Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 37

“Nitatikisa Mataifa Yote”

“Nitatikisa Mataifa Yote”

“Nitatikisa mataifa yote, na vitu vyenye samani vya mataifa yote vitaingia.”​—HAG. 2:7.

WIMBO 24 Tuende ku Mulima wa Yehova

KIFUPI YA HABARI *

1-2. Ni kutikiswa gani ya mufano nabii Hagai alisema ingetokea mu wakati wetu?

 “MU DAKIKA kidogo tu, ma magasin na majengo ya zamani ilianza kuanguka.” “Kulikuwa wasiwasi fasi yote . . . Watu wengi walisema kama ile hali ilifanya dakika mbili hivi. Lakini kwangu miye, niliona sawa vile ilikawia sana.” Ile ni maelezo ya watu fulani wenye waliokoka, wakati tetemeko fulani ilipiga inchi ya Nepali mu 2015. Kama ile hali ilishakupata, kusema kweli, haiko mwepesi kuisahau.

2 Na siye leo, tuko tunajionea tetemeko ya aina ingine, tetemeko yenye inapiga hapana tu muji ao inchi fulani. Lakini ile tetemeko inapata mataifa yote, na tayari imefanya miaka mingi tangu ianze. Ile tetemeko ao kutikiswa, ilitabiriwa na nabii Hagai. Aliandika hivi: “Yehova wa majeshi anasema hivi, ‘Na mara moja tena​—katika wakati kidogo​—na nitatikisa mbingu na dunia na bahari na inchi kavu.’”​—Hag. 2:6.

3. Ni mu njia gani hii kutikiswa ya mufano iko tofauti na tetemeko ya dunia?

3 Kutikiswa yenye nabii Hagai alionyesha, haiko sawa ile tetemeko ya dunia yenye inaletaka tu uharibifu. Lakini, kutikiswa yenye alitabiri, inaleta matokeo ya muzuri. Yehova mwenyewe anatuambia hivi: “Nitatikisa mataifa yote, na vitu vyenye samani vya mataifa yote vitaingia; na nitajaza nyumba hii utukufu.” (Hag. 2:7) Ile unabii ilikuwa na maana gani kwa wale wenye waliishi mu wakati wa Hagai? Na iko na maana gani kwetu leo? Tutazungumuzia majibu ya ile maulizo na tutaona namna tunaweza kushiriki mu kazi ya kutikisa mataifa leo.

UJUMBE WENYE ULITIA MOYO MU WAKATI WA HAGAI

4. Juu ya nini Yehova alitumia watu wake nabii Hagai?

4 Nabii Hagai, alipata mugao wa maana sana kutoka kwa Yehova. Ona mambo fulani yenye ilitokea mbele ya pale. Inawezekana Hagai alikuwa kati ya wale wenye walirudia Yerusalemu kutoka Babiloni, mu uhamisho mu 537 M.K.Y. kisha kufika kwenye walikuwa wanaenda, wale waabudu waaminifu walitia musingi wa nyumba ya Yehova, ao hekalu. (Ezr. 3:8, 10) Lakini bila kukawia, hali fulani ya mubaya ikatokea. Wakavunjika moyo na wakaacha kazi ya ujenzi kwa sababu ya upinzani. (Ezr. 4:4; Hag. 1:1, 2) Kwa hiyo, mu 520 M.K.Y., Yehova alituma Hagai ili atie tena nguvu bidii yao, na kuwachochea wamalize kujenga hekalu. *​—Ezr. 6:14, 15.

5. Juu ya nini tunasema kama ujumbe wa Hagai ulipaswa kabisa kutia moyo Wayahudi?

5 Ujumbe wa Hagai ulikuwa na kusudi ya kutia nguvu imani ya Wayahudi katika Yehova. Kwa uhodari wote, Hagai aliambia hivi Wayahudi wenye walikuwa walishavunjika moyo: “‘Ninyi watu wote wa inchi, mukuwe na nguvu,’ ni vile Yehova anasema, ‘na mufanye kazi.’ ‘Kwa maana niko pamoja na ninyi,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema.” (Hag. 2:4) Maneno “Yehova wa majeshi” ilipaswa kuwatia moyo Wayahudi. Yehova iko na jeshi kubwa sana ya wa malaika wenye wako chini ya uongozi wake, kwa hiyo, Wayahudi walipaswa kumutegemea ili wafanikiwe.

