Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Kama Munajua Mambo Haya, Ninyi Ni Wenye Furaha Ikiwa Munayatenda”

“Kama Munajua Mambo Haya, Ninyi Ni Wenye Furaha Ikiwa Munayatenda”

“Chakula changu ni kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma na kumaliza kazi yake.”​—YOH. 4:34.

NYIMBO: 80, 35

1. Namna gani tabia ya watu wa ulimwengu ya kujifikiria wenyewe inaweza kujaribu unyenyekevu wetu?

JUU ya nini haiko mwepesi kutumikisha mambo yenye tunajifunza mu Neno la Mungu? Sababu moja ni hii: ili kufanya mambo yenye kuwa sawa, tunapaswa kuwa wanyenyekevu. Katika hizi “siku za mwisho,” ni nguvu kuendelea kuwa wanyenyekevu, juu watu wengi wenye kutuzunguka ni “wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, wenye kujisifu, wenye kujivuna,” na “wenye hawajizuie.” (2 Ti. 3:1-3) Sisi watumishi wa Mungu, tunajua kama tabia hizo ni za mubaya, lakini tunaweza kuona kuwa wale wenye kuonyesha tabia hizo wanapata matokeo ya muzuri na wanafurahia kabisa maisha yao. (Zb. 37:1; 73:3) Tunaweza hata kujiuliza hivi: ‘Kutia mahitaji ya wengine pa nafasi ya kwanza kuliko mahitaji yangu, kunaleta faida kabisa? Watu wataendelea kuniheshimia kama ninaonyesha unyenyekevu?’ (Lu. 9:48) Kama tunaruhusu tabia ya watu wa ulimwengu ya kujifikiria wenyewe ituambukie, tunaweza kuharibu uhusiano wetu wa muzuri pamoja na ndugu na dada zetu. Tena, hilo linaweza kufanya ikuwe nguvu kwa wengine kutambua kama tuko Wakristo. Lakini, wakati tunajifunza mifano ya watumishi wa Mungu wenye walionyesha unyenyekevu na kuwaiga, tutapata matokeo ya muzuri.

2. Mifano ya watumishi waaminifu wa Mungu wa wakati wa zamani inaweza kutufundisha nini?

2 Ni nini ilisaidia watumishi waaminifu wa Mungu wa wakati wa zamani wakuwe marafiki wake? Walifanya nini kusudi wamupendeze? Walipata nguvu wapi ili kufanya mambo yenye kuwa sawa? Wakati tunasoma juu ya mifano yao mu Biblia na kufikiri sana juu ya mambo yenye tunasoma, imani yetu itakuwa yenye nguvu zaidi.

MAMBO YENYE KUFANYA IMANI YETU IENDELEE KUWA YENYE NGUVU

3, 4. (a) Yehova anatufundisha kupitia njia gani mbalimbali? (b) Kusudi imani yetu iendelee kuwa yenye nguvu, juu ya nini tuko na lazima ya jambo lingine zaidi ya kuwa na ujuzi?

3 Yehova anatupatia mambo yenye tuko nayo lazima kusudi imani yetu iendelee kuwa yenye nguvu. Tunapata mashauri na mazoezi ya muzuri kupitia Biblia, vichapo vyetu, site yetu ya Enternete, JW Télédiffusion, na mikutano na mikusanyiko yetu. Lakini Yesu alisema kama tuko na lazima ya jambo lingine zaidi ya kuwa na ujuzi. Alisema hivi: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma na kumaliza kazi yake.”​—Yoh. 4:34.

4 Yesu aliona kufanya mapenzi ya Mungu kama vile chakula. Kula chakula chenye kujenga mwili kunatufanya tujisikie muzuri na kunatuletea nguvu mu mwili. Vilevile, kufanya mapenzi ya Mungu kunafanya tujisikie muzuri na kunatia nguvu imani yetu. Kwa mufano, kuko siku ulienda ku mukutano kwa ajili ya mahubiri na uko mwenye kuchoka lakini kisha mahubiri ukarudia ku nyumba na uko na furaha na nguvu?

