Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI YA KUJIFUNZA YA 35

Uone Ndugu na Dada Wenye Walishazeeka Kuwa wa Maana Sana

Uone Ndugu na Dada Wenye Walishazeeka Kuwa wa Maana Sana

“Imvi ni taji la uzuri.”​—MEZ. 16:31.

WIMBO 138 Uzuri wa Kichwa Yenye Imvi

KIFUPI YA HABARI *

1-2. (a) Kulingana na Mezali 16:31, tunapaswa kuwa na mawazo gani juu ya wale wenye walishazeeka? (b) Ni maulizo gani tutajibia mu hii habari?

 MU Amerika kuko parc moya hivi mu Arkansas, kwenye unaweza kupata almasi (ao, diamands) ku udongo. Zile almasi zingali vilevile tu, ni kusema, haziyabadilishwa ili kutumiwa kutengeneza vitu sawa vile bijoux. Njo maana watu wengi wenye wanapita ile fasi hawaone kama ile majiwe iko na samani sana na hawavutiwe nayo.

2 Mu njia fulani, ndugu na dada waaminifu wenye walishazeeka wako sawa vile zile almasi; wako hazina za maana sana. Neno ya Mungu inalinganisha imvi ya wale ndugu na dada wenye walishazeeka na taji. (Soma Mezali 16:31; 20:29) Lakini, kama hatuko waangalifu hatuwezi kuona zile hazina. Wakati vijana wanaelewa kama wale wenye walishazeeka wako wa maana sana, wanajikaza ili wapate kitu fulani ya maana kutoka kwao, kitu yenye inapita utajiri. Mu hii habari tutajibia hii maulizo tatu: Juu ya nini Yehova anaona waaminifu wenye walishazeeka kuwa hazina? Juu ya nini ndugu na dada wenye walishazeeka wako wa maana sana mu tengenezo ya Yehova? Tunaweza kufanya nini juu mufano wao utuletee faida?

JUU YA NINI YEHOVA ANAONA WAAMINIFU WENYE WALISHAZEEKA KUWA HAZINA?

Waaminifu wenye walishazeeka wako wa maana sana ku macho ya Yehova na kwa watu wake (Ona fungu ya 3)

3. Kulingana na Zaburi 92:12-15, juu ya nini waaminifu wenye walishazeeka wako wa maana sana ku macho ya Yehova?

3 Waaminifu wenye walishazeeka wako wa maana sana ku macho ya Yehova Mungu. Anajua wao ni watu wa namna gani, na anasamini sana sifa zao za muzuri. Anafurahi wakati anaona wale wenye walishazeeka wako wanapatia vijana hekima yenye walipata mu utumishi wao kwa Yehova. (Yob. 12:12; Mez. 1:1-4) Tena, Yehova anasamini sana uvumilivu wao. (Mal. 3:16) Walipata magumu mingi sana mu maisha yao; lakini, hata vile imani yao hairegee. Tumaini yao juu ya wakati wenye kuja ingali nguvu sana kuliko vile ilikuwaka wakati walijfunza kweli. Na Yehova anawapenda juu wanaendelea kutangaza jina yake “hata wakati wa uzee.”​—Soma Zaburi 92:12-15.

4. Ni mambo gani inaweza kutia moyo ndugu na dada zetu wenye walishazeeka?

4 Kama ulishazeeka, ukuwe hakika kama Yehova anakumbuka kazi yenye ulifanyaka zamani. (Ebr. 6:10) Ulitegemeza kwa bidii kazi ya kuhubiri, na ile inamupendeza Baba yetu wa mbinguni. Ulivumilia magumu, hata magumu ya nguvu sana, na ulishakamana na kanuni za haki za Yehova. Ulikuwa na mapendeleo mingi ya utumishi, na ulizoeza wengine. Umefanya yako yote ili kujipatanisha na mabadiliko yenye iko mu tengenezo. Umetegemeza na kutia wengine moyo ili waendelee na utumishi wa wakati wote. Yehova anakupenda sana juu ya ushikamanifu wako. Anaahidi kama “hataacha washikamanifu wake.” (Zb. 37:28) Anakuhakikishia hivi: ‘Mupaka wakati kichwa chako kitakuwa na imvi nitaendelea kukubeba.’ (Isa. 46:4) Kwa hiyo, usiwaze kama juu ulishazeeka hauko tena wa maana mu tengenezo ya Yehova. Kusema kweli, uko wa maana sana!

