Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 38

“Mukuje Kwangu, . . . na Mimi Nitawapumuzisha”

“Mukuje Kwangu, . . . na Mimi Nitawapumuzisha”

“Mukuje kwangu, ninyi wote wenye kuteseka na wenye kulemewa na mizigo, na mimi nitawapumuzisha.”​—MT. 11:28.

WIMBO 17 ‘Nataka’

KIFUPI CHA HABARI *

1. Kulingana na Matayo 11:28-30, Yesu alitoa ahadi gani?

YESU alitolea watu wengi wenye walikuwa wanamusikiliza ahadi ya muzuri sana. Alisema hivi: “Mukuje kwangu” na “mimi nitawapumuzisha.” (Soma Matayo 11:28-30.) Ile haikukuwa ahadi ya burebure. Kwa mufano, fikiria namna alimutendea mwanamuke mwenye alikuwa anateseka na ugonjwa fulani mubaya sana.

2. Yesu alimutendea namna gani mwanamuke mumoja mwenye alikuwa mugonjwa?

2 Mwanamuke huyo alikuwa na lazima ya musaada kabisa. Alikuwa ameenda kwa wanganga wengi, kwa sababu alitumaini kama wangemuponyesha. Alikuwa ameteseka kwa miaka 12, bila kupata mutu mwenye angeweza kumuponyesha. Kulingana na Sheria, hakukuwa safi. (Law. 15:25) Kisha, akasikia kama Yesu alikuwa anaponyesha watu wenye walikuwa wanateseka, kwa hiyo, alienda kumutafuta Yesu. Wakati alimupata Yesu, aligusa sehemu ya chini ya nguo yake ya inje, na akapona palepale! Zaidi ya kumuponyesha, Yesu alimutendea kwa namna yenye ilimufanya ajisikie kuwa anapendwa na kuheshimiwa. Kwa mufano, wakati Yesu alizungumuza naye, alitumia neno “binti,” lenye kuonyesha upendo na heshima. Kwa kweli, ule mwanamuke alipata kitulizo, ao kutiwa nguvu kabisa!​—Lu. 8:43-48.

3. Tutajibu maulizo gani?

3 Tunaona kama ule mwanamuke alienda kwa Yesu. Alifanya hatua fulani. Ni vile pia leo, tunapaswa kujikaza ili ‘kuja’ kwa Yesu. Kwa sasa, Yesu hataponyesha kwa njia ya muujiza magonjwa ya kimwili ya wale wenye wanaenda kwake. Lakini angali anatualika kwa kusema hivi: “Mukuje kwangu, . . . na mimi nitawapumuzisha.” Mu habari hii, tutajibu maulizo tano: Tunapaswa kufanya nini ili ‘kuja’ kwa Yesu? Yesu alipenda kusema nini wakati alisema hivi: “Mubebe nira yangu?” Mufano wa Yesu unaweza kutufundisha nini? Juu ya nini kazi yenye ametupatia ni yenye kupumuzisha? Na tunapaswa kufanya nini ili tuendelee kupata pumuziko chini ya nira ya Yesu?

“MUKUJE KWANGU”

4-5. Ni katika njia gani fulani tunaweza ‘kuja’ kwa Yesu?

4 Njia moja ya ‘kuja’ kwa Yesu ni kujifunza mambo mingi kadiri tunaweza juu ya mambo yenye alisema na kufanya. (Lu. 1:1-4) Hakuna mutu mwenye anaweza kufanya vile pa nafasi yetu; tunapaswa kujifunza habari hizo sisi wenyewe. Pia, ‘tunakuja’ kwa Yesu wakati tunakamata uamuzi wa kubatizwa na kuwa wanafunzi wa Kristo.

