Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 31

Uko Unangojea “Muji Wenye Uko na Misingi ya Kweli”?

Uko Unangojea “Muji Wenye Uko na Misingi ya Kweli”?

“Alikuwa anangojea muji wenye uko na misingi ya kweli, wenye ule mwenye aliufanya na kuujenga ni Mungu.”​—EBR. 11:10.

WIMBO 22 Ufalme Umesimamishwa​—Na Uje!

KIFUPI CHA HABARI *

1. Watu fulani wamejiima mambo gani, na sababu gani walifanya vile?

LEO, mamilioni ya watu wa Mungu wamejiima mambo fulani. Ndugu na dada wengi wameamua kubakia bila kuoa ao kuolewa. Bibi na bwana fulani wameamua kubakia bila kuzaa kwa wakati fulani. Familia fulani zimefanya maisha yao ikuwe mwepesi. Wote wameamua kufanya vile kwa sababu wanapenda kumutumikia Yehova kwa uwezo wao wote. Wanatosheka na wanatumaini kama Yehova atawapatia mambo yote yenye wako nayo lazima kabisa. Yehova atawategemeza kabisa? Ndiyo! Sababu gani tunaweza kusema vile? Kwa sababu, zamani Yehova alipatia watumishi wake mambo yote yenye walikuwa nayo lazima. Kwa mufano, alimubariki Abrahamu, “baba ya wale wote wenye kuwa na imani.”​—Ro. 4:11.

2. (a) Kulingana na Waebrania 11:8-10, 16, sababu gani Abrahamu alikubali kuacha muji wa Uru? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

2 Abrahamu alikubali kuacha maisha ya muzuri yenye alikuwa nayo katika muji wa Uru. Sababu gani? Kwa sababu alikuwa anangojea “muji wenye uko na misingi ya kweli.” (Soma Waebrania 11:8-10, 16.) Ule “muji” ni nini? Abrahamu alipata magumu gani wakati alikuwa anangojea ule muji ujengwe? Namna gani tunaweza kumuiga na namna gani tunaweza kuiga watu wa wakati wetu wenye wamefuata mufano wake? Habari hii itatusaidia kupata majibu ya ile maulizo.

“MUJI WENYE UKO NA MISINGI YA KWELI” NI NINI?

3. Muji wenye Abrahamu alingojea ni nini?

3 Muji wenye Abrahamu alikuwa anangojea ni Ufalme wa Mungu. Ule Ufalme unafanyizwa na Yesu Kristo, na Wakristo watiwa-mafuta 144 000. Paulo aliita ule Ufalme “muji wa Mungu mwenye kuishi, Yerusalemu la mbinguni.” (Ebr. 12:22; Ufu. 5:8-10; 14:1) Yesu alifundisha wanafunzi wake waombe ule Ufalme ukuje, ili mapenzi ya Mungu ifanyike duniani kama mbinguni.​—Mt. 6:10.

4. Kulingana na Mwanzo 17:1, 2, 6, Abrahamu alijua nini kuhusu ule muji, ao Ufalme wenye Mungu aliahidi?

4 Abrahamu hakujua habari zote juu ya namna Ufalme wa Mungu ungepangwa. Kwa miaka mingi, zile habari zilikuwa “siri takatifu.” (Efe. 1:8-10; Kol. 1:26, 27) Lakini Abrahamu alijua kama wamoja kati ya wazao wake wangekuwa wafalme, kwa sababu ni vile Yehova alimuahidi. (Soma Mwanzo 17:1, 2, 6.) Abrahamu alikuwa na imani yenye nguvu katika ahadi za Mungu. Ilikuwa kama vile aliona Masiya, ao Mutiwa-Mafuta, mwenye angekuwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu. Njo maana Yesu aliambia Wayahudi wa wakati wake hii maneno: “Baba yenu Abrahamu alifurahi sana katika tumaini la kuona siku yangu, na aliiona na kufurahi.” (Yoh. 8:56) Ni wazi kama, Abrahamu alijua kuwa wazao wake wangekuwa sehemu ya Ufalme wenye Yehova angesimamisha, na alikuwa tayari kumungojea Yehova atimize ile ahadi.

