Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wenye Furaha Ni Wale Wenye Kumutumikia “Mungu Mwenye Furaha”

Wenye Furaha Ni Wale Wenye Kumutumikia “Mungu Mwenye Furaha”

“Wenye furaha ni watu wenye Mungu wao ni Yehova!”​—ZB. 144:15.

NYIMBO: 44, 125

1. Juu ya nini Mashahidi wa Yehova ni watu wenye furaha? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

MASHAHIDI WA YEHOVA ni watu wenye furaha. Kila wakati wanakutana pamoja, ikuwe ku mukutano, mukusanyiko, ao wakati wanakutana juu ya kujifurahisha, wanazungumuza na kucheka pamoja. Juu ya nini ni watu wenye furaha sana? Sababu kubwa ni hii: wanamujua Yehova, “Mungu mwenye furaha.” Wanamutumikia na wanajikaza kumuiga. (1 Ti. 1:11; Zb. 16:11) Yehova ni Chanzo cha furaha, kwa hiyo, anapenda na sisi tukuwe na furaha, na anatutolea sababu nyingi za kuwa wenye furaha.​—Kum. 12:7; Muh. 3:12, 13.

2, 3. (a) Kuwa mwenye furaha, maana yake nini? (b) Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuwa mwenye furaha?

2 Halafu wewe? Uko mwenye furaha? Kuwa mwenye furaha maana yake kujisikia muzuri, kutosheka na maisha yako, ao kuwa na shangwe sana. Biblia inaonyesha kama ni wale wenye kubarikiwa na Yehova ndio wanaweza kuwa wenye furaha kabisa. Lakini, juu ya nini inaweza kuwa nguvu kuwa mwenye furaha mu dunia ya leo?

3 Inaweza kuwa nguvu kuwa mwenye furaha wakati tuko katika hali zenye kuleta mahangaiko, kama vile wakati mutu fulani mwenye tunapenda anakufa ao anatengwa, wakati ndoa yetu inavunjika, ao wakati tunapoteza kazi yetu. Tena, inaweza kuwa nguvu kuwa mwenye furaha wakati hakuna amani mu nyumba juu ya mabishano yenye kuendelea, wakati wafanyakazi wenzetu ao wanafunzi wenzetu wanatuchekelea, ao wakati tunateswa ao tunafungwa mu gereza juu ya kumutumikia Yehova. Ao afya yetu inaweza kuwa mubaya, tunaweza kupata ugonjwa wenye kukawia, ao tunaweza kushuka moyo. Lakini, kumbuka kama Yesu Kristo, “ule mwenye furaha na yeye pekee ambaye ni Bwana Mwenye Uwezo,” ao Mutawala, alipenda kufariji watu na kuwafanya wakuwe wenye furaha. (1 Ti. 6:15; Mt. 11:28-30) Katika Mahubiri ya Mulimani, Yesu alitaja sifa fulani zenye zinaweza kutusaidia tukuwe wenye furaha hata wakati tuko na magumu mengi juu tunaishi mu ulimwengu wa Shetani.

HATUWEZI KUWA WENYE FURAHA BILA YEHOVA

4, 5. Tunaweza kufanya nini kusudi tuendelee kuwa wenye furaha?

4 Jambo la kwanza lenye Yesu alitaja ni la maana zaidi. Alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho, kwa sababu Ufalme wa mbinguni ni wao.” (Mt. 5:3) Kama tunatambua uhitaji wetu wa kiroho, maana yake, tunatambua kama tuko na lazima ya kumujua Mungu na kama tuko na lazima ya musaada na muongozo wake. Namna gani tunaonyesha jambo hilo? Kwa kujifunza Biblia, kumutii Mungu, na kutia ibada yake pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. Kufanya mambo hayo kutatusaidia tukuwe wenye furaha. Tutakuwa na imani zaidi kama ahadi za Mungu zitatimia hivi karibuni. Na “tumaini lenye furaha” lenye tunapata mu Biblia litatutia moyo.​—Tit. 2:13.

5 Kama tunapenda tukuwe wenye furaha hata kutokee mambo gani mu maisha yetu, tunapaswa kuendelea kutia nguvu urafiki wetu pamoja na Yehova. Mutume Paulo aliandika hivi: “Mufurahi sikuzote katika Bwana. Nitasema tena, Mufurahi!” (Flp. 4:4) Kusudi tukuwe marafiki wa sana wa Yehova, tunapaswa kuwa na hekima yenye anatoa. Neno la Mungu linasema hivi: “Mwenye furaha ni mutu mwenye anapata hekima na mutu mwenye anapata utambuzi. Ni muti wa uzima kwa wale wenye kuishika, na wale wenye kuishika sana wataitwa wenye furaha.”​—Mez. 3:13, 18.