5. Kama tuko na hekima tutapata faida gani?

5 Wakati tunafanya mambo yenye Yehova anatuomba tufanye, tunakuwa na hekima. (Zb. 107:43) Na watu wenye kuwa na hekima wanapataka faida nyingi. Biblia inasema kama “hakuna kitu chenye unatamani chenye kinaweza kulinganishwa nayo. . . . Ni muti wa uzima kwa wale wenye kuishika, na wale wenye kuishika sana wataitwa wenye furaha.” (Mez. 3:13-18) Yesu alisema hivi: “Kama munajua mambo haya, ninyi ni wenye furaha ikiwa munayatenda.” (Yoh. 13:17) Wanafunzi wa Yesu wangekuwa wenye furaha kama tu wangeendelea kufanya mambo yenye Yesu aliwaambia wafanye. Walifuata mafundisho yake na mufano wake mu maisha yao yote.

6. Juu ya nini tunapaswa kuendelea kutumikisha mambo yenye tunajifunza?

6 Leo, na sisi tunapaswa kuendelea kutumikisha mambo yenye tunajifunza. Wazia fundi fulani mwenye kutengeneza magari mwenye kuwa na vyombo mbalimbali na ujuzi. Vyombo hivyo na ujuzi wake vitamusaidia akuwe fundi wa muzuri kama tu anavitumikisha. Anaweza kuwa na uzoefu wa miaka mingi, lakini kama anapenda kuwa fundi wa muzuri, anapaswa kuendelea kutumikisha mambo yenye amejifunza. Vilevile, wakati tulijifunza kweli, tulikuwa wenye furaha juu tulitumikisha mambo yenye tulisoma mu Biblia. Lakini, kusudi tuendelee kuwa na furaha, tunapaswa kuendelea kutumikisha kila siku mambo yenye Yehova anatufundisha.

7. Tunapaswa kufanya nini kusudi tujifunze mambo fulani kupitia mifano ya watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia?

7 Katika habari hii, tutazungumuzia hali fulani zenye zinaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kubakia wanyenyekevu. Tutajifunza namna watu waaminifu wa zamani waliendelea kuwa wanyenyekevu. Lakini, tunapaswa kufanya mambo mengi zaidi ya kusoma tu habari hiyo. Tunapaswa kufikiri sana juu ya habari hiyo na kuitumikisha mu maisha yetu.

ONA WENGINE KUWA WAKO SAWA NA WEWE

8, 9. Andiko la Matendo 14:8-15 linatufundisha nini juu ya unyenyekevu wa Paulo? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

8 Mungu anapenda watu wa namna zote “waokolewe na wapate ujuzi wenye hauna makosa wa ile kweli.” (1 Ti. 2:4) Namna gani unaona watu hao wote wenye hawajajifunza kweli? Paulo alihubiria Wayahudi wenye tayari walijua jambo fulani juu ya Yehova. Lakini, alihubiria pia watu wenye walikuwa wanaabudu miungu ya uongo. Kuhubiria watu hao kulijaribu unyenyekevu wa Paulo. Namna gani?

9 Wakati Paulo alifanya safari yake ya kwanza ya umisionere, yeye na Barnaba walienda mu muji wa Listra. Walikaonia wenye walikuwa wanaishi mu muji huo waliona Paulo na Barnaba kuwa watu wenye hawako wa kawaida na waliwaita kwa majina ya miungu yao ya uongo Zeu na Herme. Paulo na Barnaba walikubali sifa hiyo? Waliona kuwa hilo ni badiliko lenye kupendeza kwa sababu walikuwa wameteswa mu miji mbili ya mwisho yenye walikuwa wametembelea? Je, walifikiri kama kutendewa vile kutasaidia watu wengi wasikilize habari njema? Hapana! Walikasirika sana na kusema hivi kwa sauti kubwa: “Wanaume, sababu gani munafanya mambo haya? Sisi pia ni wanadamu wenye kuwa na uzaifu uleule kama wenu.”​—Mdo. 14:8-15.

10. Juu ya nini Paulo na Barnaba hawakujiona kuwa wazuri zaidi kupita Walikaonia?

10 Wakati Paulo na Barnaba walisema kama wao pia walikuwa wanadamu, walipenda kusema kama hawakukuwa wakamilifu. Hawakupenda kusema kama namna yao ya kuabudu ilikuwa sawa na ya Walikaonia hao. Paulo na Barnaba walikuwa wametumwa ili kufanya kazi ya umisionere. (Mdo. 13:2) Walikuwa wametiwa mafuta kwa roho takatifu na walikuwa na tumaini la muzuri sana. Lakini hawakuona kuwa hiyo ni sababu ya kujiona kuwa wazuri kupita watu wengine. Waliona kuwa watu hao nao wangeweza kupata tumaini la kuenda mbinguni kama wangekubali habari njema.