Namna gani Abrahamu alionyesha imani katika ahadi za Yehova? (Ona fungu la 5)

5. Tunajua namna gani kama Abrahamu alikuwa anangojea muji wenye Mungu angefanya?

5 Namna gani Abrahamu alionyesha kama alikuwa anangojea muji, ao Ufalme wenye Mungu angefanya? Kwanza, Abrahamu hakukuwa raia wa ufalme hata moja hapa ku dunia. Aliishi maisha ya kuhama-hama, na hakuunga mukono mufalme yeyote mwanadamu. Tena, Abrahamu hakujaribu kuanzisha ufalme wake mwenyewe. Kuliko kufanya vile aliendelea kumutii Yehova na kumungojea atimize ahadi yake. Kwa kufanya vile, Abrahamu alionyesha imani kubwa kwa Yehova. Tuzungumuzie magumu fulani yenye Abrahamu alipambana nayo na tuone mambo yenye mufano wake unaweza kutufundisha.

ABRAHAMU ALIPAMBANA NA MAGUMU GANI?

6. Muji wa Uru ulikuwa namna gani?

6 Muji wa Uru wenye Abrahamu aliacha ulikuwa salama na ulilindwa muzuri. Watu wa muji huo walikuwa na elimu na walikuwa matajiri. Ule muji ulilindwa na ukuta na mufereji wenye shimo ya murefu. Watu wa Uru walijua sana mambo ya kuandika na kufanya hesabu. Na inaonekana kama watu wengi walifanya biashara katika muji huo, kwa sababu watu wenye kuchimbua vitu vya zamani walivumbua maandishi mingi yenye ilitumiwa mu mambo ya biashara. Nyumba za watu zilijengwa na matofali na kuta zilikuwa zinapakaliwa rangi ya mweupe. Nyumba fulani zilikuwa na vyumba 13 ao 14 na katikati ya vyumba hivyo kulikuwa kiwanja chenye kilijengwa kwa majiwe.

7. Juu ya nini iliomba Abrahamu akuwe hakika kama Yehova atamulinda yeye na familia yake?

7 Iliomba Abrahamu akuwe hakika kama Yehova atamulinda yeye na familia yake. Juu ya nini? Kumbuka kama Abrahamu na Sara waliacha nyumba yao ya muzuri kwenye waliishi kwa usalama katika muji wa Uru, na walienda kuishi mu mahema katika inchi ya Kanaani. Abrahamu na familia yake hawakulindwa tena na kuta za murefu na mufereji wenye kuwa na shimo ya murefu. Sasa, hawakukuwa tena na ulinzi, na haingekuwa nguvu kwa maadui kuwashambulia.

8. Wakati fulani, ni mambo gani ilimupata Abrahamu?

8 Hata kama Abrahamu alifanya mapenzi ya Mungu, wakati fulani hakukuwa na chakula ya kutosha ili kulisha familia yake. Alipaswa kupambana na njaa kali yenye ilipiga inchi yote kwenye Yehova alimutuma. Ile njaa ilikuwa kali sana hivi kwamba Abrahamu aliamua kuhama na familia yake katika Misri kwa wakati fulani. Lakini, wakati Abrahamu alikuwa Misri, Farao, mufalme wa ile inchi, alimuchukua Sara ili akuwe bibi yake. Wazia namna Abrahamu alipaswa kuhangaika mupaka wakati Yehova alimupatia Farao malipizi na Farao akamurudisha.​—Mwa. 12:10-19.

9. Abrahamu alipata matatizo gani katika familia yake?

9 Maisha ya familia ya Abrahamu ilikuwa na matatizo. Bibi yake mupendwa Sara, hakukuwa anazaa. Kwa miaka mingi, ile hali iliwavunja moyo sana. Kisha, Sara akamuambia Abrahamu azae na mutumishi wake Hagari, ili wapate watoto. Lakini wakati Hagari alipata mimba ya Ishmaeli akaanza kumuzarau Sara. Hali ilifikia kuwa mubaya sana na Sara akamufukuza Hagari.​—Mwa. 16:1-6.

