Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Mweza-Yote Lakini Anafikiria Wengine

Ni Mweza-Yote Lakini Anafikiria Wengine

“[Yehova] anajua muzuri namna tumeumbwa, anakumbuka kwamba tuko mavumbi.”​—ZB. 103:14.

NYIMBO: 30, 10

1, 2. (a) Namna Yehova anatendea watu iko tofauti na namna watu wenye mamlaka wanawatendea. Juu ya nini? (b) Tutazungumuzia nini katika habari hii?

MARA nyingi watu wenye mamlaka wanatawala wengine mubaya ao hata kuwaonea. (Mt. 20:25; Muh. 8:9) Yehova hawezi kufanya vile hata kidogo! Hata kama iko Mweza-Yote, ni kusema, Mutu mwenye nguvu zaidi katika ulimwengu wote, anafikiria sana watu wenye hawakamilike. Iko mwema na anahangaikia namna tunajisikia na mambo yenye tuko nayo lazima. Anakumbuka kama hatukamilike na anajua uzaifu wetu. Kwa hiyo, hatuombe hata kidogo tufanye mambo yenye kupita uwezo wetu.​—Zb. 103:13, 14.

2 Biblia inatuonyesha namna Yehova anafikiria sana watu wake. Tuzungumuzie basi mifano tatu: Kwanza, namna Yehova alimusaidia kijana Samweli amutolee Eli, Kuhani Mukubwa, ujumbe wa hukumu. Pili, namna Yehova alimuonyesha Musa uvumilivu wakati Musa aliwaza kama hangeweza kuongoza taifa la Israeli kutoka mu Inchi ya Misri. Na tatu, namna Yehova alifikiria Waisraeli wakati walikuwa wanatoka Misri. Mifano hiyo inatufundisha nini juu ya Yehova, na namna gani tunaweza kumuiga?

ANAFIKIRIA KIJANA MUDOGO

3. Usiku moja, ni jambo gani lenye halikukuwa la kawaida lenye lilimufikia kijana Samweli, na tunaweza kujiuliza ulizo gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Samweli alianza kutumika mu tabenakulo wakati alikuwa kijana mudogo sana. (1 Sa. 3:1) Usiku moja, wakati alienda kulala, jambo fulani lenye halikukuwa la kawaida kabisa lilitokea. * (Ona maelezo ya chini.) (Soma 1 Samweli 3:2-10.) Alisikia mutu fulani iko anaita jina lake. Samweli aliwaza kama ni Eli, Kuhani Mukubwa mwenye kuzeeka. Kwa hiyo, alionyesha utii wakati aliamuka na kukimbilia kwenye Eli alikuwa na kusema hivi: “Mimi huyu, kwa kuwa umeniita.” Lakini Eli alimuambia hivi: “Sikukuita.” Kisha jambo hilo kutokea mara mbili tena, Eli alitambua kama ni Mungu ndiye alikuwa anamuita Samweli. Kwa hiyo, Eli alimuambia Samweli jambo la kusema kama anasikia tena sauti hiyo, na Samweli alitii. Wakati Yehova alimuita Samweli kwa mara ya kwanza, juu ya nini hakumuambia kama ni yeye alikuwa anamuita? Biblia haiseme. Lakini, inawezekana Yehova alifanya mambo kwa njia hiyo juu alifikiria namna Samweli alikuwa anajisikia.

4, 5. (a) Samweli alifanya nini wakati Yehova alimupatia ujumbe wa kumuambia Eli? (b) Habari hii inatufundisha nini juu ya Yehova?

4 Soma 1 Samweli 3:11-18. Sheria ya Yehova aliamuru watoto waheshimie watu wakubwa, zaidi sana wale wenye walikuwa na mamlaka. (Kut. 22:28; Law. 19:32) Kwa hiyo, ni nguvu kuwazia kama kijana mudogo kama Samweli angeenda kwa Eli asubui, na kumuambia bila woga ujumbe mukali wa hukumu kutoka kwa Mungu. Biblia inatuambia kama Samweli ‘aliogopa kumuambia Eli kuhusu maono hayo.’ Lakini, Mungu alimuonyesha Eli waziwazi kama ni Yeye alikuwa anaita Samweli. Kwa hiyo, Eli alimuomba Samweli asimufiche hata neno moja lenye Mungu alisema. Samweli alimutii Eli na “akamuambia kila jambo.”

