Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Endelea Kuonyesha Upendo—Upendo Unajenga

Endelea Kuonyesha Upendo—Upendo Unajenga

“Upendo unajenga.”​—1 KO. 8:1.

NYIMBO: 109, 121

1. Yesu alizungumuzia jambo gani la maana katika usiku wa mwisho wenye alipitisha pamoja na wanafunzi wake?

KATIKA usiku wa mwisho wenye Yesu alipitisha pamoja na wanafunzi wake mbele akufe, alitaja upendo karibu mara 30. Aliambia wanafunzi wake kama walipaswa ‘kupendana.’ (Yoh. 15:12, 17) Upendo wao ungeonekana wazi na kwa hiyo wengine wangeona jambo hilo na kutambua kama wao ni wanafunzi wa kweli wa Yesu. (Yoh. 13:34, 35) Upendo wenye Yesu alizungumuzia haiko namna mutu anajisikia tu, ni sifa ya kujitoa kwa ajili ya wengine na yenye kuwa nguvu sana. Yesu alisema hivi: “Hakuna mwenye iko na upendo mukubwa kuliko huu, kwamba mutu atoe uzima wake kwa ajili ya marafiki wake. Ninyi ni marafiki wangu kama munafanya mambo yenye ninawaamuru.”​—Yoh. 15:13, 14.

2. (a) Leo, watumishi wa Mungu wanajulikana kupitia sifa gani? (b) Tutajibu maulizo gani katika habari hii?

2 Leo, watumishi wa Yehova wanajulikana juu ya upendo wao wa kweli na wa kujitoa kwa ajili ya wengine na umoja wao wenye nguvu. (1 Yo. 3:10, 11) Hatuangalie inchi ao kabila, luga yenye tunazungumuza, mahali kwenye tunatoka, ao namna tulikomaa. Katika dunia yote, watumishi wa Yehova wanapendana kabisa. Juu ya nini upendo ni wa maana sana leo? Namna gani Yehova na Yesu wanatujenga kupitia upendo? Na namna gani tunaweza kuonyesha upendo huo kusudi tufariji wengine na kuwatia nguvu?​—1 Ko. 8:1.

JUU YA NINI UPENDO NI WA MAANA SANA LEO?

3. ‘Nyakati hizi za hatari’ zinafanya watu wajisikie namna gani?

3 Tunaishi katika “nyakati za hatari,” na maisha “imejaa taabu na huzuni.” (2 Ti. 3:1-5; Zb. 90:10) Watu wengi wanateseka sana mupaka wanajisikia kama wamechoka. Watu zaidi ya 800 000 wanajiua kila mwaka, ni kusema, mutu mumoja anajiua kila segonde 40. Jambo la kuhuzunisha ni hili: hata ndugu na dada zetu fulani wamepata mawazo kama hayo na wamejiua wenyewe.

4. Ni watu gani wenye kuzungumuziwa mu Biblia wenye wakati fulani walijisikia kama wanapenda kufa?

4 Wakati wa zamani, watumishi fulani waaminifu wa Mungu walijisikia mubaya sana juu ya magumu yao mupaka wakapenda wakufe. Kwa mufano, Yobu alikuwa na magumu kama hayo, kwa hiyo, akasema hivi: “Ninachukia maisha yangu; sitaki kuendelea kuishi.” (Yob. 7:16; 14:13) Yona alijisikia kuwa mwenye kuvunjika moyo sana mupaka akasema hivi: “Sasa, Ee Yehova, tafazali ondoa uzima wangu, kwa sababu afazali nikufe kuliko kuishi.” (Yon. 4:3) Nabii Eliya alijisikia kuwa mwenye kukosa tumaini kabisa mupaka akasema hivi: “Imetosha! Sasa, Ee Yehova, ondoa uzima wangu.” (1 Fa. 19:4) Lakini, Yehova alipenda sana watumishi hao waaminifu na alitaka waendelee kuishi. Hakuwalaamu juu walijisikia vile. Lakini, aliwasaidia wakuwe tena na tamaa ya kuishi kusudi waendelee kumutumikia kwa uaminifu.

