Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 37

Ukuwe Tayari Kujitiisha kwa Yehova, Juu ya Nini na Namna Gani?

Ukuwe Tayari Kujitiisha kwa Yehova, Juu ya Nini na Namna Gani?

“Je, hatupaswe kujitiisha hata zaidi kwa Baba?” ​—EBR. 12:9.

WIMBO 9 Yehova Ni Mfalme Wetu!

KIFUPI CHA HABARI *

1. Juu ya nini tunapaswa kujitiisha kwa Yehova?

TUNAPASWA kujitiisha * kwa Yehova juu yeye ni Muumbaji wetu. Njo maana iko na haki ya kuwekea viumbe vyake kanuni. (Ufu. 4:11) Lakini kuko sababu ingine yenye inatuchochea tumutii: namna yake ya kutawala njo ya muzuri zaidi. Tangu zamani, wanadamu wengi wametawala wanadamu wengine. Lakini, wakati tunalinganisha namna yao ya kutawala na namna ya Yehova ya kutawala, tunaona kama Yehova njo Mutawala mwenye hekima zaidi, mwenye upendo zaidi, mwenye rehema zaidi, na mwenye huruma zaidi.​—Kut. 34:6; Ro. 16:27; 1 Yo. 4:8.

2. Kulingana na Waebrania 12:9-11, juu ya nini tunapaswa kujitiisha kwa Yehova?

2 Yehova anapenda tumutii, haiko tu kwa sababu tunamuogopa, lakini kwa sababu tunamupenda na tunamuona kuwa Baba yetu mwenye upendo. Mu barua yake kwa Waebrania, Paulo anafasiria kama tunapaswa “kujitiisha . . . kwa Baba” kwa sababu anatufundisha kwa “kwa faida yetu.”​—Soma Waebrania 12:9-11.

3. (a) Namna gani tunaonyesha kama tunajitiisha kwa Yehova? (b) Tutajibu maulizo gani?

3 Tunajitiisha kwa Yehova wakati tunajikaza sana ili kumutii katika mambo yote na wakati tunapinga muelekeo wa kutegemea uelewaji wetu wenyewe. (Mez. 3:5) Inakuwa mwepesi kwetu kujitiisha kwa Yehova wakati tunafikia kujua muzuri sifa zake za muzuri sana. Juu ya nini? Juu sifa hizo zinaonekana mu mambo yote yenye anafanya. (Zb. 145:9) Wakati tunajifunza mambo mingi juu ya Yehova, tunamupenda zaidi. Na kama tunamupenda Yehova, hatutakuwa na lazima ya liste ya sheria zenye kutuonyesha mambo yenye tunapaswa kufanya na mambo yenye hatupaswe kufanya. Tunajikaza ili kuwaza na kujisikia namna Yehova anapenda na kuepuka mambo ya mubaya. (Zb. 97:10) Lakini, wakati fulani, haiko mwepesi kumutii Yehova. Juu ya nini? Na wazee wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Gavana Nehemia? Baba wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Mufalme Daudi? Na mama wanaweza kujifunza nini kupitia mufano wa Maria, mama ya Yesu? Tutajibu ile maulizo mu habari hii.

JUU YA NINI INAWEZA KUWA NGUVU KUJITIISHA KWA YEHOVA?

4-5. Kulingana na Waroma 7:21-23, juu ya nini inaweza kuwa nguvu kujitiisha kwa Yehova?

4 Sababu moja yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kujitiisha kwa Yehova ni hii: sisi wote tuliriti zambi na hatukamilike. Kwa hiyo, mara mingi hatupendake kutii. Kisha Adamu na Eva kumuasi Mungu na kula tunda lenye Mungu aliwakataza, walijiwekea kanuni zao wenyewe. (Mwa. 3:22) Leo pia, wanadamu wengi wanaamua kumupinga Yehova na wanajiamulia wao wenyewe mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa.

