaniko hilo barua. Wakati unasoma barua hiyo, unaweza kuona kama Paulo alikuwa anapenda sana ndugu na dada zake. Aliandika hivi: “Ninatamani sana kuwaona ninyi wote kwa upendo wenye upole kama ule wenye Kristo Yesu iko nao.” (Flp. 1:8) Aliwaandikia kama alikuwa anasali juu yao. Alikuwa anamuomba Yehova awasaidie wakuwe na upendo mwingi, wahakikishe mambo ya maana zaidi, wakuwe bila kasoro, waepuke kukwaza wengine, na waendelee kuzaa tunda la haki. Kwa kweli unakubali kama maneno ya Paulo yenye kutoka mu moyo inaweza kutuletea sisi pia faida leo. Tusome basi mambo yenye Paulo aliandikia Wafilipi. (Soma Wafilipi 1:9-11.) Tutazungumuzia mambo yenye alitaja na tutaona namna tunaweza kuitumia mu maisha.

TUKUWE NA UPENDO MWINGI

4. (a) Kulingana na 1 Yohana 4:9, 10, namna gani Yehova alituonyesha upendo? (b) Tunapaswa kumupenda Mungu namna gani?

4 Yehova alituonyesha upendo mukubwa kwa kutuma Mwana wake ku dunia ili akufe kwa ajili ya zambi zetu. (Soma 1 Yohana 4:9, 10.) Upendo wenye Mungu alionyesha unatuchochea tumupende. (Ro. 5:8) Tunapaswa kumupenda Mungu namna gani? Yesu alijibu ulizo hilo wakati aliambia Mufarisayo mumoja hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.” (Mt. 22:36, 37) Hatupaswe kumupenda Mungu kwa moyo nusu-nusu. Lakini, tunataka tuendelee kumupenda zaidi kila siku. Paulo aliambia Wafilipi kama upendo wao unapaswa kuwa “mwingi zaidi na zaidi.” Tunaweza kufanya nini ili tumupende Mungu zaidi?

5. Tunaweza kufanya nini ili tumupende Mungu zaidi?

5 Ili tumupende Mungu, tunapaswa kumujua. Biblia inasema hivi: “Mutu yeyote mwenye hana upendo hajamujua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.” (1 Yo. 4:8) Mutume Paulo alionyesha kama tutamupenda Mungu zaidi ikiwa tunaendelea kuwa na “ujuzi wenye hauna makosa na utambuzi kamili” juu yake. (Flp. 1:9) Wakati tulianza kujifunza Biblia, tulianza kumupenda Yehova hata kama hatukukuwa tunajua mambo yote juu yake. Kisha, wakati tuliendelea kujifunza juu ya Yehova, tuliendelea kumupenda zaidi. Njo maana tunaona kama kujifunza Biblia kwa ukawaida na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma katika Neno la Mungu ni kati ya mambo ya maana zaidi mu maisha yetu!​—Flp. 2:16.

6. Andiko la 1 Yohana 4:11, 20, 21, linatufundisha nini juu ya kuwa na upendo mwingi?

6 Upendo mukubwa wenye Mungu alituonyesha unatuchochea tupende ndugu na dada zetu. (Soma 1 Yohana 4:11, 20, 21.) Tunaweza kuwaza kama ni mwepesi kupenda ndugu na dada zetu. Tunaweza kuwaza vile kwa sababu tunamuabudu Yehova na kujikaza kuiga sifa zake za muzuri. Tunafuata mufano wa Yesu, mwenye alikuwa na upendo mukubwa mupaka akatoa uzima wake kwa ajili yetu. Lakini, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kutii amri ya kupendana. Fikiria mufano moja katika kutaniko la Filipi.

7. Shauri lenye Paulo alitolea Euodia na Sintike, linatufundisha nini?

7 Euodia na Sintike walikuwa dada wenye bidii wenye walikuwa wametumika “bega kwa bega” pamoja na mutume Paulo. Lakini, pengine walikuwa wameacha hali ya kukosa kuelewana ivunje urafiki wao. Katika barua yenye Paulo aliandikia kutaniko kwenye dada hao walikuwa wanatumikia, alitaja jina la Euodia na la Sintike na aliwashauria waziwazi “wakuwe na akili moja.” (Flp. 4:2, 3) Paulo aliona pia kuwa ilikuwa lazima aambie ndugu na dada wote katika kutaniko hivi: “Muendelee kufanya mambo yote bila kunungunika na kubishana.” (Flp. 2:14) Kwa kweli, shauri la waziwazi la Paulo lilisaidia dada hao washikamanifu na pia ndugu na dada wote katika kutaniko watie nguvu upendo kati yao.

