Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Mambo Gani Hayatakuwa Tena Wakati Ufalme wa Mungu Utakuja?

Ni Mambo Gani Hayatakuwa Tena Wakati Ufalme wa Mungu Utakuja?

“Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 YOHANA 2:17.

NYIMBO: 134, 24

1, 2. (a) Ni katika njia gani ulimwengu huu muovu uko kama mutu mwenye alifanya makosa makubwa mwenye iko karibu kuuawa? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Wote mbinguni na duniani watakuwa na mawazo gani kisha ulimwengu huu muovu kuharibiwa?

FIKIRIA hali hii: Mutu mwenye alifanya makosa makubwa anatembea katika njia yenye kuwa katikati ya vyumba vya gereza na walinzi wenye kuwa naye wanalalamika hivi: “Maiti iko inatembea!” Sababu gani wanasema hivyo? Hata kama mutu huyo ni muzima na anaonekana kuwa na afya ya muzuri, amehukumiwa kifo na iko karibu kuuawa. Ni kama vile amekwisha kufa. *—Soma maelezo ya chini.

2 Tunaishi katika ulimwengu muovu wenye kuwa kama mutu huyo mwenye kuwa karibu kuuawa. Biblia inasema hivi: “Ulimwengu unapitilia mbali.” (1 Yohana 2:17) Yehova ameamua kama mwisho wa ulimwengu huu utafika hivi karibuni; kwa hiyo, mwisho huo utafika hakika. Lakini kuko tofauti moja kubwa kati ya mwisho wa ulimwengu huu na kuuawa kwa mutu huyo mwenye alifanya makosa makubwa. Watu fulani wanaweza kuwaza kuwa hukumu ya mutu huyo haikukuwa ya haki, na kutumaini kuwa hatauawa. Lakini, Yehova ni muamuzi mukamilifu, na uamuzi wake wa kuharibu ulimwengu huu ni wa haki kabisa. (Kumbukumbu la Torati 32:4) Uharibifu wa ulimwengu huu hautachelewa. Kisha ulimwengu huu kuharibiwa, wote wenye kuwa mbinguni na duniani watakubali kwamba hukumu ya Yehova ilikuwa sawa. Kutakuwa kitulizo kabisa!

3. Ni matatizo gani ine yenye hayatakuwa tena wakati Ufalme wa Mungu utakuja?

3 “Ulimwengu” wenye “unapitilia mbali” unatia ndani mambo gani? Unatia ndani mambo ya mubaya yenye yamekuwa katika maisha ya watu leo. Hivi karibuni, mambo hayo yote hayatakuwa tena. Kwa kweli, hiyo ni sehemu ya “habari njema ya Ufalme.” (Mathayo 24:14) Katika habari hii, tutazungumuzia matatizo ine yenye hayatakuwa tena wakati Ufalme wa Mungu utakuja: watu wabaya, mashirika yenye udanganyifu, matendo ya mubaya, na hali za mubaya. Juu ya kila tatizo tutajifunza (1) mambo yenye kutupata kwa sababu ya tatizo hilo, (2) Yehova atafanya nini juu ya tatizo hilo, na (3) ataweka nini mahali pa tatizo hilo.

WATU WABAYA

4. Ni mambo gani yanatupata leo kwa sababu ya watu wabaya?

4 Ni mambo gani yanatupata leo kwa sababu ya watu wabaya? Mutume Paulo alisema kama katika siku za mwisho kutakuwa ‘nyakati za hatari zilizo ngumu kushugulika nazo.’ Kisha aliongezea hivi: ‘Watu waovu na wajanja wataendelea kutoka ubaya mupaka ubaya zaidi.’ (2 Timotheo 3:1-5, 13) Umekwisha kujionea jambo hilo? Wengi kati yetu wamepatwa na mateso kwa sababu ya watu wenye kutendea wengine kwa jeuri, watu wenye ubaguzi wa rangi ya ngozi, na watu wenye kufanya makosa makubwa sana. Wamoja kati yao hawajaribu kuficha mambo ya mubaya yenye wanafanya. Wengine wanaonyesha kuwa wanapenda kusaidia watu, lakini ndani yao ni wabaya kabisa. Lakini, hata kama sisi wenyewe hatujatendewa mubaya, tunateseka pia kwa sababu ya watu wabaya. Tunajisikia mubaya sana wakati tunasikia namna wanatendea bila huruma watoto, watu wenye kuzeeka, na wengine wenye hawana uwezo wa kujilinda. Watu hao wabaya wanatenda katika njia yenye kuwafanya waonekane kama wanyama wakali ao hata mashetani. (Yakobo 3:15) Jambo la kufurahisha ni kwamba Neno la Yehova linatupatia tumaini.

