Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yohana Mubatizaji​—Mufano Wake Unaweza Kutusaidia Tuendelee Kuwa na Furaha

Yohana Mubatizaji​—Mufano Wake Unaweza Kutusaidia Tuendelee Kuwa na Furaha

UNAPENDA kupata pendeleo fulani katika kutaniko lakini haujapata pendeleo hilo? Pengine ni pendeleo lenye mutu mwingine iko nalo. Ao inaweza kuwa pendeleo fulani lenye ulikuwa nalo zamani. Lakini, uzee, matatizo ya afya, matatizo ya kupata feza, ao madaraka ya familia inakuzuia kufanya mambo mingi sasa. Ao pengine uliacha pendeleo lenye ulitumikia kwa miaka mingi kwa sababu ya mabadiliko yenye kufanywa katika tengenezo. Hata ikuwe sababu gani, pengine unajisikia kuwa hauko unafanya mambo yote yenye ungependa kufanya katika kazi ya Mungu. Katika hali kama hizo, inaeleweka kuwa wakati fulani unaweza kujisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo. Hata hivyo, ni nini inaweza kukusaidia usiendelee kujisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo, mwenye huzuni, ao kuwa na kinyongo? Unaweza kufanya nini ili uendelee kuwa na furaha?

Mufano wa Yohana Mubatizaji unaweza kutusaidia tujue namna ya kuendelea kuwa na furaha. Yohana alikuwa na mapendeleo ya pekee, lakini pengine hakuwazia mambo yenye ingemufikia mu maisha yake. Hakuwazia kama angepitisha wakati murefu katika gereza kuliko wakati alipitisha katika kazi ya kuhubiri. Lakini, Yohana aliendelea kuwa na furaha, na aliendelea kuwa na mutazamo huo maisha yake yote. Ni nini ilimusaidia? Na tunaweza kufanya nini ili tuendelee kuwa na furaha hata kama tunapambana na magumu?

MUGAO WENYE ULILETEA YOHANA FURAHA

Katika Mwezi wa 4 hivi, mwaka wa 29 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Yohana alianza kufanya kazi yenye Yehova alimupatia ya kusaidia watu wakuwe tayari kumupokea Masiya. Alikuwa anasema hivi: “Mutubu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia.” (Mt. 3:2; Lu. 1:12-17) Watu wengi walitubu. Kwa kweli, vikundi vya watu vilitoka mbali ili kuja kusikia ujumbe wake, na wengi walichochewa kutubu na kubatizwa. Pia, kwa uhodari Yohana alionya viongozi wa dini wenye walikuwa wanajiona kuwa wenye haki juu ya hukumu yenye ingewapata kama hawangefanya mabadiliko. (Mt. 3:5-12) Aliona namna utumishi wake unafikia mwisho katika Mwezi wa 10 hivi, mwaka wa 29, wakati alimubatiza Yesu. Kuanzia wakati huo, Yohana alitia watu moyo wamufuate Yesu, Masiya mwenye aliahidiwa.​—Yoh. 1:32-37.

Kwa sababu Yohana alikuwa na mugao wa pekee, Yesu alisema hivi: “Kati ya wale wenye walizaliwa na wanamuke, hakujatokea mutu yeyote mukubwa kuliko Yohana Mubatizaji.” (Mt. 11:11) Kwa kweli Yohana alifurahia sana baraka zenye alipata. Kama vile Yohana, leo watu wengi wamepata baraka mingi. Fikiria mufano wa ndugu mwenye kuitwa Terry. Yeye na bibi yake, Sandra, wamefanya miaka zaidi ya 50 katika utumishi wa wakati wote. Terry anasema hivi: “Nimepata mapendeleo mingi ya muzuri sana. Nimekuwa painia, Mwanabeteli, painia wa pekee, mwangalizi wa muzunguko, mwangalizi wa wilaya, na sasa niko tena painia wa pekee.” Tunafurahi sana wakati tunapata mapendeleo mu kazi ya Yehova, lakini kama vile mufano wa Yohana utatufundisha, inaomba kujikaza sana ili tuendelee kuwa na furaha wakati hali zetu zinabadilika.