5. Leo, juu ya nini ndugu na dada zetu wako na lazima tuwaonyeshe upendo?

5 Leo, ndugu na dada zetu wengi wanapiganisha hali zenye kuleta mahangaiko na wako na lazima tuwaonyeshe upendo. Wengine wanachekelewa ao kuteswa. Wengine wanapaswa kuvumilia wakati wanachokozwa ao kusemwa mubaya kwenye nafasi yao ya kazi. Ao wanachoka juu wanapaswa kutumika saa nyingi ao wanafanya kazi zenye kuleta mahangaiko sana. Na wengine wako na magumu mazito mu familia. Pengine wako na bibi ao bwana wenye hawatumikie Yehova na wenye kuwachambua-chambua kila wakati. Juu ya magumu kama hayo na magumu mengine, wengi wanajisikia kuwa hawana nguvu tena na wanaweza hata kuanza kujiona kuwa hawako watu wa maana. Ni nani anaweza kuwasaidia?

UPENDO WA YEHOVA UNATUTIA NGUVU

6. Namna gani upendo wa Yehova unatia nguvu watumishi wake?

6 Yehova anahakikishia watumishi wake kama anawapenda sasa na ataendelea kuwapenda milele. Wazia namna Waisraeli walijisikia wakati Yehova aliwaambia hivi: “Ulikuwa mwenye samani [ao, wa maana sana] mbele ya macho yangu, uliheshimiwa, na nimekupenda,” na “Usiogope, kwa maana niko pamoja na wewe”! (Isa. 43:4, 5) Tunajua kama Yehova anamuona kila mutu kati yetu kuwa wa samani. * (Ona maelezo ya chini.) Biblia inaahidi hivi: “Atakuokoa kwa kuwa ni Mwenye nguvu. Atashangilia kwa sababu yako kwa sauti za furaha.”​—Sef. 3:16, 17.

7. Namna gani upendo wa Yehova uko kama upendo wa mama mwenye kunyonyesha? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

7 Yehova anaahidi kama atatia nguvu watu wake na kuwafariji hata wapate magumu gani. Alisema hivi: “Mutanyonya na kubebwa kwenye kiuno, na mutachezeshwa kwenye magoti. Kama vile mama anamufariji mwana wake, ni vile nitaendelea kuwafariji.” (Isa. 66:12, 13) Wazia namna mutoto anajisikiaka salama wakati mama yake anamubeba ao wakati anacheza naye! Yehova anakupenda sana na anataka ujisikie salama. Ukuwe hakika kabisa kama Yehova anakuona kuwa wa maana.​—Yer. 31:3.

8, 9. Namna gani upendo wa Yesu unaweza kututia nguvu?

8 Ona sababu ingine yenye kuonyesha kama Yehova anatupenda: “Mungu alipenda ulimwengu sana na hivyo akamutoa Mwana wake muzaliwa-pekee, ili kila mutu mwenye anamuamini asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yoh. 3:16) Zabihu ya Yesu inaonyesha kama naye anatupenda, na upendo wake unatutia nguvu. Biblia inasema kama hata “taabu ao mahangaiko” haviwezi ‘kututenganisha na upendo wa Kristo.’​—Ro. 8:35, 38, 39.

9 Wakati fulani, tunapata magumu yenye kufanya mwili ao akili yetu ikuwe zaifu ao yenye kutufanya tupoteze furaha ya kumutumikia Yehova. Lakini, kukumbuka kama Kristo anatupenda sana kunaweza kutupatia nguvu ya kuvumilia. (Soma 2 Wakorinto 5:14, 15.) Upendo wa Yesu unatupatia tamaa ya kuendelea kuishi na kumutumikia Yehova. Unaweza kutusaidia kusudi tusichoke, hata kama tunasumbuka kwa sababu ya misiba, mateso, mambo yenye kuvunja moyo, ao mahangaiko.

NDUGU ZETU WAKO NA LAZIMA TUWAONYESHE UPENDO

Kujifunza mufano wa Yesu kunaweza kukuchochea utie wengine moyo (Picha hizi zinapatana na fungu la 10, 11)

10, 11. Ni nani wako na daraka la kujenga ndugu na dada wenye kuvunjika moyo? Fasiria.