Juu ya nini tunapaswa kuendelea kuona sifa za muzuri za ndugu na dada zetu? (Picha hizi zinapatana na fungu la 8) *

8. Ni nini inaweza kufanya ikuwe nguvu zaidi kupenda ndugu na dada zetu, na ni nini inaweza kutusaidia?

8 Kama vile Euodia na Sintike, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kupenda ndugu na dada zetu kwa sababu mara mingi tunakaza akili juu ya uzaifu. Sisi wote tunafanyaka makosa kila siku. Kama tunakaza akili juu ya makosa ya wengine, itakuwa nguvu zaidi kuwapenda. Kwa mufano, kama ndugu fulani anasahau kutusaidia kusafisha Jumba la Ufalme, tunaweza kukasirika. Kama tunaanza kufanya liste ya makosa yote yenye tunajua kama ndugu yetu amefanya, tutakasirika zaidi na hatutaendelea kumupenda. Kama uko na shida ya namna hiyo na mutu fulani mu kutaniko, inaweza kuwa muzuri ufikirie jambo hili: Yehova anaona uzaifu wetu na anaona uzaifu wa ndugu ao dada yetu. Lakini, hata kama anaona uzaifu huo, anaendelea kumupenda ndugu yetu na anaendelea kutupenda. Kwa hiyo, tunapaswa kuiga upendo wa Yehova na kuendelea kukaza akili juu ya sifa za muzuri za ndugu na dada zetu. Wakati tunajikaza kupenda ndugu na dada zetu, tunakuwa na umoja zaidi.​—Flp. 2:1, 2.

“MAMBO YA MAANA ZAIDI”

9. Ni mambo gani fulani ya maana zaidi yenye Paulo alitaja katika barua yake kwa Wafilipi?

9 Roho takatifu ya Mungu ilimuongoza Paulo ashaurie ndugu na dada katika Filipi, na Wakristo wote ‘wahakikishe mambo ya maana zaidi.’ (Flp. 1:10) Kati ya ile mambo ya maana zaidi kuko kutakaswa kwa jina la Yehova, kutimizwa kwa makusudi yake, na umoja na amani ya kutaniko. (Mt. 6:9, 10; Yoh. 13:35) Wakati tunatia ile mambo pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova.

10. Tunapaswa kufanya nini ili Yehova atuone kuwa hatuna kasoro?

10 Paulo alisema pia kama tunapaswa kuwa “bila kasoro.” Haiko kusema kama tunapaswa kuwa wakamilifu. Hatuwezi kuwa bila kasoro sawasawa na Yehova Mungu. Lakini Yehova atatuona kuwa hatuna kasoro ikiwa tunafanya nguvu yetu yote ili kufanya upendo wetu ukuwe mwingi na kuhakikisha mambo ya maana zaidi. Njia moja ya kuonyesha kama tuko na upendo ni kufanya nguvu yetu yote ili tusikwaze wengine.

11. Juu ya nini tunapaswa kuepuka kukwaza wengine?

11 Agizo la kuepuka kukwaza wengine ni onyo kabisa. Namna gani tunaweza kukwaza mutu fulani? Tunaweza kufanya vile kupitia mambo ya kujifurahisha yenye tunachagua, muvalio wetu, ao hata kazi yenye tunachagua kutumika. Pengine jambo lenye tuko tunafanya haliko la mubaya. Lakini kama mambo yenye tunachagua inakwaza zamiri ya mutu fulani na anamuacha Yehova, hilo ni kosa nzito. Yesu alisema kama, ikiwa tunakwaza ndugu ao dada yetu na kumufanya aharibu urafiki wake pamoja na Yehova ni muzuri zaidi wafungie jiwe nzito kwenye shingo yetu na kututupa ndani ya bahari kubwa!​—Mt. 18:6.