UENDELEE KUWA MWENYE SHUKRANI

Jambo lenye lilimusaidia Yohana Mubatizaji aendelee kuvumilia ni hili: aliendelea kuwa mwenye shukrani sana juu ya mapendeleo yenye alikuwa nayo. Fikiria mufano huu. Kisha Yesu kubatizwa, watu wenye walikuwa wanamufuata Yohana walianza kupunguka lakini watu wenye walikuwa wanamufuata Yesu walianza kuongezeka. Kwa sababu wanafunzi wa Yohana walikuwa na wasiwasi juu ya jambo hilo, walisema hivi: “Ona, anabatiza, na watu wote wanamuendea.” (Yoh. 3:26) Yohana aliwajibu hivi: “Kila mutu mwenye kuwa na bibi-arusi ndiye bwana-arusi. Lakini wakati rafiki ya bwana-arusi anasimama na kumusikia, anafurahi sana kwa sababu ya sauti ya bwana-arusi. Basi furaha yangu imefanywa kuwa kamili.” (Yoh. 3:29) Yohana hakutafuta kufanya mashindano na Yesu, na hakuwaza kama pendeleo lenye alikuwa nalo halina tena maana kwa sababu pendeleo la Yesu lilikuwa la maana zaidi. Lakini, Yohana aliendelea kuwa na furaha kwa sababu aliendelea kufurahia daraka lake la kuwa “rafiki ya bwana-arusi.”

Mutazamo wa Yohana ulimusaidia aendelee kuwa na furaha hata kama mugao wake haukukuwa mwepesi. Kwa mufano, Yohana alikuwa Munaziri tangu wakati alizaliwa, njo maana hakupaswa kunywa divai. (Lu. 1:15) Yesu alizungumuzia maisha ya mwepesi ya Yohana kwa kusema hivi: “Yohana alikuja hakukuwa anakula na hakukuwa anakunywa.” Lakini, Yesu na wanafunzi wake hawakukuwa Wanaziri, kwa hiyo, waliishi kama watu wengine. (Mt. 11:18, 19) Pia, hata kama Yohana hakufanya hata muujiza moja, alijua kama wanafunzi wa Yesu, kutia ndani wamoja wenye walikuwaka wanafunzi wa Yohana, walipewa uwezo wa kufanya miujiza. (Mt. 10:1; Yoh. 10:41) Kuliko kufikiria sana tofauti zenye zilikuwa kati ya wanafunzi wake na wanafunzi wa Yesu, Yohana aliendelea kufanya kazi yake kwa bidii.

Na sisi tunaweza kuendelea kuwa na furaha ikiwa tunaona mugao wetu wa sasa mu kazi ya Yehova kuwa wa maana. Terry, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Nilikaza akili yangu juu ya kila mugao wenye nilipewa.” Wakati anafikiria maisha yake katika utumishi wa wakati wote, anasema hivi: “Sina huzuni yoyote lakini ninaendelea kukumbuka tu mambo ya muzuri sana.”

Tunaweza kuwa na furaha zaidi kama tunafikiria mambo yenye inafanya mugao wetu mu kazi ya Yehova ukuwe wa pekee kabisa. Ni pendeleo kabisa kuwa “wafanyakazi pamoja na Mungu.” (1 Ko. 3:9) Kitu cha maana sana kinaweza kuendelea kuwa mu hali ya muzuri kama tunaendelea kukitunza. Vilevile, tunaweza kuendelea kuwa na furaha ikiwa tunaendelea kufikiri juu ya pendeleo lenye tuko nalo la kutumika pamoja na Yehova. Hatupaswe kulinganisha bidii yetu na ya watu wengine. Hatupaswe kufikiri kama mapendeleo yetu haiko ya maana na kama mapendeleo ya wengine njo ya maana zaidi.​—Gal. 6:4.

