Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 39

“Angalia! Kundi Kubwa la Watu”

“Angalia! Kundi Kubwa la Watu”

“Angalia! kundi kubwa la watu, wenye hakuna mutu mwenye aliweza kuhesabia, . . . wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.”​—UFU. 7:9.

WIMBO 60 Ni Uzima Kwao

KIFUPI CHA HABARI *

1. Mutume Yohana alikuwa mu hali gani katika mwaka wa 95 hivi?

KATIKA mwaka wa 95 hivi, mutume Yohana alikuwa mu hali ya huzuni sana. Alikuwa mwenye kuzeeka na alikuwa anafungwa mu kisiwa cha Patmo, na pengine yeye tu njo mutume mwenye alikuwa angali muzima. (Ufu. 1:9) Alijua kama wapinzani walikuwa wanafundisha mambo ya uongo na walikuwa wanafanya Wakristo wakuwe na migawanyiko. Ilionekana kuwa Wakristo wote wa kweli walikuwa karibu kuisha.​—Yud. 4; Ufu. 2:15, 20; 3:1, 17.

Mutume Yohana aliona “kundi kubwa la watu” wenye kuvaa kanzu za mweupe na wenye kuwa na matawi ya mitende mu mikono yao (Picha hii inapatana na fungu la 2)

2. Kulingana na Ufunuo 7:9-14, ni maono gani yenye kupendeza sana yenye Yohana alipewa? (Ona picha ku jalada la gazeti hili.)

2 Katika hali hizo za nguvu sana, Mungu alimuonyesha Yohana maono ya kiunabii yenye kupendeza. Katika ile maono, malaika wanaambiwa wazuie pepo za uharibifu za ile taabu kubwa mupaka kikundi cha watumwa kitiwe muhuri wa mwisho. (Ufu. 7:1-3) Kikundi hicho kinafanyizwa na watu 144 000 wenye watatawala pamoja na Yesu mbinguni. (Lu. 12:32; Ufu. 7:4) Kisha, Yohana anazungumuzia kikundi kingine, kikubwa sana mupaka anasema hivi: “Angalia!,” neno hilo linaweza kuonyesha kama mambo yenye anaona inamushangaza sana. Yohana anaona nini? “Kundi kubwa la watu, wenye hakuna mutu mwenye aliweza kuhesabia, kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga, wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.” (Soma Ufunuo 7:9-14.) Wazia namna Yohana alifurahi sana wakati alijua kama, wakati wenye kuja, watu wengi sana wangemuabudu Mungu katika njia ya muzuri!

3. (a) Juu ya nini maono ya Yohana inapaswa kutia nguvu imani yetu? (b) Tutajifunza nini mu habari hii?

3 Kwa kweli, ile maono ilitia nguvu imani ya Yohana. Ile maono inapaswa kutia nguvu zaidi imani yetu, juu tunaishi wakati wenye iko inatimia! Tumeona kukusanywa kwa mamilioni ya watu wenye kuwa na tumaini la kuokoka taabu kubwa na kuishi milele ku dunia. Mu habari hii, tutajifunza namna Yehova alisaidia watu wake watambue kundi kubwa la watu ni nani, miaka zaidi ya 80 yenye imepita. Kisha, tutazungumuzia mambo mbili juu ya kundi kubwa la watu: (1) namna ni wengi sana na (2) watu wenye kuwa mu kundi hilo wanatoka mu mataifa yote. Ile mambo itatia nguvu imani ya watu wote wa kikundi hicho.

KUNDI KUBWA LA WATU WATAISHI WAPI?

4. Ni kweli gani ya Biblia yenye dini zenye kujiita kuwa za Kikristo hazielewe, lakini Wanafunzi wa Biblia walielewa nini?

