Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 35

Heshimia Kila Mutu mu Kutaniko la Yehova

Heshimia Kila Mutu mu Kutaniko la Yehova

“Jicho haliwezi kuambia mukono, ‘Sina lazima yako,’ ao tena, kichwa hakiwezi kuambia miguu, ‘Sina lazima yenu.’”​—1 KO. 12:21.

WIMBO 124 Washikamanifu Sikuzote

KIFUPI CHA HABARI *

1. Yehova amepatia kila mutumishi wake muaminifu pendeleo gani?

KWA upendo, Yehova amepatia kila mutumishi wake muaminifu pendeleo la kuwa mu kutaniko lake. Hata kama hatufanye kazi ileile mu kutaniko, sisi wote tuko wa maana na kila mumoja iko na lazima ya mwingine. Mutume Paulo anatusaidia tuelewe ile jambo ya maana. Namna gani?

2. Kulingana na Waefeso 4:16, juu ya nini tunapaswa kuheshimiana na kutumika kwa umoja?

2 Kama vile andiko la musingi la habari hii linaonyesha, Paulo alionyesha wazi kama hakuna mutumishi wa Yehova mwenye anaweza kuambia mwenzake hivi: “Sina lazima yako.” (1 Ko. 12:21) Kama tunapenda mu kutaniko mukuwe amani, tunapaswa kuheshimiana na kutumika kwa umoja. (Soma Waefeso 4:16.) Wakati tunatumika kwa umoja, kila mutu ataona kama ndugu na dada wanamupenda na kutaniko litakuwa nguvu.

3. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

3 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia Wakristo wenzetu mu kutaniko? Mu hii habari tutaona namna wazee wanaweza kuonyeshana heshima. Kisha, tutazungumuzia namna tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia ndugu zetu wenye hawajaoa na dada zetu wenye hawajaolewa. Na ku mwisho, tutaona namna tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia wenye hawajue muzuri luga yetu.

HESHIMIA WAZEE WENZAKO

4. Ni shauri gani la Paulo lenye kuwa mu Waroma 12:10 lenye wazee wanapaswa kufuata?

4 Wazee wote wa kutaniko wanawekwa na roho takatifu ya Yehova. Lakini, kila muzee iko na uwezo wake. (1 Ko. 12:17, 18) Wazee fulani hawajakawia sana tangu wakuwe wazee na kwa hiyo hawana uzoefu kabisa. Wazee wengine hawana uwezo wa kufanya mambo mingi kwa sababu ya magonjwa ao uzee. Lakini hata vile, hakuna muzee mwenye anapaswa kufanya muzee mwenzake aone sawa vile anamuambia “sina lazima yako.” Kuliko kufanya vile, wazee wanapaswa kufuata shauri la Paulo lenye kuwa mu Waroma 12:10.​—Soma.

Wazee wanaonyesha kama wanaheshimia wazee wenzao kwa kuwasikiliza kwa uangalifu (Ona fungu la 5-6)

5. Wazee wanapaswa kufanya nini ili kuonyesha kama wanaheshimiana, na juu ya nini ni jambo la maana kufanya vile?

5 Muzee anaonyesha kama anaheshimia wazee wenzake kwa kuwasikiliza wakati wanatoa mawazo yao. Ni jambo la maana wazee wafanye vile zaidi sana wakati wanazungumuzia mambo mazito. Juu ya nini? Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 1988 ulisema hivi: “Wazee wanapaswa kujua kama Kristo, kupitia roho takatifu, anaweza kuongoza muzee yeyote mu baraza ili asaidie wazee wenzake wajue kanuni ya Biblia ya kutumia mu hali fulani ao wakati wanapenda kukamata uamuzi fulani wa maana. (Mdo. 15:6-15) Mu baraza la wazee, hakuna muzee mwenye anapaswa kuwaza kama yeye tu njo iko na roho takatifu.”

6. Ni nini inaweza kusaidia wazee watumike kwa umoja, na kufanya vile kunaweza kusaidia kutaniko namna gani?

6 Muzee mwenye kuheshimia wazee wenzake, anaepukaka kuwa wa kwanza kila mara kutoa mawazo yake ku mikutano ya wazee. Hatawalake mazungumuzo, na hawazake kama maoni yake tu njo ya muzuri. Lakini analetaka mawazo yake kwa unyenyekevu. Anasikilizaka kwa uangalifu wakati wazee wengine wako wanasema. Na jambo la maana zaidi, mawazo yake inategemeaka kanuni za Biblia na muongozo wa “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45-47) Wakati wazee wanazungumuza kwa upendo na kwa heshima, roho ya Mungu itakuwa pale, na itawasaidia wakamate maamuzi yenye itatia nguvu kutaniko.​—Yak. 3:17, 18.

