Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 34

Uko wa Maana Sana mu Kutaniko la Yehova!

Uko wa Maana Sana mu Kutaniko la Yehova!

“Kama vile mwili ni mumoja lakini uko na viungo vingi, na viungo vyote vya mwili huo, hata kama ni vingi, ni mwili mumoja, ni vile pia Kristo iko.”​—1 KO. 12:12.

WIMBO 101 Kufanya Kazi Pamoja kwa Umoja

KIFUPI CHA HABARI *

1. Tuko na pendeleo gani?

KUWA mu kutaniko la Yehova ni pendeleo kubwa sana! Tuko mu paradiso ya kiroho, na mule ndani muko watu wenye amani na wenye furaha. Lakini unawaza namna gani, uko wa maana mu kutaniko?

2. Mutume Paulo alitumia mufano gani katika barua zake fulani?

2 Mufano wenye mutume Paulo alitumia katika barua zake fulani utatusaidia kujua kama tuko wa maana mu kutaniko ao hapana. Mu zile barua, Paulo alisema kama kutaniko liko sawa vile mwili wa mwanadamu. Alisema pia kama watu mu kutaniko wako sawa vile sehemu za mwili.​—Ro. 12:4-8; 1 Ko. 12:12-27; Efe. 4:16.

3. Tutazungumuzia mambo gani tatu ya maana mu hii habari?

3 Sisi wote tuko wa maana mu kutaniko la Yehova. Kwa hiyo, sisi wote tunaweza kutia nguvu kutaniko. Ikuwe tuko wa kabila gani ao tuko wa rangi gani ya ngozi, ao ikuwe tuko na feza mingi ao hapana, ikuwe tulisoma mingi ao hapana, ao ikuwe tuko wa desturi gani, sisi wote tuko wa maana mu kutaniko. Mu hii habari, tutaona mambo tatu ya maana yenye tunaweza kujifunza kupitia mufano wenye Paulo alizungumuzia. Kwanza, tutaona kama sisi wote tuko wa maana mu kutaniko la Yehova. Pili, tutaona mambo yenye tunapaswa kufanya wakati tunawaza kama hatuko wa maana mu kutaniko. Na tatu, tutaona juu ya nini tunapaswa kuendelea kutimiza daraka lenye tuko nalo mu kutaniko.

KILA MUMOJA WETU IKO NA JAMBO LA KUFANYA MU KUTANIKO

4. Waroma 12:4, 5 inatufundisha nini?

4 Jambo la kwanza lenye tunajifunza kupitia mufano wenye Paulo alizungumuzia ni hili: sisi wote tuko wa maana katika familia ya Yehova. Ku mwanzo wa mufano wake, Paulo anasema hivi: “Kama vile tuko na viungo vingi katika mwili mumoja, lakini viungo hivyo havifanye kazi ileile, ni vile sisi pia, hata kama tuko wengi, tuko mwili mumoja katika umoja na Kristo, lakini kila mumoja wetu ni kiungo cha mwingine.” (Ro. 12:4, 5) Paulo alipenda kusema nini? Alipenda kusema kuwa hata kama hatufanye mambo ileile mu kutaniko, sisi wote tuko wa maana.

Hata kama hatufanye mambo ileile mu kutaniko, sisi wote tuko wa maana (Ona fungu la 5-12) *

5. Yehova amepatia kutaniko lake “zawadi” gani?

Pengine unawazaka kama watu wenye kuwa wa maana mu kutaniko ni wale wenye kuongoza. (1 Te. 5:12; Ebr. 13:17) Kupitia Kristo, Yehova amepatia kutaniko lake “zawadi katika wanadamu.” (Efe. 4:8) Kati ya wale ndugu wenye ni “zawadi katika wanadamu” kuko ndugu wa Baraza Lenye Kuongoza, wasaidizi wao, ndugu wa Halmashauri za Tawi, waangalizi wa mizunguko, ndugu wenye kufundisha ku masomo mbalimbali mu tengenezo, wazee wa makutaniko, na pia watumishi wa huduma. Wale ndugu wote wanawekwa na roho takatifu ili kulinda kondoo wa Yehova wenye samani sana na pia ili kutia nguvu makutaniko.​—1 Pe. 5:2, 3.

6. Kulingana na 1 Watesalonike 2:6-8, ndugu wenye wanawekwa na roho takatifu wanajikaza kufanya nini?

6 Ndugu wanawekwa na roho takatifu ili kutimiza kazi mbalimbali katika tengenezo. Sehemu mbalimbali za mwili, sawa vile mikono na miguu, zinategemezaka mwili wote, ni vile pia ndugu wenye wanawekwa na roho takatifu wanategemezaka kutaniko lote. Hawako pale juu ya kutafuta utukufu. Lakini, wanajikaza kujenga na kutia nguvu ndugu na dada zao. (Soma 1 Watesalonike 2:6-8.) Tunamushukuru Yehova kwa kutupatia wale wanaume wa kiroho, wenye wanatia faida za wengine pa nafasi ya kwanza!