4 Mara mingi dini zenye kujiita kuwa za Kikristo hazifundishe kweli ya Biblia yenye kuonyesha kama watu wenye kumutii Mungu wataishi milele ku dunia. (2 Ko. 4:3, 4) Leo, dini za mingi zenye kujiita kuwa za Kikristo zinafundisha kama watu wote wazuri wanaendaka mbinguni wakati wanakufa. Lakini, kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia wenye walikuwa wanachapisha gazeti Munara wa Mulinzi kuanzia mwaka wa 1879, hawakukuwa wanafundisha vile. Walielewa kama Mungu atarudisha Paradiso ku dunia na kama mamilioni ya watu wenye kumutii Mungu wataishi hapa ku dunia, haiko mbinguni. Lakini, iliomba wakati ili waelewe waziwazi ikiwa watu hao wenye kutii wangekuwa nani.​—Mt. 6:10.

5. Wanafunzi wa Biblia waliamini nini juu ya wale 144 000?

5 Kwa kweli, wanafunzi wa Biblia walielewa pia kupitia Maandiko kama kikundi fulani cha watu ‘wangenunuliwa kutoka katika dunia’ ili kutawala pamoja na Yesu mbinguni. (Ufu. 14:3) Kikundi hicho kingefanyizwa na Wakristo 144 000 wenye bidii na wenye kujitoa kwa Mungu, wenye walimutumikia Mungu kwa uaminifu wakati walikuwa ku dunia. Sasa, waliamini nini juu ya kundi kubwa la watu?

6. Wanafunzi wa Biblia waliamini nini juu ya kundi kubwa la watu?

6 Katika maono yake, Yohana aliona kikundi hicho cha watu “wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.” (Ufu. 7:9) Ile maneno ilifanya Wanafunzi wa Biblia wafikiri kama kundi kubwa la watu wangeishi mbinguni kama vile wale 144 000. Kama wale 144 000 na kundi kubwa la watu wangeishi mbinguni, kungekuwa tofauti gani kati ya vile vikundi mbili? Wanafunzi wa Biblia walifikiri kama kundi kubwa la watu lingefanyizwa na Wakristo wenye hawakumutii Mungu kabisa-kabisa wakati walikuwa ku dunia. Hata kama walikuwa na mwenendo muzuri kwa kiasi fulani, pengine wamoja kati yao walibakia mu dini zenye kujiita kuwa za Kikristo. Wanafunzi wa Biblia waliwaza kama watu hao walimupenda Mungu kwa kadiri fulani, lakini hawakustahili kutawala pamoja na Yesu. Kwa sababu kundi kubwa la watu walimupenda Mungu kwa kadiri fulani tu, walistahili kuwa mbinguni mbele ya kiti cha Ufalme lakini hawakupaswa kukaa ku viti vya Ufalme.

7. Kulingana na mawazo ya Wanafunzi wa Biblia, ni nani wangeishi ku dunia wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja, na Wanafunzi wa Biblia waliamini nini juu ya wanaume waaminifu wa zamani?

7 Sasa, ni nani wangeishi ku dunia? Wanafunzi wa Biblia waliamini kama kisha wale 144 000 kuenda mbinguni, mamilioni ya watu wengine wangepewa uzima ku dunia ili wapate baraka za Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu. Wanafunzi wa Biblia hawakuwaza kama ile mamilioni ya watu wangemutumikia Yehova mbele Utawala wa Kristo uanze. Lakini, waliwaza kama kikundi hicho cha watu wangefundishwa njia za Yehova wakati wa Utawala wa Miaka Elfu. Kisha, wale wenye wangetii kanuni za Yehova wangepata uzima wa milele ku dunia, lakini wale wenye wangeasi wangeharibiwa. Wanafunzi wa Biblia walifikiri pia kama pengine watu fulani wenye wangekuwa “wakubwa” ku dunia wakati huo, kutia ndani “wakubwa wa zamani” (wanaume waaminifu wenye walikufa mbele Kristo atokee) wangepata uzima mbinguni ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu Moja.​—Zb. 45:16.

8. Wanafunzi wa Biblia walifikiri kama kulikuwa vikundi ngapi katika kusudi la Mungu?

8 Kwa hiyo, Wanafunzi wa Biblia walifikiri kama kulikuwa vikundi tatu: (1) wale 144 000, wenye wangetawala pamoja na Yesu mbinguni; (2) kundi kubwa la Wakristo wenye hawakukuwa na bidii sana, wenye wangesimama mbele ya kiti cha ufalme cha Yesu mbinguni; na (3) mamilioni ya watu wenye wangefundishwa njia za Yehova ku dunia wakati wa Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja. * Lakini kisha wakati fulani, Yehova aliwasaidia waelewe jambo hilo muzuri zaidi.​—Mez. 4:18.