5 Ujumbe huo wa Samweli haungepaswa kumushangaza kabisa Eli. Mbele ya pale “mutu wa Mungu” alikuwa amemuambia Eli ujumbe kama huo. (1 Sa. 2:27-36) Habari hii inatufundisha kama Yehova ni mwenye kufikiria sana wengine na ni mwenye hekima sana.

6. Namna Mungu alimusaidia kijana Samweli, inaweza kutufundisha mambo gani?

6 Uko kijana? Kama jibu ni ndiyo, habari juu ya kijana Samweli inaonyesha kama Yehova anaelewa magumu yako na namna unajisikia. Pengine uko mutu mwenye haya na unaona kuwa ni nguvu kuhubiria watu wazima ao kuwa tofauti na watu wenye kuwa na miaka kama yako. Ukuwe hakika kama Yehova anapenda kukusaidia. Kwa hiyo, usali kwake na umuambie kabisa namna unajisikia. (Zb. 62:8) Ufikiri kwa uzito juu ya mifano ya vijana wenye kuzungumuziwa mu Biblia kama vile Samweli. Na uzungumuze na ndugu na dada wenye kuwa na miaka kama yako ao watu wazima wenye wanaweza kuwa wameshinda magumu kama yako. Wanaweza kukuambia juu ya wakati wenye Yehova aliwasaidia, pengine katika njia zenye hawakuwazia.

ANAMUFIKIRIA MUSA

7, 8. Namna gani Yehova alionyesha kama alihangaikia sana namna Musa alikuwa anajisikia?

7 Wakati Musa alikuwa na miaka 80, Yehova alimupatia mugao wa nguvu sana: kukomboa taifa la Israeli kutoka katika utumwa wa Misri. (Kut. 3:10) Pengine mugao huo ulimushitua Musa, kwa sababu alikuwa muchungaji katika Midiani kwa miaka 40. Musa alisema hivi: “Mimi niko nani ili niende kwa Farao na kutosha Waisraeli katika Misri?” Yehova alimuhakikishia Musa hivi: “Nitakuwa pamoja na wewe.” (Kut. 3:11, 12) Yehova aliahidi pia kama wazee wa Israeli “hakika watasikiliza sauti” yake. Lakini, Musa aliuliza hivi: “Tuseme hawaniamini na hawasikilize sauti yangu?” (Kut. 3:18; 4:1) Kwa kweli, Musa alikuwa anasema kama Yehova anaweza kuwa amedanganyika! Lakini, Yehova alimuvumilia Musa. Alimupatia hata uwezo wa kufanya miujiza. Kwa kweli, Musa ndiye alikuwa mwanadamu wa kwanza mwenye anatajwa mu Biblia mwenye alikuwa na uwezo huo.​—Kut. 4:2-9, 21.

8 Hata kisha mambo yote hayo, Musa alipata sababu ingine ya kujitetea. Alisema kama hangeweza kusema muzuri. Kwa hiyo, Mungu alimuambia hivi: “Nitakuwa pamoja na wewe wakati utakuwa unazungumuza, na nitakufundisha jambo lenye unapaswa kusema.” Je, Musa alisadiki sasa? Hapana, alimuomba Mungu atume mutu mwingine! Kwa hiyo, Yehova akakasirika. Lakini, Yehova aliendelea kuhangaikia namna Musa alikuwa anajisikia, kwa hiyo, akamutuma Haruni azungumuze kwa ajili yake.​—Kut. 4:10-16.

9. Namna gani uvumilivu na wema wa Yehova vilimusaidia Musa akuwe kiongozi muzuri?

9 Habari hiyo inatufundisha nini juu ya Yehova? Kwa sababu Yehova iko Mweza-Yote, angetumia uwezo wake kusudi amuogopeshe Musa na kumufanya atii. Lakini, Yehova alionyesha uvumilivu na wema, na alimuhakikishia mutumishi wake mwenye kiasi na munyenyekevu kama atakuwa pamoja naye. Njia hiyo ya kufanya mambo ilileta matokeo ya muzuri? Ndiyo! Musa akakuwa kiongozi mukubwa wa watu wa Mungu. Alijikaza kuwa mupole na mwenye kufikiria wengine, kama vile tu Yehova alimutendea.​—Hes. 12:3.