6. Kusudi tuendelee kuwa wenye furaha, tunapaswa kufanya jambo gani lingine?

6 Lakini kusudi tuendelee kuwa wenye furaha, ni jambo la maana sana tuendelee kutumikisha mambo yenye tunajifunza mu Biblia. Yesu alikazia kama hilo ni jambo la maana sana wakati alisema hivi: “Kama munajua mambo haya, ninyi ni wenye furaha ikiwa munayatenda.” (Yoh. 13:17; soma Yakobo 1:25.) Ni jambo la lazima sana kufanya vile kama tunapenda kutimiza uhitaji wetu wa kiroho na kuendelea kuwa wenye furaha. Lakini, tunaweza kufanya nini kusudi tuendelee kuwa wenye furaha wakati kuko mambo mengi yenye yanaweza kutufanya tupoteze furaha yetu? Tuone basi jambo lingine lenye Yesu alisema katika Mahubiri yake ya Mulimani.

SIFA ZENYE KUTUFANYA TUKUWE WENYE FURAHA

7. Namna gani wale wenye kuomboleza wanaweza kuwa wenye furaha?

7 “Wenye furaha ni wale wenye kuomboleza, kwa sababu watafarijiwa.” (Mt. 5:4) Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani wale wenye kuomboleza wanaweza kuwa na furaha?’ Yesu hakukuwa anazungumuzia kila mutu mwenye kuomboleza. Watu wengi wabaya wanaomboleza, ao wako na huzuni, juu wanapata magumu yenye kuleta mahangaiko katika hizi “siku za mwisho” zenye kuwa “ngumu [sana] kuvumilia.” (2 Ti. 3:1) Lakini, wanajifikiria wenyewe tu bila kumufikiria Yehova, kwa hiyo, hawafanye urafiki pamoja naye, na hawawezi kuwa wenye furaha. Yesu alikuwa anazungumuzia wale wenye kutambua uhitaji wao wa kiroho. Wanaomboleza juu wanaona kama watu wengi wamemuacha Mungu ao hawaishi namna Mungu anapenda. Tena, wanaelewa kama wako wafanya-zambi, na wanaona mambo ya mubaya yenye kufanyika mu dunia hii. Yehova anaona wale wenye kuomboleza kwelikweli, anawafariji kupitia Neno lake, na anawasaidia wakuwe wenye furaha na atawapatia uzima wa milele.​—Soma Ezekieli 5:11; 9:4.

8. Namna gani kuwa mwenye tabia ya upole kunaweza kukusaidia ukuwe mwenye furaha?

8 “Wenye furaha ni wale wenye tabia ya upole, kwa sababu watariti dunia.” (Mt. 5:5) Namna gani kuwa mwenye tabia ya upole kunaweza kukusaidia ukuwe mwenye furaha? Watu wengi hawana adabu na wako wakali sana, na hilo linaweza kuleta magumu mengi. Lakini, wakati wanajifunza kweli, wanabadilika na kuvaa “utu mupya.” Sasa wanaonyesha “upendo wenye upole wa huruma, fazili, unyenyekevu, upole, na uvumilivu.” (Kol. 3:9-12) Kwa hiyo, wako na amani, wako na uhusiano wa muzuri pamoja na wengine, na wako wenye furaha. Tena, Neno la Mungu linaahidi kama “watariti dunia.”​—Zb. 37:8-10, 29.

9. (a) Yesu alipenda kusema nini wakati alisema kama wenye tabia ya upole “watariti dunia”? (b) Juu ya nini “wale wenye njaa na kiu ya haki” wanaweza kuwa wenye furaha?

9 Yesu alipenda kusema nini wakati alisema kama wale wenye tabia ya upole “watariti dunia”? Watiwa-mafuta watariti dunia wakati wataitawala wakiwa wafalme na makuhani. (Ufu. 20:6) Watu wengine wengi wenye hawana tumaini la kuenda mbinguni nao watariti dunia wakati wataruhusiwa kuishi milele mu dunia. Watakuwa wakamilifu na watakuwa na amani na furaha. Yesu alikuwa anazungumuzia watu hao wakati alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye njaa na kiu ya haki.” (Mt. 5:6) Tamaa yao ya haki itatimizwa wakati Yehova atatosha uovu wote. (2 Pe. 3:13) Katika dunia mupya, watu wenye haki watakuwa wenye furaha na hawataombeza tena hata siku moja juu ya mambo ya mubaya yenye watu waovu wanafanya.​—Zb. 37:17.