5 Hata wale wenye wanamujua Yehova na kumupenda wanaweza kuona kama ni nguvu kujitiisha kwake mu mambo yote. Mutume Paulo alipambana na tatizo hilo. (Soma Waroma 7:21-23.) Kama Paulo, tunapenda kufanya mambo yenye kuwa sawa mu macho ya Yehova. Lakini, sikuzote, tunapaswa kupiganisha tamaa ya kufanya mambo ya mubaya.

6-7. Ni sababu gani ingine yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kujitiisha kwa Yehova? Leta mufano.

6 Sababu ingine yenye inaweza kufanya ikuwe nguvu kujitiisha kwa Yehova ni hii: tunachochewa na desturi zetu na mawazo ya watu wa mahali kwenye tulikomalia. Mawazo mingi ya wanadamu inapinga mapenzi ya Yehova, na inaweza kuomba tujikaze sana kila wakati ili tusikuwe na mawazo yenye watu wengi wako nayo. Fikiria mufano moja tu.

7 Katika maeneo fulani, ni jambo la kawaida kukaza vijana watumie maisha yao ili kutafuta feza mingi. Dada mumoja mwenye kuitwa Maria * alipambana na tatizo hilo. Mbele ya kujifunza juu ya Yehova, alisomea ku masomo moja kati ya masomo ya muzuri zaidi ya inchi yao. Watu wa familia ya Maria walimukaza atafute kazi ya mushahara muzuri sana kusudi watu wamuheshimie sana. Maria naye alipenda vile. Lakini, kisha kujifunza juu ya Yehova na kufikia kumupenda, alibadilisha miradi yake. Hata hivyo, anasema hivi: “Wakati fulani, ninapata kazi ya muzuri sana yenye inaweza kuniletea feza mingi lakini yenye inaweza kuvuruga programu yangu ya kiroho. Juu ya namna nilikomaa, ingali nguvu kwangu kukataa ile kazi. Ninapaswa kumulilia Yehova anisaidie ili nisikubali kazi yenye inaweza kufanya niache kumutumikia.”​—Mt. 6:24.

8. Tutazungumuzia nini sasa?

8 Tunajiletea faida wakati tunajitiisha kwa Yehova. Lakini, wale wenye kuwa na mamlaka fulani, kama vile wazee, baba, na mama, wako na sababu ingine ya kufuata muongozo wa Mungu: kufuata muongozo wa Mungu kunaletea wengine faida. Tuzungumuzie basi mifano fulani ya Biblia yenye inatufundisha namna ya kutumia mamlaka mu njia yenye inamupendeza Yehova.

MAMBO YENYE WAZEE WANAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MUFANO WA NEHEMIA

Wazee wanasaidia katika kazi yenye inafanywa ku Jumba la Ufalme, kama vile Nehemia alisaidia katika kazi ya kujenga upya Yerusalemu (Picha hizi zinapatana na fungu la 9-11) *

9. Nehemia alipambana na magumu gani?

9 Yehova amepatia wazee daraka la maana la kuchunga watu wake. (1 Pe. 5:2) Namna Nehemia alitendea watu wa Yehova inaweza kufundisha wazee mambo mingi. Juu Nehemia alikuwa gavana wa Yuda, alikuwa na mamlaka makubwa. (Ne. 1:11; 2:7, 8; 5:14) Wazia magumu fulani yenye Nehemia alipambana nayo. Alipata habari kama watu walikuwa wamechafua hekalu na hawakukuwa wanategemeza Walawi kwa kuwapatia michango kama vile Sheria iliamuru. Wayahudi walikuwa wanavunja sheria ya Sabato, na wanaume fulani walikuwa wameoa wanamuke wa mataifa ingine. Gavana Nehemia alipaswa kushugulikia hali hiyo ya nguvu.​—Ne. 13:4-30.

10. Namna gani Nehemia alishugulikia magumu yenye alipambana nayo?

10 Nehemia hakutumia mamlaka yake mubaya kwa kulazimisha watu wafuate kanuni zake mwenyewe. Lakini, alisali kwa bidii ili kumuomba Yehova muongozo, na alifundisha watu sheria ya Yehova. (Ne. 1:4-10; 13:1-3) Pia, Nehemia alifanya kazi kwa unyenyekevu pamoja na ndugu zake, na hata aliwasaidia kujenga upya kuta za Yerusalemu.​—Ne. 4:15.