7. Watumishi wa wakati wote wanapata baraka gani?

7 Ndugu na dada fulani mu kutaniko wako wamisionere, mapainia wa pekee, ao mapainia wa kawaida. Wameamua kupitisha wakati mingi mu kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. Kazi yenye wanafanya inasaidia watu mingi wakuwe wanafunzi wa Kristo Yesu. Ni kweli kama wale watumishi wa wakati wote hawana vitu mingi vya kimwili, lakini Yehova anawabariki sana. (Mk. 10:29, 30) Tunawapenda sana na tunafurahi kuwa nao mu kutaniko!

8. Juu ya nini kila muhubiri wa habari njema iko wa maana kwa Yehova?

8 Tutasema kama ndugu wenye kuwa na madaraka na pia watumishi wa wakati wote, wao tu njo wako wa maana mu kutaniko? Hapana! Kila muhubiri wa habari njema iko wa maana kwa Yehova na pia mu kutaniko. (Ro. 10:15; 1 Ko. 3:6-9) Tunasema vile juu kazi moja ya maana yenye sisi wote tuko nayo mu kutaniko ni kufanya wanafunzi wa Bwana wetu Yesu Kristo. (Mt. 28:19, 20; 1 Ti. 2:4) Wahubiri wote, ikuwe walishabatizwa ao hapana, wanajikaza kutia kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza.​—Mt. 24:14.

9. Juu ya nini tunapenda sana dada zetu Wakristo?

9 Yehova anaheshimia sana dada Wakristo. Anaona bibi, mama, wajane, na dada wenye hawajaolewa, wenye wanamutumikia kwa uaminifu, kuwa wa maana sana. Biblia inazungumuzia wanamuke waaminifu wenye walimufurahisha Mungu. Biblia inawasifu sana juu walionyesha hekima, imani, bidii, uhodari, ukarimu, na matendo ya muzuri. (Lu. 8:2, 3; Mdo. 16:14, 15; Ro. 16:3, 6; Flp. 4:3; Ebr. 11:11, 31, 35) Tunamushukuru sana Yehova juu mu makutaniko yetu muko wanamuke Wakristo wenye kuonyesha zile sifa za muzuri!

10. Juu ya nini tunapenda sana ndugu na dada zetu wenye kuzeeka?

10 Tunafurahi pia kuwa na ndugu na dada wenye kuzeeka. Mu makutaniko fulani muko ndugu na dada wenye kuzeeka. Wamoja kati yao wamemutumikia Yehova kwa uaminifu maisha yao yote na wengine wangali wapya mu kweli. Wote wanaweza kuwa na magumu ya afya juu wamezeeka. Ile magumu inaweza kupunguza uwezo wao wa kufanya mambo mingi mu kutaniko ao mu kazi ya kuhubiri. Lakini wanahubiri kulingana na uwezo wao, na wanatumia nguvu yao yote ili kutia wengine moyo na kuwazoeza. Na tunajifunza mambo mingi kupitia uzoefu wao. Wako wa maana sana kwa Yehova na kwetu.​—Mez. 16:31.

11-12. Fasiria namna vijana wa kutaniko lenu wamekutia moyo.

11 Tuzungumuzie pia vijana. Wanapambana na magumu mingi kwa sababu wanakomalia mu ulimwengu wenye kutawaliwa na Shetani Ibilisi na wenye kujaa mawazo yake ya mubaya. (1 Yo. 5:19) Lakini, vijana wanatutia moyo sana wakati wanatoa maelezo ku mikutano, wanahubiri, na wakati wanatetea imani yao kwa uhodari. Kwa kweli, vijana ni wa maana sana mu kutaniko la Yehova!​—Zb. 8:2.

12 Lakini, kuko ndugu na dada fulani wenye wanawaza kama hawakuwake wa maana mu kutaniko. Ni nini inaweza kutusaidia sisi wote tusikuwe na mawazo ya vile? Acha tuone.

UKO WA MAANA MU KUTANIKO

13-14. Ni nini inaweza kufanya mutu awaze kama haiko wa maana mu kutaniko?

13 Tuone sasa jambo la pili lenye tunajifunza kupitia mufano wenye Paulo alizungumuzia. Alizungumuzia tatizo lenye watu wengi wako nalo leo; watu mingi wanawaza kama hawakuwake wa maana mu kutaniko. Paulo anasema hivi: “Kama muguu ungesema, ‘Kwa sababu mimi siko mukono, mimi siko sehemu ya mwili,’ hilo halifanye usikuwe sehemu ya mwili. Na kama sikio lingesema, ‘Kwa sababu mimi siko jicho, siko sehemu ya mwili,’ hilo halifanye lisikuwe sehemu ya mwili.” (1 Ko. 12:15, 16) Paulo alipenda kufundisha nini?

