Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 32

Utembee kwa Unyenyekevu na kwa Kiasi Pamoja na Mungu Wako

Utembee kwa Unyenyekevu na kwa Kiasi Pamoja na Mungu Wako

“Utembee kwa kiasi pamoja na Mungu wako!”​—MIK. 6:8.

WIMBO 31 Tembea Pamoja na Mungu!

KIFUPI CHA HABARI *

1. Daudi alisema nini juu ya unyenyekevu wa Yehova?

TUNAWEZA kusema kama Yehova ni munyenyekevu? Ndiyo. Wakati fulani Daudi alisema hivi: “Unanipatia ngao yako ya wokovu, na unyenyekevu wako unanifanya nikuwe mukubwa.” (2 Sa. 22:36; Zb. 18:35) Wakati Daudi alisema vile, pengine alikuwa anakumbuka siku nabii Samweli alikuja kwao ili kutia mafuta mwenye angekuwa mufalme wa Israeli. Baba ya Daudi alikuwa na watoto wanaume munane, na Daudi njo alikuwa mudogo zaidi kati yao. Lakini, yeye njo Yehova alichagua ili akamate nafasi ya Mufalme Sauli.​—1 Sa. 16:1, 10-13.

2. Tutajifunza nini katika habari hii?

2 Bila shaka Daudi alikubaliana na mawazo ya muandikaji wa zaburi ya 113, mwenye alisema: “Anainama ili aangalie mbingu na dunia, anainua mutu wa hali ya chini kutoka katika mavumbi. Anainua maskini . . . ili kumufanya akae pamoja na watu wenye vyeo.” (Zb. 113:6-8) Katika habari hii, tutajifunza kwanza mambo fulani ya maana kuhusu sifa ya unyenyekevu kwa kuchunguza namna Yehova alionyesha ile sifa katika hali mbalimbali. Kisha, tutaona mambo yenye mufano wa Mufalme Sauli, nabii Danieli, na Yesu unatufundisha kuhusu sifa ya kiasi.

MUFANO WA YEHOVA UNAWEZA KUTUFUNDISHA NINI?

3. Yehova anatutendea namna gani, na ile inaonyesha nini?

3 Namna Yehova anatendea watumishi wake wenye hawakamilike inaonyesha kama iko munyenyekevu. Anakubali ibada yetu na anatuona kuwa marafiki wake. (Zb. 25:14) Ili tuweze kuwa marafiki wake, Yehova alimutoa Mwana wake akufe kwa ajili ya zambi zetu. Ile inaonyesha kama Yehova iko na huruma sana.

4. Yehova alitupatia nini, na juu ya nini?

4 Fikiria jambo lingine lenye linaonyesha kama Yehova ni munyenyekevu. Yehova angependa, angetuumba bila uhuru wa kujichagulia mambo yenye tutafanya mu maisha yetu. Lakini hakufanya vile. Alituumba kwa mufano wake na alitupatia uhuru wa kuchagua. Hata kama sisi wanadamu tuko wa hali ya chini sana, Yehova anapenda tuchague sisi wenyewe kumutumikia. Na anapenda tufanye vile juu tunamupenda na juu tunajua faida za kumutii. (Kum. 10:12; Isa. 48:17, 18) Tunapaswa kumushukuru Yehova sana kwa sababu iko munyenyekevu!

Picha yenye kuonyesha Yesu akiwa mbinguni. Pembeni yake kuko wamoja kati ya wale wenye watatawala pamoja naye. Wote wako wanaangalia malaika wengi. Malaika fulani wako wanaenda ku dunia ili kufanya kazi yenye walipewa. Yehova amepatia mamlaka wote wenye kuwa kwenye hii picha (Ona fungu la 5)

5. Namna gani Yehova anatufundisha unyenyekevu? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

5 Yehova anatufundisha unyenyekevu kupitia namna anatutendea. Yehova njo Mutu mwenye hekima zaidi katika ulimwengu wote. Hata vile, iko tayari kukubali mawazo ya wengine. Kwa mufano, Yehova alimuruhusu Mwana wake atumike naye mu kazi ya kuumba vitu vyote. (Mez. 8:27-30; Kol. 1:15, 16) Na hata kama Yehova ni Mweza-Yote, anapatiaka wengine mamlaka fulani. Kwa mufano, alimuweka Yesu kuwa Mufalme wa Ufalme wake, na atapatia mamlaka fulani wale 144 000 wenye watatawala na Yesu. (Lu. 12:32) Yehova alimuzoeza Yesu ili akuwe Mufalme na Kuhani Mukubwa. (Ebr. 5:8, 9) Anazoeza pia wale wenye watatawala na Yesu, lakini hatakuwa anafuatilia-fuatilia ao kuchunguza-chunguza kazi yao. Kuliko kufanya vile, anawatumainia na anajua kama watafanya kazi yao muzuri.​—Ufu. 5:10.

