Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 33

“Wale Wenye Wanakusikiliza” Wataokolewa

“Wale Wenye Wanakusikiliza” Wataokolewa

“Endelea kuwa muangalifu juu yako mwenyewe na kuhusu kufundisha kwako. Endelea kufanya mambo hayo, kwa maana kwa kufanya vile utajiokoa wewe mwenyewe na utaokoa pia wale wenye wanakusikiliza.”​—1 TI. 4:16.

WIMBO 67 “Lihubiri Neno”

KIFUPI CHA HABARI *

1. Sisi wote tunapenda watu wa jamaa yetu wafanye nini?

DADA mumoja mwenye kuitwa Pauline * anasema hivi: “Tangu wakati nilijifunza kweli, nimependa watu wa jamaa yangu wakuwe pamoja na mimi mu Paradiso. Zaidi sana, nilipenda bwana yangu Wayne na mutoto wangu mwanaume wakuwe pia watumishi wa Yehova.” Uko na watu wa jamaa wenye hawajamujua Yehova na kumupenda? Kama vile Pauline, pengine na wewe unapenda watu wa jamaa yako wamutumikie Yehova.

2. Tutazungumuzia maulizo gani mu habari hii?

2 Hatuwezi kukaza watu wa jamaa yetu wakubali habari njema, lakini tunaweza kuwasaidia wakuwe tayari kukubali ujumbe wa Biblia. (2 Ti. 3:14, 15) Juu ya nini tunapaswa kuhubiria watu wa jamaa yetu? Juu ya nini tunapaswa kujitia pa nafasi yao? Tunaweza kufanya nini ili kusaidia watu wa jamaa yetu wafikie kumupenda Yehova kama sisi? Ndugu na dada wote katika kutaniko wanaweza kufanya nini ili kutusaidia?

JUU YA NINI TUNAPASWA KUHUBIRIA WATU WA JAMAA YETU?

3. Kulingana na 2 Petro 3:9, juu ya nini tunapaswa kuhubiria watu wa jamaa yetu?

3 Hivi karibuni, Yehova ataleta mwisho wa ulimwengu huu. Ni wale tu wenye kuwa na “muelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uzima wa milele” njo wataokolewa. (Mdo. 13:48) Tunatumia wakati mingi na nguvu mingi ili kuhubiria watu wa eneo letu wenye hatujue, kwa hiyo, tunapenda hata zaidi kuhubiria watu wa jamaa yetu ili nao watumikie Yehova. Yehova, Baba yetu mwenye upendo, “hataki mutu yeyote aharibiwe lakini anataka wote wafikie kutubu.”​—Soma 2 Petro 3:9.

4. Tunaweza kufanya kosa gani wakati tunahubiria watu wa jamaa yetu?

4 Tunapaswa kukumbuka kama kuko namna ya muzuri na namna ya mubaya ya kuhubiria watu ujumbe wa wokovu. Tunaweza kuonyesha heshima wakati tunahubiria mutu mwenye hatujue, lakini tunaweza kuzungumuza bila heshima wakati tunahubiria watu wa jamaa yetu.

5. Tunapaswa kukumbuka nini mbele ya kuhubiria watu wa jamaa yetu?

5 Kama tunafikiria wakati tulijaribu kuhubiria watu wa jamaa yetu kwa mara ya kwanza, wengi kati yetu wanaweza kuona kama hawakutumiaka njia ya muzuri na kuwaza kama wangepaswa kutumia njia ingine. Mutume Paulo alishauria Wakristo hivi: “Maneno yenu yakuwe yenye kupendeza sikuzote, yenye kukolezwa chumvi, ili mujue namna munapaswa kumujibu kila mutu.” (Kol. 4:5, 6) Ni muzuri tukumbuke shauri hilo wakati tunahubiria watu wa jamaa yetu. Kama hatufanye vile, tunaweza kuwakwaza kuliko kuwasaidia wasikilize ujumbe wetu.

TUNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUSAIDIA WATU WA JAMAA YETU?

Sifa ya kujitia pa nafasi ya wengine na mwenendo wako vinaweza kutoa ushahidi mukubwa zaidi (Picha hizi zinapatana na fungu la 6-8) *

6-7. Leta mufano wenye kuonyesha kama ni jambo la maana Mukristo ajitie pa nafasi ya bibi ao bwana yake mwenye haiko Shahidi.

6 Ujitie pa nafasi ya wengine. Pauline, mwenye tumekwisha kuzungumuzia ku mwanzo, anasema hivi: “Ku mwanzo, nilikuwa ninapenda kuzungumuza na bwana yangu juu ya mambo ya kiroho tu. Hatukukuwa tunazungumuzia mambo ingine.” Lakini, Wayne, bwana ya Pauline, hakukuwa anajua mambo mingi juu ya Biblia na hakukuwa anaelewa mambo yenye Pauline alikuwa anazungumuzia. Bwana yake aliona kama hakukuwa anawaza juu ya mambo ingine, alikuwa anawaza juu ya dini yake tu. Aliogopa kama bibi yake alikuwa anajiunga na zehebu ao kikundi hatari cha dini na alikuwa anadanganywa.