HESHIMIA NDUGU WENYE HAWAJAOA NA DADA WENYE HAWAJAOLEWA

7. Yesu alikuwa na mawazo gani juu ya kubakia bila kuoa ao kuolewa?

7 Mu kutaniko muko familia zenye hazina watoto na zenye ziko na watoto, lakini muko pia ndugu wengi wenye hawajaoa na dada wengi wenye hawajaolewa. Tunapaswa kuwa na mawazo gani juu ya wale wenye hawajaoa ao kuolewa? Tuone mawazo ya Yesu kuhusu kubakia bila kuoa ao kuolewa. Wakati alikuwa ku dunia Yesu hakuoaka. Ile ilimusaidia akaze akili yake juu ya mugao wake. Hakuna siku Yesu alifundisha kama kila Mukristo anapaswa kuoa ao kuolewa, ao kama anapaswa kubakia bila kuoa ao bila kuolewa. Lakini, alisema kama Wakristo fulani wanaweza kuamua kubakia bila kuoa ao kuolewa. (Mt. 19:11, 12) Yesu alikuwa anaheshimia wale wenye hawajaoa ao kuolewa. Hakuwazarau ao kuona kama wanakosa kitu fulani.

8. Mu 1 Wakorinto 7:7-9, Paulo anatia moyo kila Mukristo afikirie nini?

8 Kama Yesu, mutume Paulo alimutumikia Yehova bila kuwa na bibi. Hakuna siku Paulo alisema kama ni mubaya kuoa ao kuolewa. Alijua kama ile ni uamuzi wa mutu yeye mwenyewe. Lakini, Paulo alitia moyo kila Mukristo afikirie ikiwa anaweza kumutumikia Yehova bila kuoa ao kuolewa. (Soma 1 Wakorinto 7:7-9.) Ile yote inaonyesha kama Paulo hakuzarau Wakristo wenye walikuwa hawajaoa ao kuolewa. Kwa mufano, alimuchagua Timoteo, ndugu mwenye alikuwa hajaoa, ili atumikie madaraka mazito. * (Flp. 2:19-22) Njo maana, haiko muzuri kuwaza kama ndugu fulani anastahili kupata madaraka juu tu alishaoa, ao kuwaza kama hastahili juu tu hajaoa.​—1 Ko. 7:32-35, 38.

9. Tunapaswa kuwa na mawazo gani kuhusu kuoa ao kuolewa, na pia kuhusu kubakia bila kuoa ao kuolewa?

9 Yesu na Paulo hawakufundisha kama Wakristo wanapaswa kufunga ndoa ao kama wanapaswa kubakia bila kufunga ndoa. Sasa, tunapaswa kuwa na mawazo gani kuhusu kuoa ao kuolewa, na pia kuhusu kubakia bila kuoa ao kuolewa? Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 10, 2012, unajibia muzuri sana ile ulizo kwa kusema hivi: “Kwa kweli, tunaweza kusema kama kufunga ndoa ao kutofunga ndoa ni zawadi kutoka kwa Mungu. . . . Yehova haone kutofunga ndoa kuwa jambo la haya ao la huzuni.” Njo maana tunapaswa kuheshimia ndugu wenye hawajaoa na dada wenye hawajaolewa.

Tunapaswa kuepuka nini ili kuonyesha kama tunaheshimia Wakristo wenzetu wenye hawajaoa ao kuolewa? (Ona fungu la 10)

10. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia Wakristo wenzetu wenye hawana bibi ao bwana?

10 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia Wakristo wenzetu wenye hawana bibi ao bwana? Tujue kama Wakristo fulani waliamua kubakia bila kuoa ao kuolewa. Wengine wako na nia ya kuoa ao kuolewa, lakini hawajapata mutu mwenye wanafurahia. Na wengine pengine walifisha bibi ao bwana. Ikuwe ni sababu gani inafanya wakuwe vile, haiko muzuri kuanza kuwauliza juu ya nini hawana bibi ao bwana, ao hata kujaribu kuwatafutia bibi ao bwana. Ni kweli kama ndugu ao dada fulani wanaweza kutuomba tuwasaidie wapate bibi ao bwana. Lakini ikiwa hawakutuomba musaada, unawaza watajisikia namna gani kama tunafanya vile? (1 Te. 4:11; 1 Ti. 5:13) Acha tuone maelezo ya Wakristo fulani waaminifu wenye hawajaoa ao kuolewa.

11-12. Ni nini inaweza kuvunja moyo Wakristo wenye hawajaoa ao kuolewa?