WANAELEWA MAMBO MUZURI ZAIDI

Ku mukusanyiko wa mwaka wa 1935, watu wengi sana wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia walibatizwa (Picha hii inapatana na fungu la 9)

9. (a) Ni katika njia gani kundi kubwa la watu ku dunia wanasimama “mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo”? (b) Juu ya nini mafasirio ya andiko la Ufunuo 7:9 inapatana na akili?

9 Katika mwaka wa 1935, Mashahidi wa Yehova walielewa muzuri kundi kubwa la watu wenye kuzungumuziwa mu maono ya Yohana. Mashahidi wa Yehova walifikia kuelewa kama haiko lazima kundi kubwa la watu wakuwe mbinguni moja kwa moja ili wasimame “mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya Mwana-Kondoo.” Lakini, wanasimama mbinguni kwa njia ya mufano. Hata kama wanaishi ku dunia, kundi kubwa la watu wanasimama “mbele ya kile kiti cha ufalme” kwa kutambua mamlaka ya Yehova na kwa kujitiisha chini ya Mamlaka yake Makubwa. (Isa. 66:1) Wanasimama “mbele ya Mwana-Kondoo” kwa kuonyesha imani katika zabihu ya bei ya ukombozi ya Yesu. Vilevile, andiko la Matayo 25:31, 32, linasema kama Yesu atakaa ku kiti chake cha ufalme chenye utukufu na “mataifa yote,” kutia ndani watu waovu, “yatakusanywa mbele” yake. Ni wazi kama ile mataifa yote haiko mbinguni, lakini iko ku dunia. Ile mafasirio ya mupya inapatana na akili. Inaonyesha juu ya nini Biblia haiseme kama kundi kubwa la watu watapelekwa mbinguni. Ni kikundi kimoja tu njo kinapewa ahadi ya kupata uzima wa milele mbinguni, ni kusema, wale 144 000, wenye “watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia” pamoja na Yesu.​—Ufu. 5:10.

10. Juu ya nini ni jambo la lazima kundi kubwa la watu wafundishwe njia za Yehova mbele Utawala wa Miaka Elfu Moja uanze?

10 Kwa hiyo, kuanzia mwaka wa 1935, Mashahidi wa Yehova wameelewa kama kundi kubwa lenye Yohana aliona mu maono linafanyizwa na kikundi cha Wakristo waaminifu wenye wako na tumaini la kuishi milele ku dunia. Ili kuokoka taabu kubwa, kundi kubwa la watu wanapaswa kufundishwa njia za Yehova mbele Utawala wa Miaka Elfu Moja uanze. Wanapaswa kuonyesha imani yenye nguvu ili “kuponyoka mambo haya yote yenye yanapaswa kutokea” mbele Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu Moja uanze.​—Lu. 21:34-36.

11. Juu ya nini Wanafunzi fulani wa Biblia walifikiri kama pengine watu fulani wangeenda mbinguni kisha Utawala wa Miaka Elfu Moja?

11 Tuseme nini juu ya wazo lenye lilionyesha kama watu fulani wenye kuwa mifano ya muzuri ku dunia wangeenda mbinguni kisha Utawala wa Miaka Elfu Moja? Wazo hilo lilizungumuziwa miaka fulani mbele mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 Mwezi wa 2, 1913. Pengine mutu angejiuliza hivi: ‘Juu ya nini watu waaminifu wa zamani wapate uzima hapa ku dunia lakini watu wenye hawakukuwa waaminifu kabisa wapate zawadi ya uzima mbinguni?’ Kwa kweli, waliwaza vile juu ya mawazo mbili yenye kufuata yenye ilikuwa na makosa, yenye ilionyesha kama: (1) kundi kubwa la watu wangeishi mbinguni na (2) kama kundi kubwa la watu lingefanyizwa na Wakristo wenye hawakukuwa waaminifu kabisa-kabisa.