10. Yehova alimuambia Abrahamu afanye nini yenye ingefanya ikuwe nguvu kwa Abrahamu kumutumainia?

10 Sara alifikia kupata mimba na akazaa mutoto mwenye Abrahamu aliita Isaka. Abrahamu alipenda watoto wake wote wawili, Ishmaeli na Isaka. Lakini kwa sababu Ishmaeli alikuwa anamutendea Isaka mubaya, Yehova alimuambia Abrahamu amufukuze Ishmaeli na Hagari. (Mwa. 21:9-14) Kisha miaka mingi, Yehova alimuambia Abrahamu amutolee Isaka, mwana wake. (Mwa. 22:1, 2; Ebr. 11:17-19) Katika hali hizo mbili, Abrahamu alipaswa kutumaini kama Yehova atatimiza ahadi zenye alitoa kuhusu watoto wake.

11. Sababu gani Abrahamu alipaswa kumungojea Yehova kwa uvumilivu?

11 Mu ile wakati yote Abrahamu alipaswa kumungojea Yehova kwa uvumilivu. Inawezekana Abrahamu alikuwa na miaka zaidi ya 70 wakati yeye na familia yake walitoka Uru. (Mwa. 11:31–12:4) Na kwa miaka karibu mia moja Abrahamu aliishi mu mahema na alisafiri huku na huku katika inchi ya Kanaani. Abrahamu alikufa wakati alikuwa na miaka 175. (Mwa. 25:7) Lakini hakuona Yehova anatimiza ahadi ya kupatia wazao wake inchi ya Kanaani. Na alikufa mbele ule muji, ni kusema Ufalme wa Mungu usimamishwe. Hata hivyo, Biblia inasema kama alikufa akiwa “muzee na mwenye kutosheka.” (Mwa. 25:8) Hata kama Abrahamu alivumilia magumu mingi aliendelea kuwa na imani yenye nguvu na alikuwa tayari kumungojea Yehova. Sababu gani aliweza kuvumilia? Kwa sababu katika maisha yake yote, Yehova alimulinda na alimutendea kama rafiki.​—Mwa. 15:1; Isa. 41:8; Yak. 2:22, 23.

Namna gani watumishi wa Mungu wanaonyesha imani na uvumilivu kama Abrahamu na Sara? (Ona fungu la 12) *

12. Tuko tunangojea nini, na tutazungumuzia nini?

12 Kama Abrahamu, sisi pia tuko tunangojea muji wenye uko na misingi ya kweli. Lakini sisi hatungojee ule muji ujengwe. Ufalme wa Mungu ulisimamishwa mu mwaka wa 1914 na ulishaanza kutawala mbinguni. (Ufu. 12:7-10) Lakini tunangojea utawale ku dunia. Mbele ile wakati ifike tutapambana na magumu yenye inaweza kufanana na ile ya Abrahamu na Sara. Watumishi wa Yehova wa leo wamejikaza kumuiga Abrahamu. Habari mbalimbali juu ya maisha ya watu, zenye kutolewa katika Munara wa Mulinzi zinaonyesha kama watu wengi leo wameonyesha imani na uvumilivu kama Abrahamu na Sara. Tuzungumuzie habari fulani kati ya hizo na tuone mambo yenye tunaweza kujifunza.