12. Mufano wa bwana mumoja na bibi yake wenye kuwa mapainia, unatufundisha nini?

12 Ona namna bwana mumoja na bibi yake wenye kuwa mapainia walitii onyo hilo la Yesu. Walikuwa wanatumikia mu kutaniko fulani pamoja na bwana mumoja na bibi yake wenye walitokea tu kubatizwa na wenye walikomalia mu familia zenye zilikataza mambo mingi. Bibi na bwana hao waliamini kama Wakristo hawapaswe kuenda kuangalia filme, hata filme zenye hazionyeshe mambo ya mubaya. Walikwazika wakati walisikia kama bwana huyo na bibi yake wenye kuwa mapainia waliangalia filme fulani. Kwa hiyo, mapainia hao waliacha kuenda kuangalia filme mupaka wakati watu hao wenye walitokea tu kubatizwa walizoeza zamiri yao na kuelewa muzuri mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. (Ebr. 5:14) Kwa kufanya vile, bwana huyo na bibi yake wenye kuwa mapainia walionyesha kama wanapenda ndugu huyo na bibi yake hapana kwa maneno tu lakini pia kwa matendo yao.​—Ro. 14:19-21; 1 Yo. 3:18.

13. Namna gani tunaweza kuchochea mutu fulani afanye zambi?

13 Tunaweza pia kukwaza mutu fulani kwa kumuchochea afanye zambi. Namna gani? Fikiria hali hii. Kisha kupiganisha sana na kwa wakati murefu, mwanafunzi wa Biblia anafikia kuachana na tabia yake ya kuzoea kunywa pombe sana. Kisha anaamua kama hatakunywaka tena pombe. Anafanya mabadiliko mbiombio na anabatizwa. Kisha, Mukristo mumoja mwenye hana nia ya mubaya anaalika ndugu na dada fulani ili wajifurahishe na anaomba ule ndugu mupya akunywe pombe. Anamuambia hivi: “Ulishakuwa Mukristo sasa; uko na roho ya Yehova. Sifa moja ya tunda la roho ni kujizuia. Kama uko na sifa ya kujizuia, utakunywa pombe kwa kiasi.” Wazia mambo yenye inaweza kutokea ikiwa ule ndugu mupya anasikiliza shauri hilo la mubaya!

14. Namna gani mikutano ya Kikristo inatusaidia kutumia maagizo yenye kupatikana mu Wafilipi 1:10?

14 Mikutano yetu inatusaidia kutumia katika njia mbalimbali maagizo yenye kupatikana mu Wafilipi 1:10. Njia ya kwanza, mambo yenye tunazungumuzia ku mikutano inatuonyesha mambo yenye Yehova anaona kuwa ya maana zaidi. Njia ya pili, tunajifunza namna ya kutumia mambo yenye tunajifunza ili tukuwe bila kasoro. Na Njia ya tatu, tunatiwa moyo kupendana na kufanya matendo ya muzuri. (Ebr. 10:24, 25) Wakati ndugu na dada zetu wanatutia moyo, tunamupenda Mungu zaidi na tunapenda ndugu na dada zetu zaidi. Kama tunapenda Mungu na ndugu na dada zetu kwa moyo wetu wote, tutafanya nguvu yetu yote ili tuepuke kuwakwaza.

MUENDELEE ‘KUJAA TUNDA LA HAKI’

15. ‘Kujaa tunda la haki,’ kunatia ndani mambo gani?

15 Paulo alisali kwa bidii kwamba Wafilipi ‘wajae tunda la haki.’ (Flp. 1:11) Kwa kweli, ‘kujaa tunda [hilo] la haki’ kulitia ndani kumupenda Yehova na kupenda watu wake. Pia, kulitia ndani kuzungumuza na wengine juu ya imani yao katika Yesu na juu ya tumaini lao la muzuri sana. Wafilipi 2:15 inatumia maneno ingine, ni kusema, ‘kuangaza kama vitu vya kutoa mwangaza katika ulimwengu.’ Ile maneno inafaa kabisa kwa sababu Yesu aliita wanafunzi wake kuwa “mwangaza wa ulimwengu.” (Mt. 5:14-16) Aliamuru pia wanafunzi wake ‘wafanye wanafunzi,’ na alisema kama ‘wangekuwa mashahidi . . . mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Mt. 28:18-20; Mdo. 1:8) Tunazaa “tunda la haki” wakati tunafanya kwa bidii kazi hiyo ya maana zaidi.