12-13. Watiwa-mafuta na kundi kubwa la watu wanaelewa nini juu ya zawadi yao?

12 Lakini, kama vile tumeona, kuanzia mwaka wa 1935, Mashahidi wa Yehova wameelewa waziwazi kama wenye wataokoka Armagedoni ni kundi kubwa la watu wenye Yohana aliona mu maono. ‘Watatoka katika ile taabu kubwa’ hapa ku dunia, na “wataendelea kusema kwa sauti kubwa: ‘Wokovu wetu unatoka kwa Mungu wetu, mwenye kukaa kwenye kiti cha ufalme, na kwa Mwana-Kondoo.’” (Ufu. 7:10, 14) Zaidi ya hilo, Maandiko inafundisha kama wale wenye watafufuliwa ili kupata uzima mbinguni wanapata “kitu kizuri zaidi” kupita watu waaminifu wa zamani. (Ebr. 11:40) Ile mafasirio ya mupya yenye ndugu na dada walipata mu mwaka wa 1935, iliwachochea waalike kwa bidii watu wenye wangemutumikia Yehova wakiwa na tumaini la kupata uzima wa milele ku dunia.

13 Wale wa kundi kubwa la watu wanafurahia tumaini lao. Wanaelewa kama Yehova anaamua kwenye watumishi wake waaminifu watamutumikia, ikuwe mbinguni ao ku dunia. Watiwa-mafuta na kundi kubwa la watu, wote wanaelewa kama hawatapata zawadi kwa nguvu yao wenyewe, lakini watapata zawadi hiyo kupitia tu fazili zenye hazistahiliwe za Yehova zenye anaonyesha kupitia bei ya ukombozi ya Kristo.​—Ro. 3:24.

NI WENGI SANA

14. Kisha mwaka wa 1935, juu ya nini watu wengi walikuwa wanajiuliza namna unabii juu ya kundi kubwa la watu ungetimizwa?

14 Kisha watu wa Yehova kuelewa mambo muzuri juu ya kundi kubwa la watu mu mwaka wa 1935, wengi waliendelea kujiuliza namna gani wale wenye kuwa na tumaini la kuishi milele ku dunia wangekuwa wengi sana. Kwa mufano, Ronald Parkin alikuwa na miaka 12 wakati kundi kubwa la watu lilitambulishwa waziwazi. Anakumbuka hivi: “Wakati huo, kulikuwa wahubiri karibu 56 000 mu dunia yote na wengi, pengine karibu wote, walikuwa watiwa-mafuta. Watu wa kundi kubwa hawakuonekana kuwa wengi sana.”

15. Namna gani kundi kubwa la watu liliendelea kukusanywa?

15 Lakini, mu miaka yenye ilifuata, wamisionere walitumwa mu inchi mingi na hesabu ya Mashahidi wa Yehova iliongezeka haraka. Kisha, mu mwaka wa 1968, tulianza kujifunza Biblia na watu kwa kutumia kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele. Kitabu hicho kilifasiria kweli ya Biblia kwa njia ya mwepesi, na hilo lilifanya watu wengi wapole wavutwe kwa Yehova kuliko zamani. Mu miaka ine, wanafunzi zaidi ya nusu milioni walibatizwa. Wakati Kanisa Katoliki lilianza kupoteza mamlaka yake mu Amerika ya Latini na mu inchi zingine na wakati kazi yetu iliondolewa vizuizi mu Ulaya Mashariki na mu sehemu fulani za Afrika, mamilioni ingine ya watu walibatizwa. (Isa. 60:22) Mu miaka ya juzi-juzi, tengenezo la Yehova limetoa vyombo vingine vyenye kufaa ili kusaidia watu wajifunze mambo yenye Biblia inafundisha. Kwa kweli, kundi kubwa la watu, lenye kuwa sasa na watu zaidi ya milioni munane, limekusanywa.