6. Kutikiswa yenye Hagai alitabiri, ingekuwa na matokeo gani?

6 Kupitia roho yake takatifu, Yehova alimuongoza Hagai atoe ujumbe wenye kuonyesha kama angetikisa mataifa yote. Ile ufunuo, ilitia moyo wale wajenzi wa hekalu wenye walikuwa walishavunjika moyo na iliwahakikishia kama Yehova alikuwa karibu kutikisa Uajemi, mamlaka makubwa yenye ilikuwa inatawala mataifa mingi ile wakati. Na ile kutikiswa, ingekuwa na matokeo gani? Kwanza, watu wa Mungu wangemaliza kazi ya kujenga hekalu. Kisha, hata watu wenye hawakukuwa Wayahudi wangekuja kuabudu Yehova mu hekalu yenye ilikuwa imejengwa upya. Kusema kweli, ile ujumbe ilipaswa kutia moyo watu wa Mungu!​—Zek. 8:9.

KAZI YENYE IKO INATIKISA DUNIA LEO

Je, uko unashiriki kabisa mu hii kazi yenye kutikisa dunia yenye iko inafanywa leo? (Ona fungu ya 7-8) *

7. Ni kazi gani ya kutikisa yenye tunaunga mukono leo? Fasiria.

7 Unabii wa Hagai, uko na maana gani kwetu leo? Mara ingine tena Yehova iko anatikisa mataifa yote, na mara hiyo, siye wote tunahusika. Fikiria hii jambo: Mu 1914, Yehova alimuweka Yesu Kristo kuwa Mufalme wa Ufalme wake wa mbinguni. (Zb. 2:6) Viongozi wa dunia waliona ile kuwa habari ya mubaya sana. Ilimaanisha kama “nyakati zenye ziliwekwa za mataifa,” ni kusema, kipindi yenye hakungekuwa mutawala mwenye angemwakilisha Yehova, ilikuwa imetimia ao ilifikia mwisho. (Lu. 21:24) Juu ya ile sababu, zaidi sana tangu 1919, watu wa Yehova wako wanatangaza kama Ufalme wa Mungu njo tumaini pekee ya wanadamu wote. Hii kazi ya kuhubiri “habari njema ya Ufalme” iko inatikisa dunia yote.​—Mt. 24:14.

8. Kulingana na Zaburi 2:1-3, mataifa mingi imetenda namna gani kuhusu ujumbe wenye tuko tunatangaza?

8 Watu wako na mawazo gani juu ya ule ujumbe? Watu wengi wanaukatala. (Soma Zaburi 2:1-3.) Mataifa iko katika musukosuko. Inakatala kukubali mutawala mwenye Yehova aliweka. Mataifa haione kama ujumbe wa Ufalme wenye tuko tunatangaza ni “habari njema.” Kusema kweli, serikali fulani zimekataza hata kazi ya kuhubiri! Hata kama viongozi wengi wa mataifa wanasema kama wako wanamuabudu Mungu, kusema kweli, hawaache mamlaka yenye wako nayo. Sawa vile viongozi wa wakati wa Yesu, leo pia, viongozi wako wanamupinga mutiwa-mafuta wa Yehova, kwa kushambulia wafuasi wake washikamanifu.​—Mdo. 4:25-28.

9. Yehova anatenda namna gani wakati anaona mataifa iko inakatala ujumbe wake?

9 Yehova anatenda namna gani wakati anaona mataifa iko inakatala ujumbe wake? Zaburi 2:10-12 inasema hivi: “Basi sasa, ninyi wafalme, muonyeshe ufahamu; mukubali kurekebishwa, ninyi waamuzi wa dunia. Mumutumikie Yehova kwa woga, na mushangilie mukitetemeka. Mumuheshimie mwana, kama hamufanye vile Mungu atakasirika sana na ninyi mutaangamia kutoka katika njia, kwa maana kasirani Yake inawaka haraka. Wenye furaha ni wale wote wenye wanamukimbilia Yeye.” Yehova anapatia wapinzani wake nafasi ya kubadilisha namna yao ya kufikiri na ya kukubali Ufalme wake. Hata vile, wakati inabakia kidogo. Tuko tunaishi “mu siku za mwisho” za huu mupangilio wa mambo. (2 Ti. 3:1; Isa. 61:2) Leo hakuna jambo ya haraka sana kwa watu sawa vile kujifunza kweli na kukamata uamuzi wa kumutumikia Yehova.