5. (a) Watu wabaya wangali na nafasi ya kufanya nini? (b) Ni nini itawapata wale wenye wanakataa kubadilika?

5 Yehova atafanya nini? Kwa sasa, Yehova anapatia watu wabaya nafasi ya kubadilika. (Isaya 55:7) Hata kama ulimwengu huu utaharibiwa hivi karibuni, hawajapata hukumu yao. Hata hivyo, ni nini itawapata wale wenye wanakataa kubadilika na wenye wataendelea kuunga mukono ulimwengu huu mupaka wakati wa ziki kubwa? Yehova ameahidi kama ataondoa watu wabaya wote katika dunia. (Soma Zaburi 37:10.) Leo, watu wengi wamejifunza kuficha mambo ya mubaya yenye wanafanya, na mara nyingi hawapewe malipizi. (Ayubu 21:7, 9) Lakini Biblia inatukumbusha kama ‘macho yake [Mungu] yako juu ya njia za mwanadamu, naye anaziona hatua zake zote. Hakuna giza wala kivuli kizito kwa ajili ya wale wanaozoea kufanya mazara [mabaya] kujificha humo.’ (Ayubu 34:21, 22) Kwa hiyo, haiwezekane kujificha mbele ya Yehova. Anaona mambo yote yenye watu wabaya wanafanya. Kisha Har-Magedoni, tutaangalia mahali walizoea kupatikana, lakini hatutawaona. Watakuwa wameharibiwa milele!—Zaburi 37:12-15.

6. Ni nani watabakia wakati watu wabaya hawatakuwa tena, na sababu gani hiyo ni habari njema?

6 Ni nani watabakia wakati watu wabaya hawatakuwa tena? Yehova anaahidi hivi: “Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.” Kisha mustari mwingine wa zaburi hiyo, unasema hivi: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (Zaburi 37:11, 29) “Wapole” na “waadilifu” ni nani? Wapole ni watu wanyenyekevu wenye kufundishwa na Yehova na wenye kumutii. Waadilifu ni wale wenye wanapenda kufanya mambo yenye Mungu anasema kuwa ni sawa. Leo katika ulimwengu, watu wabaya ni wengi zaidi kuliko waadilifu. Lakini katika ulimwengu mupya, kutakuwa tu watu wapole na waadilifu, na watafanya dunia kuwa paradiso!

MASHIRIKA YENYE UDANGANYIFU

7. Ni mambo gani yanatupata leo kwa sababu ya mashirika yenye udanganyifu?

7 Ni mambo gani yanatupata leo kwa sababu ya mashirika yenye udanganyifu? Mambo mengi ya mubaya yenye kuwa katika ulimwengu leo hayaletwe na watu mumoja-mumoja, lakini yanaletwa na mashirika mbalimbali. Dini zinadanganya mamilioni ya watu. Kwa mufano zinasema uongo juu ya Mungu, zinasema kama hatuwezi kutumainia Biblia, na zinadanganya watu juu ya wakati unaokuja wa dunia na wanadamu. Serikali zenye udanganyifu zinachochea vita, zinaonea watu masikini na wenye hawana uwezo wa kujitetea, zinachochea watu watendeane mubaya kwa sababu ya ubaguzi wa rangi ya ngozi. Serikali hizo zinakuwa na mali na mamlaka kwa sababu ya kuonyesha upendeleo ao kwa kukubali rushwa (kata-midomo). Kompanyi zenye pupa zinachafua mazingira, zinaharibu mali ya asili, na zinatumikisha watu kwa faida yazo ili hesabu kidogo ya watu ndio wakuwe matajiri. Kwa kweli, mashirika yenye udanganyifu ndiyo yanaleta mateso mengi yenye kuwa katika ulimwengu leo.

8. Kulingana na Biblia, mashirika yenye watu wengi leo wanaona kuwa yenye nguvu, yatapatwa na nini?

8 Yehova atafanya nini? Ziki kubwa itaanza wakati serikali zitashambulia dini zote za uongo, zenye Biblia inaita Babiloni Mukubwa. (Ufunuo 17:1, 2, 16; 18:1-4) Dini hizo zote zitaharibiwa kabisa. Lakini, mashirika mengine yote yenye udanganyifu yatapatwa na nini? Biblia inalinganisha mashirika hayo na milima na visiwa kwa sababu yanaonekana kuwa yenye nguvu sana. (Soma Ufunuo 6:14.) Lakini inaongezea kuwa serikali na mashirika mengine yote yenye hayaunge mukono Ufalme wa Mungu, yataharibiwa. Hiyo itakuwa sehemu ya mwisho ya ziki kubwa. (Yeremia 25:31-33) Kisha hapo, hakutakuwa tena hata kidogo mashirika yenye udanganyifu!