10 Yehova anatumia pia kutaniko ili kutujenga kupitia upendo wake. Wakati tunapenda ndugu na dada zetu, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova. Tunafanya kila jambo lenye tunaweza kusudi tusaidie ndugu na dada zetu wajue kama wako wa maana na kama Yehova anawapenda. (1 Yo. 4:19-21) Mutume Paulo aliandika hivi: “Muendelee kutiana moyo na kujengana, kama vile muko munafanya.” (1 Te. 5:11) Hiyo haiko tu kazi ya wazee. Kila mutu kati yetu anaweza kumuiga Yehova na Yesu kwa kufariji ndugu na dada zetu.​—Soma Waroma 15:1, 2.

11 Wengine mu kutaniko wenye wanateseka juu ya kushuka moyo sana ao juu ya mahangaiko wanaweza kuwa na lazima ya kuonana na wanganga kusudi wapate matunzo. (Lu. 5:31) Wazee na ndugu wengine mu kutaniko wanajua kwamba, hata kama hawana mazoezi ya kinganga, musaada na faraja yenye wanatoa ni vya maana. Watu wote mu kutaniko wanaweza ‘kusema kwa namna yenye kufariji wale wenye wameshuka moyo, kusaidia wazaifu, kuwa wavumilivu kwa watu wote.’ (1 Te. 5:14) Tunapenda kujikaza kuelewa namna ndugu zetu wanajisikia. Tunapaswa kuwaonyesha uvumilivu na kusema kwa njia yenye itawafariji wakati wanavunjika moyo. Unajikaza kuwatia nguvu? Unaweza kufanya nini kusudi ukuwe mwenye kufariji na kutia moyo zaidi?

12. Namna gani upendo wa ndugu na dada mu kutaniko ulitia Mukristo fulani moyo? Leta mufano.

12 Dada mumoja wa Ulaya alisema hivi: “Wakati fulani ninakuwa na mawazo ya kujiua, lakini niko na musaada. Ndugu na dada wa kutaniko langu wameokoa uzima wangu. Sikuzote wananitia moyo sana na kunionyesha upendo. Hata kama wengi hawajue kama niko na ugonjwa wa kushuka moyo, kutaniko linanisaidia sikuzote. Bwana mumoja na bibi yake wako kama wazazi wangu wa kiroho. Wananihangaikia na wako tayari kunisaidia wakati wote.” Kwa kweli, watu wote hawawezi kutoa musaada kwa kadiri ileile. Lakini sisi wote tunaweza kufanya mambo mengi ili kusaidia ndugu na dada zetu. * (Ona maelezo ya chini.)

NAMNA YA KUJENGA WENGINE KUPITIA UPENDO WETU

13. Tunapaswa kufanya nini kusudi tufariji wengine?

13 Ukuwe musikilizaji muzuri. (Yak. 1:19) Tunaonyesha upendo wakati tunasikiliza kwa huruma. Uliza maulizo yenye yanaweza kukusaidia uelewe namna ndugu ao dada yako anajisikia. Atajua ikiwa unamuhangaikia kabisa, hata kupitia ishara za uso wako. Wakati iko anaongea, ukuwe na uvumilivu na umuache ajieleze bila kumukatiza. Kama uko musikilizaji muzuri, unaweza kumuelewa muzuri na unaweza kumusaidia akutumainie. Hilo litamusaidia akuwe tayari kusikiliza mambo yenye unasema wakati unajikaza kumusaidia. Wakati unawahangaikia wengine kabisa, unaweza kuwafariji muzuri.

14. Juu ya nini hatupaswe kuchambua-chambua mutu mwenye kushuka moyo?

14 Usimuchambue-chambue. Mutu mwenye kushuka moyo atajisikia mubaya zaidi kama anaona kuwa tunamuchambua-chambua. Hilo linaweza kufanya ikuwe nguvu sana kwetu kumusaidia. “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.” (Mez. 12:18) Hata kama hatuwezi hata kidogo kuumiza kimakusudi kupitia maneno yetu mutu mwenye ameshuka moyo, tunaweza kumuumiza kabisa wakati tunasema bila kufikiri. Kusudi tutie ndugu ao dada yetu moyo, tunapaswa kumufanya aone kabisa kama tunajikaza kuelewa hali yake.​—Mt. 7:12.