WATU FULANI WANAKUBALI UJUMBE WENYE KUTIKISA

10. Kazi ya kutikisa iko na matokeo gani ya muzuri sawa vile Hagai 2:7-9 inaonyesha?

10 Kutikiswa ya mufano yenye Hagai alitabiri, iko na matokeo ya muzuri kwa watu fulani. Anatuambia matokeo ya ile kutikiswa: “Vitu vyenye samani [watu wenye kuwa na mioyo mizuri] vya mataifa yote, vitaingia” ili kumuabudu Yehova. * (Soma Hagai 2:7-9.) Isaya na Mika walitabiri pia kama ile mambo ingetokea katika “siku za mwisho.”​—Isa. 2:2-4, maelezo ya chini; Mik. 4:1, 2, maelezo ya chini.

11. Ndugu moja alitenda namna gani kisha kusikia kwa mara ya kwanza ujumbe wa Ufalme?

11 Ona matokeo yenye ile ujumbe yenye kutikisa dunia ilikuwa nayo juu ya ndugu Ken, mwenye iko anatumikia ku makao makubwa. Anakumbuka kabisa wakati alisikia kwa mara ya kwanza ujumbe wa Ufalme kumepita miaka 40 hivi. Ken anasema: “Wakati nilisikia kwa mara ya kwanza kweli yenye kuwa mu Neno ya Mungu, nilifurahi sana juu nilijifunza kama tuko tunaishi mu siku za mwisho ya huu mupangilio wa mambo. Niliona kama, juu Mungu anikubali na juu nipate uzima wa milele, napaswa kujitenga kabisa na hii dunia na kubakia upande wa Yehova. Kisha kusali, nikafanya vile mara moja. Niliacha kuunga mukono mambo yote ya dunia, na nikakimbilia Ufalme wa Mungu kwenye naweza kupata usalama, ndiyo, Ufalme wenye hauwezi kutikiswa.”

12. Namna gani hekalu ya kiroho ya Yehova imejaa utukufu mu hizi siku za mwisho?

12 Ni wazi kama Yehova iko anabariki watu wake. Mu hizi siku za mwisho, tumeona kama hesabu ya wale wenye wako wanamuabudu inaendelea kuongezeka. Mu 1914 walikuwa watu kidogo tu. Lakini leo wako zaidi ya milioni munane wenye kumuabudu Mungu kwa bidii, na kuko mamilioni ingine ya watu wenye wako wanajiunga na siye kila mwaka ili kukumbuka kifo ya Yesu. Mu ile njia, vyumba vya inje vya kidunia vya hekalu ya kiroho ya Yehova, ni kusema, mupango wake kwa ajili ya ibada safi, vimejaa “vitu vyenye samani vya mataifa yote.” Mabadiliko yenye wale watu wanafanya wakati wanajikaza kuvaa utu mupya, inaletea pia jina ya Yehova utukufu.​—Efe. 4:22-24.

13. Ongezeko ya waabudu wa Yehova imetimiza maunabii gani ingine? (Ona picha kwenye jalada.)

13 Ile ongezeko yote imetimiza maunabii ingine, sawa ile yenye inapatikana mu Isaya sura ya 60. Tunasoma hivi mu mustari wa 22 wa ile sura: “Mudogo atakuwa elfu (1 000) na mutu wa hali ya chini atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.” Kwa sababu kuko watu wengi wenye wanaanza kumuabudu Yehova, jambo fulani ya pekee iko inatokea. Hivi “vitu vyenye samani” viko na uwezo mbalimbali, tena viko na roho ya kujitoa ili kujiunga mu kazi ya kuhuburi “habari njema ya Ufalme.” Na matokeo ni kwamba watu wa Yehova wanaweza kutumia ule uwezo mbalimbali wenye Isaya anaita kuwa “maziwa ya mataifa.” (Isa. 60:5, 16) Kwa musaada wa wale wanaume na wale wanamuke wenye kuwa wa maana sana, kazi ya kuhubiri habari njema inaendelea kufanywa mu inchi 240 na vichapo vinaendelea kuchapishwa mu luga zaidi ya 1 000.

