Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ni Mambo Gani Yenye Mungu Amefanya?

Ni Mambo Gani Yenye Mungu Amefanya?

Kama unapenda kujua mutu fulani muzuri, ni jambo lenye kufaa ujue mambo yenye ametimiza na vizuizi vyenye alishinda. Vilevile, kama unapenda kumujua Mungu muzuri, ni jambo la lazima ujifunze mambo yenye amekwisha kufanya. Kama unajifunza, utashangaa kujua kama amekwisha kufanya mambo mingi sana yenye kutusaidia leo na yenye inafanya iwezekane kuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja.

MUNGU ALIUMBA VITU VYOTE KWA AJILI YA FAIDA YETU

Yehova Mungu ni Muumbaji Mukubwa, na “sifa zake zenye hazionekane zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaonekana kupitia vitu vyenye vilifanywa.” (Waroma 1:20) “Yeye ndiye Mutengenezaji wa dunia kwa nguvu zake, Ule mwenye alifanya imara inchi yenye kuzaa kwa hekima yake na mwenye alitandika mbingu kwa uelewaji wake.” (Yeremia 10:12) Maajabu ya uumbaji inaonyesha pia kama Mungu anatuhangaikia.

Fikiria namna Yehova amefanya maisha yetu ikuwe ya pekee sana kwa kuumba wanadamu “kwa mufano wake.” (Mwanzo 1:27) Ile inamaanisha kama alifanya iwezekane tuige kwa kiasi kidogo sifa zake za ajabu. Ametuumba na uwezo wa kutambua mambo ya kiroho, ao uwezo wa kuelewa mawazo yake na kanuni zake kuhusu mwenendo. Wakati tunajikaza kuishi kulingana na ile mambo, tunakuwa na furaha kubwa na maisha yenye kusudi. Zaidi ya ile, alitupatia uwezo wa kufanya urafiki pamoja naye.

Vitu vyenye Mungu aliumba ku dunia vinaonyesha namna anajisikia kwa ajili yetu. Mutume Paulo alisema kama Mungu ‘hakukosa kutoa ushahidi juu yake mwenyewe kwa kututendea mema, alitupatia [sisi] mvua kutoka mbinguni na vipindi vya kuzaa matunda, na kutupatia chakula kwa wingi na kujaza mioyo yetu furaha.’ (Matendo 14:17) Mungu alitupatia zaidi ya vitu vyenye tuko navyo lazima ili tuishi. Alitutolea vitu mingi zaidi na vya kila aina ili tuweze kufurahia maisha. Ile ni mambo kidogo sana kati ya mambo yenye Mungu alipanga kufanya kwa ajili yetu.

Yehova aliumba dunia ili wanadamu waishi juu yake milele. Biblia inasema hivi: “Dunia ameipatia wana wa binadamu,” na “hakuiumba tu bila sababu, lakini aliifanya ili ikaliwe na watu.” (Zaburi 115:16; Isaya 45:18) Ikaliwe na watu gani na kwa miaka ngapi? “Wenye haki watariti dunia, na wataishi milele juu yake.”​—Zaburi 37:29.

Kwa hiyo, Yehova aliumba mwanaume wa kwanza na mwanamuke wa kwanza, Adamu na Eva, na aliwatia mu paradiso ku dunia ‘ili wailime na kuitunza.’ (Mwanzo 2:8, 15) Mungu aliwapatia kazi mbili za maana na zenye kufurahisha: “Muzae na mukuwe wengi, mujaze dunia na kuitawala.” (Mwanzo 1:28) Kwa hiyo, Adamu na Eva walikuwa na tumaini la kuwa na maisha yenye haina mwisho juu ya dunia. Jambo la kuhuzunisha ni kuwa, walichagua kukosa kumutii Mungu na njo maana walipoteza nafasi yenye walikuwa nayo ya kuwa kati ya “wenye haki” wenye “watariti dunia.” Lakini, kama vile tutaona, matendo yao haikubadilisha kusudi la Yehova kwa ajili yetu ao kwa ajili ya dunia. Kwanza, tuone jambo lingine lenye Mungu ametufanyia.

MUNGU ALITUPATIA NENO LAKE LENYE KUANDIKWA

Biblia inaitwa pia Neno la Mungu. Juu ya nini Yehova alitupatia Biblia? Sababu kubwa ni ili tujifunze juu yake. (Mezali 2:1-5) Ni kweli kwamba, Biblia hailete jibu la kila ulizo lenye tunaweza kuwa nalo juu ya Mungu; na hakuna kitabu kingine chenye kinaweza kufanya vile. (Muhubiri 3:11) Lakini, kila jambo lenye kuwa mu Biblia, linatusaidia kumujua Mungu. Tunaelewa yeye ni mutu wa namna gani kupitia namna anatendea watu. Tunajua ni watu wa namna gani anapenda na wale wenye anachukia. (Zaburi 15:1-5) Tunajua mawazo yake kuhusu ibada, mwenendo, na vitu vya kimwili. Tena, Biblia inatusaidia kujua muzuri zaidi sifa za Yehova kupitia maneno na matendo ya Mwana wake, Yesu Kristo.​—Yohana 14:9.

Sababu ingine ilifanya Yehova atupatie Neno lake, Biblia, ni juu tujue kile tunaweza kufanya ili kuwa na maisha yenye furaha na yenye kusudi. Kupitia Biblia, Yehova anatuambia namna ya kuwa na familia yenye furaha, namna ya kutosheka, na namna ya kupambana na mahangaiko. Na kama vile itazungumuziwa mu gazeti hili, Biblia iko na majibu ya maulizo ya maana sana kuhusu maisha, kama vile: Juu ya nini kuko mateso ya mingi? Mambo itakuwa namna gani wakati wenye kuja? Inaonyesha pia mambo yenye Mungu amefanya ili kuhakikisha kama kusudi lake la ku mwanzo litatimia.