7 Pauline alisema kama wakati fulani alikuwa anapitisha wakati mingi mangaribi na ku mwisho wa juma pamoja ndugu na dada, ku mikutano ya kutaniko ao katika mahubiri na ku mikutano ya kujifurahisha. Pauline anasema hivi: “Wakati fulani Wayne alikuwa anafika ku nyumba na hakuna mutu, na alikuwa anajisikia kuwa peke yake.” Kwa kweli, Wayne alikuwa anapenda bibi yake na mutoto wake mwanaume wakuwe pamoja naye. Hakukuwa anajua ikiwa walikuwa pamoja na watu gani, na ilionekana kuwa Pauline alikuwa anaona marafiki wake wapya kuwa wa maana zaidi kuliko bwana yake. Juu ya ile yote, Wayne alimuogopesha Pauline kuwa atavunja ndoa yao. Unawaza Pauline alipaswa kufanya nini ili ajitie pa nafasi ya bwana yake?

8. Kulingana na 1 Petro 3:1, 2, ni nini inaweza kuvutia zaidi watu wa jamaa yetu?

8 Uhubiri kupitia mwenendo wako. Mara mingi, watu wa jamaa yetu wanaangalia sana mambo yenye tunafanya kuliko mambo yenye tunasema. (Soma 1 Petro 3:1, 2.) Kisha wakati fulani, Pauline alielewa vile. Anasema hivi: “Nilijua kama Wayne alikuwa anatupenda na hakutaka kabisa kuvunja ndoa yetu. Lakini wakati aliniogopesha kuwa atavunja ndoa yetu, hilo lilinisaidia kutambua kama ninapaswa kutumia mashauri ya Yehova juu ya ndoa. Kuliko kusema mingi, nilipaswa kuonyesha mufano muzuri kupitia mwenendo wangu.” Pauline aliacha kumukaza Wayne wazungumuze juu ya mambo ya Biblia, na alianza kuzungumuza naye juu ya mambo ingine. Wayne aliona kama bibi yake alikuwa sasa mutu mwenye kufanya amani, na aliona kama mutoto wao mwanaume alikuwa sasa na mwenendo muzuri. (Mez. 31:18, 27, 28) Wakati Wayne aliona namna ujumbe wa Biblia ulikuwa umesaidia familia yake, akakuwa tayari kusikiliza ujumbe wa Biblia.​—1 Ko. 7:12-14, 16.

9. Juu ya nini hatupaswe kuchoka kusaidia watu wa jamaa yetu?

9 Usichoke kusaidia watu wa jamaa yako. Yehova anatuonyesha mufano muzuri. “Tena na tena,” anapatia watu nafasi ya kusikiliza habari njema ili wapate uzima. (Yer. 44:4) Na mutume Paulo alimuambia Timoteo asichoke kusaidia wengine. Sababu gani? Kwa sababu, kwa kufanya vile, angejiokoa yeye mwenyewe na wale wenye walimusikiliza. (1 Ti. 4:16) Tunapenda watu wa jamaa yetu, kwa hiyo tunapenda wajue mafundisho ya Neno la Mungu. Kisha wakati fulani, maneno na matendo ya Pauline ilisaidia familia yake. Sasa iko na furaha juu anamutumikia Yehova pamoja na bwana yake. Wote wawili wako mapainia, na tena bwana yake iko muzee wa kutaniko.

10. Juu ya nini tunapaswa kuwa na uvumilivu?

10 Ukuwe na uvumilivu. Wakati tunatumia kanuni za Mungu katika maisha yetu, watu wa jamaa yetu wanaweza kuona kuwa ni vigumu kukubali mambo ya mupya yenye tunaamini na maisha yetu ya mupya. Mara mingi, jambo la kwanza lenye wanaona ni kuwa hatujiunge tena nao katika sikukuu za dini na katika mambo ya politike. Ku mwanzo, watu fulani wa jamaa yetu wanaweza kutukasirikia. (Mt. 10:35, 36) Lakini hatupaswe kuchoka kuwasaidia. Kama tunaacha kuwasaidia waelewe mambo yenye tunaamini, ni kama vile tunawahukumu kuwa hawastahili kupata uzima wa milele. Yehova hakutupatia kazi ya kuhukumu watu, Yesu njo amepatia ile kazi. (Yoh. 5:22) Kama tuko na uvumilivu, kisha wakati fulani, watu wa jamaa yetu wanaweza kuwa tayari kusikiliza ujumbe wetu.​—Ona kisanduku “ Tumia Site Yetu ya Enternete ili Kufundisha.”