11 Mwangalizi mumoja wa muzunguko mwenye hajaoa, mwenye anatimiza mugao wake muzuri, anaona kama kubakia bila kuoa kuko na faida mingi. Lakini alisema kama wakati fulani anavunjikaka moyo wakati ndugu na dada, wenye hawana nia ya mubaya, wanamuuliza: “Juu ya nini haujaoa?” Ndugu mwingine mwenye naye hajaoa, mwenye anatumikia ku biro fulani ya tawi anasema hivi: “Wakati fulani ndugu na dada wanawaza kama mutu mwenye hajaoa ao kuolewa ni mutu wa kusikilia huruma. Ile inaweza kufanya ionekane kama kubakia bila kuoa ao kuolewa haiko zawadi lakini ni muzigo.”

12 Dada mumoja mwenye hajaolewa, mwenye anatumikia ku Beteli alisema hivi: “Ndugu na dada fulani wanawazaka kama watu wote wenye hawajaoa ao kuolewa wako natafuta bibi ao bwana, ao kama wakati wanakutana na watu wengine wanaona kama ile njo wakati ya kupata bibi ao bwana. Wakati fulani niliendaka mu eneo lingine kwa ajili ya mugao fulani, na wakati nilikuwa kule nilienda ku mukutano. Dada mwenye nilipanga kwake aliniambia kama mu kutaniko lao muko ndugu wawili wa miaka yangu. Aliniambia nisiwaze kama iko nanitafutia bwana. Lakini wakati tu tuliingia mu Jumba la Ufalme, alinipeleka kwenye wale ndugu walikuwa juu nionane nao. Kusema kweli, mimi na wale ndugu wawili tulisikia haya.”

13. Dada mumoja mwenye hajaolewa alisema nini juu ya mapainia wenye hawajaoa ao kuolewa?

13 Dada mwingine mwenye hajaolewa, mwenye anatumikia ku Beteli alisema hivi: “Ninajua mapainia wenye hawajaoa ao kuolewa wenye wako na usawaziko, wanajikaza kufikia miradi yao, wako tayari kusaidia wengine, na wako na furaha. Wanasaidia sana kutaniko. Wako na mawazo yenye kufaa kuhusu hali yao. Hawajione kuwa wa maana kuliko wengine juu tu hawajaoa ao kuolewa wala hawaone kuwa wanakosa kitu juu tu hawana bibi ao bwana ao watoto.” Njo vile mutu anajisikiaka wakati wengine mu kutaniko wanamuheshimia na wanamuona kuwa wa maana. Anajua kama hawamusikilie huruma ao kumusikilia wivu, wala hawamuzarau ao kumuona kuwa wa maana kuliko wengine. Anajua tu kama wanamupenda.

14. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia Wakristo wenzetu wenye hawajaoa ao kuolewa?

14 Wakristo wenzetu wenye hawajaoa ao kuolewa watafurahi sana kama tunawaona kuwa wa maana kwa sababu ya sifa zao za muzuri. Haiko muzuri kuwasikilia huruma juu tu hawana bibi ao bwana, juu kama tunafanya vile, itakuwa sawa vile tunawaambia: “Sina lazima yako.” (1 Ko. 12:21) Tunapaswa kuwapenda kwa sababu ya uaminifu wao. Kama tunafanya vile, wataona kama tunawaheshimia na tunawaona kuwa wa maana mu kutaniko.

HESHIMIA WENYE HAWAJUE MUZURI LUGA YAKO

15. Wahubiri fulani wamefanya mabadiliko gani ili kufanya mengi mu kazi ya Yehova?

15 Mu miaka fulani yenye imepita wahubiri wengi wamejikaza kujifunza luga ingine ili waweze kufanya mengi zaidi mu kazi ya Yehova. Ili kufanya vile, iliomba wafanye mabadiliko ya mingi. Waliacha kutaniko la luga yao ili waende kutumikia mu kutaniko la luga ingine lenye kuwa na lazima ya wahubiri. (Mdo. 16:9) Ule ni uamuzi wa kipekee wenye wale Wakristo wanakamata ili kumutumikia Yehova zaidi. Wanasaidia sana kutaniko, hata kama inaweza kuwakamata wakati murefu mbele wajue muzuri ile luga ya mupya. Wanatia nguvu ndugu na dada kupitia sifa zao za muzuri na uzoefu wao. Tunawapenda sana kwa sababu wanajitoa ili kusaidia wengine!

16. Wazee wanachunguza nini wakati wanapenda kupendekeza ndugu fulani?

16 Baraza la wazee halitakosa kupendekeza ndugu ili akuwe mutumishi wa huduma ao muzee juu tu hajue muzuri luga ya kutaniko lao. Wakati wazee wanapenda kuamua ikiwa ndugu fulani anastahili kutumikia ile madaraka hawataangalia kama anajua muzuri luga ya kutaniko lao ao hapana, lakini watachunguza kama anatimiza sifa zenye kuzungumuziwa katika Maandiko.​—1 Ti. 3:1-10, 12, 13; Tit. 1:5-9.