5 Njia ingine ya ‘kuja’ kwa Yesu ni kuenda kuona wazee wa kutaniko wakati tuko na lazima ya musaada. Yesu anatumia “zawadi [hizo] katika wanadamu” ili kuhangaikia kondoo wake. (Efe. 4:7, 8, 11; Yoh. 21:16; 1 Pe. 5:1-3) Tunapaswa kufanya hatua ya kuomba musaada wao. Hatupaswe kuwaza kama wazee watajua mawazo yetu na mambo yenye tuko nayo lazima. Fikiria mambo yenye ndugu mumoja mwenye kuitwa Julian anasema: “Nilipaswa kutoka ku Beteli juu ya ugonjwa fulani, na rafiki yangu mumoja alinishauria niombe wazee wanitembelee ili wanitie moyo. Kwanza, niliwaza kama sikukuwa na lazima ya kutembelewa na wazee. Lakini kisha niliomba musaada, na wakati wazee walinitembelea, hiyo iligeuka kuwa zawadi moja kati ya zawadi za muzuri sana zenye nimekwisha kupata.” Wazee washikamanifu, kama wale wazee wawili wenye walimutembelea Julian, wanaweza kutusaidia kujua “akili ya Kristo,” ni kusema, kuelewa na kuiga mawazo yake na mutazamo wake. (1 Ko. 2:16; 1 Pe. 2:21) Wakati wazee wanatusaidia kwa njia hiyo, ni zawadi moja kati ya zawadi za muzuri zaidi zenye wanaweza kutupatia.

“MUBEBE NIRA YANGU”

6. Yesu alipenda kusema nini wakati alisema: “Mubebe nira yangu”?

6 Wakati Yesu alisema: “Mubebe nira yangu,” pengine alipenda kusema “Mukubali mamlaka yangu.” Ao pengine alipenda kusema “Muingie chini ya nira yangu, na tutamutumikia Yehova pamoja.” Ile mawazo yote mbili inaonyesha kama tunapaswa kufanya kazi.

7. Kulingana na Matayo 28:18-20, ni kazi gani yenye Yesu ametupatia tufanye, na tunaweza kuwa hakika na jambo gani?

7 Tunakubali mwaliko wa Yesu wakati tunatoa maisha yetu kwa Yehova na kubatizwa. Yesu anatolea watu wote mwaliko huo, hawezi kukataa hata mutu mumoja mwenye anapenda kabisa kumutumikia Mungu. (Yoh. 6:37, 38) Wanafunzi wote wa Kristo wamepewa pendeleo la kusaidia katika kazi yenye Yehova amemupatia Yesu afanye. Tunaweza kuwa hakika kama, sikuzote, Yesu atakuwa pamoja na sisi ili kutusaidia kufanya kazi hiyo.​—Soma Matayo 28:18-20.

“MUJIFUNZE KUPITIA MIMI”

Upumuzishe wengine kama vile yesu alifanya (Picha hizi zinapatana na fungu la 8-11) *

8-9. Juu ya nini watu wanyenyekevu walikuwa wanamukaribia Yesu, na tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

8 Watu wanyenyekevu walikuwa wanamukaribia Yesu. (Mt. 19:13, 14; Lu. 7:37, 38) Juu ya nini? Fikiria tofauti yenye ilikuwa kati ya Yesu na Wafarisayo. Viongozi hao wa dini hawakukuwa na upendo na walikuwa na majivuno. (Mt. 12:9-14) Lakini, Yesu alikuwa na upendo na alikuwa munyenyekevu. Wafarisayo walipenda sifa na walikuwa wanajiona kuwa wa maana kuliko watu wengine. Yesu alikataza roho hiyo ya kupenda sifa, na alifundisha wanafunzi wake wajione kuwa watumishi wa hali ya chini. (Mt. 23:2, 6-11) Wafarisayo walikuwa wanatawala watu kwa kuwaogopesha. (Yoh. 9:13, 22) Lakini Yesu alipumuzisha watu kupitia matendo ya upendo na maneno ya muzuri.

9 Umeiga mufano wa Yesu? Ujiulize hivi: ‘Ninajulikana kuwa mutu mwenye tabia ya upole na munyenyekevu? Niko tayari kufanya kazi za hali chini ili kutumikia wengine? Ninatendea wengine muzuri?’