11. Wakati tunahubiri, namna gani tunaweza kuwa wanyenyekevu kama Paulo?

11 Hii ni njia moja ya kuonyesha kama tuko wanyenyekevu kama Paulo. Hatuone hata kidogo kama kazi yetu ya kuhubiri ao mambo yenye Yehova anatusaidia kutimiza vinatufanya tukuwe watu wa hali ya juu kupita wengine. Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani ninaona watu wa eneo langu? Ninabagua vikundi fulani vya watu?’ Mu dunia yote, Mashahidi wa Yehova wanajikaza kutafuta watu wenye wanapenda kusikiliza habari njema. Wengine hata wanajikaza kujifunza luga ao desturi za watu wenye wengine wanaona kuwa wa hali ya chini. Hawajione hata kidogo kuwa watu wazuri kupita wale wenye wanahubiria. Lakini, wanajikaza kumuelewa kila mutu kusudi wasaidie watu wengi kadiri inawezekana ili wakubali ujumbe wa Ufalme.

SALI KWA AJILI YA WENGINE KWA KUTAJA MAJINA YAO

12. Namna gani Epafra alionyesha kama alihangaikia kabisa wengine?

12 Njia ingine ya kuonyesha kama tuko wanyenyekevu ni kusali kwa ajili ya ndugu na dada zetu, wenye tayari “wamepata imani yenye samani kama yetu.” (2 Pe. 1:1) Ni vile Epafra alikuwa anafanya. Biblia inamutaja mara tatu tu. Wakati Paulo alikuwa anafungwa mu muji wa Roma, aliandikia Wakristo wa muji wa Kolosai juu ya Epafra. Alisema hivi: “Sikuzote anajikaza kwa ajili yenu katika sala zake.” (Kol. 4:12) Epafra alikuwa anajua muzuri ndugu na dada, na aliwahangaikia sana. Paulo alimuita “mwenzangu wa utekwa,” kwa hiyo Epafra alikuwa na magumu yake. (Flm. 23) Lakini aliendelea kuhangaikia mahitaji ya wengine, na alifanya jambo fulani kusudi awasaidie. Epafra alikuwa anasali kwa ajili ya ndugu na dada zake, na sisi tunaweza kufanya vile, hata tunaweza kutaja majina yao. Sala kama hizo ni zenye nguvu sana.​—2 Ko. 1:11; Yak. 5:16.

13. Namna gani unaweza kumuiga Epafra wakati unasali?

13 Fikiria mutu fulani mwenye unaweza kusali kwa ajili yake kwa kutaja jina lake. Pengine unajua marafiki mu kutaniko ao familia mbalimbali zenye zinapiganisha magumu fulani. Pengine wanapaswa kukamata maamuzi fulani ya nguvu ao wanapaswa kupinga majaribu fulani. Unaweza pia kusali kwa ajili ya ndugu na dada wenye majina yao yanaonyeshwa kwenye jw.org mu habari yenye kichwa “Mashahidi wa Yehova Wenye Kufungwa kwa Sababu ya Imani Yao.” (Fungua sehemu CHUMBA CHA HABARI > MAMBO YA SHERIA.) Unaweza pia kusali kwa ajili ya wale wenye wamefiwa na wapendwa wao, wale wenye wameokoka hivi karibuni musiba fulani wa asili ao vita, na wale wenye kuwa na magumu ya kupata feza. Kuko ndugu na dada wengine wenye wako na lazima tusali kwa ajili yao! Wakati tunasali kwa ajili yao, tunaonyesha kama hatufikirie tu mahitaji yetu wenyewe lakini tunafikiria pia mahitaji ya wengine. (Flp. 2:4) Yehova anasikiaka sala kama hizo.

“UKUWE MWEPESI WA KUSIKILIZA”

14. Namna gani Yehova anaonyesha mufano muzuri wa kusikiliza?

14 Njia ingine ya kuonyesha kama tuko wanyenyekevu ni kuwa wasikilizaji wazuri. Andiko la Yakobo 1:19 linatuambia tukuwe ‘wepesi wa kusikiliza.’ Yehova ni musikilizaji muzuri zaidi. (Mwa. 18:32; Yos. 10:14) Kwa mufano, soma mazungumuzo yenye kupatikana katika Kutoka 32:11-14. (Soma.) Hata kama Yehova hakukuwa na lazima ya mawazo ya Musa, alimuruhusu Musa aeleze namna alikuwa anajisikia. Je, unaweza kumusikiliza kwa uvumilivu mutu fulani mwenye alifanya makosa zamani na kisha ufuate pendekezo lake? Lakini, Yehova anasikilizaka kwa uvumilivu wanadamu wote wenye kusali kwa imani.

