Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wakristo Wenye Kuzeeka—Yehova Anapendezwa Sana na Ushikamanifu Wenu

Wakristo Wenye Kuzeeka—Yehova Anapendezwa Sana na Ushikamanifu Wenu

KATIKA dunia yote, watu wenye kuzeeka wanapendezwa sana na mapendeleo ya utumishi yenye wako nayo katika tengenezo la Mungu. Wazee hao ni baraka kabisa kwetu sisi wote! Lakini, hivi karibuni, kulikuwa badiliko fulani. Wazee wenye kuzeeka waliombwa waachie wazee vijana madaraka yao fulani mazito. Katika njia gani?

Mupango huo mupya ni kwamba waangalizi wa muzunguko na walimu wa masomo mbalimbali za kiteokrasi waache aina hizo za utumishi wakati wanafikia miaka 70. Tena, wazee wenye kuwa na miaka 80 waachie wazee vijana migao mbalimbali, kama vile kuwa muratibu wa Halmashauri ya Tawi ao kuwa muratibu wa baraza la wazee mu kutaniko. Ndugu hao wapendwa wenye kuzeeka walitenda namna gani juu badiliko hilo? Wameonyesha ushikamanifu kwa Yehova na tengenezo lake!

Ken, mwenye alikuwa muratibu wa Halmashauri ya Tawi kwa miaka karibu 49 anasema hivi: “Nilikubaliana kabisa na uamuzi huo. Kwa kweli, asubui ileile yenye nilijua badiliko hilo, nilikuwa nimesali kwa Yehova; nilimuonyesha kama ilikuwa lazima muzee kijana akuwe muratibu.” Namna Ken alitenda ni mufano tu wenye kuonyesha namna wazee waaminifu walijisikia katika dunia yote. Kwa kweli, kwa sababu walipenda kutumikia ndugu na dada, ku mwanzo walivunjika moyo kwa kadiri fulani.

Esperandio mwenye alikuwa muratibu wa baraza la wazee katika kutaniko lake anasema hivi: “Mupango huo ulinihuzunisha kidogo.” Lakini, anasema hivi: “Nilikuwa na lazima ya wakati zaidi kusudi nihangaikie afya yangu yenye inaendelea kuharibika.” Kama vile tunaweza kutazamia, Esperandio anaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu na kuwa baraka kwa kutaniko lake.

Tuseme nini juu ya waangalizi wasafiri wenye walitumika kwa muda murefu lakini sasa wanafanya aina zingine za utumishi? Allan, mwenye alikuwa mwangalizi mwenye kusafiri kwa miaka 38, anasema hivi: “Wakati nilipata habari hiyo, niliishiwa kabisa.” Lakini, alielewa faida za kuzoeza ndugu vijana kusudi wafanye kazi hiyo, na anaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu.

Russell, mwenye alikuwa mwangalizi mwenye kusafiri na mwalimu wa masomo mbalimbali za kiteokrasi kwa miaka 40, anasema kama ku mwanzo yeye na bibi yake walivunjika moyo. “Tulikuwa tunafurahia sana mugao wetu na tuliona kama tulikuwa na nguvu ya kuendelea.” Russell na bibi yake wako wanatumia mazoezi na uzoefu wao mu kutaniko lao, na wahubiri wa kutaniko hilo wanafurahi kutumika pamoja nao.

Hata kama wewe mwenyewe haujajisikia kama vile ndugu wenye tumekwisha kutaja walijisikia, habari yenye kuwa mu 2 Samweli inaweza kukusaidia uelewe ndugu hao.

MWANAUME MWENYE KIASI NA MWENYE KUONA MAMBO KWA NJIA YENYE KUFAA

Fikiria wakati Absalomu, mwana wa Daudi, aliasi. Daudi alikimbia kutoka Yerusalemu na akaenda Mahanaimu, ngambo ya mashariki ya Muto Yordani. Wakati Daudi na wanaume wenye walikuwa pamoja naye walikuwa kule, walikosa mambo fulani ya lazima ya maisha. Unakumbuka jambo lenye lilitokea?