KUNDI KUBWA KUTOKA KATIKA MATAIFA YOTE

16. Watu wa kundi kubwa wenye kukusanywa wanatoka wapi?

16 Wakati Yohana aliandika maono yake, alisema kama kundi kubwa la watu wangetoka mu “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga.” Mbele ya pale, nabii Zekaria alikuwa ametabiri jambo fulani lenye kufanana na hilo. Aliandika hivi: “Katika siku hizo watu kumi (10) kutoka katika luga zote za mataifa watashika, ndiyo, watashika kwa nguvu kanzu ya Muyahudi, wakisema: ‘Tunataka kuenda pamoja na ninyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu iko pamoja na ninyi.’”​—Zek. 8:23.

17. Ni kazi gani inafanywa ili kusaidia watu wa mataifa yote na luga zote?

17 Mashahidi wa Yehova wanaelewa kama ili kukusanya watu wa luga zote, habari njema inapaswa kuhubiriwa mu luga za mingi. Tumetafsiri vichapo vya kusaidia kujifunza Biblia kwa miaka zaidi ya 130, lakini, leo tunafanya kazi kubwa zaidi ya kutafsiri katika mamia ya luga. Ni wazi, Yehova iko anafanya muujiza mu siku zetu: kukusanya kundi kubwa la watu kutoka mu mataifa yote. Juu chakula cha kiroho kinapatikana mu luga za mingi zaidi, kikundi hicho chenye kutoka mu mataifa yote kinamuabudu Yehova katika umoja. Na Mashahidi wanajulikana kupitia kazi yao ya kuhubiri kwa bidii na kupitia upendo wao wa kindugu. Jambo hilo linatia sana nguvu imani yetu!​—Mt. 24:14; Yoh. 13:35.

ILE MAONO IKO NA MAANA GANI KWETU?

18. (a) Kulingana na Isaya 46:10, 11, juu ya nini hatushangae kuona kama Yehova ametimiza unabii juu ya kundi kubwa la watu? (b) Juu ya nini wale wenye kuwa na tumaini la kuishi ku dunia hawaone kama wanakosa kitu fulani?

18 Tunafurahia sana unabii juu ya kundi kubwa la watu! Hatushangae kuona kama Yehova ametimiza unabii huo mu njia ya ajabu sana. (Soma Isaya 46:10, 11.) Watu wa kundi kubwa wako wenye shukrani juu ya tumaini lenye Yehova amewapatia. Hawaone kama wanakosa kitu fulani kwa sababu hawatiwe mafuta kwa roho ya Mungu ili kutumika na Yesu mbinguni. Maandiko inazungumuzia wanaume na wanamuke wenye imani wenye waliongozwa na roho takatifu; lakini hawako kati ya wale 144 000. Mufano moja ni Yohana Mubatizaji. (Mt. 11:11) Mufano mwingine ni Daudi. (Mdo. 2:34) Watu hao pamoja na watu wengine wengi watafufuliwa ili kupata uzima mu paradiso hapa ku dunia. Wote, pamoja na watu wa kundi kubwa, watapata nafasi ya kuonyesha ushikamanifu wao kwa Yehova na utawala wake.

19. Kama tunaelewa maana ya maono ya Yohana juu ya kundi kubwa la watu, tutafanya nini?

19 Leo kuliko zamani, Mungu anaunganisha mamilioni ya watu kutoka mu mataifa yote. Ikuwe tuko na tumaini la kuishi mbinguni ao ku dunia, tunapaswa kusaidia watu wengi zaidi kadiri tunaweza ili wakuwe kati ya kundi kubwa la watu wa “kondoo wengine.” (Yoh. 10:16) Hivi karibuni, Yehova ataleta taabu kubwa yenye ilitabiriwa yenye itaharibu serikali na dini zenye zimetesa wanadamu. Watu wote wa kundi kubwa wako na pendeleo la pekee sana: kumutumikia Yehova ku dunia milele!​—Ufu. 7:14.

WIMBO 139 Wazia Wakati Vitu Vyote Vitakuwa Vipya

^ fu. 5 Habari hii itazungumuzia maono ya kiunabii ya Yohana juu ya kukusanywa kwa “kundi kubwa la watu.” Kwa kweli, itatia nguvu imani ya watu wote wa kikundi hicho chenye kubarikiwa sana.

^ fu. 8 Ona kitabu Mashahidi wa Yehova​—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu, uku. 159-163.