9. Sababu gani tunaweza kuwa hakika kama dunia mupya itakuwa yenye kupangwa muzuri?

9 Ni nini itachukua nafasi ya mashirika yenye udanganyifu? Kisha Har-Magedoni, kutakuwa shirika fulani duniani? Biblia inasema hivi: ‘Kulingana na ahadi yake tunangojea mbingu mupya na dunia mupya, na humo uadilifu utakaa.’ (2 Petro 3:13) Mbingu na dunia za zamani ni serikali zenye udanganyifu na watu wenye zinaongoza. Kisha mbingu na dunia hizo kuharibiwa, nini itachukua nafasi yazo? ‘Mbingu mupya na dunia mupya.’ Mbingu mupya inamaanisha serikali mupya, ni kusema, Ufalme wenye unafanyizwa na Yesu Kristo na watawala wenzake 144000. Dunia mupya inamaanisha watu wenye kutawaliwa na Ufalme wa Mungu. Yesu na watawala wenzake wataiga Yehova Mungu kwa ukamilifu, ambaye ni Mungu mwenye kupanga mambo muzuri. (1 Wakorintho 14:33) Kwa hiyo, ‘dunia mupya’ itakuwa yenye kupangwa muzuri. Kutakuwa wanaume wazuri wenye wataongoza mambo. (Zaburi 45:16) Wanaume hao wataongozwa na Kristo na wale 144000. Fikiria wakati mashirika yote yenye udanganyifu yataondolewa, na nafasi ya mashirika hayo itachukuliwa na shirika moja lenye umoja lenye haliwezi kuwa na udanganyifu hata kidogo, ni kusema, Ufalme wa Mungu.

MATENDO YA MUBAYA

10. Ni matendo gani ya mubaya yenye watu wanazoea kufanya mahali kwenye unaishi, na hilo liko na matokeo gani juu yako na familia yako?

10 Ni mambo gani yanatupata leo kwa sababu ya matendo ya mubaya? Tunaishi katika ulimwengu wenye kujaa mwenendo muchafu, udanganyifu, na jeuri nyingi. Mambo ya kujifurahisha ya ulimwengu huu yanaonyesha matendo hayo kuwa yenye kupendeza na kuzarau kanuni za Yehova za mema na mabaya. (Isaya 5:20) Zaidi sana wazazi wanapaswa kujikaza sana ili kujilinda wao wenyewe na kulinda watoto wao juu ya mambo hayo ya mubaya. Kwa kweli, Wakristo wote wa kweli wanapaswa kujikaza sana ili kulinda urafiki wao pamoja na Yehova katika ulimwengu wenye kuwa na watu wenye hawaheshimie kanuni za Mungu.

11. Hukumu ya Yehova juu ya Sodoma na Gomora, inatufundisha nini?

11 Yehova atafanya nini juu ya matendo ya mubaya? Fikiria jambo lenye Yehova alifanya juu ya mambo ya mubaya yenye yalikuwa yanafanyika katika miji ya Sodoma na Gomora. (Soma 2 Petro 2:6-8.) Loti alikuwa mwanaume muadilifu, na yeye na familia yake waliteseka sana kwa sababu ya mambo yote ya mubaya yenye watu wenye kuwazunguka walikuwa wanafanya. Yehova aliharibu eneo hilo lote ili kumaliza mambo ya mubaya yenye yalikuwa yanafanyika. Lakini alikuwa pia ‘anaweka kielelezo [mufano]’ kwa ajili ya watu wabaya leo. Kama tu vile Yehova alimaliza matendo yote ya mubaya wakati huo, atayamaliza pia leo wakati ataharibu ulimwengu huu.

12. Unangojea kwa hamu kufanya mambo gani wakati ulimwengu huu hautakuwa tena?

12 Ni nini itachukua nafasi ya matendo ya mubaya? Katika dunia mupya tutakuwa na mambo mengi ya kufanya yenye kufurahisha. Kwa mufano, tutageuza dunia kuwa paradiso na kujenga manyumba kwa ajili yetu na wapendwa wetu. Tutakaribisha pia mamilioni ya watu wenye watafufuliwa na kuwafundisha juu ya Yehova na mambo yote yenye amefanyia wanadamu. (Isaya 65:21, 22; Matendo 24:15) Wakati huo, tutakuwa na mambo mengi ya kufanya yenye yatatuletea furaha na kumuletea Yehova sifa!