10. Yesu alifanya watu wenye walitumika pamoja naye wajisikie namna gani?

10 Yesu alifanya wale wenye walitumika pamoja naye wajisikie muzuri na alifanya wakuwe mu hali ya amani, na alifurahia kuwazoeza. (Lu. 10:1, 19-21) Alitia moyo wanafunzi wake waulize maulizo, na alifurahia kusikia mawazo yao. (Mt. 16:13-16) Wanafunzi waliendelea muzuri kama vile mimea yenye inalindwa ili isiharibiwe na mambo kama vile jua, mvua, upepo, ao baridi kali. Walisikiliza kwa uangalifu mambo yenye Yesu aliwafundisha na walizaa matunda, ni kusema, matendo ya muzuri.

Ukuwe mwenye kukaribiwa kwa vyepesi na mwenye kufanya urafiki

Ukuwe mwenye bidii

Ukuwe munyenyekevu na mwenye kufanya kazi kwa bidii *

11. Tunapaswa kujiuliza maulizo gani?

11 Uko na mamlaka fulani juu ya watu wengine? Kama ni vile, ujiulize hivi: ‘Namna gani ninatendea wengine ku kazi ao ku nyumba? Ninajikaza ili kukuwe na amani? Ninatia wengine moyo waulize maulizo? Na niko tayari kusikiliza mawazo yao?’ Hatupendi hata kidogo kuwa kama Wafarisayo, wenye walikuwa wanakasirikia watu wenye walishakia mawazo yao na kutesa watu wenye walikuwa na mawazo yenye ilikuwa tofauti na yao.​—Mk. 3:1-6; Yoh. 9:29-34.

“MUTAPATA PUMUZIKO”

12-14. Juu ya nini kazi yenye Yesu ametupatia tufanye inatuletea pumuziko?

12 Juu ya nini kufanya kazi yenye Yesu ametupatia kunatuletea pumuziko? Kuko sababu za mingi, lakini tuzungumuzie tu sababu fulani.

13 Tuko na waangalizi wazuri sana. Yehova, Mwangalizi wetu Mukubwa Zaidi, haiko bwana mukali ao mwenye hana shukrani. Anafurahia kazi yenye tunafanya. (Ebr. 6:10) Na anatupatia uwezo wenye tuko nao lazima ili kufanya kazi hiyo yenye ametupatia. (2 Ko. 4:7; Gal. 6:5) Yesu, Mufalme wetu, ametuonyesha mufano muzuri sana juu ya namna ya kutendea wengine. (Yoh. 13:15) Na wazee wenye wanatuchunga wanajikaza kumuiga Yesu, “muchungaji mukubwa.” (Ebr. 13:20; 1 Pe. 5:2) Wanajikaza ili kuwa wema, wenye kutia moyo, na hodari wakati wanatufundisha na kutulinda.

14 Tuko na marafiki wazuri sana. Hakuna watu wengine wenye wako na marafiki wenye upendo na kazi ya maana kama vile sisi. Waza kidogo: Tuko na pendeleo la kufanya kazi pamoja na watu wenye wanafuata kanuni za juu zaidi lakini wenye hawajione kuwa wenye haki. Wako na uwezo mbalimbali wa kizalikio lakini hawajivune, na wanaona wengine kuwa wazuri kuwapita. Hawatuone tu kuwa wafanyakazi wenzao lakini wanatuona pia kuwa marafiki. Na wanatupenda sana, na kwa hiyo, wako tayari kufa kwa ajili yetu!

15. Tunapaswa kuona namna gani kazi yenye tuko tunafanya?

15 Tuko na kazi ya muzuri sana. Tunafundisha watu kweli juu ya Yehova na tunafunua uongo wa Ibilisi. (Yoh. 8:44) Shetani anabebesha watu mizigo yenye hawawezi kubeba. Kwa mufano, anapenda tuamini kama Yehova hatasamehe zambi zetu na kama hatustahili kupendwa. Huo ni uongo mubaya sana wenye kuvunja moyo sana! Wakati ‘tunakuja’ kwa Kristo, zambi zetu zinasamehewa. Na kusema kweli, Yehova anatupenda sana sisi wote. (Ro. 8:32, 38, 39) Tunafurahi sana wakati tunasaidia watu wajifunze kumutegemea Yehova na wakati tunaona maisha yao inabadilika na kuwa ya muzuri!