WATU FULANI WENYE WALIFUATA MUFANO WA ABRAHAMU

Bill Walden alikuwa tayari kujiima mambo fulani na alijionea baraka za Yehova

13. Habari juu ya maisha ya ndugu Walden inakufundisha nini?

13 Ukuwe tayari kujiima mambo fulani. Kama tunapenda kutia ule muji, ni kusema Ufalme wa Mungu, pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu, tunapaswa kuwa kama Abrahamu, mwenye alikuwa tayari kujiima mambo fulani ili kumupendeza Mungu. (Mt. 6:33; Mk. 10:28-30) Fikiria mufano wa ndugu mumoja mwenye kuitwa Bill Walden. * Katika mwaka wa 1942, Bill alianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Wakati huo, alikuwa karibu kupata diplome ya ufundi wa ujenzi kwenye masomo fulani ya juu katika Amerika. Mwalimu mumoja wa Bill alifanya mipango ili Bill apate kazi kisha kumaliza masomo, lakini Bill alikataa. Na alimufasiria kama aliamua kujitoa sana mu kazi ya Mungu kuliko kuitika kazi yenye ingemupatia feza mingi. Wakati kidogo kisha pale, wakubwa wa serikali walimuomba Bill ajiandikishe katika jeshi, lakini alikataa. Ile ilifanya alipishwe dola 10 000 na kuhukumiwa kifungo cha miaka tano mu gereza. Alifunguliwa kisha miaka tatu. Kisha wakati fulani, alialikwa kusoma Masomo ya Gileadi, akakuwa misionere na akaenda kutumikia mu Afrika. Kisha, Bill alimuoa Eva na walitumika katika Afrika. Ile iliwaomba wajiime mambo fulani. Kisha miaka mingi walirudia katika Amerika ili kuhangaikia mama ya Bill. Bill anasema hivi juu ya maisha yake: “Machozi inanitokaka wakati ninafikiri juu ya pendeleo la muzuri sana, lenye nimepata la kutumiwa na Yehova kwa zaidi ya miaka 70 katika kazi yake. Ninamushukuru mara mingi kwa sababu alinisaidia nimutumikie mu maisha yangu yote.” Wewe pia, unaweza kufanya utumishi wa wakati wote mu maisha yako yote?

Eleni na Aristotelis Apostolidis waliona namna Yehova aliwasaidia kuvumilia

14-15. Mambo yenye ilimufikia ndugu Apostolidis na bibi yake inatufundisha nini?

14 Usitazamie kama maisha yako haitakuwa na magumu. Kupitia mufano wa Abrahamu tunajifunza kama hata wale wenye wametoa maisha yao yote ili kumutumikia Yehova watapata tu magumu. (Yak. 1:2; 1 Pe. 5:9) Maisha ya ndugu Aristotelis Apostolidis inahakikisha jambo hilo. * Alibatizwa katika mwaka wa 1946 katika inchi ya Ugiriki, na katika mwaka wa 1952 alichumbia dada mumoja mwenye kuitwa Eleni; ule dada alikuwa na miradi kama yake. Lakini, Eleni akagonjwa na alivumbuliwa na kivimba kwenye ubongo. Kivimba kiliondolewa, lakini miaka kidogo kisha kufunga ndoa, kile kivimba kikarudia tena. Wanganga walimupasua tena, lakini Eleni alipooza sehemu fulani ya mwili na hakukuwa anasema tena muzuri. Aliendelea kuhubiri kwa bidii, hata kama alikuwa mugonjwa na hata kama wakubwa wa serikali walileta mateso ile wakati.

15 Aristotelis alimuhangaikia bibi yake kwa miaka 30. Wakati huo, alikuwa muzee wa kutaniko, na alikuwa anatumika katika halmashauri za mikusanyiko, na alisaidia kujenga Jumba la Mukusanyiko. Kisha, mu mwaka wa 1987, wakati Eleni alikuwa mu mahubiri, mulango mukubwa wa chuma ulijifunga nyuma yake, ukamurusha na kumuangusha mu barabara. Alipoteza ufahamu, na alibakia mu ile hali kwa miaka tatu, kisha akakufa. Aristotelis alifasiria namna alijisikia juu ya mambo yenye ilimufikia. Ku mwisho wa habari juu ya maisha yake alisema hivi: “Kwa miaka mingi, nilipata magumu mingi na magumu fulani kati ya hiyo ilitokea kwa njia yenye hatukutazamia. Kwa hiyo, nilikuwa na lazima ya kuendelea kuvumilia na sikuacha kitu chochote kinivunje moyo. Kwa kweli sikuzote Yehova alinipa nguvu yenye nilikuwa nayo lazima ili nivumilie ile magumu.” (Zb. 94:18, 19) Yehova anapenda sana wale wenye wanafanya yote yenye wanaweza hata kama wako wanapata magumu!