Kuko njia zingine mingi zenye kuonyesha kama Biblia ni kitabu cha pekee sana na kama mwenye aliitunga ni Mungu. Biblia iliandikwa na watu 40 hivi katika kipindi cha miaka 1 600, lakini inalinda kichwa chake kikubwa juu Mutungaji ni Mungu. (2 Timoteo 3:16) Tofauti na vitabu vingine vya zamani, kimelindwa kwa miaka mingi bila kuingizwa makosa, kama vile maandishi ya zamani ya Biblia yanahakikisha. Zaidi ya ile, Biblia inaendelea kuwako, hata kama watu fulani walijikaza kuzuia ili isitafsiriwe, isigawanywe, na isisomwe. Leo, ni kitabu chenye kinagawanywa sana na kutafsiriwa sana mu dunia. Kuwako kwa Biblia ni ushuhuda wenye kuonyesha kama “neno la Mungu wetu linadumu milele.”​—Isaya 40:8.

MUNGU ALIHAKIKISHA KUWA KUSUDI LAKE LITATIMIA

Jambo lingine lenye Mungu amefanya ni mipango yenye alikamata ili kuhakikisha kuwa kusudi lake kwa ajili yetu litatimia. Kama vile tuliona ku mwanzo, kusudi la Mungu lilikuwa kwamba watu waishi milele juu ya dunia. Lakini, wakati Adamu alichagua kukosa kumutii Mungu na kufanya zambi, alipoteza nafasi ya kuishi milele na alifanya pia watoto wenye angezaa wapoteze ile nafasi. “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.” (Waroma 5:12) Kukosa kutii kwa mwanadamu kulifanya ionekane kuwa kusudi la Mungu halitatimia. Yehova alitenda namna gani?

Namna Yehova alitenda ilipatana na sifa zake. Alionyesha haki kwa kuhukumu Adamu na Eva juu ya matendo yao, lakini alionyesha upendo kwa kukamata mipango kwa ajili ya watoto wenye wangezaa. Kwa hekima, Yehova aliamua namna ya kupambana na ile tatizo, na bila kukawia alitangaza jambo lenye lingemaliza ile tatizo. (Mwanzo 3:15) Njia moja ya kutukomboa mu zambi na kifo, ingetolewa kupitia Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. Ile iliomba nini?

Ili kukomboa wanadamu kutokana na matokeo ya uasi wa Adamu, Yehova alituma Yesu ku dunia ili kufundisha watu namna ya kupata uzima na ili “atoe uzima wake kuwa bei ya ukombozi pa nafasi ya wengi.” * (Matayo 20:28; Yohana 14:6) Yesu angeweza kutoa bei ya ukombozi juu alikuwa mutu mukamilifu kama Adamu. Lakini tofauti na Adamu, Yesu alitii kwa ukamilifu, hata kama ilimuomba kufa. Kwa kuwa Yesu hakustahili kufa, Yehova alimufufua ili aishi mbinguni. Yesu angeweza sasa kufanya kile Adamu alishindwa kufanya​—kutolea wanadamu watiifu tumaini la kuishi milele. “Kwa maana kama vile kupitia kukosa kutii kwa ule mutu mumoja wengi walifanywa kuwa watenda-zambi, vilevile pia kupitia kutii kwa mutu mumoja wengi watafanywa kuwa wenye haki.” (Waroma 5:19) Kupitia bei ya ukombozi ya Yesu, Mungu atatimiza ahadi yake ya kufanya wanadamu waishi milele ku dunia.

Tumejifunza mambo mingi kumuhusu Yehova kupitia namna alihangaikia matatizo yenye ililetwa na kukosa kutii kwa Adamu. Tunaona kama hakuna kitu kinaweza kumuzuia Yehova kumaliza mambo yenye alianza; neno lake “hakika litafanikiwa.” (Isaya 55:11) Tunajifunza pia kuwa Yehova anatupenda sana. “Kwa jambo hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwetu, kwamba Mungu alimutuma Mwana wake muzaliwa-pekee katika ulimwengu ili tupate uzima kupitia yeye. Ni hivi upendo uko, hapana kwamba sisi tumemupenda Mungu, lakini kwamba yeye alitupenda akamutuma Mwana wake kuwa zabihu ya kufunika kwa ajili ya zambi zetu.”​—1 Yohana 4:9, 10.

Mungu “hakujizuia kutoa hata Mwana wake mwenyewe lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote,” kwa hiyo tuko hakika kama Mungu ‘atatupatia vitu vingine vyote kwa fazili’ vyenye alituahidi. (Waroma 8:32) Mungu ameahidi kutufanyia nini? Tunakutia moyo usome habari yenye kufuata.

NI MAMBO GANI YENYE MUNGU AMEFANYA? Yehova aliumba wanadamu ili waishi milele ku dunia. Alitutolea Biblia ili tuweze kujifunza kumuhusu. Kupitia Yesu Kristo, Yehova alifanya bei ya ukombozi itolewe, ili kuhakikisha kama kusudi lake litatimia

^ fu. 16 Ili kupata habari zaidi juu ya bei ya ukombozi, ona sura ya 5 ya kitabu Biblia Inatufundisha Nini? chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na kinapatikana ku site yetu www.pr418.com.