KAZA AKILI YAKO JUU YA MAMBO YA KIROHO

Pengine Yohana alijua kama utumishi wake haungefanya wakati murefu, lakini pengine hakujua namna utumishi wake ungeisha bila kutazamia. (Yoh. 3:30) Katika mwaka wa 30 kisha kuzaliwa kwa Yesu, miezi sita hivi kisha Yohana kumubatiza Yesu, Mufalme Herode, alimufunga Yohana katika gereza. Lakini, Yohana aliendelea kufanya nguvu yake yote ili kuhubiri. (Mk. 6:17-20) Ni nini ilimusaidia aendelee kuwa na furaha wakati alikuwa mu ile hali? Aliendelea kukaza akili yake juu ya mambo ya kiroho.

Wakati Yohana alikuwa katika gereza, alipata habari za mingi juu ya utumishi wa Yesu wenye ulikuwa unaongezeka. (Mt. 11:2; Lu. 7:18) Yohana alikuwa hakika kama Yesu alikuwa Masiya lakini pengine alikuwa anajiuliza namna gani Yesu angetimiza mambo yote yenye Maandiko ilisema kama Masiya angetimiza. Kwa sababu Yohana alikuwa anajua kama Masiya angekuwa Mufalme, pengine alijiuliza kama Yesu alikuwa karibu kuanza kutawala. Tena, pengine alijiuliza ikiwa Yesu angemutosha katika gereza. Yohana alipenda kujua zaidi juu ya mambo yenye Yesu alikuwa karibu kufanya, kwa hiyo, alituma wanafunzi wake wawili ili wamuulize Yesu ulizo hili: “Wewe ndiye Ule Mwenye Anakuja, ao tungojee mwingine?” (Lu. 7:19) Wakati walirudia, inawezekana kabisa Yohana aliwasikiliza kwa uangalifu wakati walikuwa wanaeleza namna Yesu aliponyesha watu kwa njia ya muujiza na kisha aliwatuma wamuambie Yohana hivi: “Sasa vipofu wanaona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanafanywa kuwa safi, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanatangaziwa habari njema.”​—Lu. 7:20-22.

Kwa kweli, habari hizo zilimutia Yohana moyo. Zilihakikisha kama Yesu alikuwa anatimiza unabii juu ya Masiya. Hata kama Yesu hakumutosha Yohana katika gereza, Yohana alijua kama kazi yake haikukuwa ya bure. Hata kama alikuwa katika hali gani, alikuwa na sababu ya kuwa na furaha.

Kukaza akili juu ya habari za muzuri zenye kuonyesha namna kazi yetu ya kuhubiri mu dunia yote inaendelea, kunaweza kutusaidia tuendelee kuwa na furaha

Kama vile Yohana, tutaweza kuvumilia kwa furaha na uvumilivu kama tunakaza akili yetu juu ya mambo ya kiroho. (Kol. 1:9-11) Tunaweza kufanya vile kwa kusoma Biblia na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma, na hilo litatukumbusha kama mambo yenye tunatimiza mu kazi ya Mungu haiko ya bure hata kidogo. (1 Ko. 15:58) Sandra anasema hivi: “Kusoma sura moja ya Biblia kila siku kumenisaidia nimukaribie Yehova zaidi. Kunanisaidia kukaza akili juu ya Yehova kuliko kukaza akili juu yangu mwenyewe.” Tunaweza pia kukaza akili yetu juu ya habari zenye zinazungumuzia mambo yenye ndugu na dada wako wanatimiza mu kazi ya Yehova, na kufanya vile kutatusaidia tuache kujifikiria sisi wenyewe lakini tukaze akili yetu juu ya mambo yenye Yehova iko anatimiza. Sandra anasema hivi: “Programu za kila mwezi za JW Télédiffusion zinatusaidia tujisikie kuwa karibu na tengenezo la Yehova, na zinatusaidia tuendelee kuwa na furaha mu mugao wetu.”

Mu kipindi kifupi chenye Yohana Mubatizaji alifanya kazi ya kuhubiri, aliiga “roho na nguvu za Eliya,” na kama vile Eliya, “alikuwa mutu mwenye hisia kama zetu.” (Lu. 1:17; Yak. 5:17) Kama tunaiga mufano wake wa kuonyesha shukrani na kukaza akili juu ya mambo ya kiroho, sisi pia tunaweza kuendelea kuwa na furaha mu kazi yetu ya Ufalme hata kutokee nini.