11. Kulingana na 1 Watesalonike 2:7, 8, namna gani wazee wanapaswa kutendea ndugu na dada wa kutaniko?

11 Pengine wazee hawatapambana na magumu kama ile ya Nehemia, lakini wanaweza kumuiga mu njia za mingi. Kwa mufano, wanatumika kwa bidii ili kusaidia ndugu na dada zao. Na hawaache mamlaka yao iwafanye wakuwe na majivuno. Lakini, wanatendea ndugu na dada zao kwa upendo. (Soma 1 Watesalonike 2:7, 8.) Kwa sababu wako wanyenyekevu na wanapenda kabisa ndugu zao, wanazungumuza nao kwa upole. Andrew, mwenye amekuwa muzee wa kutaniko kwa miaka mingi, anasema hivi: “Nimetambua kama wakati muzee iko na upendo na iko mwenye urafiki, hilo linagusa mioyo ya ndugu na dada. Sifa hizo zinachochea ndugu na dada wa kutaniko waunge wazee mukono.” Tony, ndugu mwingine mwenye amekuwa muzee kwa miaka mingi, anasema hivi: “Ninajikaza kutumia shauri lenye kuwa mu Wafilipi 2:3 na sikuzote ninajikaza ili kuona wengine kuwa wazuri zaidi kuliko mimi. Kufanya vile kunanisaidia niepuke kulazimisha wengine wanitii.”

12. Juu ya nini wazee wa kutaniko wanapaswa kuwa wanyenyekevu?

12 Wazee wanapaswa kuwa wanyenyekevu, kama vile Yehova. Hata kama Yehova njo Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi katika ulimwengu wote, “anainama” ili kuinua “mutu wa hali ya chini kutoka katika mavumbi.” (Zb. 18:35; 113:6, 7) Kwa kweli, Yehova anachukia watu wenye kuwa na kiburi na majivuno.​—Mez. 16:5.

13. Juu ya nini muzee anapaswa “kuzuia ulimi wake”?

13 Muzee mwenye kujitiisha kwa Yehova anapaswa “kuzuia ulimi wake.” Kama hafanye vile, anaweza kuzungumuza kwa ukali na ndugu ao dada mwenye anamukosea heshima. (Yak. 1:26; Gal. 5:14, 15) Andrew, mwenye tumekwisha kuzungumuzia, anasema hivi: “Wakati fulani, ninataka kuzungumuza kwa ukali na ndugu ao dada mwenye anaonekana kama ananikosea heshima. Lakini, nimefikiri sana juu ya mifano ya wanaume waaminifu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, na hilo limenisaidia nione kama, kuwa munyenyekevu na mupole ni jambo la maana.” Wazee wanaonyesha kama wanajitiisha kwa Yehova wakati wanazungumuza kwa upendo na upole na ndugu na dada wa kutaniko, hata na wazee wenzao.​—Kol. 4:6.

MAMBO YENYE BABA WANAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MUFANO WA MUFALME DAUDI

14. Yehova amepatia baba daraka gani, na anawaomba wafanye nini?

14 Yehova amepatia baba daraka la kuwa kichwa cha familia, na anamuomba azoeze watoto wake, awapatie nizamu ao kuwarekebisha. (1 Ko. 11:3; Efe. 6:4) Lakini mamlaka ya baba iko na mipaka; atatoa hesabu kwa Yehova, mwenye alianzisha familia. (Efe. 3:14, 15) Baba wanaonyesha kama wanajitiisha kwa Yehova wakati wanatumia mamlaka yao kwa njia yenye inamupendeza. Wanaweza kujifunza mambo mingi kwa kujifunza maisha ya Mufalme Daudi.