14 Wakati unaangalia uwezo wako na uwezo wa wengine, unaweza kuwaza kama hauko wa maana mu kutaniko. Kuko watu fulani mu kutaniko wenye wako na kipaji ya kufundisha, wanajua kupanga mambo muzuri, ao ni wachungaji wazuri sana. Ile inaweza kufanya uwaze kama wanakupita na kama uwezo wako uko chini sana. Haiko mubaya kuwaza vile, juu ile inaonyesha kama uko munyenyekevu na mwenye kiasi. (Flp. 2:3) Lakini ukuwe muangalifu. Kama kila wakati unazoea kulinganisha uwezo wako na uwezo wa wengine, utavunjika moyo bure. Na kama vile mutume Paulo alisema, pengine unaweza kuwaza kama hauko wa maana mu kutaniko. Sasa dawa ni nini?

15. 1 Wakorinto 12:4-11 inatusaidia kujua nini juu ya zawadi zenye tunaweza kuwa nazo?

15 Waza kidogo juu ya Wakristo fulani wa karne ya kwanza (1-100). Yehova aliwapatia zawadi za kimuujiza za roho takatifu, lakini wote hawakupata zawadi zilezile. (Soma 1 Wakorinto 12:4-11.) Hata kama Yehova aliwapatia zawadi na uwezo mbalimbali, kila Mukristo alikuwa wa maana. Leo, hakuna mutu mwenye iko na zawadi za kimuujiza za roho takatifu. Lakini wazo kubwa ni kwamba, hata kama hatuna uwezo uleule, sisi wote tuko wa maana kwa Yehova.

16. Mutume Paulo alitutolea shauri gani la muzuri?

16 Kuliko kujilinganisha na Wakristo wengine, ni muzuri tufuate shauri lenye liliongozwa na roho lenye Paulo aliandika: “Kila mutu achunguze matendo yake mwenyewe, kisha atakuwa na sababu ya kufurahi juu yake yeye mwenyewe, na hapana kwa kujilinganisha na mutu mwingine.”​—Gal. 6:4.

17. Ni faida gani tutapata kama tunafuata shauri la Paulo?

17 Kufuata shauri la Paulo na kuchunguza matendo yetu, kutatusaidia kuona kama tuko na uwezo wenye wengine hawana. Kwa mufano, pengine muzee fulani wa kutaniko hafundishake muzuri sana wakati iko ku jukwaa, lakini mu mahubiri anafundishaka muzuri kabisa. Ao pengine hajue kupanga mambo muzuri kabisa kama vile wazee wengine, lakini ni muchungaji muzuri mwenye wahubiri hawaogope kukaribia ili kupata mashauri ya Biblia. Ao pengine iko na zoezi ya kukaribisha watu kwake. (Ebr. 13:2, 16) Kujua kama wewe pia uko na uwezo fulani wenye pengine wengine hawana, kutakusaidia ufurahi kwa sababu unajua kama wewe pia unaweza kusaidia kutaniko. Ile inaweza kukusaidia usikuwe na wivu wakati unaona kama wengine wako na uwezo wenye hauna.

18. Ni nini inatusaidia tukuwe wafundishaji wazuri zaidi?

18 Hata ikuwe tuko na daraka gani mu kutaniko, sisi wote tunapaswa kujikaza kufanya maendeleo mu kazi yetu ya kuhubiri. Juu ya kufikia ile kusudi, Yehova anatupatia mazoezi ya muzuri sana kupitia tengenezo lake. Kwa mufano, ku mukutano wetu wa katikati ya juma, tunapata mazoezi yenye inatusaidia tukuwe wafundishaji wazuri zaidi. Je, unatumikishaka ile mazoezi?

19. Unaweza kufanya nini juu usome Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme?

19 Mazoezi ingine ya muzuri sana yenye tuko nayo ni Masomo kwa Ajili ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Ndugu na dada wenye kuwa mu utumishi wa wakati wote na wenye wako na miaka kati ya 23 na 65 njo wenye wanaweza kusoma ile masomo. Pengine unawaza kama hauwezi kusoma ile masomo. Kama ni vile, kuliko kufikiria sana sababu zenye zinaweza kufanya usisome ile masomo, fikiria sana sababu zenye zinafanya upende ile masomo. Kisha, fanya yako yote ili utimize mambo yenye inaombwa. Kama unafanya mambo yenye unaweza na pia kupitia musaada wa Yehova, unaweza kushangaa kuona jambo lenye lilikuwa ndoto linakuwa kweli.