WALE WENYE WALISHAZEEKA WAKO WA MAANA SANA MU TENGENEZO YA YEHOVA

5. Ni jambo gani wale wenye walishazeeka wanapaswa kuchunga mu akili?

5 Wale wenye walishazeeka wako wa maana sana mu njia mbalimbali mu tengenezo ya Yehova. Pengine hawana nguvu tena sawa vile zamani, lakini wako na uzoefu mingi. Yehova anaweza kuendelea kuwatumia mu njia mbalimbali, sawa vile mifano yenye kufuata ya zamani na ya leo inaonyesha.

6-7. Leta mifano fulani yenye kuwa mu Biblia ya watu wenye walikuwa wazee wenye walibarikiwa juu ya ushikamanifu wao kwa Yehova.

6 Mu Biblia muko mifano ya waaminifu fulani wa zamani wenye waliendelea kumutumikia Yehova hata wakati walikuwa wazee. Kwa mufano, Musa alikuwa na miaka 80 hivi wakati alianza kumutumikia Yehova akiwa nabii na mwakilishi wake ku taifa ya Israeli. Yehova aliendelea kutumia nabii Danieli sawa vile musemaji wake. Na inawezekana wakati alimutumia alikuwa na miaka 90 hivi. Na pengine mutume Yohana na yeye alikuwa na miaka 90 hivi wakati Mungu alimuongoza kupitia roho yake ili aandike kitabu ya Ufunuo.

7 Waaminifu wengine wengi hawajulikane sana, na kama hatuko waangalifu tunaweza kuona kama hawako wa maana. Lakini, Yehova anawajua na aliwabariki juu ya ushikamanifu wao. Kwa mufano, Simeoni mwenye “alikuwa mwenye haki na mwenye kumuogoa Mungu,” anatajwa kwa kifupi tu mu Biblia, lakini Yehova alijua Simeoni alikuwa mutu gani na alimupatia pendeleo ya kuona mutoto Yesu na ya kutoa unabii juu ya ule mutoto na mama yake. (Lu. 2:22, 25-35) Fikiria pia Ana, mwenye alikuwa nabii lakini pia mujane. Alikuwa na miaka 84 lakini “hakukuwa anakosekana hata kidogo katika hekalu.” Leo tunaweza kusema kama Ana hakukuwa anakosa mikutano. Juu alikuwa anafanya vile, alibarikiwa wakati siku moja na yeye aliona Yesu wakati alikuwa angali mutoto. Simeoni na Ana walikuwa wa maana sana ku macho ya Yehova.​—Lu. 2:36-38.

Dada Didur, mwenye iko na miaka 80 hivi, anaendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu (Ona fungu ya 8)

8-9. Dada fulani alifanya nini mu utumishi wa Yehova wakati bwana yake alikufa?

8 Leo, ndugu na dada wengi waaminifu wenye walishazeeka wako mufano muzuri sana kwa vijana. Ona mufano wa dada Lois Didur. Alikuwa tu na miaka 21 wakati alianza kutumika akiwa painia wa pekee mu Kanada. Kisha pale, yeye na bwana yake John, walipitisha miaka fulani mu kazi ya muzunguko. Kisha pale wakatumikia ku Beteli ya Kanada kwa zaidi ya miaka 20. Wakati Lois alikuwa na miaka 58, yeye na John walialikwa ili kuenda kutumikia mu inchi ya Ukraine. Je, wangeitika? Ao wangesema kama walishazeeka sana na kama ni nguvu kwao kutumikia mu inchi ingine? Walikubali ile mugao, na John akawekwa kuwa mushiriki wa Halmashauri ya Tawi ya inchi ya Ukraine. Kisha kutumikia miaka saba mu ile inchi John akakufa, lakini Lois akaamua kubakia mu mugao wake. Leo, Lois iko na miaka 81, na anaendelea kutumika kwa bidii na anapendwa sana na familia ya Beteli ya Ukraine.

9 Inawezekana dada wenye kuwa wajane, sawa vile Lois, wasihangaikiwe sana sawa vile ilikuwaka wakati bwana zao walikuwa wangali wazima; lakini hata vile, haiko kusema juu wako wajane njo hawako tena wa maana. Yehova anapenda sana dada wenye walitegemeza bwana zao kwa miaka mingi na wenye wanaendelea kuonyesha bidii ileile. (1 Ti. 5:3) Zaidi ya ile, wako kitia-moyo kwa watu wote lakini pia kwa vijana.