HII NJO WAKATI WA KUCHAGUA

Watu wa Mungu mu dunia yote wako na furaha ya kuhubiria wengine kuhusu Ufalme wa Mungu (Ona habari ya kujifunza ya 37, fungu ya 13)

14. Ni uamuzi gani watu wanapaswa kukamata sasa?

14 Mu hizi siku za mwisho, kutikiswa ya mataifa inafanya watu wakamate uamuzi fulani. Je, watategemeza Ufalme wa Mungu? Ao wataendelea kutumainia serikali za hii dunia? Ile ni uamuzi wenye wanapaswa kukamata. Hata kama watumishi wa Yehova wanatii sheria za serikali za inchi yao, hawajiingize mu mambo ya politike ya hii dunia. (Ro. 13:1-7) Wanajua kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza magumu yote ya wanadamu. Ile Ufalme haiko sehemu ya hii ulimwengu.​—Yoh. 18:36, 37.

15. Ni jaribu gani kubwa ya ushikamanifu yenye inazungumuziwa mu kitabu ya Ufunuo?

15 Kitabu ya Ufunuo inafasiria jaribu ya ushikamanifu ya watumishi wa Yehova mu siku za mwisho. Na ile jaribu itaendelea kuongezeka tena na tena. Serikali za hii dunia zitapenda tuzitolee ibada na zitatesa wale wenye watakatala kuzitegemeza. (Ufu. 13:12, 15) ‘Zitalazimisha watu wote​—wadogo na wakubwa, matajiri na maskini, watu wenye kuwa huru na watumwa​—ili wote watiwe alama kwenye mukono wao wa kuume ao kwenye paji la uso wao.’ (Ufu. 13:16) Zamani watumwa walikuwa wanawekwa alama fulani ili kuonyesha kama walikuwa wa nani. Vilevile mu siku zetu, watu watatazamia kama kila mutu atakuwa na alama ya mufano ku mukono ao ku paji la uso wake. Mawazo na matendo yao itaonyesha kama wao ni wa nani na kama wanaunga mukono serikali gani.

16. Juu ya nini ni jambo ya haraka kutia nguvu ushikamanifu wetu kwa Yehova tangu sasa?

16 Je tutakubali ile alama ya mufano na tutaunga mukono serikali za hii dunia? Wale wenye wanakatala kuwekwa alama watapatwa na magumu na watakuwa mu hatari. Kitabu ya Ufunuo inaendelea kwa kusema hivi: “Mutu yeyote asiweze kununua ao kuuzisha isipokuwa tu mutu mwenye kuwa na ile alama.” (Ufu. 13:17) Lakini watu wa Mungu wanajua kile Mungu atafanyia wale wenye wako na alama yenye kuzungumuziwa mu Ufunuo 14:9, 10. Kuliko kutiwa ile alama, kusema kweli, wataandika hivi kwenye mukono wao: “Mali ya Yehova.” (Isa. 44:5) Sasa njo wakati wa kuhakikisha kama ushikamanifu wetu kwa Yehova uko nguvu. Kama uko nguvu, Yehova atafurahi kusema kama tuko mali yake!

KUTIKISWA YA MWISHO

17. Ni jambo gani hatupaswe kusahau kuhusu uvumilivu wa Yehova?

17 Yehova ameonyesha uvumilivu mu hizi siku za mwisho. Hapendi mutu yeyote aharibiwe. (2 Pe. 3:9) Amepatia watu wote nafasi ya kutubu na kukamata uamuzi wa muzuri. Lakini uvumilivu wake uko na mipaka. Wale wenye watakatala hii nafasi yenye inatolewa kwao wanaweza kujikuta mu hali yenye ilifikia Farao mu wakati wa Musa. Yehova alimuambia Farao hivi: “Kwa maana kufikia sasa ningekuwa nimenyoosha mukono wangu ili kukupiga wewe na watu wako kwa pigo kali, na ungekuwa umeondolewa juu ya dunia. Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.” (Kut. 9:15, 16) Ku mwisho ya yote, mataifa yote itafikia kujua kama Yehova tu njo Mungu wa kweli. (Eze. 38:23) Ile itafanyika namna gani?