Sala za baba Mukristo zinapaswa kuonyesha familia yake kama iko munyenyekevu (Picha hii inapatana na fungu la 15-16) *

15. Juu ya nini Mufalme Daudi ni mufano muzuri wenye baba wanapaswa kufikiria?

15 Yehova alimuweka Daudi kuwa kichwa cha familia yake na pia kichwa cha taifa lote la Israeli. Kwa sababu Daudi alikuwa mufalme, alikuwa na mamlaka makubwa. Wakati fulani, alitumia mubaya mamlaka yake na akafanya makosa mazito. (2 Sa. 11:14, 15) Lakini alionyesha kama alijitiisha kwa Yehova kwa kukubali nizamu. Katika sala, alimuambia Yehova mambo yote yenye ilikuwa mu moyo wake. Na alijikaza sana ili kutii mashauri ya Yehova. (Zb. 51:1-4) Tena, alikuwa munyenyekevu sana, na hilo lilifanya akubali mashauri yenye wanaume wenzake walimutolea, na hata wanamuke. (1 Sa. 19:11, 12; 25:32, 33) Daudi alijifunza mambo fulani kupitia makosa yake na alitia utumishi wa Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yake.

16. Baba wanaweza kujifunza mambo gani kupitia mufano wa Daudi?

16 Ona mambo fulani tu yenye baba wanaweza kujifunza kupitia mufano wa Mufalme Daudi: Usitumie mubaya mamlaka yenye Yehova amekupatia. Ukubali makosa yako, na ukubali mashauri yenye kutegemea Biblia yenye wengine wanakutolea. Ukifanya vile, familia yako itakuheshimia juu ya unyenyekevu wako. Wakati unasali pamoja na familia yako, umuelezee Yehova mambo yenye iko mu moyo wako, uache wasikie kama unamutegemea kabisa. Na zaidi ya yote, utie utumishi wa Yehova pa nafasi ya kwanza mu maisha yako. (Kum. 6:6-9) Mufano wako muzuri uko kati ya zawadi za maana sana zenye unaweza kupatia familia yako.

MAMBO YENYE MAMA WANAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA MUFANO WA MARIA

17. Yehova amepatia mama daraka gani?

17 Yehova amepatia mama daraka la maana sana mu familia, na amemupatia mamlaka fulani juu ya watoto wake. (Mez. 6:20) Kwa kweli, mambo yenye mama anafanya na kusema inaweza kuwa na matokeo juu ya watoto wake maisha yao yote. (Mez. 22:6) Ona mambo yenye mama wanaweza kujifunza kupitia mufano wa Maria, mama ya Yesu.

18-19. Mama wanaweza kujifunza mambo gani kupitia mufano wa Maria?

18 Maria alijua Maandiko muzuri sana. Alikuwa anamuheshimia Yehova sana na alikuwa na urafiki wa pekee pamoja naye. Alikuwa tayari kutii muongozo wa Yehova, hata kama kufanya vile kungebadilisha maisha yake yote.​—Lu. 1:35-38, 46-55.

Kama mama anachoka ao anakasirika, inaweza kuomba ajikaze sana ili aonyeshe watu wa familia yake upendo (Picha hii inapatana na fungu la 19) *

19 Mama, munaweza kumuiga Maria mu njia mbalimbali. Namna gani? Njia ya kwanza, kwa kufanya urafiki pamoja na Yehova ukuwe nguvu kupitia funzo la pekee la Biblia na sala za kipekee. Njia ya pili, kwa kuwa tayari kufanya mabadiliko mu maisha yako ili kumupendeza Yehova. Kwa mufano, pengine wazazi wako wenye walikukomalisha walikuwa wanakasirika haraka na walikuwa wanazungumuza kwa ukali na watoto wao. Kwa hiyo, unaweza kuwaza kama ni jambo la kawaida kutendea watoto wako vile. Hata kisha kujifunza kanuni za Yehova, unaweza kuona kama ni nguvu kuendelea kuonyesha uvumilivu na utulivu, zaidi sana kama watoto wako wanafanya makosa wakati uko mwenye kuchoka. (Efe. 4:31) Wakati kama huo, ni jambo la maana sana umuombe Yehova musaada katika sala. Mama mumoja mwenye kuitwa Lydia anasema hivi: “Wakati fulani, nilipaswa kusali sana ili nisiseme kwa ukali wakati mutoto wangu alikosa kunitii. Na hata nilikuwa ninaacha kusema mambo yenye nilikuwa ninasema, na nilisali kwa Yehova kimya-kimya ili kumuomba musaada. Sala inanisaidia niendelee kutulia.”​—Zb. 37:5.