10. Tony anatuachia mufano gani muzuri?

10 Waaminifu wengi wenye walishazeeka wenye wanaishi mu makao kwa ajili ya wazee, wao pia ni hazina ya kiroho. Kwa mufano, ndugu Tony anaishi pia mu moja kati ya ile makao. Alibatizwa Pennsylvanie, mu inchi ya Amerika, mu Mwezi wa 8, 1942 wakati alikuwa na miaka 20. Bila kukawia walimukaza ajiingize mu mambo ya politike na ile ilifanya afungwe miaka mbili na nusu mu gereza. Yeye na bibi yake Hilda, walikomalisha watoto wawili katika kweli. Kwa miaka fulani, Tony alikuwa mwangalizi musimamizi (leo anaitwa muratibu wa baraza ya wazee) mu makutaniko tatu na pia musimamizi ku mukusanyiko wa muzunguko. Alikuwa anaongoza mikutano na pia mafunzo ya Biblia wakati alikuwa anatembelea gereza. Leo iko na miaka 98, na hana wazo ya kuachia pale na kazi ya Yehova. Anaendelea kufanya yote yenye anaweza ili kumutumikia Yehova na pia kutumika pamoja na kutaniko yake!

11. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaona wale wenye kuishi mu makao kwa ajili ya wazee kuwa wa maana sana?

11 Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia wale wenye walishazeeka wenye wanaishi mu makao kwa ajili ya wazee? Kama inawezekana, wazee wa kutaniko wanapaswa kujikaza ili kusaidia wale ndugu na dada wahuzurie ao wasikilize mikutano na kuhubiri pamoja nao. Siye kipekee, tunaweza kuonyesha kama tunawaona kuwa wa maana kwa kuwatembelea ao kuzungumuza nao kupitia vidéoconférence. Ni jambo ya maana kuona ndugu na dada wenye walishazeeka, wenye pengine wako mu makao ya wazee yenye iko mbali na kutaniko yao kuwa wa maana sana. Kama hatuko waangalifu, tunaweza kuwasahau. Kwa wamoja inaweza kuwa nguvu kuzungumuza juu yao wenyewe. Lakini tutapata faida sana saa yenye tunakamata wakati wa kuwakaribia na kuwasikiliza kwa uangalifu wakati wako wanatufasiria furaha zenye walipata mu tengenezo ya Yehova.

12. Ni ndugu na dada wa namna gani tunaweza kupata mu kutaniko yetu?

12 Pengine tunaweza kushangaa, kupata mu kutaniko yetu, mifano ya muzuri sana ya ndugu na dada wenye walishazeeka. Dada Harriette alimutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi mu kutaniko yao kule New Jersey, mu inchi ya Amerika. Kisha pale akaenda kuishi na mutoto yake mwanamuke. Ndugu na dada wa kutaniko yake ya mupya walikamata wakati wa kumujua, na walivumbula kama alikuwa hazina. Dada Harriette aliwatia moyo kwa kuwafasiria mambo ya muzuri yenye alikutana nayo mu utumishi wa Yehova wakati alijifunza kweli mu miaka ya 1920. Ile wakati, kila mara hakukuwa anasahau brosse yake ya meno juu ingemusaidia kama angefungwa. Mu 1933 alifanya juma moja mu gereza. Mu ile kipindi, bwana yake mwenye haiko Shahidi na mwenye alikuwa anamutegemeza sana, njo alikuwa anachunga watoto wao watatu. Kusema kweli, waaminifu wenye walishazeeka sawa vile Harriette ni hazina kabisa!

13. Tunajifunza nini kuhusu ndugu na dada wenye walishazeeka?

13 Ndugu na dada wenye walishazeeka wako wa maana sana mu tengenezo ya Yehova. Wamejionea na macho yao namna Yehova amewabariki mu njia mbalimbali lakini pia namna amebariki tengenezo yake. Wamejifunza pia mambo fulani kupitia makosa yenye walifanya. Uwaone kuwa kama vile “chemchemi ya hekima,” na ujifunze mambo mingi kwao. (Mez. 18:4) Ukikamata wakati wa kuwajua muzuri, imani yako itatiwa nguvu na utajifunza mambo mingi!