TUMIA UWEZO WAKO ILI KUTIA NGUVU KUTANIKO

20. Waroma 12:6-8 inatufundisha nini?

20 Jambo la tatu lenye tunajifunza kupitia mufano wenye Paulo alizungumuzia liko mu Waroma 12:6-8. (Soma.) Mara ingine tena Paulo anaonyesha kama kila mutu mu kutaniko iko na uwezo wake. Lakini sasa anakazia wazo ingine. Anasema kama kila mutu anapaswa kutumia uwezo wenye iko nao ili kutia nguvu kutaniko.

21-22. Mambo yenye ilimufikia Robert na Felice inaweza kutufundisha nini?

21 Fikiria mufano wa ndugu mwenye tutaita Robert. Kisha kutumikia mu inchi ingine, alipewa mugao wa kutumikia ku Beteli, mu inchi yao. Ndugu walimuhakikishia kama hakuna kosa lenye alifanya juu mugao wake ubadilike. Lakini alisema hivi: “Kwa miezi mingi sikukuwa na furaha juu niliwaza kama nilishindwa mu mugao wangu wa mbele. Na wakati fulani nilianza kuwa na mawazo ya kutoka ku Beteli.” Ni nini ilimusaidia akuwe tena na furaha? Ndugu mumoja mwenye ni muzee wa kutaniko kama yeye, alimukumbusha kama mazoezi yenye Yehova alimupatiaka mu mugao wake wa zamani haikukuwa ya bure, na kama ingeweza kumusaidia sana hata mu mugao wake wa sasa. Robert alielewa kama alipaswa kuacha kuwaza sana juu ya mambo ya zamani lakini alipaswa kukaza akili juu ya mambo yenye angeweza kufanya sasa.

22 Hali ya kufanana na ile ilimufikia pia ndugu Felice Episcopo. Yeye na bibi yake walisoma masomo ya Gileadi mu mwaka wa 1956 na walifanya kazi ya muzunguko mu inchi ya Bolivia. Mu mwaka wa 1964 walipata mutoto. Felice alisema hivi: “Ilikuwa nguvu kuacha mugao wetu wenye tulipenda sana. Kusema kweli, nilifanya karibu mwaka muzima na niko mwenye kuvunjika moyo. Lakini Yehova alinisaidia nibadilishe mawazo yangu na nijikaze kutimiza daraka langu la kuwa muzazi.” Hali yako inafanana na ya Robert ao ya Felice? Ulishavunjika moyo juu hauna tena mapendeleo ya utumishi yenye ulikuwaka nayo zamani? Kama ni vile, badilisha mawazo yako na ukaze akili juu ya mambo yenye unaweza kufanyia ndugu na dada zako kwa sasa. Ukifanya vile, utakuwa na furaha sana. Kwa hiyo, ukuwe na mambo mingi ya kufanya mu kazi ya Yehova, utumie uwezo wako ili kusaidia wengine, na ujue kama utapata furaha wakati unaendelea kutia nguvu kutaniko.

23. Unapaswa kufikiri sana juu ya mambo gani, na tutazungumuzia nini mu habari yenye kufuata?

23 Sisi wote tuko wa maana kwa Yehova. Anapenda tuendelee kuwa mu familia yake. Kama unafikiri sana juu ya mambo yenye unaweza kufanya ili kutia nguvu ndugu na dada na kama unajikaza kufanya vile, ile itakusaidia usijione kuwa hauko wa maana mu kutaniko! Sasa, tuseme nini juu ya mawazo yenye unakuwaka nayo juu ya wengine mu kutaniko? Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama unawaheshimia na kuwapenda? Tutazungumuzia ile maulizo mu habari yenye kufuata.

WIMBO 24 Njooni Kwenye Mlima wa Yehova

^ fu. 5 Sisi wote tunapenda Yehova atuone kuwa wa maana. Lakini wakati fulani tunaweza kujiuliza kama kweli tuko wa maana. Habari hii itatusaidia tuelewe kama kila mutu iko wa maana mu kutaniko.

^ fu. 61 MAFASIRIO YA PICHA: Picha tatu zenye kuonyesha mambo yenye kufanyika mbele ya mukutano, wakati wa mukutano, na kisha mukutano. Picha ya 1: Muzee mumoja wa kutaniko anasalimia mugeni kwa uchangamufu, ndugu mumoja kijana anatayarisha vifaa vya sauti, na dada mumoja iko anaongea na dada mwenye kuzeeka. Picha ya 2: Vijana na watu wakubwa wanainua mikono yao ili kujibu wakati wa Funzo la Munara wa Mulinzi. Picha ya 3: Bibi na bwana wanasaidia kusafisha Jumba la Ufalme. Mama anasaidia mutoto wake atie feza mu kisanduku cha michango. Ndugu mumoja kijana iko anapanga vichapo, na ndugu mwingine iko anatia moyo dada mwenye kuzeeka.