Tunamuiga Yehova wakati tunazoeza wengine na kuwapatia kazi (Ona fungu la 6-7) *

6-7. Yehova anapatiaka wengine mamlaka fulani, ile inatufundisha nini?

6 Baba yetu wa mbinguni, mwenye hana lazima ya musaada wa mutu yeyote, anapatiaka wengine mamlaka fulani. Unawaza sisi tuko na sababu ya kukosa kufanya vile? Kwa mufano, uko kichwa cha familia ao muzee mu kutaniko? Kama ni vile, fuata mufano wa Yehova; patia wengine kazi na uepuke kufuatilia-fuatilia ao kuchunguza-chunguza namna wanaifanya. Kama unafuata mufano wa Yehova, kazi itafanywa muzuri, utazoeza wengine, na utawasaidia wakuwe hakika kama wao pia wanaweza kufanya kazi muzuri. (Isa. 41:10) Mufano wa Yehova unaweza kufundisha wale wenye wako na mamlaka fulani jambo gani lingine?

7 Biblia inaonyesha kama wakati fulani Yehova anapendaka kujua mawazo ya malaika zake. (1 Fa. 22:19-22) Wazazi, namna gani munaweza kufuata mufano wa Yehova? Wakati fulani, kama ni lazima, muulize watoto wenu kama wanapenda kazi fulani ifanywe namna gani. Na kama munaona mawazo yao inafaa, muifuate.

8. Namna gani Yehova alionyesha Abrahamu na Sara uvumilivu?

8 Jambo lingine pia lenye linaonyesha kama Yehova ni munyenyekevu ni uvumilivu wake. Kwa mufano, Yehova anavumilia watumishi wake wakati, kwa heshima, wanatilia mashaka maamuzi yake. Alisikiliza kwa uvumilivu wakati Abrahamu alimuambia mashaka yenye alikuwa nayo kuhusu uamuzi wake wa kuharibu Sodoma na Gomora. (Mwa. 18:22-33) Fikiria pia namna Yehova alimutendea Sara, bibi ya Abrahamu. Sara alicheka wakati Yehova alisema kama atapata mimba mu miaka ya uzee, lakini Yehova hakumukasirikia. (Mwa. 18:10-14) Kuliko kufanya vile, alimutendea Sara kwa heshima.

9. Wazazi na wazee wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Yehova?

9 Wazazi na wazee, mufano wa Yehova unaweza kuwafundisha nini? Fikiria namna unatendaka wakati watoto wako ao ndugu na dada katika kutaniko wanatilia mashaka maamuzi yako. Jambo la kwanza lenye unafanyaka ni kujitetea na kujaribu kuwaonyesha kama wao njo hawaelewe? Ao unajikazaka kuelewa mawazo yao? Wakati wazazi na wazee wanafuata mufano wa Yehova, ile inasaidia familia na kutaniko ikuwe na furaha. Mupaka hapa, tumeona mambo yenye inaonyesha kama Yehova ni munyenyekevu na namna tunaweza kumuiga. Tuone sasa mambo yenye mifano fulani yenye kuwa mu Biblia inaweza kutufundisha kuhusu sifa ya kiasi.

MIFANO YA WENGINE INAWEZA KUTUFUNDISHA NINI?

10. Namna gani Yehova anatumia mifano ya wengine ili kutufundisha?

10 Yehova, “Mufundishaji [wetu] Mukubwa,” aliandikisha mifano mingi katika Neno lake ili kutufundisha. (Isa. 30:20, 21) Tunajifunza mambo mingi wakati tunafikiri sana juu ya habari za Biblia za watu wenye walionyesha sifa za muzuri, kama vile sifa ya kiasi. Tunajifunza pia mambo mingi wakati tunachunguza mambo yenye ilipata wale wenye hawakuonyesha zile sifa za muzuri.​—Zb. 37:37; 1 Ko. 10:11.