11-13. Namna Alice alitendea wazazi wake inaweza kutufundisha nini?

11 Ukuwe na heshima lakini usiache watu wa jamaa wabadilishe maamuzi yako. (Mez. 15:2) Fikiria mufano wa Alice. Alijifunza kweli juu ya Yehova wakati alikuwa anaishi mbali na wazazi wake, wenye walikuwa wanapenda sana mambo ya politike na hawakukuwa wanaamini kama Mungu iko. Alielewa kama, bila kukawia, alipaswa kuzungumuza nao juu ya mambo ya muzuri yenye alikuwa anajifunza. Alice anasema hivi: “Kama unakawia kuonyesha watu wa jamaa yako mambo ya mupya yenye uko unajifunza na kama hautafanyaka tena desturi fulani, watavunjika moyo sana.” Alikuwa anaandikia wazazi wake barua, na kuwauliza mawazo yao juu ya mafundisho fulani ya Biblia yenye aliwaza kama inaweza kuwapendeza, kwa mufano aliwauliza mawazo yao juu ya upendo. (1 Ko. 13:1-13) Alishukuru wazazi wake juu walimukomalisha na walimuhangaikia, na aliwatumia zawadi mbalimbali. Wakati alikuwa anaenda kuona wazazi wake, alikuwa anajikaza sana kusaidia mama yake kufanya kazi za mu nyumba. Ku mwanzo, wazazi wa Alice hawakufurahi wakati alizungumuza nao juu ya mambo ya mupya yenye alikuwa ameamini.

12 Wakati Alice alikuwa ku nyumba pamoja na wazazi wake, aliendelea kuheshimia programu yake ya kusoma Biblia. Alice anasema hivi: “Kufanya vile kulisaidia mama yangu aelewe kama nilikuwa ninaona Biblia kuwa ya maana sana.” Wakati huo, baba ya Alice aliamua kujifunza mambo fulani juu ya Biblia ili aelewe juu ya nini mutoto wake alikuwa amebadilisha mawazo yake, na alipenda kutafuta mambo yenye ingemufanya achambue-chambue Biblia. Alice anasema hivi: “Nilimupatia Biblia, na nilimuandikia maneno fulani ndani ya ile Biblia.” Matokeo ilikuwa nini? Baba ya Alice hakupata mambo yenye ingemufanya achambue-chambue Biblia lakini alifurahia mambo yenye alisoma mu Biblia.

13 Tunapaswa kuwa na heshima lakini hatupaswe kuacha watu wa jamaa wabadilishe maamuzi yetu, hata kama tunapaswa kuvumilia mateso. (1 Ko. 4:12b) Kwa mufano, Alice alipaswa kuvumilia wakati mama yake alimupinga. Alice anasema hivi: “Wakati nilibatizwa, Mama aliniita ‘mutoto mubaya.’” Alice alifanya nini? Alice anasema hivi: “Kuliko kuepuka kuzungumuza juu ya dini yangu ya mupya, nilimuelezea kwa heshima kama nilikuwa nimeamua kuwa Shahidi wa Yehova na kama singebadilisha uamuzi wangu. Nilijikaza kumuhakikishia mama yangu kama ninamupenda kabisa. Sisi wote wawili tulilia, na nilimupikia chakula cha muzuri sana. Kuanzia wakati huo, mama yangu alianza kuelewa kama Biblia ilikuwa inanisaidia nikuwe mutu muzuri.”

14. Juu ya nini hatupaswe kuacha hata kidogo watu wa jamaa yetu wabadilishe uamuzi wetu?

14 Inaweza kuomba wakati ili watu wa jamaa yetu waelewe muzuri kama tunaona kumutumikia Yehova kuwa jambo la maana sana. Kwa mufano, wakati Alice aliamua kuwa painia kuliko kufanya kazi yenye wazazi wake walipenda afanye mu maisha yake, mama yake alilia tena. Lakini Alice hakubadilisha uamuzi wake. Alice anasema hivi: “Kama unaacha watu wa jamaa wabadilishe uamuzi wako juu ya jambo fulani, wanaweza pia kujaribu kubadilisha maamuzi yako juu ya mambo ingine. Lakini kama unaonyesha watu wa familia yako heshima bila kubadilisha maamuzi yako, wamoja wanaweza kusikiliza ujumbe wako.” Alice alijionea jambo hilo. Sasa wazazi wake wote wako mapainia, na tena baba yake iko muzee wa kutaniko.

NDUGU NA DADA WOTE KATIKA KUTANIKO WANAWEZA KUFANYA NINI ILI KUTUSAIDIA?