15. Namna gani tunaweza kumuiga Yehova kwa kuonyesha wengine heshima?

15 Ujiulize hivi: ‘Kama Yehova alionyesha unyenyekevu sana mupaka akasikiliza watu kama vile alimusikiliza Abrahamu, Raheli, Musa, Yoshua, Manoa, Eliya, na Hezekia, mimi pia sipaswe kufanya vile? Ninaweza kuonyesha ndugu na dada zangu wote heshima zaidi kwa kuwasikiliza na kufuata mapendekezo yao kama inawezekana? Kuko mutu fulani mu kutaniko letu ao mu familia yetu mwenye ninapaswa kuhangaikia zaidi? Nitafanya nini juu ya jambo hilo?’​—Mwa. 30:6; Amu. 13:9; 1 Fa. 17:22; 2 Ny. 30:20.

“PENGINE YEHOVA ATAONA MATESO YANGU”

Daudi alisema hivi: “Mumuache!” Wewe ungefanya nini? (Picha hii inapatana na fungu la 16, 17)

16. Namna gani Mufalme Daudi alitenda wakati Shimei alimutendea mubaya?

16 Unyenyekevu pia unatusaidia tuonyeshe sifa ya kujizuia wakati wengine wanatutendea mubaya. (Efe. 4:2) Tunaona mufano muzuri sana juu ya jambo hilo katika 2 Samweli 16:5-13. (Soma.) Shimei, mutu wa jamaa ya Mufalme Sauli, alitukana na kushambulia Daudi na watumishi wake. Daudi angeweza kumuzuia Shimei, lakini alivumilia matusi yake. Daudi alifanya nini kusudi ajizuie vile? Tunaweza kujua kwa kuchunguza Zaburi ya 3.

17. Ni nini ilimusaidia Daudi ajizuie, na namna gani tunaweza kumuiga?

17 Daudi alitunga Zaburi ya 3 wakati Absalomu mwana wake alikuwa anajaribu kumuua. Shimei alimushambulia Daudi wakati huo, lakini Daudi alipata nguvu ya kubakia kimya. Alipata nguvu hiyo namna gani? Katika Zaburi 3:4, tunasoma maneno haya ya Daudi: “Nitamuita Yehova kwa sauti kubwa, naye atanijibu kutoka katika mulima wake mutakatifu.” Wakati mutu fulani anatutendea mubaya, tunapaswa kusali kama vile Daudi alifanya. Kama tunafanya vile, Yehova atatupatia roho yake takatifu kusudi tuweze kuvumilia. Unaweza kujizuia zaidi ao kuwa mwenye kusamehe zaidi wakati mutu fulani anakutendea mubaya? Uko hakika kama Yehova anahangaikia mateso yako na atakusaidia na kukubariki?

“HEKIMA NDILO JAMBO LA MAANA ZAIDI”

18. Tutapata faida gani wakati tunatumikisha maagizo ya Yehova?

18 Wakati tunafanya mambo yenye kuwa sawa, tutakuwa na hekima na Yehova atatubariki. Katika Mezali 4:7, Biblia inasema hivi: “Hekima ndilo jambo la maana zaidi.” Hata kama hekima inategemea ujuzi, inatia ndani mambo mengi zaidi ya kuelewa ukweli wa mambo. Hekima inatia ndani maamuzi yenye tunafanya. Hata siafu wanaonyesha hekima kwa sababu wanaweka chakula kwa ajili ya kipindi cha baridi. (Mez. 30:24, 25) Kristo, mwenye kuitwa “hekima ya Mungu,” anafanya sikuzote mambo yenye kumupendeza Baba yake. (1 Ko. 1:24; Yoh. 8:29) Mungu atatubariki wakati sisi pia tunaonyesha hekima kwa kuamua kufanya mambo yenye tunajua kuwa sawa na kuendelea kuwa wanyenyekevu. (Soma Matayo 7:21-23.) Kwa hiyo, endelea kujikaza kusudi ufanye kutaniko likuwe mahali kwenye watu wote wanaweza kumutumikia Yehova kwa unyenyekevu. Inaomba wakati na uvumilivu kusudi tutumikishe mambo yenye tunajua kuwa ni sawa. Lakini wakati tunafanya vile, tunaonyesha kama tuko wanyenyekevu, na sifa ya unyenyekevu itatufanya tukuwe na furaha leo na milele.