Wanaume tatu wa eneo hilo waliwaletea kwa ukarimu vitanda, vyakula mbalimbali, na vyombo vyenye walikuwa navyo lazima. Barzilai alikuwa kati ya wanaume hao. (2 Sa. 17:27-29) Wakati uasi wa Absalomu ulifikia mwisho, Daudi alirudia Yerusalemu, na Barzilai alimusindikiza mupaka Yordani. Daudi alimuomba aende pamoja naye Yerusalemu. Mufalme alimuahidi Barzilai kama atamupatia chakula, hata kama alikuwa “tajiri sana” na hakukuwa na lazima ya chakula hicho. (2 Sa. 19:31-33) Lakini, pengine Daudi alifurahia sana sifa za Barzilai na mashauri yoyote yenye angeweza kumutolea. Kwa kweli, angepata pendeleo la muzuri sana la kuishi na kutumika mu makao ya mufalme!

Kwa sababu Barzilai aliona mambo kwa njia yenye kufaa na alikuwa mwenye kiasi, alisema kama alikuwa na miaka 80. Kisha aliongeza hivi: “Je, ninaweza kufanya tofauti kati ya mema na mabaya?” (2 Sa. 19:35) Alipenda kusema nini? Barzilai alipaswa kuwa amepata hekima juu alikuwa ameishi miaka mingi. Na angeweza kutoa mashauri ya muzuri, kama vile tu “wanaume wazee” walimutolea Mufalme Rehoboamu mashauri ya muzuri wakati wa utawala wake. (1 Fa. 12:6, 7; Zb. 92:12-14; Mez. 16:31) Kwa hiyo, maelezo ya Barzilai juu ya kutambua mema na mabaya yanaweza kuzungumuzia mipaka ao uzaifu wa kimwili wenye alikuwa nao kwa sababu ya miaka yake. Alikubali kama uzee wake tayari ulikuwa umeharibu uwezo wake wa kuonja chakula na kusikia. (Muh. 12:4, 5) Kwa hiyo, Barzilai yeye mwenyewe alimuomba Daudi akamate kijana Kimhamu aende naye Yerusalemu. Pengine kijana huyo alikuwa mwana wa Barzilai.​—2 Sa. 19:36-40.

KUFANYA MIPANGO KWA AJILI YA WAKATI WENYE KUJA

Mabadiliko yenye kuhusu miaka yenye kuzungumuziwa ku mwanzo wa habari hii yanaonyesha maoni kama ile ya Barzilai. Kwa kweli, wakati wetu, mambo mengi zaidi yamechunguzwa kuliko tu kuchunguza hali ya mutu na uwezo wake, kama vile mufano wa Barzilai unaonyesha. Ilikuwa lazima kufikiria kwa njia yenye kufaa faida ya wazee waaminifu mu dunia yote.

Wakristo hao waaminifu wenye kuzeeka na wenye kiasi walikuwa tayari kuona kama tengenezo la Yehova lingetiwa nguvu ili kushugulikia ongezeko la wakati wenye kuja ikiwa madaraka yenye walikuwa nayo kwa wakati murefu yangepewa ndugu vijana. Katika hali nyingi, ni ndugu hao wenye kuzeeka ndio walizoeza vijana wenye walipewa migao hiyo, kama vile inawezekana kabisa kuwa Barzilai alimuzoeza mwana wake na kama vile mutume Paulo alimuzoeza Timoteo. (1 Ko. 4:17; Flp. 2:20-22) Ndugu hao vijana wameonyesha kama wako sasa “zawadi katika wanadamu,” wako na uwezo wa kusaidia ili “kujenga mwili wa Kristo.”​—Efe. 4:8-12; linganisha na Hesabu 11:16, 17, 29.

NAFASI ZINGINE ZA KUSAIDIA

Watu wengi mu kutaniko la watu wa Mungu katika dunia yote wenye wametolea wengine madaraka yao fulani wanatumia sasa nafasi za mupya ao nafasi nyingi zaidi za kumutumikia Yehova.