HALI ZA MUBAYA

13. Uasi wenye ulitokea katika Edeni umeleta matokeo gani?

13 Ni mambo gani yanatupata leo kwa sababu ya hali za mubaya? Ulimwengu wenye kujaa watu wabaya, mashirika yenye udanganyifu, na matendo ya mubaya umefanya hali za maisha zikuwe za mubaya. Sisi wote tunateseka kwa sababu ya mambo kama vile vita, umasikini, ubaguzi wa rangi ya ngozi, magonjwa, na kifo. Hali hizo za mubaya zilianza kwa sababu Shetani, Adamu, na Eva walimuasi Yehova. Na sisi wote tunaendelea kuteseka kwa sababu ya uasi wao.

14. Yehova atafanya nini juu ya hali za mubaya?

14 Yehova atafanya nini juu ya hali za mubaya? Fikiria mifano fulani. Yehova anaahidi kumaliza vita yote. (Soma Zaburi 46:8, 9.) Atamaliza magonjwa. (Isaya 33:24) Atameza kifo milele. (Isaya 25:8) Atamaliza umasikini. (Zaburi 72:12-16) Na Yehova ataondoa hali zingine zote za mubaya zenye zinafanya maisha yakuwe magumu sana leo. Ataondoa Shetani na mashetani wake ili wasichochee watu kufanya mambo ya mubaya!—Waefeso 2:2.

Wazia namna maisha yatakuwa katika ulimwengu wenye hauna vita, magonjwa, ao kifo! (Picha hii inapatana na fungu la 15)

15. Ni mambo gani yenye hayatakuwa tena hata kidogo kisha Har-Magedoni?

15 Wazia kidogo namna maisha yatakuwa katika ulimwengu wenye hauna vita, magonjwa, ao kifo! Hakutakuwa maaskari, silaha, ao mambo yenye kukumbusha watu vita. Hatutakuwa na lazima ya hospitali, wanganga, ao vyumba vya kuwekea maiti. Watu hawatatendeana mubaya; kwa hiyo, hatutakuwa na lazima ya polisi, kengele za kujulisha hatari, ao pengine hata kufuli na funguo! Hali hizo zote za mubaya zenye kutuletea mahangaiko hazitakuwa tena hata kidogo.

16, 17. (a) Wale wenye wataokoka Har-Magedoni watajisikia namna gani? Toa mufano. (b) Unaweza kufanya nini ili ukuwe hakika kama utaendelea kuishi wakati ulimwengu huu hautakuwa tena?

16 Maisha yatakuwa namna gani wakati hali za mubaya hazitakuwa tena? Ni vigumu kuwazia namna hali itakuwa. Tumeishi katika hali za mubaya kwa miaka mingi sana hivi kwamba pengine hatuone tena kama hali hizo zinatuletea mahangaiko mengi. Kwa mufano, watu wenye kuishi karibu na mahali kwenye treni zinazoea kusimama, inawezekana wasitambue tena makelele ya mahali hapo. Na watu wenye kuishi karibu na mahali pa kutupia uchafu inawezekana wasitambue tena harufu ya uchafu. Lakini wakati Yehova ataondoa hali zote za mubaya, hilo litaleta kitulizo kabisa!

17 Ni nini itachukua nafasi ya mahangaiko yote yenye tuko nayo leo? Andiko la Zaburi 37:11 linasema hivi: “Watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.” Ni jambo lenye kutia moyo sana kujua kwamba hilo ndilo jambo lenye Yehova anapenda tupate! Katika wakati huu wenye mahangaiko, fanya yako yote ili ubakie karibu na Yehova na tengenezo lake. Tumaini lako la wakati unaokuja ni la maana sana; kwa hiyo, ufikiri sana juu ya tumaini hilo, uhakikishe kwamba unaliona kuwa la kweli, na uelezee wengine juu ya tumaini hilo. (1 Timotheo 4:15, 16; 1 Petro 3:15) Ikiwa unafanya hivyo, unaweza kuwa hakika kwamba wakati mwisho wa ulimwengu huu utafika, utaendelea kuishi na utakuwa na furaha milele!

^ fu. 1 Fungu hili linazungumuzia desturi yenye ilikuwa inafanywa kumepita miaka mingi katika magereza ya sehemu fulani za inchi ya Amerika.