Audrey Hyde aliendelea kukaza akili juu ya wakati wenye kuja

16. Ni shauri gani ya muzuri yenye Ndugu Knorr alipatia bibi yake?

16 Kaza akili juu ya wakati wenye kuja. Abrahamu alikaza akili juu ya zawadi zenye Yehova angemupatia wakati wenye kuja, na ile ilimusaidia avumilie magumu. Dada Audrey Hyde alikaza akili juu ya tumaini la wakati wenye kuja, hata kama bwana yake wa kwanza Nathan Knorr, alikufa na ugonjwa wa kansere na bwana yake wa pili, Glenn Hyde, alipata ugonjwa wa kupoteza akili wenye kuitwa Alzheimer. * Alisema kama mambo yenye bwana yake wa kwanza alimuambia majuma fulani mbele akufe, ilimusaidia aendelee kuvumilia bila kupoteza furaha. Anasema hivi: “Nathan alinikumbusha kama: ‘Hata kama tunakufa, tumaini letu liko hakika, na wakati tumaini hilo litatimia, hatutateseka tena hata kidogo.’ Kisha akanishauria hivi: ‘Angalia mbele, kwa sababu ni kule njo kuko malipo yako.’ . . . Kisha akaongezea hivi: ‘Ujikaze kuwa na mambo mingi ya kufanya, ni kusema, utumie maisha yako ili kusaidia wengine. Ile itakusaidia ukuwe na furaha.’” Ile ni shauri ya muzuri hata kwetu pia! Ili tushinde magumu, tunapaswa kuwa na mambo mingi ya kufanya kwa kusaidia wengine na ‘kufurahi katika tumaini.’​—Ro. 12:12.

17. (a) Sababu gani ni jambo la maana tukaze akili juu ya wakati wenye kuja? (b) Kulingana na Mika 7:7 tunapaswa kufanya nini ili tupate baraka za wakati wenye kuja?

17 Kuliko wakati mwingine wowote, leo tuko na lazima ya kukaza akili juu ya wakati wenye kuja. Mambo yenye tunaona mu dunia leo, inaonyesha waziwazi kama tunaishi katika sehemu ya mwisho ya siku za mwisho za mupangilio huu wa mambo. Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utatawala dunia yote, kwa hiyo hatutakuwa tena na lazima ya kungojea Ufalme huo. Kutakuwa baraka mingi zenye tutapata, kati ya baraka hizo, tutafurahia kuona wapendwa wetu wenye watafufuliwa. Ile wakati, Yehova atamubariki Abrahamu kwa sababu ya imani na uvumilivu wake. Atamufufua yeye pamoja na familia yake hapa ku dunia. Utakuwa pale ili kuwakaribisha? Unaweza, ikiwa unamuiga Abrahamu, kwa kuwa tayari kujiima mambo fulani kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, kwa kumutumainia Yehova hata kama uko na magumu, na kwa kuendelea kumungojea Yehova kwa uvumilivu.​—Soma Mika 7:7.

WIMBO 74 Shiriki Kuimba Wimbo wa Ufalme!

^ fu. 5 Kungojea ahadi za Mungu zitimie, kunaweza kujaribu uvumilivu wetu na hata imani yetu. Katika habari hii tutaona mambo yenye mufano wa Abrahamu unaweza kutufundisha; na tutaona namna mufano wake unaweza kutusaidia tungojee kwa uvumilivu kutimizwa kwa ahadi za Yehova. Tutaona pia mambo yenye tunaweza kujifunza kupitia mifano ya watumishi wa Yehova wa leo.

^ fu. 13 Habari juu ya maisha ya ndugu Walden ilitolewa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 12, 2013, uku. 8-10.

^ fu. 14 Habari juu ya maisha ya ndugu Apostolidis ilitolewa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 2, 2002, uku. 24-28.

^ fu. 16 Habari juu ya maisha ya dada Hyde ilitolewa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 mwezi wa 7, 2004, uku. 23-29.

^ fu. 56 MAFASIRIO YA PICHA: Bibi na bwana wenye kuzeeka wanaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu hata kama wako na magumu. Wanaendelea kumutumainia Yehova kwa kukaza akili juu ya ahadi zake za wakati wenye kuja.