Marco, mwenye alikuwa mwangalizi mwenye kusafiri kwa miaka 19, anasema hivi: “Hali zangu za sasa zinaniruhusu kupata nafasi ya kusaidia bwana wenye hawako Mashahidi wa dada fulani katika kutaniko letu.”

Geraldo, mwenye alikuwa mu kazi ya kusafiri kwa miaka 28, anasema hivi: “Muradi wetu wa mupya unatia ndani kusaidia wale wenye hawahubiri na kukusanyika tena na kuongoza mafunzo mengi ya Biblia.” Anasema kama yeye na bibi yake, mupaka sasa, wanaongoza mafunzo 15 ya Biblia na kama wahubiri wengi wenye waliacha kuhubiri na kukusanyika wameanza tena kuja ku mikutano.

Allan, mwenye tumekwisha kutaja, anasema hivi: “Sasa tuko na nafasi ya kujitoa zaidi mu kazi ya kuhubiri. Tunafurahia kuhubiri mahali pa watu wengi, katika eneo la biashara, na kuhubiria majirani wetu, wawili kati yao wamekwisha kuja ku mikutano.”

Kama wewe uko ndugu muaminifu na mwenye uwezo na umepata mugao mupya mu tengenezo la Mungu, unaweza kusaidia katika njia ingine ya pekee. Unaweza kuunga mukono kazi ya Yehova kwa kusaidia ndugu vijana mu kutaniko kupitia uzoefu wako wa maana sana. Russell, mwenye tumekwisha kutaja, anasema hivi: “Yehova iko anazoeza na kutumia ndugu vijana wazuri na wenye kuwa na uwezo mbalimbali wa kizalikio. Kazi ya kufundisha na ya uchungaji yenye wanafanya kwa bidii inaletea ndugu na dada faida!”​—Ona kisanduku “ Saidia Vijana Wanaume Watumie Uwezo Wao Wote.”

YEHOVA ANAPENDEZWA SANA NA USHIKAMANIFU WAKO

Kama umeanza hivi karibuni aina ingine ya utumishi, uendelee kuwa na mawazo ya muzuri. Kazi yako yenye ulifanya kwa moyo wako wote imesaidia watu wengi mu maisha yao, na unaweza kuendelea kufanya vile. Wamekupenda na kwa kweli, wataendelea kukupenda.

Jambo la maana zaidi ni kwamba umefanya jambo lenye Yehova ataendelea kukumbuka. ‘Hatasahau kazi yako na upendo wenye ulionyesha kwa ajili ya jina lake kwa kutumikia na kuendelea kutumikia watakatifu.’ (Ebr. 6:10) Maneno hayo yenye yaliongozwa na roho ya Mungu yanatuhakikishia sisi wote kama Mungu hawezi kusahau kazi za jasho zenye tulifanya wakati wenye umepita. Yehova anakuona kuwa mutu wa maana, kwa hiyo, hawezi kukusahau kwa sababu ya bidii yenye ulifanya zamani na ile yenye unaendelea kufanya ili kumupendeza!

Halafu kama hauko kati ya wale wenye migao yao ilibadilika, wenye tumezungumuzia? Habari hii inaweza kukusaidia pia sana. Namna gani?

Kama kwa sasa unashirikiana na ndugu muaminifu mwenye kuzeeka mwenye mugao wake ulibadilishwa, ukomavu na uzoefu wake wa miaka mingi unaweza kukuletea faida. Umuombe mashauri na mapendekezo. Na uangalie namna anatumia uzoefu wake kwa ushikamanifu katika mugao wake wa sasa.

Kama uko ndugu mwenye kuzeeka mwenye amepewa mugao mupya ao uko ndugu ao dada mwenye anaweza kupata faida kupitia uzoefu wa ndugu mwenye kuzeeka, kumbuka kama Yehova anapendezwa sana na ushikamanifu wa wale wenye wamemutumikia wakati murefu na wenye wanaendelea kufanya vile.