10. Kuwa mwenye rehema maana yake nini?

10 “Wenye furaha ni wale wenye rehema, kwa sababu wataonyeshwa rehema.” (Mt. 5:7) Kuwa mwenye rehema maana yake kuwa mwenye urafiki, kuwa mupole ao mwenye kuonyesha huruma, ni kusema, kusikilia huruma wale wenye kuteseka. Lakini, rehema haimaanishe kusikia tu huruma. Biblia inafundisha kama kuwa mwenye rehema kunatia ndani kufanya jambo fulani juu ya kusaidia wengine.

11. Mufano wa Musamaria mwema unatufundisha nini?

11 Soma Luka 10:30-37. Mufano wa Yesu wa Musamaria mwema unaonyesha muzuri maana ya kuwa mwenye rehema. Musamaria alimusikilia huruma mwanaume mwenye alikuwa anateseka, na hilo lilimuchochea amusaidie. Kisha Yesu kutoa mufano huo, alisema hivi: “Uende, na ufanye vilevile.” Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Niko nafanya vile? Niko nafanya mambo yenye Musamaria mwema alifanyaka? Wakati wengine wanateseka, ninaweza kufanya jambo fulani kusudi niwasaidie? Kwa mufano, ninaweza kusaidia wale wenye kuzeeka katika kutaniko, wajane, ao watoto wenye wazazi wao hawamutumikie Yehova? Ninaweza ‘kusema kwa namna yenye kufariji wale wenye wameshuka moyo’ kusudi niwatulize?’​—1 Te. 5:14; Yak. 1:27.

Kamata hatua ya kusaidia wengine, na utaona namna kila mutu atakuwa mwenye furaha sana (Picha hii inapatana na fungu la 12)

12. Juu ya nini tunakuwa wenye furaha wakati tuko wenye rehema?

12 Juu ya nini tunakuwa wenye furaha wakati tunaonyesha rehema? Wakati tunaonyesha wengine rehema, tunatoa, na Yesu alisema kama kutoa kunatufanya tukuwe wenye furaha. Sababu ingine ni hii: wakati tunaonyesha rehema, tunajua kama tunamufurahisha Yehova. (Mdo. 20:35; soma Waebrania 13:16.) Juu ya mutu mwenye kuonyesha rehema, Mufalme Daudi alisema hivi: “Yehova atamuchunga na kulinda uzima wake. Atatangazwa kuwa mwenye furaha katika dunia.” (Zb. 41:1, 2) Kama tunaonyesha wengine rehema na huruma, Yehova atatuonyesha pia rehema na tunaweza kuwa wenye furaha milele.​—Yak. 2:13.

JUU YA NINI “WALE WENYE MOYO SAFI” NI WENYE FURAHA?

13, 14. Juu ya nini ni jambo la maana kuwa “wenye moyo safi”?

13 Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye moyo safi, kwa sababu watamuona Mungu.” (Mt. 5:8) Kusudi tukuwe na moyo safi, tunapaswa kuendelea kufanya mawazo na tamaa zetu vibakie safi. Hilo ni jambo la maana sana ikiwa tunapenda Yehova akubali ibada yetu.​—Soma 2 Wakorinto 4:2; 1 Ti. 1:5.

14 Wale wenye moyo safi wanaweza kuwa na urafiki wa muzuri pamoja na Yehova, mwenye alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye wanafua kanzu zao.” (Ufu. 22:14) ‘Kufua kanzu zao’ maana yake nini? Kuhusu Wakristo watiwa-mafuta, maana yake, Yehova anawaona kuwa safi, atawapatia uzima wenye hauwezi kufa mbinguni, na watakuwa wenye furaha milele. Kuhusu watu wa kundi kubwa, wenye wako na tumaini la kuishi ku dunia, maana yake, Yehova anawaruhusu wakuwe marafiki wake juu anawaona kuwa wenye haki. Biblia inasema kama “wamefua kanzu zao na kuzifanya mweupe katika damu ya Mwana-Kondoo.”​—Ufu. 7:9, 13, 14.

15, 16. Namna gani wale wenye moyo safi wanaweza ‘kumuona Mungu’?

15 Yehova alisema hivi: “Hakuna mwanadamu mwenye anaweza kuniona na kuishi.” (Kut. 33:20) Sasa, namna gani wale wenye moyo safi wanaweza ‘kumuona Mungu’? Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “kuona” linaweza kuwa na maana ya kuwazia, kuelewa, ao kujua. Kwa hiyo, ‘kumuona Mungu’ maana yake kuelewa yeye ni Mutu wa namna gani na kupenda sifa zake. (Efe. 1:18) Yesu aliiga sifa za Mungu kwa ukamilifu, ndiyo maana alisema hivi: “Mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.”​—Yoh. 14:7-9.