11. Mufano mubaya wa Sauli unatufundisha nini?

11 Fikiria mufano wa Mufalme Sauli. Wakati alikuwa kijana, alikuwa na kiasi. Alijua mipaka yake na hata aliogopa kukubali madaraka. (1 Sa. 9:21; 10:20-22) Lakini, wakati fulani kisha Sauli kuwa mufalme, alianza kuwa na kimbelembele. Wakati fulani, Sauli alikuwa anangojea nabii Samweli akuje kutoa zabihu. Kuliko kuonyesha kiasi na kutumaini kama Yehova atatenda kwa ajili ya watu wake, Sauli alikosa uvumilivu na akatoa zabihu ya kuteketezwa hata kama hakukuwa na ruhusa ya kufanya vile. Kwa hiyo, Yehova hakumukubali tena na hangeendelea tena kuwa mufalme. (1 Sa. 13:8-14) Ile habari inatufundisha kama tunapaswa kuepuka kimbelembele.

12. Namna gani Danieli alionyesha sifa ya kiasi?

12 Tofauti na mufano mubaya wa Sauli, fikiria mufano muzuri wa nabii Danieli. Mu maisha yake yote, Danieli aliendelea kuwa munyenyekevu na mwenye kiasi kwa kutafuta kila mara muongozo wa Yehova. Kwa mufano, wakati Yehova alimutumia ili kufasiria ndoto ya Nebukadneza, Danieli hakusema kama ile mafasirio ilikuwa yake. Lakini, alionyesha kiasi kwa kumupatia Yehova utukufu. (Da. 2:26-28) Ile inatufundisha nini? Kama ndugu wanafurahiaka hotuba zetu na kama tuko tunapata matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri, tunapaswa kumupatia Yehova utukufu. Tunapaswa kuonyesha kiasi kwa kukubali kama hatuwezi kutimiza ile mambo bila musaada wa Yehova. (Flp. 4:13) Wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko tunaiga pia mufano wa Yesu. Juu ya nini tunasema vile?

13. Namna gani Yohana 5:19, 30 inaonyesha kama Yesu alikuwa na kiasi?

13 Hata kama Yesu alikuwa Mwana mukamilifu wa Yehova, alikuwa anamutegemea. (Soma Yohana 5:19, 30.) Hakujaribu hata siku moja kunyanganya mamlaka ya Baba yake wa mbinguni. Wafilipi 2:6 inasema kama Yesu “hakufikiria kuchukua nafasi ya Mungu, ni kusema, kwamba yeye akuwe sawa na Mungu.” Kwa sababu Yesu alikuwa na kiasi, alijua mipaka yake na aliheshimia mamlaka ya Baba yake.

Yesu alijua mipaka yake na aliiheshimia (Ona fungu la 14)

14. Yesu alifanya nini wakati walimuomba jambo lenye hakukuwa na mamlaka ya kufanya?

14 Fikiria jambo lenye Yesu alifanya wakati mama ya Yakobo na Yohana alikuja kumuomba apatie watoto wake pendeleo lenye Yesu hakukuwa na mamlaka ya kupana. Bila kuenda huku na huku, Yesu alimuambia kama ni Baba yake wa mbinguni tu njo iko na mamlaka ya kuamua nani njo atakaa ku mukono wa kuume ao wa kushoto wa Yesu katika Ufalme. (Mt. 20:20-23) Yesu alionyesha kama aliheshimia mipaka yake. Alikuwa na kiasi. Hakufanya hata siku moja mambo yenye Yehova hakumupatia mamlaka ya kufanya. (Yoh. 12:49) Namna gani tunaweza kufuata mufano wa Yesu?

Yesu alikuwa na kiasi. Namna gani tunaweza kuiga mufano wake? (Ona fungu la 15-16) *

15-16. Namna gani tunaweza kutumikisha shauri la Biblia lenye kuwa katika 1 Wakorinto 4:6?

15 Tunafuata mufano wa Yesu wakati tunatii shauri la Biblia lenye kuwa katika 1 Wakorinto 4:6. Ile andiko inasema hivi: “Musipite mambo yenye yaliandikwa.” Kwa hiyo wakati mutu anatuomba shauri, hatupaswe kumujibia bila kufikiri ao kumujibia kulingana na mawazo yetu. Kuliko kufanya vile, tunapaswa kumuonyesha mashauri yenye kuwa mu Biblia ao mu vichapo vyetu. Kama tunafanya vile, tunaonyesha kama tunajua mipaka yetu. Kwa sababu tuko na kiasi, tunaelewa kama mashauri ya Yehova njo ya muzuri kuliko mawazo yetu.​—Ufu. 15:3, 4.

16 Tunaonyesha sifa ya kiasi kwa sababu tunapenda kumutukuza Yehova. Lakini, kuko sababu zingine zenye zinatuchochea kuwa na kiasi na unyenyekevu. Tuone sasa namna zile sifa zinaweza kutuletea furaha na kutusaidia tuishi kwa amani na wengine.