15. Tunaweza kutumikisha vyombo gani vya maana kusudi tufariji wengine?

15 Tumikisha Neno la Mungu juu ya kufariji wengine. (Soma Waroma 15:4, 5.) Biblia inatoka kwa “Mungu mwenye anatoa uvumilivu na faraja,” kwa hiyo, hatuwezi kushangaa kuona kama maneno yenye kuwa mu Biblia yanatufariji sana. Tuko pia na Index des publications des Témoins de Jéhovah na kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova. Wakati tunatumia vyombo hivyo, tunaweza kupata maandiko na vichapo vyenye tunaweza kutumikisha kusudi tufariji na kutia moyo ndugu na dada zetu.

16. Ni sifa gani zinaweza kutusaidia kutia moyo mutu fulani mwenye kushuka moyo?

16 Ukuwe mwenye huruma na mupole. Yehova iko “Baba wa rehema nyingi na Mungu wa faraja yote,” na iko na “huruma nyingi” kuelekea watumishi wake. (Soma 2 Wakorinto 1:3-6; Lu. 1:78; Ro. 15:13) Paulo alionyesha mufano muzuri juu ya jambo hilo kwa sababu alimuiga Yehova. Aliandika hivi: “Tulikuwa wapole katikati yenu, kama vile wakati mama mwenye kunyonyesha anahangaikia kwa upendo watoto wake mwenyewe. Basi, kwa kuwa tulikuwa na upendo wenye upole kuwaelekea ninyi, hatukupenda tu kuwapatia ninyi habari njema ya Mungu, lakini pia tulipenda kuwapatia uzima wetu wenyewe, kwa sababu mulikuwa wapendwa sana kwetu.” (1 Te. 2:7, 8) Wakati tuko wenye huruma kama Yehova, tunaweza kumutolea ndugu ao dada yetu faraja yenye iko anaomba Yehova katika sala!

17. Tunapaswa kuwa na mawazo gani yenye usawaziko juu ya ndugu na dada zetu kusudi tuwatie moyo?

17 Usitazamie ndugu na dada zako wakuwe wakamilifu. Ukuwe na usawaziko. Kama unatazamia ndugu na dada zako wakuwe wakamilifu, utavunjika moyo. (Muh. 7:21, 22) Kumbuka kama Yehova anaonyesha usawaziko katika mambo yenye anatuomba. Kwa hiyo, tunapaswa kuvumiliana. (Efe. 4:2, 32) Hatupendi hata kidogo kufanya ndugu ao dada zetu wajisikie kuwa hawafanye mengi na hatupendi kuwalinganisha na wengine. Lakini, tunawatia moyo na kukaza akili juu ya mambo ya muzuri yenye wanafanya. Kufanya vile kutawasaidia wakuwe na furaha wakati wanaendelea kumutumikia Yehova.​—Gal. 6:4.

18. Juu ya nini tunapenda kujenga wengine kupitia upendo?

18 Yehova na Yesu wanaona kila mutu kati yetu kuwa wa maana. (Gal. 2:20) Tunapenda sana ndugu na dada zetu, kwa hiyo, tunapaswa kuwatendea kwa upole. ‘Tunafuatilia mambo yenye yanafanya kukuwe amani na mambo ya kujengana mumoja na mwingine.’ (Ro. 14:19) Tunangojea sana maisha mu Paradiso, wakati huo, hakuna mutu mwenye atakuwa na sababu ya kuvunjika moyo! Hakutakuwa tena magonjwa na vita. Watu hawatakufa tena juu ya zambi yenye tuliriti, na hakutakuwa mateso, magumu ya familia, ao mambo yenye kuvunja moyo mu maisha. Ku mwisho wa miaka elfu, wanadamu wote watakuwa wakamilifu. Wale wenye watabakia waaminifu wakati wa jaribu la mwisho, Yehova atawafanya kuwa wana wake ku dunia na watakuwa na “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Ro. 8:21) Basi, sisi wote tuonyeshe upendo wenye kujenga na tusaidiane kusudi tuokoke na kuingia mu dunia mupya ya Mungu ya muzuri sana.

^ fu. 6 Ona sura ya 24 ya kitabu Mkaribie Yehova.

^ fu. 12 Ili kusaida wale wenye kuwa na mawazo ya kujiua, ona habari za Amuka! Sababu Gani Uendelee Kuishi? Chunguza Sababu Tatu” (Mwezi wa 4, 2014); “Unapohisi Kwamba Hutaki Kuendelea Kuishi” (Mwezi wa 1, 2012); na “Uhai Una Thamani” (Tarehe 22 Mwezi 10, 2001).