16 Tena, ‘tunamuona Mungu’ wakati tunaona namna anatusaidia mu maisha yetu. (Yob. 42:5) Tunaweza pia “kuona” ao kukaza akili juu ya mambo ya muzuri yenye Yehova anaahidi kufanya kwa ajili ya wale wenye wanabakia safi na kumutumikia kwa ushikamanifu. Na watiwa-mafuta watamuona Yehova moja kwa moja wakati wanafufuliwa na kuenda mbinguni.​—1 Yo. 3:2.

TUNAWEZA KUWA WENYE FURAHA HATA KAMA TUKO NA MAGUMU

17. Juu ya nini wale wenye kufanya amani ni wenye furaha?

17 Kisha Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wenye kufanya amani.” (Mt. 5:9) Wakati tunakamata hatua ya kufanya amani na wengine, tunaweza kuwa wenye furaha. Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: “Tunda la haki linapandwa katika hali zenye amani kwa ajili ya wale wenye kufanya amani.” (Yak. 3:18) Kwa hiyo, kama uko unajikaza kufanya amani na mutu fulani mu kutaniko ao mu familia yenu, umuombe Yehova sana kusudi akusaidie ukuwe mutu mwenye kufanya amani. Kama unafanya vile, Yehova atakupatia roho yake takatifu, na roho hiyo itakusaidia kuonyesha sifa za Kikristo, na utakuwa mwenye furaha zaidi. Yesu alikazia kama ni jambo la maana sana kukamata hatua ili kufanya amani. Alisema hivi: “Basi, kama unaleta zawadi yako kwenye mazabahu na pale unakumbuka kama ndugu yako iko na jambo fulani juu yako, acha zawadi yako pale mbele ya mazabahu, na uende. Fanya kwanza amani na ndugu yako, na kisha urudie na utoe zawadi yako.”​—Mt. 5:23, 24.

18, 19. Juu ya nini Wakristo wanaweza kuwa wenye furaha hata kama wanateswa?

18 “Wenye furaha ni ninyi wakati watu wanawalaumu na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya uovu kwa sababu yangu.” Yesu alipenda kusema nini? Aliongeza hivi: “Mushangilie na kufurahi sana, kwa sababu zawabu [ao malipo] yenu ni kubwa mbinguni, kwa maana ni vile walitesa manabii wenye waliwatangulia.” (Mt. 5:11, 12) Wakati mitume walipigwa na kuamuriwa waache kuhubiri, ‘walitoka mbele ya Sanhedrini, wakiwa na furaha.’ Kwa kweli, hawakufurahi kwa sababu walipigwa. Lakini, walifurahi “kwa sababu walikuwa wamehesabiwa kuwa wanastahili kuvunjiwa heshima” juu ya jina la Yesu.​—Mdo. 5:41.

19 Leo, watu wa Yehova nao wanavumilia kwa furaha wakati wanateswa juu ya jina la Yesu. (Soma Yakobo 1:2-4.) Kama mitume, hatufurahi wakati tunapata magumu ao wakati tunateswa. Lakini, kama tunabakia waaminifu kwa Yehova, atatupatia ujasiri wenye tuko nao lazima kusudi tuvumilie. Fikiria jambo lenye lilimufikia Henryk Dornik na ndugu yake. Mu Mwezi wa 8, 1944, walitumwa mu kambi ya mateso. Wale wenye walikuwa wanawatesa walisema hivi: “Hawawezi kusadikishwa wafanye jambo lolote. Wanafurahia kufa juu ya imani yao.” Henryk alieleza hivi: “Hata kama sikutaka kufa juu ya imani yangu, kuteseka kwa ujasiri na heshima kwa sababu ya ushikamanifu wangu kwa Yehova kuliniletea furaha.” Aliongeza hivi: “Sala zenye nilikuwa ninatoa kwa bidii zilinisaidia nimukaribie Yehova, na alionekana kuwa Musaidizi wangu mwenye kutumainika.”

20. Juu ya nini kumutumikia “Mungu mwenye furaha” kunatuletea furaha?

20 Wakati Yehova, “Mungu mwenye furaha,” anapendezwa na sisi, tunaweza kuwa wenye furaha hata kama tunateswa, hata kama familia yetu inatupinga, hata kama tunagonjwa, ao hata kama tunazeeka. (1 Ti. 1:11) Tena, tunaweza kuwa wenye furaha kwa sababu Mungu wetu, “mwenye hawezi kusema uongo,” ametuahidi mambo mengi ya muzuri sana. (Tit. 1:2) Wakati Yehova atatimiza ahadi zake, hatutakumbuka tena magumu yenye tuko nayo leo. Kwa kweli, maisha yatakuwa muzuri sana mu Paradiso na tutakuwa wenye furaha sana kupita vile tunaweza kuwazia! Ndiyo, ‘tutapata furaha nyingi sana katika wingi wa amani.’​—Zb. 37:11.