Unatendea wengine kama vile Yehova anawatendea? (Picha hii inapatana na fungu la 10)

10. Tunapata faida gani wakati tunafikiria wengine kama vile Yehova anafanya?

10 Hilo linatufundisha nini leo? Kama uko bwana, muzazi, ao muzee wa kutaniko, uko na mamlaka fulani juu ya wengine. Ndiyo maana, ni jambo la maana sana umuige Yehova kwa kufikiria bibi yako, watoto wako, na wengine katika kutaniko na kuwaonyesha wema, na uvumilivu. (Kol. 3:19-21; 1 Pe. 5:1-3) Kama unamuiga Yehova Mungu na Yesu Kristo, Musa Mukubwa Zaidi, hilo litafanya wengine wakuwe tayari kukukaribia na kuzungumuza na wewe, na utawatia moyo. (Mt. 11:28, 29) Tena, utawaonyesha mufano muzuri.​—Ebr. 13:7.

MWOKOZI MWENYE NGUVU LAKINI MWENYE KUFIKIRIA WENGINE

11, 12. Yehova alifanya nini kusudi Waisraeli wajisikie salama kabisa wakati alikuwa anawaongoza kutoka Misri?

11 Inawezekana Waisraeli wenye walitoka katika inchi ya Misri mu mwaka wa 1513 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, walikuwa zaidi ya milioni 3. Katika kikundi hicho kulikuwa watoto, watu wenye kuzeeka, na pengine watu wengine wenye walikuwa wagonjwa ao wazaifu. Kikundi hicho kikubwa cha watu kilikuwa na lazima ya Kiongozi mwenye kuwahangaikia na mwenye kuwaelewa. Ni vile Yehova alikuwa kabisa kupitia Musa. Kwa hiyo, Waisraeli walijisikia salama wakati waliacha makao moja tu yenye walikuwa wanajua.​—Zb. 78:52, 53.

12 Yehova alifanya nini kusudi watu wake wajisikie salama kabisa? Alifanya Waisraeli ‘wajipange kwa ajili ya vita’ wakati walitoka Misri. (Kut. 13:18) Kwa sababu walikuwa wamepangwa katika njia hiyo, wangeweza kuona waziwazi kama ni Mungu wao ndiye alikuwa anaongoza mambo. Tena, Yehova aliwapatia “wingu wakati wa muchana” na “mwangaza wa moto” wakati wa usiku kusudi awakumbushe kama alikuwa pamoja nao, alikuwa anawaongoza, na kuwalinda. (Zb. 78:14) Na taifa la Israeli lilikuwa na lazima ya uhakika huo juu ya jambo lenye lilitokea kisha pale.

Namna gani Yehova alihangaikia Waisraeli kwenye Bahari Nyekundu? (Picha hii inapatana na fungu la 13)

13, 14. (a) Namna gani Yehova alihangaikia Waisraeli kwenye Bahari Nyekundu? (b) Namna gani Yehova alionyesha kama alikuwa mwenye nguvu sana kupita Wamisri?

13 Soma Kutoka 14:19-22. Wazia kama ulikuwa pale pamoja na Waisraeli. Hakuna mahali pa kukimbilia. Jeshi la Wamisri liko nyuma yenu, na Bahari Nyekundu iko mbele yenu. Kisha Mungu anatenda. Nguzo ya wingu yenye ilizoea kuwa mbele yenu inaenda nyuma ya kambi, kati yenu na Wamisri. Sasa Wamisri wako mu giza, lakini kambi yenu iko na mwangaza wenye munapata kwa njia ya muujiza! Kisha unamuona Musa ananyoosha mukono wake juu ya bahari, na upepo mukali wa mashariki unatokea, na kufungua njia kubwa mupaka ngambo ingine. Kwa hiyo, wewe, familia yako, na wanyama wenu, ninyi wote munatembea juu ya udongo wenye kukauka pamoja na watu wengine kwa namna yenye kupangwa muzuri kabisa. Unashangaa sana wakati unaona kuwa udongo hauna matope na hautereze. Udongo unakauka na uko nguvu-nguvu kwa kadiri fulani, ni mwepesi kutembea juu yake. Kwa hiyo, hata wale wenye kutembea polepole wanafika salama ngambo ingine ya bahari.