17. Wazazi fulani wanaweza kuwa na lazima ya kuamua nini wakati wanahamia mu inchi ingine?

17 Wakristo fulani pamoja na familia zao wamehamia mu inchi ingine kwa sababu ya magumu yenye kuwa mu inchi yao, ao ili kutafuta kazi. Kwa hiyo, pengine ku masomo watoto wao wanafundishwa mu luga ya inchi kwenye wamehamia. Wazazi pia wanaweza kuwa na lazima ya kujifunza luga ya ile inchi ili wapate kazi. Sasa watafanya nini kama kuko kutaniko ao kikundi cha luga yao? Wataenda mu kutaniko la luga ya inchi kwenye wamehamia ao wataenda mu kutaniko la luga yao?

18. Kulingana na Wagalatia 6:5, tunaweza kufanya nini ili kuonyesha kama tunaheshimia uamuzi wa kichwa cha familia?

18 Kichwa cha familia anapaswa kuamua ikiwa familia yake itaenda mu kutaniko la luga gani. Anapaswa kufikiria ni mu kutaniko la luga gani njo watu wa familia yake wanaweza kuwa nguvu kiroho. (Soma Wagalatia 6:5.) Kwa kuwa ule ni uamuzi wa kipekee, tunapaswa kuheshimia uamuzi wenye anakamata. Hata aamue nini, tutaonyesha kuwa tunaheshimia uamuzi wake kama tunawakaribisha na kuwaonyesha upendo.​—Ro. 15:7.

19. Kichwa cha familia anapaswa kufikiri sana na kusali kuhusu nini?

19 Familia zingine zinaweza kuwa mu kutaniko la luga ya wazazi, lakini pengine watoto hawajue muzuri ile luga. Kama ile kutaniko iko mu eneo lenye watu wanazungumuza luga yenye watoto wanafundishwa ku masomo, pengine watoto wanaweza kuwa na magumu ya kuelewa mambo yenye inafundishwa ku mikutano. Pia wanaweza kuwa na magumu ya kufanya maendeleo ya kiroho. Kama ni vile, kichwa cha familia anapaswa kufikiri sana na kumuomba Yehova amusaidie ili akamate uamuzi wenye utasaidia familia yake imukaribie Yehova na watu wake. Pengine itaomba asaidie watoto wake wajue muzuri luga yao, ao itaomba wahamie mu kutaniko la luga yenye watoto wake wanajua muzuri. Hata aamue nini, ndugu na dada wa kutaniko lenye anachagua wanapaswa kumuheshimia yeye na familia yake na kuwaonyesha upendo.

Tutaepuka kufanya nini ili kuonyesha kama tunapenda ndugu na dada zetu wenye hawajue muzuri luga yetu? (Ona fungu la 20)

20. Tutaepuka kufanya nini ili kuonyesha kama tunaheshimia ndugu na dada wenye hawajue muzuri luga ya kutaniko letu?

20 Wakati tunafikiria ile mambo yote yenye tumezungumuzia, tunaweza kusema kama mu kutaniko hamutakosaka ndugu na dada wenye hawajue muzuri luga ya ile kutaniko. Wanaweza kuwa na magumu ya kusema mawazo yao. Lakini, kama hatukazie akili namna yao ya kusema, tutaona kama wanamupenda Yehova na wanapenda sana kumutumikia. Ile itafanya tuwapende sana na tuwaheshimie. Hata kama hawajue muzuri luga yetu, hatutafanya waone sawa vile tunawaambia “sina lazima yako.”

YEHOVA ANATUONA KUWA WA MAANA

21-22. Tuko na pendeleo gani la muzuri sana?

21 Yehova ametupatia pendeleo la muzuri sana la kuwa mu kutaniko lake. Ikuwe uko mwanaume ao mwanamuke, ulishafunga ndoa ao hapana, ikuwe uko kijana ao mwenye kuzeeka, unajua muzuri luga fulani ao hapana, Yehova anakuona kuwa wa maana, na ndugu na dada zako pia wanakuona kuwa wa maana.​—Ro. 12:4, 5; Kol. 3:10, 11.

22 Tuendelee basi kukumbuka mambo yenye tumejifunza kupitia mufano wenye Paulo alizungumuzia wenye unahusu mwili wa mwanadamu. Ile itatusaidia tusisahau kama tuko wa maana mu kutaniko la Yehova. Itatusaidia pia tupende na kuheshimia wengine mu kutaniko.

WIMBO 90 Tianeni Moyo

^ fu. 5 Watumishi wa Yehova wako tofauti na wote hawafanye kazi ileile mu kutaniko. Hii habari itatusaidia kuona juu ya nini ni jambo la maana kuheshimia kila mutu mu familia ya Yehova.

^ fu. 8 Hatuwezi kuhakikisha kama Timoteo alibakiaka bila kuoa.