ENDELEA KUPATA PUMUZIKO CHINI YA NIRA YA YESU

16. Juu ya nini muzigo wenye Yesu anatuomba tubebe uko tofauti na mizigo ingine yenye tunapaswa kubeba?

16 Muzigo wenye Yesu anatuomba tubebe uko tofauti na mizigo ingine yenye tunapaswa kubeba. Kwa mufano, kisha kutumika kazi ya kimwili muchana muzima, watu wengi wanajisikia kuwa wamechoka na hawana furaha. Lakini, kisha kupitisha wakati fulani mu kazi ya Yehova na Kristo, tunajisikia kuwa wenye furaha sana. Tunaweza kuwa wenye kuchoka kisha kutumika muchana muzima na kujikaza ili kuenda ku mukutano wa kutaniko ile mangaribi. Lakini, mara mingi kisha mukutano tunarudia ku nyumba na tuko wenye kupumuzishwa na wenye nguvu tena. Ni vile pia wakati tunajikaza kuhubiri na kufanya funzo letu la pekee la Biblia. Baraka yenye tunapata ni kubwa sana kupita nguvu yenye tunatumia!

17. Tunapaswa kuelewa nini na tunapaswa kuwa waangalifu juu ya mambo gani?

17 Tunapaswa kuelewa kama kila mumoja wetu hana nguvu ya kufanya mambo yote. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa waangalifu juu ya mambo yenye tunataka kufanya. Kwa mufano, tunaweza kupoteza nguvu yetu juu ya kujirundikia vitu vya kimwili. Ona mambo yenye Yesu aliambia kijana mumoja tajiri mwenye alimuuliza hivi: “Ninapaswa kufanya nini ili niriti uzima wa milele?” Tayari, kijana huyo alikuwa anatii Sheria. Inawezekana kabisa alikuwa mutu muzuri juu Injili ya Marko inasema waziwazi kama Yesu ‘alimupenda.’ Yesu alialika kijana huyo tajiri. Alisema hivi: “Uende, uuzishe vitu vyenye uko navyo, . . . kisha ukuje ukuwe mufuasi wangu.” Mwanaume huyo alipenda kumufuata Yesu, lakini inaonekana kama hakuweza kuacha “vitu vingi” vyenye alikuwa navyo. (Mk. 10:17-22) Kwa hiyo, alikataa nira ya Yesu na akaendelea kuwa mutumwa “wa Utajiri.” (Mt. 6:24) Wewe ungechagua nini?

18. Mara kwa mara tunapaswa kufanya nini, na juu ya nini?

18 Mara kwa mara, tunapaswa kuchunguza mambo yenye tunatia pa nafasi ya kwanza mu maisha yetu. Juu ya nini? Juu ya kuhakikisha kama tuko tunatumia nguvu yetu kwa hekima. Ona mambo yenye kijana mumoja mwenye kuitwa Mark anasema: “Kwa miaka mingi, niliwaza kama nilikuwa ninaishi maisha ya mwepesi. Nilikuwa painia, lakini sikuzote, nilikuwa ninafikiri juu ya feza na juu ya kufanya maisha yangu ikuwe muzuri zaidi. Nilijiuliza juu ya nini maisha yangu ilikuwa imekuwa muzigo. Kisha, nilitambua kama nilikuwa ninatia faida zangu pa nafasi ya kwanza na nilikuwa ninamupatia Yehova wakati na nguvu yenye ilibakia.” Mark alibadilisha mawazo yake na namna yake ya kuishi na akaanza kufanya mambo mingi katika utumishi wa Yehova. Mark anasema hivi: “Wakati fulani ninakuwa na mahangaiko juu ya feza, lakini kwa musaada wa Yehova na Yesu, nimeshinda matatizo yenye nilikuwa nayo.”