Wakati alikuwa anafungwa mu nyumba moja kule Roma, Paulo aliandikia kutaniko la Filipi barua. Wakati huo, Paulo alitumia muzuri nafasi zenye zilijitokeza ili kuhubiria maaskari wenye walikuwa wanamuchunga na watu wenye walikuwa wanamutembelea. (Picha hii inapatana na fungu la 16)

16. Namna gani Wafilipi 1:12-14 inaonyesha kama tunaweza kuangaza kama vitu vya kutoa mwangaza hata kama tuko katika hali za nguvu? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

16 Hata tukuwe mu hali gani, tunaweza kutoa mwangaza kama vitu vya kutoa mwangaza. Mu hali fulani, mambo yenye inaonekana kuwa inatuzuia kuhubiri habari njema, inaweza kugeuka na kuwa nafasi ya kuhubiria watu wengine. Kwa mufano, mutume Paulo alikuwa anafungwa mu nyumba moja kule Roma wakati aliandikia Wafilipi barua yake. Lakini hata kama Paulo alikuwa mufungwa, hilo halikumuzuia kuhubiria watu wenye walikuwa wanamuchunga na watu wenye walikuwa wanamutembelea. Paulo alihubiri kwa bidii katika hali hizo, na mufano wake ulisaidia ndugu na dada wakuwe na uhodari “wa kusema neno la Mungu bila woga.”​—Soma Wafilipi 1:12-14; 4:22.

Sikuzote, tutafute namna za kuhubiri kulingana na uwezo wetu wote (Picha hizi zinapatana na fungu la 17) *

17. Namna gani ndugu na dada wanaendelea kuhubiri hata wakati ni nguvu kufanya vile? Leta mufano.

17 Ndugu na dada wengi wako wanaonyesha uhodari kama wa Paulo. Wanaishi katika inchi kwenye hawawezi kuhubiri waziwazi ao nyumba kwa nyumba, kwa hiyo wanatafuta njia zingine za kuhubiri habari njema. (Mt. 10:16-20) Katika inchi moja kati ya inchi hizo, mwangalizi mumoja wa muzunguko aliomba kila muhubiri amalize “eneo” lake lote, ni kusema, ahubirie watu wa jamaa yake, majirani wake, wanafunzi wenzake, wafanyakazi wenzake, na watu wenye anajuana nao. Kisha miaka mbili, hesabu ya makutaniko katika muzunguko huo iliongezeka sana. Pengine tunaishi mu inchi kwenye tunaweza kuhubiri waziwazi. Lakini, mufano wa ndugu na dada wenye ufundi unaweza kutufundisha jambo hili la maana: Sikuzote, tutafute namna za kuhubiri kulingana na uwezo wetu wote, tukuwe hakika kama Yehova atatupatia uwezo wenye tuko nao lazima ili kushinda kila kizuizi.​—Flp. 2:13.

18. Tunapaswa kuazimia kufanya nini?

18 Katika wakati huu wa maana sana, tuazimie basi kutumia shauri lenye liliongozwa na roho ya Mungu lenye kupatikana mu barua yenye Paulo aliandikia Wafilipi. Tuhakikishe mambo ya maana zaidi, tukuwe bila kasoro, tuepuke kukwaza wengine, na tuzae tunda la haki. Kama tunafanya vile, tutakuwa na upendo mwingi na tutamuletea utukufu Yehova, Baba yetu mwenye upendo.

WIMBO 17 ‘Nataka’

^ fu. 5 Leo njo wakati wenye tunapaswa kupenda zaidi ndugu na dada zetu. Barua kwa Wafilipi inatusaidia kuona namna tunaweza kuwa na upendo mwingi, hata wakati ni nguvu kuonyesha upendo.

^ fu. 54 MAFASIRIO YA PICHA: Wakati wa kusafisha Jumba la Ufalme, ndugu mumoja mwenye kuitwa Joe, anaacha kutumika na anaanza kuongea na ndugu mwingine na mutoto wake. Ndugu Mike, mwenye iko anatumia chombo cha kuvuta vumbi, anakasirika wakati anaona vile. Anawaza hivi: ‘Joe anapaswa kutumika, hapana kuongea na watu.’ Kisha, Mike anaangalia namna Joe anamusaidia kwa upole dada mumoja mwenye kuzeeka. Jambo hilo lenye kugusa moyo linakumbusha Mike kama anapaswa kufikiria sifa za muzuri za ndugu huyo.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Mu inchi moja kwenye Mashahidi wa Yehova hawawezi kuhubiri waziwazi, ndugu mumoja anahubiria kwa uficho mutu fulani mwenye anajuana naye. Ndugu huyo anazungumuza naye juu ya ujumbe wa Ufalme lakini iko muangalifu ili wasafiri wengine wasijue. Kisha, wakati wa mapumuziko ku kazi, ndugu huyo anahubiria mufanyakazi mwenzake.