TUNAWEZA KUFANYA NINI JUU MUFANO WA WALE WENYE WALISHAZEEKA UTULETEE FAIDA?

Sawa vile tu Elisha alipata faida sana kutoka kwa Eliya, ndugu na dada wanaweza pia kupata faida wakati watu wenye walishazeeka wanawafasiria mambo ya muzuri yenye walipata mu utumishi wa Yehova (Ona fungu ya 14-15)

14. Kumbukumbu la Torati 32:7 inatia moyo vijana wafanye nini?

14 Ukamate hatua ya kuzungumuza na wale wenye walishazeeka. (Soma Kumbukumbu la Torati 32:7.) Kusema kweli, pengine hawaone tena muzuri, wanaanza kutembea polepole, na kusema polepole, lakini upendo wao kwa Yehova ungali uleule, na wamejifanyia “jina la muzuri” ku macho ya Yehova. (Muh. 7:1) Kumbuka sababu yenye inafanya Yehova awaone kuwa wa maana. Endelea kuwaheshimia. Ukuwe sawa vile Elisha. Hakupenda kuachana na Eliya mu masiku kidogo tu yenye ilibakia mbele waachane. Mara tatu Elisha alisema: “Sitakuacha.”​—2 Fa. 2:2, 4, 6.

15. Ni maulizo gani unaweza kuuliza wale wenye walishazeeka?

15 Uonyeshe kama unapendezwa kabisa na wale wenye walishazeeka kwa kuwauliza maulizo fulani. (Mez. 1:5; 20:5; 1 Ti. 5:1, 2) Unaweza kuwauliza maulizo sawa hii: “Wakati ulikuwaka kijana, nini ilikuhakikishia kama hii njo kweli?” “Namna gani mambo yenye ulijionea mu maisha imefanya ukuwe karibu tena zaidi na Yehova?” “Unawaza nini njo siri ya kuendelea kuwa na furaha mu utumishi wa Yehova?” (1 Ti. 6:6-8) Kisha umusikilize kwa uangalifu wakati iko anakuelezea.

16. Wakati mutu mwenye alishazeeka na kijana wanazungumuza pamoja, namna gani wote wawili wanapata faida?

16 Wakati mutu mwenye alishazeeka anazungumuza na kijana, wote wawili wanapata faida. (Ro. 1:12) Nyie vijana, mutakuwa wenye shukrani zaidi wakati mutasikia namna Yehova iko anahangaikia watumishi wake waaaminifu, na wale wenye walishazeeka watajisikia kuwa wanaheshimiwa. Watafurahi kukuelezea baraka zenye walipata kutoka kwa Yehova.

17. Juu ya nini tunaweza kusema kama wale wenye walishazeeka wanaendelea kuwa wazuri zaidi hata kisha miaka?

17 Uzuri wa sura unapoteaka polepole vile mutu iko anakomala, lakini wale wenye wako washikamanifu kwa Yehova wanaendeleaka kuwa wazuri tena sana hata kisha miaka. (1 Te. 1:2, 3) Juu ya nini ile ni kweli? Juu vile miaka iko inapita, wale wenye wako washikamanifu kwa Yehova wanaacha roho yake iwafinyange na kuwafanya wakuwe wazuri tena zaidi. Kadiri tunaendelea kujua muzuri zaidi ndugu na dada zetu wenye walishazeeka, kuwaheshimia, na kujifunza mambo fulani kwao, ni vile tutawaona kuwa hazina za maana sana!

18. Ni mambo gani tutazungumuzia mu habari ya kufuata?

18 Kutaniko inaendelea kuwa nguvu zaidi, hapana tu wakati vijana wanaona wale wenye walishazeeka kuwa wa maana, lakini pia wakati wale wenye walishazeeka wanaona vijana kuwa wa maana. Mu habari ya kufuata, tutaona namna ndugu na dada wenye walishazeeka wanaweza kuonyesha kama wanaona vijana wa mu kutaniko kuwa wa maana sana.

WIMBO 144 Kaza Macho ku Zawadi!

^ fu. 5 Ndugu na dada waaminifu wenye walishazeeka wako kama hazina yenye samani sana. Hii habari itatutia moyo tuendelee kuwapenda na kuwaheshimia sana na itaonyesha nini tunaweza kufanya ili hekima na uzoefu wao ituletee faida. Tena, itahakikishia ndugu na dada wenye walishazeeka kama wako wa maana sana mu tengenezo ya Yehova.