19. Juu ya nini ni jambo la maana sana tukuwe na mawazo ya muzuri?

19 Tutaendelea kupata pumuziko chini ya nira ya Yesu kama tunafanya mambo tatu. Jambo la kwanza, tuendelee kuwa na mawazo ya muzuri. Kazi yenye tunafanya ni ya Yehova, kwa hiyo, tunapaswa kuifanya namna anapenda. Sisi tuko wafanyakazi, na Yehova njo Bwana wetu. (Lu. 17:10) Kama tunajaribu kufanya kazi yake namna sisi tunapenda, tutafanya maisha yetu ikuwe nguvu. Hata ngombe-dume mwenye nguvu anaweza kujiumiza na kujichokesha kama anajaribu kufuata njia yenye anapenda na kupigana na nira yenye bwana wake anaongoza. Lakini, tunaweza kufanya mambo ya ajabu na kushinda kizuizi chochote kama tunafuata muongozo wa Yehova. Tukumbuke kama, hakuna mutu mwenye anaweza kuzuia mapenzi yake isitimizwe!​—Ro. 8:31; 1 Yoh. 4:4.

20. Tunapaswa kuja chini ya nira ya Yesu na nia gani?

20 Jambo la pili, tufanye kazi na nia ya muzuri. Muradi wetu ni kumuletea utukufu Yehova, Baba yetu mwenye upendo. Wakati wa mitume, wale wenye walichochewa na pupa na wenye walikuwa wanatafuta faida zao wenyewe, bila kukawia walikosa furaha na wakaacha nira ya Yesu. (Yoh. 6:25-27, 51, 60, 66; Flp. 3:18, 19) Lakini, wale wenye walichochewa na upendo wa kweli kwa Mungu na upendo kwa jirani walibeba ile nira kwa furaha maisha yao yote ku dunia, wakiwa na tumaini la kutumika pamoja na Kristo mbinguni. Kama wao, tutaendelea kuwa na furaha ikiwa tunabeba nira ya Yesu na nia ya muzuri.

21. Kulingana na Matayo 6:31-33, tunaweza kutumaini kama Yehova atatufanyia nini?

21 Jambo la tatu, tujue kama Yehova hatatuacha. Tumechagua maisha ya kujitoa na kufanya kazi ya nguvu. Yesu alituonya kama tutateswa. Lakini, tunatumaini kama Yehova atatupatia nguvu ya kuvumilia magumu yoyote. Kama tunavumilia zaidi, tutakuwa na nguvu zaidi. (Yak. 1:2-4) Pia, tunatumaini kama Yehova atatupatia mambo yenye tuko nayo lazima, tunatumaini kama Yesu atatuchunga, na tunatumaini kama ndugu na dada zetu watatutia moyo. (Soma Matayo 6:31-33; Yoh. 10:14; 1 Te. 5:11) Kwa hiyo, tuko na mambo yote yenye tuko nayo lazima ili kuvumilia.

22. Tunaweza kuwa wenye shukrani juu ya jambo gani?

22 Mwanamuke mwenye Yesu aliponyesha alipata pumuziko siku ileile yenye aliponyeshwa. Lakini, angepata pumuziko la milele kama tu angekubali kuwa mwanafunzi mushikamanifu wa Kristo. Unawaza alifanya nini? Kama alichagua kuingia chini ya nira ya Yesu, wazia zawadi yenye atapata: kutumika pamoja na Yesu mbinguni! Baraka hiyo inapita kabisa kila kitu chenye angejiima ili kumufuata Kristo. Ikuwe tumaini letu ni kuishi mbinguni ao ku dunia, tunaweza kuwa wenye shukrani kwa sababu tumekubali mwaliko huu wa Yesu: “Mukuje kwangu!”

WIMBO 13 Kristo, Kielelezo Chetu

^ fu. 5 Yesu anatualika tukuje kwake. Tunapaswa kufanya nini ili tukubali mwaliko wake? Habari hii itajibu ulizo hilo, na itatukumbusha namna tunaweza kupata pumuziko wakati tunafanya kazi pamoja na Kristo.

^ fu. 60 MAFASIRIO YA PICHA: Yesu alipumuzisha wengine mu njia za mingi.

^ fu. 66 MAFASIRIO YA PICHA: Vilevile, ndugu mumoja anapumuzisha wengine mu njia mbalimbali.