18. (a) Ni aina gani ingine ya kutikiswa inazungumuziwa mu Hagai 2:6, 20-22? (b) Namna gani tunajua kama ile maneno ya Hagai itatimia wakati wenye kuja?

18 Miaka fulani kisha siku za Hagai, mutume Paulo aliongozwa na roho ya Mungu ili kuonyesha kama maneno yenye kuwa mu Hagai 2:6, 20-22 ingetimia wakati wenye kuja. (Soma.) Paulo aliandika hivi: “Sasa ameahidi: ‘Na mara moja tena nitatikisa hapana dunia tu lakini pia mbingu. Sasa maneno ‘na mara moja tena’ yanaonyesha kuondolewa kwa vitu vyenye kutikiswa, vitu vyenye vilifanywa, ili vitu vyenye havitikiswe vibakie.” (Ebr. 12:26, 27) Tofauti na kutikiswa yenye inazungumuziwa mu Hagai 2:7, hii kutikiswa sasa itamaanisha uharibifu wa milele kwa wale wenye, sawa vile Farao, wanakatala kukubali kama Yehova njo iko na haki ya kutawala.

19. Ni nini haitatikiswa, na nini njo inatusaidia kujua vile?

19 Ni nini haitatikiswa ao kuondolewa? Paulo anasema tena hivi: “Kwa kuwa tutapokea Ufalme wenye hauwezi kutikiswa, tuendelee kupokea fazili zenye hazistahiliwe, zenye kupitia hizo tutamutolea Mungu utumishi mutakatifu kwa njia yenye kukubalika, kwa kumuogopa Mungu na kumuheshimia.” (Ebr. 12:28) Ndiyo, kisha hii kutikiswa ya mwisho, ni Ufalme wa Mungu tu njo hautatikiswa. Utaendelea kusimama imara!​—Zb. 110:5, 6; Da. 2:44.

20. Ni uamuzi gani watu wanapaswa kukamata, na namna gani tunaweza kuwasaidia?

20 Hakuna tena wakati wa kupoteza! Watu wanapaswa kuchagua kama wataunga mukono namna ya kuishi ya hii dunia, yenye inapeleka ku uharibifu, ao kama watajikaza kuwa na maisha ya muzuri yenye inapatana na mapenzi ya Mungu, yenye itawaongoza ku uzima wa milele. (Ebr. 12:25) Kupitia kazi yetu ya kuhubiri, tunaweza kusaidia watu wakamate uamuzi wa muzuri sana. Kwa hiyo basi, tujikaze kusaidia hawa watu wenye kuwa wa maana sana ili waunge mukono Ufalme wa Mungu. Na tusisahau mu akili yetu hii maneno ya Bwana wetu Yesu: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—Mt. 24:14.

WIMBO 40 Weye Ni wa Nani?

^ fu. 5 Hii habari, inaleta mafasirio ya mupya kuhusu namna yetu ya kuelewa andiko ya Hagai 2:7. Mu hii habari, tutaona namna tunaweza kuunga mukono hii kazi ya muzuri sana ya kutikisa mataifa yote. Tutaona pia namna kazi ya kutikisa mataifa yote inafanya watu fulani wakubali ujumbe wenye tunawatangazia na wengine waukatale.

^ fu. 4 Tunajua kama Hagai alimaliza kazi yenye Yehova alimuambia afanye juu hekalu ilimalizwa kujengwa mu 515 M.K.Y.

^ fu. 10 Hii ni mafasirio ya mupya kuhusu namna yetu ya kuelewa. Zamani tulisema kama haiko kutikiswa ya mataifa njo ingevuta watu wenye mioyo mizuri kwa Yehova. Ona habari “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” yenye kuwa mu Munara wa Mulinzi wa tarehe 15, Mwezi wa 5, 2006.

^ fu. 63 MAFASIRIO YA PICHA: Hagai alitia moyo watu wa Mungu wakuwe wenye bidii na wamalize kazi ya kujenga upya hekalu; wakati wetu watu wa Mungu wako wanatangaza ujumbe wa Mungu kwa bidii. Bibi na bwana fulani wako wanahubiri ujumbe kuhusu kutikiswa ya mwisho yenye iko inakuja.