Ndugu na dada katika kutaniko wanaweza kufanya nini ili kusaidia watu wa jamaa yetu wenye hawako Mashahidi? (Picha hizi zinapatana na fungu la 15-16) *

15. Kulingana na Matayo 5:14-16 na 1 Petro 2:12, namna gani “matendo ya muzuri” ya wengine inasaidia watu wa jamaa yetu?

15 Yehova anavuta watu kwake kupitia “matendo ya muzuri” ya kutaniko la Kikristo. (Soma Matayo 5:14-16; 1 Petro 2:12.) Ikiwa bibi ao bwana yako haiko Shahidi wa Yehova, amekwisha kukutana na ndugu na dada wa kutaniko lenu? Pauline, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, alialika ndugu na dada ku nyumba yake ili Wayne, bwana yake, awajue muzuri. Wayne anakumbuka namna ndugu mumoja alimusaidia ajue muzuri Mashahidi wa Yehova ni watu wa namna gani. Wayne anasema hivi: “Alikamata mapumuziko ya siku moja kwenye kazi yake ili tuangalie muchezo mumoja wa kabumbu kwenye televizyo. Na niliwaza hivi: ‘Iko sawa na watu wengine!’”

16. Juu ya nini tunapaswa kualika watu wa jamaa yetu kwenye mikutano?

16 Njia ya muzuri zaidi ya kusaidia watu wa jamaa yetu ni kuwaalika wakuje ku mikutano ya kutaniko. (1 Ko. 14:24, 25) Mukutano wa kwanza wenye Wayne alihuzuria, ulikuwa Ukumbusho, kwa sababu mukutano huo ulifanywa kisha kazi na programu hiyo haikukamata wakati murefu. Wayne anasema hivi: “Sikuelewa mambo yote yenye ilizungumuziwa katika hotuba, lakini ninakumbuka watu. Walinikaribia na kunikaribisha na walinisalimia kwa furaha. Nilitambua kama walikuwa watu wazuri.” Bwana mumoja na bibi yake walikuwa wamemuonyesha Pauline wema kwa kumusaidia kuhangaikia mutoto wake mwanaume ku mikutano na katika mahubiri. Kwa hiyo, wakati Wayne alifikia kujua mambo mingi juu ya mambo ya mupya yenye Pauline alikuwa ameamini, aliomba ule bwana ajifunze Biblia pamoja naye.

17. Hatupaswe kujilaumu juu ya jambo gani, lakini juu ya nini hatupaswe kuchoka kusaidia watu wa jamaa yetu?

17 Tunapenda watu wote wa jamaa yetu wakuwe pia watumishi wa Yehova. Lakini, hata kama tunajikaza sana ili kuwasaidia wakuwe watumishi wa Mungu, pengine hawatakubali kweli. Kama hawakubali kweli, hatupaswe kujilaumu juu ya uamuzi wao. Kwa kweli, hatuwezi kukaza mutu akubali mambo yenye tunaamini. Lakini, kama watu wa jamaa yako wanaona namna uko na furaha sana juu unamutumikia Yehova, hilo linaweza kuwachochea wao pia wamutumikie. Usali kwa ajili yao. Uzungumuze nao kwa heshima. Usichoke kuwasaidia! (Mdo. 20:20) Ukuwe hakika kama Yehova atabariki bidii yako. Na kama watu wa jamaa yako wanaamua kukusikiliza, wataokolewa!

WIMBO 57 Kuwahubiria Watu wa Namna Zote

^ fu. 5 Tunapenda watu wa jamaa yetu wafikie kumujua Yehova, lakini wanapaswa kuamua ikiwa watamutumikia ao hapana. Habari hii itazungumuzia mambo yenye tunaweza kufanya ili watu wa jamaa yetu wakuwe tayari zaidi kutusikiliza.

^ fu. 1 Majina fulani imebadilishwa. Mu habari hii, maneno “watu wa jamaa” maana yake watu wa jamaa wenye hawajaanza kumutumikia Yehova.

^ fu. 53 MAFASIRIO YA PICHA: Ndugu kijana anasaidia baba yake mwenye haiko Shahidi kutengeneza motokari yake. Kwa wakati wenye kufaa, anamuonyesha video ku jw.org®.

^ fu. 55 MAFASIRIO YA PICHA: Dada mumoja anasikiliza kwa uangalifu bwana yake mwenye haiko Shahidi wakati anazungumuzia mambo mingi yenye alifanya muchana. Kisha anajifurahisha pamoja na familia yake.

^ fu. 57 MAFASIRIO YA PICHA: Dada mumoja amealika ndugu na dada wa kutaniko ku nyumba yake. Wanajikaza kujua muzuri bwana yake. Kisha, bwana yake anahuzuria Ukumbusho pamoja naye.