14 Soma Kutoka 14:23, 26-30. Wakati mambo hayo yote yanatokea, Farao, mwenye kiburi na mupumbavu, anaanza kukufuatilia wewe na Waisraeli wenzako. Kisha Musa ananyoosha tena mukono wake juu ya bahari, na kuta mbili za maji zinaanguka. Maji yanamufunika Farao na jeshi lake. Hakuna mutu kati yao mwenye anaokoka!​—Kut. 15:8-10.

15. Habari hii inakufundisha nini juu ya Yehova?

15 Habari hii inatufundisha jambo lingine juu ya Yehova. Yehova haiko Mungu wa muvurugo, na sifa hiyo inatusaidia tujisikie salama kabisa. (1 Ko. 14:33) Kama muchungaji mwenye kupenda na kutunza kondoo zake, Yehova anahangaikia watu wake mu njia mbalimbali. Anafanya wajisikie salama na kuwalinda juu ya maadui wao. Jambo hilo linatutia moyo na kututuliza sana wakati tunaendelea kukaribia mwisho wa ulimwengu huu.​—Mez. 1:33.

16. Tunaweza kupata faida gani kwa kuzungumuzia namna Yehova aliokoa watu wake?

16 Leo, Yehova anaendelea kuhangaikia watu wake wakiwa kikundi. Anawasaidia waendelee kuwa na urafiki wa muzuri pamoja naye na anawalinda juu ya maadui wao. Na ataendelea kufanya vile wakati wa taabu kubwa yenye itaanza hivi karibuni. (Ufu. 7:9, 10) Kwa hiyo, watu wa Mungu hawataogopa wala kutetemeka wakati wa taabu kubwa, ikuwe wako vijana ao wazee, wenye afya ya muzuri ao wazaifu. * (Ona maelezo ya chini.) Lakini, watakuwa na ujasiri kabisa! Watakumbuka maneno haya ya Yesu: “Musimame wima na kuinua vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu unakaribia.” (Lu. 21:28) Hata wakati watu wa Mungu wanashambuliwa na Gogu, ni kusema, muungano wa mataifa wenye nguvu zaidi kupita Farao, watakuwa hakika kama Yehova atawalinda. (Eze. 38:2, 14-16) Juu ya nini? Juu wanajua kama Yehova hawezi kubadilika. Ataonyesha tena kama iko mwenye upendo na iko Mwokozi mwenye kuhangaikia watu wake.​—Isa. 26:3, 20.

17. (a) Tunaweza kupata faida gani wakati tunajifunza habari za Biblia zenye kuonyesha namna Yehova anafikiria watu wake? (b) Tutazungumuzia nini katika habari yenye kufuata?

17 Katika habari hii, tumeona mifano fulani yenye kuonyesha namna Yehova anafikiria watu wake na kuwaonyesha wema wakati anawahangaikia, anawaongoza na kuwaokoa. Wakati unafikiri sana juu ya habari kama hizo, ujikaze kujifunza jambo fulani la mupya juu ya Yehova kwa kutafuta maelezo fulani yenye pengine haukukuwa unajua. Wakati unaendelea kujifunza mambo mengi juu ya sifa za muzuri za Yehova, utamupenda zaidi na imani yako kwake itakuwa yenye nguvu zaidi. Katika habari yenye kufuata, tutajifunza ni katika njia gani mbalimbali tunaweza kumuiga Yehova kwa kufikiria wengine mu familia, mu kutaniko, na mu kazi ya kuhubiri.

^ fu. 3 Mwanahistoria Muyahudi Yosefo anasema kama Samweli alikuwa na miaka 12 wakati huo.

^ fu. 16 Ni jambo lenye kupatana na akili kuwaza kama watu fulani wenye wataokoka Armagedoni watakuwa na uzaifu mbalimbali wa kimwili. Wakati Yesu alikuwa ku dunia, aliponyesha watu wenye walikuwa na “kila namna ya uzaifu,” ao kila namna ya ulemavu. Mambo yenye alifanya wakati huo yanaonyesha mambo yenye atafanyia wale wenye wataokoka Armagedoni. (Mt. 9:35) Wale wenye watafufuliwa, watakuwa na miili yenye afya ya muzuri.