FAIDA ZA KUWA NA SIFA YA UNYENYEKEVU NA YA KIASI

17. Juu ya nini watu wenye kuwa na unyenyekevu na kiasi wanakuwaka na furaha?

17 Kuwa na sifa ya unyenyekevu na ya kiasi kunatusaidia tukuwe na furaha. Juu ya nini tunasema vile? Kama tunajua mipaka yetu, tutakubali musaada wowote wenye wengine wanatupatia. Kwa mufano, fikiria wakati Yesu aliponyesha watu kumi wenye walikuwa na ukoma. Ni mumoja tu njo alirudia ili kumushukuru juu alimuponyesha ule ugonjwa mubaya sana wenye hakuna mwanadamu angeweza kuponyesha. Kwa sababu alikuwa na unyenyekevu na kiasi, ule mwanaume alionyesha shukrani kwa ajili ya musaada wenye alipata na alimutukuza Mungu.​—Lu. 17:11-19.

18. Juu ya nini kuwa na sifa ya unyenyekevu na ya kiasi kunatusaidia tuishi kwa amani na wengine? (Waroma 12:10)

18 Kuwa na sifa ya unyenyekevu na ya kiasi kunatusaidia tuishi kwa amani na wengine na tupate marafiki wa sana. Juu ya nini? Juu kama tuko na zile sifa, tutakubali kama wengine pia wako na sifa za muzuri na tutawatumainia. Mutu munyenyekevu na mwenye kiasi anafurahiaka wakati wengine wanatimiza muzuri migao yao na iko tayari kuwapongeza na kuwaonyesha heshima.​—Soma Waroma 12:10.

19. Sababu gani tunapaswa kuepuka kiburi?

19 Tofauti na ile, mutu mwenye kuwa na kiburi anashindwaka kupongeza wengine, anapendaka wengine tu njo wamupongeze. Anapendaka kujilinganisha na wengine na kuchochea roho ya kushindana. Kuliko kuzoeza wengine na kuwapatia madaraka, anawazaka kama wengine hawawezi kufanya jambo fulani muzuri, yeye tu njo anaweza. Mutu mwenye kiburi anapendaka kuwa wa maana kuliko wengine na anasikiaka wivu wakati wengine wanafanya mambo muzuri zaidi kuliko yeye. (Gal. 5:26) Mara mingi urafiki na mutu wa vile haukawiake. Kama tunatambua kuwa tuko na kiburi, tunapaswa kumulilia Yehova atusaidie ‘kufanya upya akili yetu’ kusudi ile tabia ya mubaya isikomae ndani yetu.​—Ro. 12:2.

20. Juu ya nini tunapaswa kuwa wanyenyekevu na wenye kiasi?

20 Tuko na furaha sana kwa sababu Yehova ni munyenyekevu! Tunaona kama Yehova ni munyenyekevu kupitia namna anatendea watumishi wake, na tunapenda kumuiga. Tena, tunapenda kuiga mifano ya muzuri yenye kuwa katika Biblia ya watu wenye kiasi wenye walitembea pamoja na Mungu. Tujikaze kila siku kumupatia Yehova heshima na utukufu wenye anastahili. (Ufu. 4:11) Kama tunafanya vile, tutaendelea kutembea pamoja na Baba yetu wa mbinguni, kwa sababu anapendaka watu wanyenyekevu na wenye kiasi.

WIMBO 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu

^ fu. 5 Mutu munyenyekevu anasikiliaka wengine huruma. Yehova anasikiliaka wengine huruma, njo maana tunaweza kusema kama iko munyenyekevu. Katika habari hii, tutaona namna mufano wa Yehova unaweza kutusaidia tukuwe wanyenyekevu. Tutaona pia mambo yenye mufano wa Mufalme Sauli, nabii Danieli, na Yesu unatufundisha kuhusu sifa ya kiasi.

^ fu. 58 MAFASIRIO YA PICHA: Muzee anazoeza ndugu kijana ili ajue namna ya kushugulikia maeneo ya kutaniko. Kisha, ule muzee hamufuatilie-fuatilie ao kumuchunguza-chunguza. Lakini, anamuacha atimize mugao wake yeye mwenyewe.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Dada anauliza muzee kama inafaa kukubali mualiko wa kuhuzuria ndoa yenye itafanyika mu kanisa. Muzee hamujibie kulingana na mawazo yake lakini anamuonyesha kanuni fulani za Biblia.