Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kujifunza Juu ya Mungu Kunaweza Kukuletea Faida Gani?

Kujifunza Juu ya Mungu Kunaweza Kukuletea Faida Gani?

Kufikia hapa, tumejifunza mambo yenye imetusaidia kupata jibu la ulizo, Mungu ni nani? Tulianza kwa kujifunza mu Biblia kama jina lake ni Yehova na kama sifa yake kubwa zaidi ni upendo. Tulijifunza pia mambo yenye amefanya na ile yenye angali atafanya kwa faida ya wanadamu wote. Kwa kuwa kuko mambo mingi ya kujifunza juu ya Mungu, pengine unaweza kujiuliza kama kufanya vile kunaweza kukuletea faida gani.

Yehova anaahidi kuwa “kama unamutafuta, atajiacha umupate.” (1 Mambo ya Nyakati 28:9) Kadiri unamutafuta Mungu na kufikia kumujua utapata jambo fulani la maana sana, “urafiki wa karibu pamoja na Yehova”! (Zaburi 25:14) Kuwa na urafiki wa karibu pamoja na Yehova kunaweza kukuletea faida gani?

Furaha ya Kweli. Yehova anaitwa “Mungu mwenye furaha.” (1 Timoteo 1:11) Kumukaribia na kuiga njia zake kutakuletea furaha ya kweli, jambo lenye linaweza kuwa na matokeo ya muzuri juu ya afya yako ya moyoni, ya kiakili, na ya kimwili. (Zaburi 33:12) Utaweza pia kuwa na maisha yenye furaha: kwa kuepuka tabia zenye hatari, kukomalisha tabia zenye kuwa muzuri kwa afya, na kwa kuendelea kuwa na uhusiano wa muzuri pamoja na wengine. Utafikia kukubaliana na maneno ya muandikaji mumoja wa zaburi mwenye alisema hivi: “Kumukaribia Mungu ni jambo la muzuri kwangu.”​—Zaburi 73:28.

Yehova atakulinda na kukuhangaikia kipekee. Yehova aliahidi watumishi wake hivi: “Nitakupatia shauri jicho langu likikuangalia.” (Zaburi 32:8) Ile inamaanisha kama Yehova anahangaikia kila mutumishi wake na anamupatia mambo yenye iko nayo kabisa lazima. (Zaburi 139:1, 2) Wakati unakomalisha urafiki wa muzuri pamoja na Yehova, utaona kama sikuzote iko tayari kukusaidia.

Wakati wako wenye kuja utakuwa wa muzuri sana. Zaidi ya kukusaidia kuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha leo, Yehova Mungu anakupatia nafasi ya kuwa na wakati wenye kuja wa muzuri sana. (Isaya 48:17, 18) Biblia inasema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3) Katika huu wakati wa magumu, tumaini lenye Mungu anatoa linaweza kutenda kama nanga yenye inatusaidia tuendelee kuwa ‘hakika na imara.’​—Waebrania 6:19.

Hizi ni sababu kidogo tu kati ya sababu mingi za maana zenye kutuchochea kumujua Mungu muzuri zaidi na kukomalisha urafiki pamoja naye. Tunakutia moyo uzungumuze na Shahidi yeyote wa Yehova ao ufungue jw.org ili kupata habari zaidi zenye zinaweza kukusaidia.