20. Mama fulani wako na tatizo gani, na wanaweza kufanya nini ili kushinda tatizo hilo?

20 Mama fulani wako na tatizo lenye kufanana na hilo: wanaona kama ni nguvu kuonyesha watoto wao kama wanawapenda. (Tit. 2:3, 4) Wanamuke fulani wamekomalia mu familia kwenye wazazi wao hawakukuwa na uhusiano muzuri pamoja na watoto wao. Kama njo vile ulikomaa, haupaswe kufanya makosa ileile yenye wazazi wako walifanya. Mama mwenye anapenda kuishi kulingana na mapenzi ya Yehova anaweza kuwa na lazima ya kujifunza namna ya kuonyesha watoto wake kama anawapenda. Inaweza kuwa nguvu kwake kubadilisha namna yake ya kuwaza, ya kujisikia, na kutenda. Lakini inawezekana, na kufanya vile kutamuletea faida yeye mwenyewe na familia yake.

ENDELEA KUJITIISHA KWA YEHOVA

21-22. Kulingana na Isaya 65:13, 14, kujitiisha kwa Yehova kunatuletea faida gani?

21 Mufalme Daudi alijua kama kujitiisha kwa Yehova kunaleta faida. Aliandika hivi: “Maagizo kutoka kwa Yehova ni yenye haki, yanafanya moyo ushangilie; amri ya Yehova ni safi, inafanya macho yangae. Mutumishi wako ameonywa kupitia hizo; katika kuzishika, kuko zawabu kubwa.” (Zb. 19:8, 11) Leo, tunaweza kuona tofauti kati ya watu wenye wanajitiisha kwa Yehova na wale wenye wanakataa mashauri yake yenye upendo. Wale wenye wanajitiisha kwa Yehova ‘wanapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya hali ya muzuri ya moyo.’​—Soma Isaya 65:13, 14.

22 Wakati wazee, baba, na mama wanajitiisha kwa Yehova, maisha yao inakuwa muzuri zaidi, familia zao zinakuwa zenye furaha zaidi, na kutaniko lote linakuwa na umoja zaidi. Na jambo la maana zaidi, wanamufurahisha Yehova. (Mez. 27:11) Hakuna jambo lingine lenye linapita kumufurahisha Yehova.

WIMBO 123 Kutii Utaratibu wa Kitheokrasi kwa Ushikamanifu

^ fu. 5 Habari hii itazungumuzia juu ya nini tunapaswa kujitiisha kwa Yehova. Itazungumuzia pia mambo yenye wazee, baba, na mama, ni kusema wale wote wenye kuwa na mamlaka fulani, wanaweza kujifunza kupitia mufano wa Gavana Nehemia; Mufalme Daudi; na Maria, mama ya Yesu.

^ fu. 1 MAFASIRIO YA MANENO FULANI: Maneno kujitiisha na ujitiisho iko na maana ya mubaya kwa wale wenye wanalazimishwa kutii mutu fulani. Lakini, watu wa Mungu wanachagua kumutii, kwa hiyo, hawaone kama ni jambo la mubaya kujitiisha kwa Mungu.

^ fu. 7 Majina fulani imebadilishwa katika habari hii.

^ fu. 62 MAFASIRIO YA PICHA: Muzee wa kutaniko na mutoto wake mwanaume wanasaidia kufanya kazi ya kutunza Jumba la Ufalme, kama vile Nehemia alisaidia kufanya kazi ya kujenga upya kuta za Yerusalemu.

^ fu. 64 MAFASIRIO YA PICHA: Baba anasali kwa Yehova kwa ajili ya familia yake.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Mutoto mwanaume anacheza michezo ya video kwa saa mingi hata kama hajamaliza kazi zake za masomo na kazi za mu nyumba. Mama yake, mwenye anatoka ku kazi na amechoka, anamupatia nizamu, bila kukasirika na bila kutumia maneno makali.